cold water
Senior Member
- Oct 6, 2021
- 175
- 618
Jamani, jamani, ofisi zimetulia, majengo ni mazuri yanapendeza na kuvutia, na watu wake wanapendeza ukiwaangalia kwa nje lakini?! Lets go to the point,
Mwezi fulani hapa kati kati katika kutafuta sehemu za kujitolea nikaenda ofisi moja hivi sehemu fulani, jamani nilikutana na kaka mmoja alinipokea vizuri tu, nikampa barua yangu na CV zangu lakini alionesha kutokuridhika na nilichokiandika, ilibidi afanye kazi upya kuanzia kuandika barua hadi CV.
Tukiwa pale ofisini huku ananifanyia ile kazi huku ananilazimisha niende nyumbani kwake, na kunilazimisha kupima HIV ili niweze kumpa mzigo! Nikamkatalia, nikamwambia kaka kama hautaki kunisaidia basi naomba barua zangu niondoke watanisaidia wengine!
Akaniambia nina mda mrefu sijafanya mapenzi, mke wangu yuko mbali naomba nipunguze kidogo zimejaa! Nikamwambia mimi sihitaji, naomba barua zangu. Akaniambia kwahiyo wewe unataka mimi nikusaidie lakini wewe kunisaidia mmi hutaki?
Nikamwambia nitafanya huu mchezo kwa watu wangapi katika maofisi wakati mimi bado naendelea kutafuta kazi? Hivi ninavyowaambia barua niliziacha na sijapata hiyo nafasi ya kujitolea hadi leo.
Ofisini kwake nilienda karibu mara tatu akidai vitu havijakamilika na siku hizo zote alinidai ngono. Nilikosa furaha kila nilipokuwa nikirudi nyumbani. Basi nilivyoona miezi inakatika nikaenda sehemu nyingine, nako nilisaidiwa na kupewa hela juu, lakini nikaendelea kuombwa ngono kama kawaida.
Mtu ananiambia njoo nyumbani nifulie nguo, mara kuna kitu inabidi unitimizie, nikakataa pia. Nikaenda tena ofisi nyingine hivyo hivyo, oh dada naomba unipe nafasi, nimekuelewa sana, nakupenda, hii barua yako leo hii hii napeleka sehemu husika. Nikaipotezea tena hiyo sehemu hadi leo sijafatilia.
Nikaenda tena sehemu nyingine huyo sasa alikuwa Meneja, akaniambia njoo uripoti lakini naomba uwe na mimi, nitakufungulia na biashara pia! Ikabidi nimwambie basi nimegairi nitatafuta sehemu nyingine.
Siwachafui watu jamani huu mwaka nimepitia mikasa tu. Nimekata hadi tamaa ya kuomba kujitolea, hapo tu kujitolea vipi nikiwaambia waniajiri? Yani nimechoka kuzunguka. Namba za hawa watu zote nimezifuta, yaani ni kuniomba ngono tu hamna msaada wowote.
Nasemaje, ofisini kuna mambo! Ilishanitokea hadi kipindi cha field wababa wanaomba sana ngono maofisini, acha kabisa.
Mwezi fulani hapa kati kati katika kutafuta sehemu za kujitolea nikaenda ofisi moja hivi sehemu fulani, jamani nilikutana na kaka mmoja alinipokea vizuri tu, nikampa barua yangu na CV zangu lakini alionesha kutokuridhika na nilichokiandika, ilibidi afanye kazi upya kuanzia kuandika barua hadi CV.
Tukiwa pale ofisini huku ananifanyia ile kazi huku ananilazimisha niende nyumbani kwake, na kunilazimisha kupima HIV ili niweze kumpa mzigo! Nikamkatalia, nikamwambia kaka kama hautaki kunisaidia basi naomba barua zangu niondoke watanisaidia wengine!
Akaniambia nina mda mrefu sijafanya mapenzi, mke wangu yuko mbali naomba nipunguze kidogo zimejaa! Nikamwambia mimi sihitaji, naomba barua zangu. Akaniambia kwahiyo wewe unataka mimi nikusaidie lakini wewe kunisaidia mmi hutaki?
Nikamwambia nitafanya huu mchezo kwa watu wangapi katika maofisi wakati mimi bado naendelea kutafuta kazi? Hivi ninavyowaambia barua niliziacha na sijapata hiyo nafasi ya kujitolea hadi leo.
Ofisini kwake nilienda karibu mara tatu akidai vitu havijakamilika na siku hizo zote alinidai ngono. Nilikosa furaha kila nilipokuwa nikirudi nyumbani. Basi nilivyoona miezi inakatika nikaenda sehemu nyingine, nako nilisaidiwa na kupewa hela juu, lakini nikaendelea kuombwa ngono kama kawaida.
Mtu ananiambia njoo nyumbani nifulie nguo, mara kuna kitu inabidi unitimizie, nikakataa pia. Nikaenda tena ofisi nyingine hivyo hivyo, oh dada naomba unipe nafasi, nimekuelewa sana, nakupenda, hii barua yako leo hii hii napeleka sehemu husika. Nikaipotezea tena hiyo sehemu hadi leo sijafatilia.
Nikaenda tena sehemu nyingine huyo sasa alikuwa Meneja, akaniambia njoo uripoti lakini naomba uwe na mimi, nitakufungulia na biashara pia! Ikabidi nimwambie basi nimegairi nitatafuta sehemu nyingine.
Siwachafui watu jamani huu mwaka nimepitia mikasa tu. Nimekata hadi tamaa ya kuomba kujitolea, hapo tu kujitolea vipi nikiwaambia waniajiri? Yani nimechoka kuzunguka. Namba za hawa watu zote nimezifuta, yaani ni kuniomba ngono tu hamna msaada wowote.
Nasemaje, ofisini kuna mambo! Ilishanitokea hadi kipindi cha field wababa wanaomba sana ngono maofisini, acha kabisa.