Kitine: Nchi sasa yaongozwa kienyeji

Kitine: Nchi sasa yaongozwa kienyeji

Haya ndiyo mambo aliyosema Kitine ya kuendesha nchi kienyeji. Msekwa badala ya kutoa maoni yake na nini kifanywe ili kuondokana na matatizo makubwa tuliyokuwa nayo ya uongozi wa juu nchi kwetu yanayosababisha nchi kuendeshwa kienyeji analeta usanii wa hali ya juu!!!! 🙁

Date::2/19/2009
Msekwa asema hawezi kujadili maoni ya Dk Kitine

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Pius Msekwa, hana cha kumjibu, Dk Hassy Kitine

Na Exuper Kachenje
Mwananchi​
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Pius Msekwa amesema, Mkurugenzi mkuu wa zamani wa Idara ya Usalama wa Taifa Hassy Kitine ametumia haki yake ya kikatiba kutoa maoni kuhusu mwelekeo wa taifa.

Amesema yeye akiwa Kiongozi wa CCM hawezi kujadili maoni ya binafsi ya mtu kwani ni sawa na kuingilia haki yake.

Msekwa alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam jana alipotakiwa na Mwananchi kutoa maoni yake binafsi na CCM kufuatia kauli iliyotolewa na Kitine juzi kwamba tangu kipindi cha mwisho cha utawala wa Rais Benjamin Mkapa nchi, ilivurugika na kwamba maadili yameporomoka kuanzia ndani ya CCM.

Katika mkutano wake maalum na baadhi ya vyombo vya habari katika mgahawa wa Gymkana jijini Dar es Salaam pamoja na mambo mengine Kitine alisema mfano wa kuoza kwa maadili ndani ya CCM upo wazi pale waziri anapojiuzulu wadhifa wake kwa tuhuma, lakini bado anabaki kuwa mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Mbunge.

Akizungumza na Mwananchi jana katika hoteli ya Regency, Msasani, Msekwa alisema "Sioni kama ni utaratibu mzuri kutolea maoni yaliyotolewa na mtu mwingine."

Alisema kutoa maoni ni haki ya kila mtanzania ambayo amepewa kikatiba ili mradi asivunje sheria, na kuongeza kuwa Kitine ametumia haki yake ya kikatiba.

"Kila mtanzania ana haki ya kutoa maoni ili mradi asivunje sheria," alisema Msekwa. Aliongeza kuwa kwa maoni yake binafsi CCM haitazungumzia maoni ya mtu binafsi na wala si utaratibu mzuri kwa viongozi kuzungumzia na kutolea kauli maoni ya watu.

Alifafanua kuwa kiongozi kuzungumzia maoni au kauli ya mtu binafsi ni sawa na kuvunjavunja maoni na mtazamo wa mtu huyo hali ambayo inaweza kuwatia woga wananchi katika kutumia haki yao ya kutoa maoni.

"Kiongozi au Chama kuzungumzia maoni ya mtu binafsi ni kuvunjavunja demokrasia, mtazamo na maoni ya mtu. Hiyo itawatia watu woga wa kutoa maoni yao wakihofia viongozi kuingilia," alisema Msekwa na kusisitiza hatua hiyo itachangia kuua demokrasia kwa kuwa demokrasia huanzia ngazi ya chini kwa mtu mmoja mmoja.
 
Mkuu FMES,
Nimekusikia. Nakubaliana na mengi unayosema lakini ujumbe wangu umelenga zaidi
aliyoyasema Kitine. Unajua hapa Marekani kuna benki ilimwajiri mwizi aliyekubuhu katika bank robbery awasaidie kupambana na wizi huo. Sasa kama Kitine ni fisadi naye ameona kuwa mambo nchini hayaendi vizuri, tusikilize ujumbe wake. He may have some inside information, no?

Kweli kabisa Mkuu, Mjumbe hauwawi anachokisema Kitine kina ukweli na kuungwa mkono na Watanzania walio wengi.
 
