Kitabu Kinachofichua utapeli katika baadhi ya Makanisa

Kitabu Kinachofichua utapeli katika baadhi ya Makanisa

Na wewe niwalewale tu unatafuta ulaji, unatafuta kupitia migongo ya wenzako

Pole ndugu maana umesema usichokijua! watunzi wa vitabu, watunzi wa nyimbo, na kila aina ya biashara Duniani unayoijua na usiyoijua lazima ipitie katika migongo ya watu, yaani No seller no buyer and virse versa! Hata Biblia na Quran zote zinauzwa! Kitu gani ambacho wewe unacho hukukinunua?
 
Lakini hiyo cover mkuu haijatulia sana, tafuta mtu akufanyie design nzuri ya cover!
Unaweza kudesign picha ya mchungaji aliyevalia suti za gharama, kanisa amelipamba kwa dhahabu, bodyguards wenye vitambi, huku akihubiria watu wenye njaa vibaya mno, wamevaa ovyoovyo wako peku, wengine wamejipanga kwenye foleni wakikung'uta mifuko yao kutoa sadaka! Itapendeza sana mkuu!

Good idea
 
bora umemwambia maana naona anataka kuwa kichaa huyo

ladyfurahia, niambie Bwana YESU alikuwa kichaa kwa kuwasema peupee mafarisayo na waandishi (wayahudi) kwa kukosoa matendo ya imani yao?! Nipe andiko moja tu katika Biblia ambalo lina-support watu kutoa pesa ili wafanyiwe maombi! Mimi kusema ukweli niwe kichaa! Haa haaa that is a daylight dream!
 
Kitabu hakitaji majina ya wachungaji bali kinaeleza yanayofanywa na wachungaji katika kuwakamua watu pesa zao na jinsi wayafanyayo katika ukamuaji huo yanavyokinzana na Maandiko Matakatifu. Kwa kukisoma tu mtu ataweza ku-point mwenyewe kwamba fulani ni mchungaji anayetekeleza wito wa Mungu na fulani ni mjanja mchumia tumbo! Atakayekubali ukweli heri yake atakayekataa ukweli shauri yake!
 
mkuu swala la imani achana nalo mkuu, huko ni habari nyingine, hutakua na uhakika 100% ya utakacho andika zaidi ya speculations tu ambazo tumeshazizoea na uhakika kua katika hayo makanisa Mungu hayupo hutakua nao andika tu kama unataka kuandika utimize lengo..ila maswala ya imani ni hatari
 
Kitabu hakitaji majina ya wachungaji bali kinaeleza yanayofanywa na wachungaji katika kuwakamua watu pesa zao na jinsi wayafanyayo katika ukamuaji huo yanavyokinzana na Maandiko Matakatifu. Kwa kukisoma tu mtu ataweza ku-point mwenyewe kwamba fulani ni mchungaji anayetekeleza wito wa Mungu na fulani ni mjanja mchumia tumbo! Atakayekubali ukweli heri yake atakayekataa ukweli shauri yake!
ili kubalance na kitabu chako utupe yanayojiri na misikitini pia, mimi binafsi nishakutana na sheikh tapeli unasemaje kuhusu hilo, does one case generalize all of them??
 
Hilo kwenye cover ni kasri la Mama Lwakatare nini?

Maana huyu katika hicho kitabu anatakiwa kuwa na chapter yake peke yake kuelezea alivyojipenyeza kwenye siasa, academia na dini.

Wewe ni miongoni mwa watu wenye mawazo ya kimaskini. Watanzania ndiyo maana tunachechemea kwenye maendeleo kwa kuwa na fikra kuwa kila aliyefanikiwa ni ujanja ujanja.
Fanyeni kazi mtafute pesa acha porojo. Pia huyu mwandishi ni mjasiriamali tu anatafuta pesa, kwa maana nyingine ni mganga njaa.
 
Kitabu hakitaji majina ya wachungaji bali kinaeleza yanayofanywa na wachungaji katika kuwakamua watu pesa zao na jinsi wayafanyayo katika ukamuaji huo yanavyokinzana na Maandiko Matakatifu. Kwa kukisoma tu mtu ataweza ku-point mwenyewe kwamba fulani ni mchungaji anayetekeleza wito wa Mungu na fulani ni mjanja mchumia tumbo! Atakayekubali ukweli heri yake atakayekataa ukweli shauri yake!

Wewe hiyo sifa huna.
 
mkuu hapa unataka kuongelea nini hasa maana kuna mambo mawili yananizonga kidogo. Mambo ya imani ni magumu kidogo kwangu pengine hata kwa wengi wetu.

Kama mtu anatoa sadaka kwa hiari yake mwenyewe hata kama ameshawishiwa lakini si anatoa kutokana na uwezo wake au alivyojaliwa na mungu wake. Na kwa mfano mtu ameombewa na amepona kwa hiyari yake akaamua kumtolea mungu wake sadaka kuna tatizo hapo?

Tuseme sasa tatizo lipo hapo jinsi hiyo sadaka inavyotumika je ni kwa mapenzi ya mungu au laa, ni kwa ajili ya matumbo yao.

