Kwa uislam huyo mtoto alozaliwa kwa mchepuko si wa mwanaume.
Kama atamhudumia basi anatoa msaada wa kibinadam tu.
Hivyo MKE wa ndoa hana wajibu wa kumtunza huyo mtoto kwa namna yeyote ile kwa sababu sheria za kidini zinamlinda.
Pili mama mkwe anazidi kushadadia UZINZI wa kijana wake,nae hesabu zake ziko palepale,mtoto amezini hadi amezaa na yeye anajichetua,nae kama ameamua kumlea "Mjukuu" basi ni kwa utashi tu wa kumsaidia binadam mwenzie sio mtoto wa mwanae,
Mjukuu wake halali ni yuleee alozaliwa ndani ya ndoa.
Ndugu nao wanacheza ngoma sawa na mama mkwe nao ni wa kupuuzwa.
Kuhusu maradhi,uislam umeruhusu kama mke anaumwa hasa maradhi yasiyoponyeka basi MUME anaruhusiwa kuoa mke wa pili,lakini si KUCHEPUKA.
Isipokuwa ulimwengu leo umechukulia kawaida ndo maana hata hili la jamaa linaonekana la kawaida sana.
Kupitia kisa hiki ndo maana waislam walipaswa kuwa na KADHI,haya masuala ni ya kisheria zaidi ambayo mahakama za kisekula haziwezi kuyatatua.
Tanbihi:Nimeongelea hili kama ni ndoa ya KIISLAM.
Wassalam