Kama Kitine alikuwa fisadi zamani basi kwa maneno aliyoyasema kuhusu uongozi wa nchi yetu sasa ameokoka, amebadilika. Aliyoyasema ni kweli na sahihi kabisa. Wenye mapenzi mema na nchi yetu hawana budi kuyaunga mkono aliyoyasema badala ya kumsakama. Kama Kitene bado ni fisadi vema ifunguliwe thread nyingine juu yake ili wenye ushahidi wa ufisadi wake wauanike na wana JF waujadili. Thread hii ibaki kuwa ni mjadala kuhusu hoja aliyoitoa Kitene badala ya kumjadili kitine mwenyewe.

Kwangu Kitine amethubutu kusema yale ambayo waheshimiwa wengi wanaoujua udhaifu wa serikali yetu na chama tawala lakini wanaogopa kusema. Kama mmoja alivyosema hapa JF ukweli unabaki kuwa ukweli tu hata kama aliyeusema ni shetani.
 
ijapokuwa aliyoyasema yote yanajulikana lakini wengine ametuthibitishia kuwa ni kweli kwamba kamatakamata ya kisutu ni changa la macho.mtu wa aina ya kitine kusema kuwa kesi za kisutu ni maandalizi ya uchaguzi ni pigo kwa ccm na wapinzani waitumie hii kauli ili ccm wanyimwe kura 2010!
 
Katika mkutano wake maalum na baadhi ya vyombo vya habari katika mgahawa wa Gymkana jijini Dar es Salaam pamoja na mambo mengine Kitine alisema mfano wa kuoza kwa maadili ndani ya CCM upo wazi pale waziri anapojiuzulu wadhifa wake kwa tuhuma, lakini bado anabaki kuwa mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Mbunge.

- Kitine ameiba akafukuzwa na Mwalimu uwt, mkewe akaiba akajizulu uwaziri, lakini sio ubunge mpaka wananchi wa Makete, walipoamua kumtosa kwa sababu ya ufisadi wake kwa taifa, huko kote hakuona madhara ya kuiba na kubaki mbunge huku akijiuzulu uwaziri tu,

- Leo baada ya kuwa on the sidelines kwa muda mrefu sana, sasa anataka mabadiliko, lakini yaanzie na wengine sio yeye, lakini ninatakiwa hapa nisimjadili Kitine maana ninakuwa siitakii mema Tanzania, haya mnaoitakia mema Tanzania kwa kujadili hoja yake tu endeleeni wakuu.
 
- Kitine ameiba akafukuzwa na Mwalimu uwt, mkewe akaiba akajizulu uwaziri, lakini sio ubunge mpaka wananchi wa Makete, walipoamua kumtosa kwa sababu ya ufisadi wake kwa taifa, huko kote hakuona madhara ya kuiba na kubaki mbunge huku akijiuzulu uwaziri tu,

- Leo baada ya kuwa on the sidelines kwa muda mrefu sana, sasa anataka mabadiliko, lakini yaanzie na wengine sio yeye, lakini ninatakiwa hapa nisimjadili Kitine maana ninakuwa siitakii mema Tanzania, haya mnaoitakia mema Tanzania kwa kujadili hoja yake tu endeleeni wakuu.

FMES, nakubaliana kabisa na wewe kuhusu Kitine, lakini cha kujiuliza je alichokisema kuhusiana na uongozi wa nchi yetu kina ukweli? Je, Watanzania tunakubaliana naye kwamba nchi inaendeshwa kienyeji?

Kwa mantiki hayo basi pamoja na matatizo aliyokuwa nayo Kitine huko miaka ya nyuma alichosema wengi ndicho tunachokiona kuhusiana na uongozi wa nchi yetu. Mambo yanaendeshwa kienyeji mno.

Kitine kazungumza mambo ambayo Watanzania wengi tunayaona yana ukweli kuhusu hali ya uongozi katika nchi yetu. Msekwa anadai hawezi kuongelea juu ya hoja za mtu binafsi lakini anasahau kwamba hoja hizo za Kitine zinaungwa mkono na Watanzania walio wengi ndani na nje ya nchi kwani kuna ushahidi wa kutosha kwamba nchi inaendeshwa kienyeji na hili si jambo la wiki moja iliyopita au mwezi mmoja uliopita ni miaka sasa tangu Kikwete aingie madarakani hali hii ya kuendesha nchi kienyeji imekuwa ikiendelea.

