Mtanzania2020
JF-Expert Member
- May 23, 2020
- 370
- 764
Serikali ya Uganda imewashauri wanaume kuacha kufanya vipimo vya vinasaba (DNA) kubaini ukweli wa uzazi, ikisema kuwa haina manufaa kwa ustawi wa nchi hiyo.
Waziri wa Afya Msingi wa nchi hiyo, Margaret Muhanga, anasema haijalishi kama wanaume wanaolea watoto ni baba zao kwa damu au la, na vipimo vya uraia vinathibitisha tu kuleta machafuko.
Uganda imekuwa ikiripoti visa vya vurugu katika familia kutokana na matokeo ya vipimo vya DNA vya uraia, baadhi yake vikisababisha vifo.
Hivi majuzi tu, mwanamume raia wa Israeli anadaiwa kumuua mkewe Mganda na kuzika mabaki yake katika tangi la maji taka baada ya matokeo ya sampuli ya DNA ya mtoto wao wa miezi 6 kuwa hasi.
East Africa TV