Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,918
- 30,259
- Thread starter
- #341
Ndugu yangu,
Hapa ndipo mnapokosea.Binafsi naamini kwa mfano harakati za uhuru wa nchi kama Tanganyika iliyokuwa Trusteeship ya UN chini ya Waingereza ulikuwa tofauti na Kenya ambapo "waliopigana kikwelikweli" dhidi ya Ukoloni wa Waingereza na kujipatia uhuru kwa kumwaga damu.Sina maana ya kubeza "harakati za Uhuru" wa Tanganyika lakini nataka kusema kuwa kuendelea kulilia credit kuhusu nani " alileta uhuru' kunanifanya nicheke kidogo. Besides, kipindi kile wimbi la kuyaachia makoloni unproductive lilikuwa linafagia kila mahali! Wawepo waislam au wapagani bado Uhuru ungekuja tu! Hivi tu tunataka kutoana roho kuhusu " nani alileta uhuru, ingekuwaje kama watu kweli wangeingia kwenye mapambano? Na ndio maana kwangu mimi na baadhi ya wengine hapa, tumeuliza mara nyingi - je katika " real" mapambano kama yale yaliyofanywa dhidi ya Wajerumani (na wajerumani wakaenda kuleta Mamluki wa kiislam akina Sykes kama Mwandishi wa hiki kitabu alivyoandika) je mchango wa wapagani, wakristo na hata waislam ulikuwaje?
Samahani kama nitasomeka ndivyo sivyo.
Kuhusu Ukatoliki wa Nyerere na kuhusishwa kwa Kanisa katika lawama na shutuma nzito hizi, hamuoni mnakosea? Ni kama kuhusisha vitendo vya mtu mmoja muislam na Uislam ( assuming kweli mtu huyo alitumia dini/imani yake kufanya dhuluma au uonevu)!
Hiki ni kitabu tu nimeandika kuhusu historia ya wazee wangu.
Soma chukua kile unachoona kinakufaa kile unachoona hakina maana kiache.