Pamoja na kufanya mabadiliko ya baraza la mawaziri mara mbili lakini hakuna ahueni yoyote. Pia Watanzania tunakumbuka kauli ya Pinda, Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwamba Mafisadi ni matajiri wakubwa na kama wakikamatwa basin chi itawaka moto. Pamoja na kuwa baadhi walikamatwa na kutiwa ndani lakini tunaona kesi hizo hazijapewa kipaumbele chochote ni usanii tu wa kutaka kuonyesha kwamba wanashughulikia ufisadi lakini hakuna lolote lile. Hizi kesi za mafisadi zilibidi kupewa kipaumbele na kusikilizwa angalau mara tatu au hata zaidi kwa wiki, lakini tutakachokiona ni kupigwa kalenda tu na kisha kuambiwa watuhumiwa wote wameachiwa huru kwa sababu hakuna ushahidi wa kutosha.

Tume ya Mwakyembe ilitoa mapendekezo ya kuondolewa madarakani Mkuu Wa TAKUKURU na Mwanasheria Mkuu, lakini hadi hii leo bado wanapeta tu sijui kwa faida ya nani!? Haya ndiyo mambo ya kuendesha nchi kienyeji. Tuna matatizo chungu nzima kwenye kilimo, elimu, matibabu, upatikanaji maji safi lakini Serikali haikuona hayo yanastahili kipaumbele bali kutumia mapesa chungu nzima eti kutengenezesha vitambulisho vya uraia!!! Haya ndiyo mambo ya kienyeji tunayosema na kutoweka mbele maslahi ya nchi.

Sijui Msekwa anataka nani atoe tuhuma zilizotolewa na Kitine ili awe tayari kuzijadili kwa faida ya nchi yetu.

Huu ndiyo mchango wangu wa thumni
 
Kwenye kitabu kitakatifu hakuna mtu aliyekuwa mchafu kama Saulo. Lakini leo hii Wakristo wote tunajitahidi kufuata maagizo ya Saulo ambaye baada ya kuona mwanga akiwa njiani kuelekea Damascus aligeuka na kuwa Mtakatifu Paulo. Kitine naye huenda ana madhambi yake, lakini tusikilize ujumbe wake. Je,anayoyasema ni kweli? Tukianza kutafuta watakatifu peke yake katika vita vya ufisadi hatutafika mbali.

Jasusi:

Saulo hakuwa mchafu. Naomba soma kitabu vizuri na historia. Ujumbe wa Yesu uliwagawa waYahudi katika makundi mawili. Kuna walioamini kuwa Yesu ni Messiah na wale waliokuwa wanasubiri kuja kwa Messiah.

Saul alikuwa fundamental Jew ambaye hakuamini ujuo wa Yesu. Na aliona waumini wa Yesu wanawagawa waYahudi.

Saul hakuwa mchafu, alichopigania yeye kilikuwa ni watu kubakia katika uYahudi. Hivyo Saul matatizo yake yalikuwa katika ideology tu. Lakini katika imani yake ya mwanzo ya uHayudi alikuwa amebobea na hiyo inathibitishwa na maandiko yake.

Ninajibu mfano huu. Kwa sababu nikiwa shule watu walikuwa nasema kuwa wakipata nafasi, wataiba na baadaye kutubu kama Saul. Hii ni theology mbovu na inayopotosha ukweli.

Tukirudi kwenye mada. Ingekuwa Kitine ni bepari lakini sio mwizi na baadaye anahamua kufuata siasa za ujamaa kwa moyo wake wote hapo tungetumia mfano wa Saul.
 
Mengi ya aliyosema Kitine, karibu yote, ni kweli tupu. Nasupport ukweli bila kujali umesemwa lini na nani
 
Kitine: Nchi sasa yaongozwa kienyeji

na Edward Kinabo
Tanzania Daima~Sauti ya watu​

MKURUGENZI Mkuu mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Dk. Hassy Kitine, amesema taifa linakabiliwa na tatizo kubwa la uongozi, ambalo halijawahi kutokea katika historia ya nchi.

Kitine ambaye aliiongoza idara hiyo nyeti kwa karibu miaka 30 zama za Serikali ya Awamu ya Kwanza na ya Pili, alisema ukosefu huo wa uongozi umesababisha nchi iongozwe kienyeji.

