Ndugu naomba nikujibu hivi:
"Mungu", hili ni jina linalojaribu kuelezea, hapa niite nguvu iliyofanya ulimwengu, binadamu na vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana. Jina hili " Mungu" lina maana hasa ya kuelezea uwezo wa mwisho wa binadamu kwenye kutambua hii nguvu kuu.
Ukweli hapa, ni 'hii nguvu' iliyofanya hivi vitu, ulimwengu, binadamu na viumbe vingine kwa jinsi hiyo ya ajabu: kamilifu, pangilifu na nyoofu.
Dini, hatahivyo, tangu mwanzo imekuwa na inaendelea kusema juu ya NGUVU HII 'MUNGU'. Yesu Kristo ni mfano bora zaidi kuliko mwanadamu mwingine yoyote (sublime moral) duniani aliyekuja kuifunua hii nguvu. Ingawa siyo kwa ukamilifu wote.