Na je hapo kwenye kitabu chako unataka kuhumu au.....!!

Au utaongelaea pia mahubiri na miujiza inayofanywa na wahubiri hao na pengine ni ya kutengeneza ili wapate waumini wangi na kuongeza sadaka yao.
 
mkuu hapa unataka kuongelea nini hasa maana kuna mambo mawili yananizonga kidogo. Mambo ya imani ni magumu kidogo kwangu pengine hata kwa wengi wetu.

Kama mtu anatoa sadaka kwa hiari yake mwenyewe hata kama ameshawishiwa lakini si anatoa kutokana na uwezo wake au alivyojaliwa na mungu wake. Na kwa mfano mtu ameombewa na amepona kwa hiyari yake akaamua kumtolea mungu wake sadaka kuna tatizo hapo?

Tuseme sasa tatizo lipo hapo jinsi hiyo sadaka inavyotumika je ni kwa mapenzi ya mungu au laa, ni kwa ajili ya matumbo yao.

Na je hapo kwenye kitabu chako unataka kuhumu au.....!!

Au utaongelaea pia mahubiri na miujiza inayofanywa na wahubiri hao na pengine ni ya kutengeneza ili wapate waumini wangi na kuongeza sadaka yao.

Ni kweli mtu anatoa sadaka kwa hiyari yake! Kitabu changu hakiwashawishi watu wasitoe sadaka wala zaka! Bali kinawashawishi watu kufanya hivyo kwa watumishi wa kweli wa Mungu maana huko ndiko kuna thawabu na baraka za Mungu. Ingawaje hata kwenye masuala ya zaka pia kuna tatizo kubwa ila huko sigusii hata!
Kitabu kinaeleza njia ambazo sio sahihi ambazo zinakinzana na Maandiko ambazo wanazitumia hao wanaojiita watumishi wa Mungu kuwashawishi watu kutoa pesa kumbe sio bali watumishi wa Matumbo yao.
 
Hata baadhi ya wana_JF mkinipiga madongo kitabu kitatoka tu ukifika wakati wa Mungu. Yeye ndiye Mhukumu wa wote wenye mwili. Bwana Yesu alipendwa na watu wangapi wakati akiisema KWELI? wengi walimtukana na kumbeza lakini kamwe hakusitisha kusudi lake chini ya jua! Alilolipanga Mungu hakuna awezaye kulipangua!
Nawashukuru sana woteee manaotoa mawazo yenu, iwe ni kwa kuniunga mkono au kunipinga!
Kumbukeni nimesema sintomtaja mchungaji au mtumishi yeyote katika kitabu changu. Mimi siye Mhukumu wa wanadamu maana nami nitahukumiwa nisipotenda vema katika kuishi kwangu. Yaliyoandikwa katika kitabu yatamfanya msomaji ahukumu mwenyewe nani ni mtumishi wa kweli na nani sio! Mtume Paulo alisema 'hukumuni wenyewe', nami nasema 'mtahukumu wenyewe'!
Nawapenda wooote na kuwaombea baraka tele! Mungu awabariki sana!
 
Wewe wasema!!
ladyfurahia, niambie bwana yesu alikuwa kichaa kwa kuwasema peupee mafarisayo na waandishi (wayahudi) kwa kukosoa matendo ya imani yao?! Nipe andiko moja tu katika biblia ambalo lina-support watu kutoa pesa ili wafanyiwe maombi! Mimi kusema ukweli niwe kichaa! Haa haaa that is a daylight dream!
 
Makopo kwa kusema ukweli?! Haaa...that is a big joke! Mungu si Mungu wa ku-side na waovu na hakuna laana kwa kusema ukweli!
Ukweli upi? suala ni jeee yeye ni msafiii? ukihukumu utahukumiwa. Watu walimtuhumu mwanamke kwa uzinzi na kumleta mbele za Yesu awape hukumu ya kumpiga kwa mawe mpaka afe na yeye akawaambia asiye na dhambi aanze kurusha jiwe; kilichoendelea pale unakijua? je yesu alikuwa anatetea uzinzi? na je uzinzi si zaidi ya kutafuna sadaka?
 
Ni kweli mtu anatoa sadaka kwa hiyari yake! Kitabu changu hakiwashawishi watu wasitoe sadaka wala zaka! Bali kinawashawishi watu kufanya hivyo kwa watumishi wa kweli wa Mungu maana huko ndiko kuna thawabu na baraka za Mungu. Ingawaje hata kwenye masuala ya zaka pia kuna tatizo kubwa ila huko sigusii hata!
Kitabu kinaeleza njia ambazo sio sahihi ambazo zinakinzana na Maandiko ambazo wanazitumia hao wanaojiita watumishi wa Mungu kuwashawishi watu kutoa pesa kumbe sio bali watumishi wa Matumbo yao.

Hapa kidogo nataka kukuelea ila utawatambuaje hao watumishi wa kweli na wasio wa kweli.

Maana hata Biblia inasema ''Wengi watakuja kwa jina langu, watatoa pepo na kuponya wagonjwa''

Utufahamishe kwa uzuri kabisa wewe uliyefunuliwa hii neema ya kuwatambua hawa??
 
Back
Top Bottom