Kachero huyo namba moja kwa miaka mingi, ambaye alilazimika kujiuzulu wadhifa wa uwaziri wa nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora) wakati wa utawala wa Benjamin Mkapa, mwishoni mwa miaka ya 1990 kutokana na kuhusishwa na kashfa ya mkewe kufuja fedha za umma kiasi cha shilingi milioni 40, alirejea kutoa kilio chake cha miaka mingi cha kuporomoka kwa maadili ya uongozi nchini.

Kitine ambaye aliwahi pia kuwa Mbunge wa Makete kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), alitoa matamshi hayo mazito katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam jana, alipozungumza na waandishi wa vyombo kadhaa vya habari.

“Hali tuliyofikia si nzuri, tena niseme ni mbaya sana. Kuna kuporomoka kwa kiasi kikubwa kwa maadili ya uongozi. Na hii nawaambia, nchi haijawahi kuwa katika hali mbaya huko nyuma kama ilivyo sasa. Kwa hali tuliyofikia, ni vigumu kurekebisha maadili ya uongozi.

“Tatizo kubwa ni viongozi kukosa integrity (uadilifu). Kwanza ni integrity ya viongozi wenyewe, pili ni commitment (wito), tatu ni nationalism (utaifa). Haya ndiyo yalikuwepo wakati wa Mwalimu,” alisema Dk. Kitine.


Akizungumza kwa kujiamini kama ilivyo kawaida yake, Kitine alisema viongozi wengi wa serikali wamepoteza sifa kuu tatu za uongozi ambazo ni kuwa na uadilifu, wito na kuweka mbele utaifa, sifa ambazo alisema ndizo zilikuwa nguzo ya uongozi wakati wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, chini ya Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

“That was possible (hilo liliwezekana) chini ya Mwalimu. Kama alikuwa akifanya kosa, basi kosa hilo lilikuwa likitokea tu wakati akifanya jambo kwa ajili ya kuwasaidia Watanzania.

“Philosophy (falsafa) ya Mwalimu, ilikuwa kwanza Mungu, pili Tanzania, halafu yeye binafsi. Kila kiongozi anayetofautiana na Mwalimu tu hulifikisha taifa hili kubaya, if you differ with him, utaishia kubaya,” alisema Dk. Kitine akionyesha hali ya masikitiko.


Alisema uteuzi mbaya wa viongozi, hususan ule wa mawaziri, umechangia kwa kiasi kikubwa kupatikana kwa viongozi wasio waadilifu, wengi wao wakijihusisha na vitendo vya rushwa.

“Haiwezekani viongozi wakateuliwa kwa misingi ya mitandao …sijui, kwa msingi wa politics of division (siasa za makundi) ndani ya chama. Haiwezekani nchi ikaendeshwa kienyeji. Integrity should be number one (uadilifu unapaswa kuwa kitu cha kwanza kuzingatiwa).

“Mtu anajiuzulu, anafukuzwa uwaziri kwa sababu ya kashfa, kwa sababu ya kukosa maadili, halafu anabakia kuwa mbunge na mjumbe wa kamati kuu ya chama, nini hii? Hii haifai. Waziri akikosa uadilifu anatakiwa aondolewe mara moja nyadhifa nyingine zote alizobakiwa nazo. Nadhani hii itasaidia,” alisema Dk. Kitine pasipo kutaja jina la kiongozi yeyote.

Kitine ambaye wakati wote wa mazungumzo yake alisema alikuwa anataka kujadili masuala muhimu na si watu, alieleza namna asivyo na imani na hatua zinazochukuliwa na serikali katika kukabiliana na tatizo la rushwa kubwa.

Kwa mujibu wa kachero, mwanasiasa na mwanazuoni huyo, hatua hizo ambazo zinahusisha baadhi ya watu wenye majina makubwa kufikishwa mahakamani, zimechukuliwa kwa ajili tu ya maandalizi ya uchaguzi ujao.

“Nilikuwa kiongozi wa kwanza kuzungumzia rushwa kubwa miaka 10 iliyopita. Nilisema ndiyo inayovuruga uchumi kuliko hata rushwa ya nesi, hakimu, polisi,.… hakuna hata mkubwa mmoja aliyekamatwa. Ilinigharimu sana, na mimi nilipata adhabu ya kuzuiliwa kikao kwa miezi miwili, kama huyu nani huyu, Zitto (Kabwe). Wakati huo ilikuwa ndani ya CCM.

