Wakuu,
hili suala la uthibitisho wa uwepo wa mungu ni suala dogo sana, halihitaji kuchukua hata dakika 3 kulithibitisha. Tatizo sio kukosekana kwa uthibitisho wa mungu, ila tatizo ni njia tunazo tumia kutafuta huo uthibitisho. Kuna njia nyingi sana za kupata uthibitisho, na chaguo la hizo njia linategemea na Subject matter to be proven. Miongon mwa hizo njia ni Logical proof, mathematical proof,empirical proof, histoeical-logical proof, axiomatical proof na zinginezo.
Sasa subject yetu hapa ni kuhusu Mungu, na tatzo linakuja pale ambapo tunachagua logic ama empirical proof kutafuta uthibitisho bila ya kujua kwamba kwa kufanya hivyo tumekiuka taratibu za kiudadisi kwa sababu tumechagua njia zisizoendana na subject yetu na hivyo si ajabu tukakosa kupata uthibitisho ulio sahihi.
Kuna watu ( hasa
Kiranga ) wanaamin kuwa logical, empirical & mathematical proof ndio njia sahihi na bora Zaidi kuliko zingine, na kutokana na iman hiyo potofu wanaamini kuwa uthibitisho wowote usiotokana na logical, etc basi ushahidi huo unakuwa batili.
Huu mjadala hauwezi kuisha na uthibitisho hautaweza kupatikana kwasababu ya njia mlizo chagua, mmeiacha axiomaticcal proof ambayo ndio njia bora kabisa kwa hii dhana tunayojadili.
Na hata hivyo napenda kuwaambia kuwa "kukosekana kwa uthibitisho wa dhana haimanishi kuwa eti hiyo dhana haipo"
"silence isn't a proof of absence "
Kunavitu vingi binadamu hatuvifahamu, lakini Hatuwez kusema kwamba hivyo vitu havipo.
Kama umeshindwa kupata uthibitisho wa dhana flan, basi usihitimishe kwamba hicho kitu hakipo, inachotakiwa ni wewe kuangalia mapungufu yako katika njia ulizotumia kudadisi dhana husika.
Kama
Kiranga na wenzako hamjapata uthibitisho wa Mungu, msihitimishe kuwa Mungu hayupo.