“Mimi nadhani hatua hizi zinazochukuliwa hazilengi kukomesha tatizo la rushwa, ni siasa tu za uchaguzi,” alisema Dk. Kitine.

Alipoulizwa nini kifanyike ili kukabiliana na tatizo hilo la uongozi mbaya, pamoja na mambo mengine, alielekeza changamoto zake kwa Idara ya Usalama wa Taifa.

“Usalama wa Taifa should be completely clean (unapaswa kuwa safi kabisa). Idara hii inatakiwa kuwa, juu ya mambo ya rushwa, iwe safi kabisa. Usalama wa Taifa ndiyo unayoteua viongozi, ndiyo inayoshirikiana na rais kwa kumshauri katika kuteua mawaziri. Sasa kama Usalama wa Taifa ukiwa mchafu ndio tunapata viongozi wala rushwa. Nafikiri vigezo vinavyotumika kuteua viongozi pia vina matatizo,” alisema Dk. Kitine.

Kada huyo wa CCM ambaye kitaaluma ni mchumi na mwanasheria, akizungumzia hali ya uchumi nchini, alisema kwa kiasi kikubwa uchumi umeshikiliwa na wageni kuliko wazawa, na kuelezea kusikitishwa kwake juu ya kuwepo kwa pengo kubwa kati ya matajiri na maskini.

Akitoa mfano alisema, miongoni mwa mambo yanayoonyesha kuparaganyika kwa mambo ni kukithiri kwa idadi ya ombaomba mitaani.

“Mwalimu asingeruhusu watu hawa waombeombe barabarani. Kazi za Watanzania ni udereva teksi, daladala, mabasi, kazi ya uboi ndani ya nyumba na kazi ya kufagia barabarani. Hizi ndizo kazi za Watanzania na hawa ndio wenye mali.

“Uchumi huu wa Watanzania si wa kwao. Watanzania ambao ni matajiri hawazidi hata watano. Hakuna sera bora za kusaidia kutumia maliasili zetu ili zitupe fedha ya kujenga shule, madaraja, hospitali…..” alisema Dk. Kitine.

Akizungumzia utendaji wa kazi wa Bunge katika kusimamia utendaji wa serikali, Kitine alisema kazi inayofanywa na taasisi hiyo hivi sasa ni kubwa kuliko ilivyopata kuwa wakati wowote huko nyuma.

Hata hivyo katika kuusifia utendaji wa kazi wa Bunge, aliupongeza mchango mkubwa na muhimu wa wabunge wa upinzani katika kuiimarisha taasisi hiyo muhimu.

“Ni Bunge zuri kuliko lilivyowahi kuwa huko nyuma. Linaonyesha kila dalili za uhuru. Upinzani unafanya kazi nzuri. Bunge liko wazi zaidi na wabunge wanatoa michango mingi yakinifu, yenye manufaa kwa taifa. Likiendelea hivi tutafika mahali pazuri,” alisema.

Yaani Kitine aliyeiba US$64,000 mwaka 1997 akishirikiana na Mkapa leo ana nguvu za kusema nchi inaongozwa kienyeji? Huyu ndie alitakiwa apelekwe kisutu faster faster kwa kuiba na kutumia madaraka vibaya....tunapoteza muda kuwajadiri akina Masha wakati ushahidi wa wizi wa Kitine ni more convincing.

Kwanza Kitine atueleze jitihada alizofanya kuzirudisha US$64,000 alizoiba ndipo atupe msimamo wake juu ya mapungufu ya serikali ya sasa. Vinginevyo anakuwa kama padre anayehubiri kuacha usherati baada ya kushinda tuzo kadhaa za usherati.
 
Hata kama anayosema Kitine ni kweli, uzito wa anayosema unapungua kwa sababu naye anatuhuma zinazofanana fanana na za hao anaowasema. Ndio maana criticism za Nyerere, hasa kwenye mambo ya ufisadi, umomonyokaji wa maadili ya viongozi na mengineyo zilikuwa na nguvu na watu angalau walikuwa wanajaribu kusikiliza.
 
Hata kama anayosema Kitine ni kweli, uzito wa anayosema unapungua kwa sababu naye anatuhuma zinazofanana fanana na za hao anaowasema. Ndio maana criticism za Nyerere, hasa kwenye mambo ya ufisadi, umomonyokaji wa maadili ya viongozi na mengineyo zilikuwa na nguvu na watu angalau walikuwa wanajaribu kusikiliza.

Miafrika Ndivyo Tulivyo.......hihihihihih
 
Yaani Kitine aliyeiba US$64,000 mwaka 1997 akishirikiana na Mkapa leo ana nguvu za kusema nchi inaongozwa kienyeji? Huyu ndie alitakiwa apelekwe kisutu faster faster kwa kuiba na kutumia madaraka vibaya....tunapoteza muda kuwajadiri akina Masha wakati ushahidi wa wizi wa Kitine ni more convincing.

Kwanza Kitine atueleze jitihada alizofanya kuzirudisha US$64,000 alizoiba ndipo atupe msimamo wake juu ya mapungufu ya serikali ya sasa. Vinginevyo anakuwa kama padre anayehubiri kuacha usherati baada ya kushinda tuzo kadhaa za usherati.

- Mkulu wangu, mwenyekiti wa kamati ya bunge iliyombana Kitine, ili arudishe zile pesa badala ya mke wake kwenda jela, alikuwa Kaburu wakati huo ndio anatafuta deal ya kuhamia CCM, akaifisadi hii process Kitine akaishia kujiuzulu na kulipa only half of the money ambazo ni zetu walipa kodi yaani wananchi, Kaburu ndio akajipatia tiketi ya kuingia CCM na ubunge wa EAC juu!

- Sasa kiboko akajakukipata kule jimboni kwenye ubunge, maana wananchi wa kule walikua wamemsubiri sana tena kwa hamu sana, infact kiongozi wa CCM aliyesimamia uchaguzi wake kwenye kura za maoni, aliniambia kwamba wananchi wa huko were so fed up na huyu Kitine, kwamba kuna kata ambazo wananchi walidiriki hata kumfukuza na mawe.

Eti tujadili hoja tu ya Kitine na sio yeye, sawa sawa then kwa nini tusijadili hoja tu ya Mkapa kwamba sisi wananchi wa Tanzania ni wavivu na tuna wivu naye tu, na kwamba ana kinga ya kutofikishwa mahakamani?

Tupo pamoja mkuu hapa.
 

“That was possible chini ya Mwalimu. Kama alikuwa akifanya kosa, basi kosa hilo lilikuwa likitokea tu wakati akifanya jambo kwa ajili ya kuwasaidia Watanzania.

“Mwalimu asingeruhusu watu hawa waombeombe barabarani...”

Du, Mzee anatunga facts mchana mchana kwamba wakati wa Nyerere kulikuwa hakuna ombaomba barabarani!

Halafu katika kutathmini ubora wa kiongozi, Kitine anavyoona, kama mtu kafanya makosa wakati akiwa katika harakati za kufanya kazi za Wananchi basi poa, almuradi hakuwa na nia mbaya. Na hii ndio falsafa ya uwajibikaji ambayo tumekuwanayo toka uhuru, kwamba hakuna kulaumiana kwa uzembe, hakuna kutafuta mtu mwenye mbinu bora zaidi, kiongozi bora zaidi, mfanyakazi mwenye uwezo zaidi. Yani fanya makosa utakavyo almuradi usifanya kwa hila mbaya, utashamiri katika mfumo huo. Kama Mkapa vile, tunaambiwa alilifanyia Taifa mengi mazuri. So what? Kitine anaongea kuhusu Mwalimu kana kwamba hatujui ukweli vile, kama tuko communist China, hakuna rekodi, hakuna kubadilishana habari huru, hakuna mtandao, hakuna vitabu, na watu wooote tuko hoodwinked! Kiongozi akifanya uzembe katika efforts zake za kusaidia wananchi, au akiwa ineffective basi tumsafishe tu? Boloney! No body thinks like that anymore, Mr. Kitine. Boloney!

Anakemea ufisadi wakati yeye mwenyewe yuko tainted. Na hawa kina Kitine hawa ndo waliokuwa wasaidizi waliomzunguka Nyerere. Mkapa, Kitine, Mramba etc. etc. vifisadi vya kuchoma na mkaa. Kina Warioba nao, tainted. Yani Nyerere kufa tu ikawa fungulia mbwa!

Kwenye kitabu kitakatifu hakuna mtu aliyekuwa mchafu kama Saulo. Lakini leo hii Wakristo wote tunajitahidi kufuata maagizo ya Saulo ambaye baada ya kuona mwanga akiwa njiani kuelekea Damascus aligeuka na kuwa Mtakatifu Paulo. Kitine naye huenda ana madhambi yake, lakini tusikilize ujumbe wake. Je,anayoyasema ni kweli? Tukianza kutafuta watakatifu peke yake katika vita vya ufisadi hatutafika mbali.

Jasusi,

Basi kama ndo hivyo, Kitine kabla hajaanza kunyooshea mtu kidole, angefanya kama mwenzake alivyofanya:
"Mmesikia habari za mwenendo wangu zamani… kwamba nililiudhi kanisa la Mungu kupita kiasi, nikariharibu…

"Kweli, mimi mwenyewe naliona ndani ya nafsi yangu kwamba yanipasa kutenda mambo mengi yaliyopingamana na jina lake Yesu Mnazareti;

Nami nikayafanya hayo Yerusalemu;

Niliwafunga wengi miongoni mwa watakatifu ndani ya magereza, nikiisha kupewa amri na wakuu wa makuhani; na walipouawa nalitoa idhini yangu. Na mara nyingi katika masinagogi yote naliwaadhibu, nikawashurutisha kukufuru; nikawaonea hasira kama mwenye wazimu, nikawaudhi hata katika miji ya ugenini. Basi katika kazi hiyo nilipokuwa nikienda Dameski, mwenye mamlaka na maagizo ya wakuu wa makuhani ... nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya kiebrania, Sauli! Sauli! Mbona waniudhi?
Ni vigumu kwako kuupiga mateke mchokoo."
 
Last edited:
Kitine lacks the moral high ground to be running his mouth like this....
 
CCM wamefilisika kweli kisiasa!!!! Mbona wamemvua haraka Katibu Mkuu wa UVCCM madaraka yake wakati za kwake bado ni tuhuma pia!!!? Kwanini wasiwavue ubunge mafisadi wote akiwemo Lowassa, Mramba, Karamagi, Chenge na wengineo? Yaani ufisadi wote wa akina Chenge, Mramba, Lowassa, Karamagi bado tu CCM haijaridhika kwamba kuna ushahidi wa kutosha dhidi yao!!!!? Kazi kweli kweli!!!

CCM yamjibu Dk. Kitine

na Edward Kinabo
Tanzania Daima~Sauti ya Watu​
SIKU moja baada ya Mkurugenzi mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa nchini, Dk. Hassy Kitine, kudai nchi inaendeshwa kienyeji na kukilalamikia Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuendelea kuwakumbatia wanachama wake wanaokabiliwa na kesi za ufisadi, chama hicho kimesema hakiwezi kuwavua nyadhifa hizo, kwa sababu kesi zao bado ni tuhuma tu.

Sambamba na hilo, CCM imesema kauli ya Dk. Kitine kwamba nchi inaendeshwa kienyeji ni maoni yake binafsi, kwani hayana ukweli.

Msimamo huo wa CCM ulitolewa jana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, John Chiligati, alipozungumza na Tanzania Daima, akijibu shutuma nzito zilizotolewa juzi na Dk. Kitine dhidi ya serikali.

"Sisi tunasema, yeye kama raia ana haki ya kutoa mawazo yake, na hiyo ndiyo demokrasia. Lakini si lazima kila anayetoa mawazo yake yawe sahihi. Mtu anaweza kujiuzulu nafasi yake kupisha uchunguzi ufanyike, hiyo haimaanishi kwamba hilo jambo amelifanya kweli.

"Uchunguzi unapofanyika kuna mambo mawili yanaweza kutokea, la kwanza huyo mtu anaweza kubainika alifanya hicho kitu na la pili anaweza kuonekana hana hatia.

"Hatuwezi kuwavua watu uanachama au nyadhifa zao ndani ya chama kwa sababu hiyo tu. Yeye aliyesema hivyo atutajie ni kiongozi gani wa serikali ambaye pia ni kiongozi wa chama, ameshathibitika kuwa hana maadili halafu kama chama tumeendelea kumwacha. Atuambie…..hakuna," alisema Chiligati.

Alipoulizwa kwanini CCM isiwafukuze uanachama na kuwavua nyadhifa zao za kichama na ubunge, baadhi ya viongozi wake, ambao tayari serikali ya chama hicho ilisharidhika kwamba walikiuka maadili ya uongozi kwa kutumia vibaya madaraka yao, hata ikaamua kuwafungulia kesi, alisema: "Hatuwezi kuwachukulia hatua kwa sababu kesi zao bado ni tuhuma tu. Wakithibitika kama kweli walifanya hivyo, hatutawaacha," alisema Chiligati.

Chiligati alipinga madai ya nchi kuongozwa kienyeji na kusisitiza kuwa kauli ya Dk. Kitine, haina ukweli wowote.

Alisema nchi inaongozwa vizuri kwa kufuata utawala wa sheria na mihimili yote ya dola, ikiwemo utawala, Bunge na Mahakama, inafanya kazi zake vizuri.

Alibainisha kuwa kielelezo kuwa nchi haiongozwi kienyeji, ni amani na utulivu vilivyopo nchini, kwani kama nchi ingekuwa inaongozwa kienyeji kusingekalika.

"Kwa mfano, hilo alilosema nchi inaongozwa kienyeji, maana yake nini? Nchi kuongozwa kienyeji maana yake hakuna mfumo wa utawala kabisa, hakuna utawala wa sheria. Mahakama hazipo wala Bunge halipo…serikali haipo.

"Kungekuwa na hali hiyo, ingekuwa sawa na kusema nchi inaongozwa kienyeji. Lakini sisi hatujafikia hatua hiyo. Bunge lipo, Mahakama ipo, Serikali ipo. Utawala wa sheria. Nchi haiongozwi kienyeji, ndiyo maana kuna amani na utulivu," alisema Chiligati.


Mbali ya CCM kutoa kauli hiyo, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), aliunga mkono kauli ya Dk. Kitine.

"Mzee Kitine ameongea jambo ambalo ninaliongea kila siku kwamba, kuna tatizo kubwa serikalini. Tuhuma za ufisadi zimeshamiri sana, watendaji hawachukui maamuzi, wanasiasa wenye nyadhifa serikalini wamejaza nafasi na hawako tayari kuwajibika. Tunahitaji muafaka wa kitaifa kwenye mambo mengi," alisema Zitto.

Alisema ili mambo yaende vizuri, Tanzania inahitaji kelele za wazee wastaafu kama Dk. Kitine, wasimamie kunena na kushauri na hata kukemea na wananchi wawapigie kura wabunge wengi wa upinzani ili Bunge liwe na meno.


Juzi, Dk. Kitine alisema taifa linakabiliwa na tatizo la uongozi, ambalo halijawahi kutokea katika historia ya nchi.

Kada huyo wa siku nyingi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), aliyewahi kuwa mbunge wa Makete, mkoani Iringa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, chini ya uongozi wa Rais mstaafu Benjamin Mkapa, alisema nchi imekuwa ikiendeshwa kienyeji, kwa sababu ya kuporomoka kwa maadili ya uongozi.

"Hali tuliyofikia si nzuri, tena niseme ni mbaya sana. Kuna kuporomoka kwa kiasi kikubwa kwa maadili ya uongozi. Na hii nawaambia, nchi haijawahi kuwa katika hali mbaya huko nyuma kama ilivyo sasa. Kwa hali tuliyofikia ni ngumu kurekebisha maadili ya uongozi.

"Tatizo kubwa ni viongozi kukosa integrity (uadilifu). Kwanza ni integrity ya viongozi wenyewe, pili ni commitment (wito), tatu ni nationalism (utaifa). Haya ndiyo yalikuwepo wakati wa Mwalimu," alisema Dk. Kitine.

Alisema baadhi viongozi wa serikali wamepoteza sifa kuu tatu za uongozi ambazo ni kuwa na uadilifu, wito na kuweka mbele utaifa, sifa ambazo alisema ndizo zilikuwa nguzo ya uongozi wakati wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, chini ya Baba wa Taifa, hayati, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Alisema uteuzi mbaya wa viongozi hususan uteuzi wa mawaziri, umechangia kupatikana kwa viongozi wasio waadilifu, wengi wao wakijihusisha na vitendo vya rushwa.
 
Back
Top Bottom