Kiranga sio atheist ni non-believer

Kiranga sio atheist ni non-believer

Mungu akijua kesho utaua, unaweza kuepuka kuua kesho?
Mungu anajua kila kitu. Anajua leo unafanya hili, kesho hili. Anajua mawazo yako yote. Ni mjuzi wa mambo yote.
Mungu kwa mapenzi yake anaweza kukuepusha usiuwe kesho, kwa mapenzi hayo hayo anakuacha uuwe kesho.
 
Mungu anajua kila kitu. Anajua leo unafanya hili, kesho hili. Anajua mawazo yako yote. Ni mjuzi wa mambo yote.
Mungu kwa mapenzi yake anaweza kukuepusha usiuwe kesho, kwa mapenzi hayo hayo anakuacha uuwe kesho.
Hujajibu swali nililokuuliza.

Mungu akijua kesho utaua, unaweza kuepuka kuua kesho?
 
Nimeshakujibu tayari hapo juu.
"Mungu akijua kesho utaua...", nimekunukuu ili nikwambie kwamba, "Mungu akijua", siyo sifa ya Mungu.
"Mungu anajua" hii ndio sifa ya Mungu daima.
"Akijua", hii ni sifa ya viumbe.
Haya, sasa kama Mungu anajua kesho utaua, wewe unaweza kuepuka kuua?

Usiniambie Mungu atakuepusha, nauliza wewe, unaweza kuepuka kuua?
 
Haya, sasa kama Mungu anajua kesho utaua, wewe unaweza kuepuka kuua?

Usiniambie Mungu atakuepusha, nauliza wewe, unaweza kuepuka kuua?
Kabla ya kujibu swali lako, utaona kuna swali lingine muhimu sana kuliko hata swali ulilo uliza: kwanini unaua?
Kujibu swali lako: ndio ninaweza kuepuka kuua. Mtu anaweza kuepuka kuua.
 
Kabla ya kujibu swali lako, utaona kuna swali lingine muhimu sana kuliko hata swali ulilo uliza: kwanini unaua?
Kujibu swali lako: ndio ninaweza kuepuka kuua. Mtu anaweza kuepuka kuua.
Mungu akijua kwamba Nundu ataua kesho.

Halafu Nundu akaepuka kuua.

Hapo huoni kwamba Mungu atakuwa amekosea kujua atakachofanya Nundu kesho, na hivyo habari ya kwamba "ujuzi wa Mungu hauna makosa" itakuwa imeingia mawaa, kasoro na shaka?
 
Mungu akijua kwamba Nundu ataua kesho.
Mungu "akijua", Mungu hana hii sifa. 'Akijua', maana yake hakuwa anajua kabla. Hii haiwezi, kwa vyovyote kuwa sifa ya Mungu.
Sifa ya Mungu, ni 'ANAJUA'. Hii ndio sifa ya Mungu. Ndio hali Yake, ndivyo alivyo.
 
Hapo huoni kwamba Mungu atakuwa amekosea kujua atakachofanya Nundu kesho, na hivyo habari ya kwamba "ujuzi wa Mungu hauna makosa" itakuwa imeingia mawaa, kasoro na shaka?
"Mungu akijua". Hii ingekuwa ndio sifa ya Mungu, vitu hivi tunavyoviona visingekuwa na mfumo au mpangilio (system or structure) huo vilivyonao.
 
Kwa jibu langu hapo juu, utaona Mungu alimuumba mwanadamu akampatia akili na utashi. Kwa vitu hivi, Mungu anataka mwanadamu awe huru kujua mema na mabaya. Amtafute Yeye. Ingawa Mungu haachi kila wakati kumwita au kumvuta kwake mwanadamu.
Hujajibu swali.

Ikiwa, kwa mujibu wa imani yako, Mungu anajua yote, na ujuzi wake hauna makosa, kwa hivyo hawezi kujua kitu kitakuwa, halafu kisiwe.

Halafu akajua Nundu ataua.

Halafu Nundu asiue.

Hapo ule ujuzi wa kwanza wa Mungu kwamba Nundu ataua utakuwa una makosa?

Kama utakuwa una makosa, Mungu anakosea?

Na kama, Mungu akijua Nundu ataua, ni lazima Nundu aue, hata Nundu akijitahidi vipi asiue, je, hapo Nundu ana uhuru wa kuamua asiue?
 
Naomba nikuulize swali. Thibitisha Kiranga yupo. Na thibitisha Kiranga haukuumbwa.
Kwanza hilo si swali.

Pili, kwa nini nithibitishe Kiranga yupo? Kiranga ni nani? Mimi siitwi Kiranga, hilo ni jina la JF tu. Sasa unaponiambia nithibitishe Kiranga yupo, unaniambia nithibitishe nani yupo?

Nikisema siwezi kuthibitisha Kiranga yupo, kwa sababu simjui, sijawahi kumuona, siwezi kuthibitisha yupo, kwa sababu Kiranga ni character wa kutungwa tu, hilo linathibitisha Mungu yupo?
 
Huu uzi bwana, unaweza jikuta umesoma page zote 190, ila hujaona mahali pa kuingilia ili nawe uchangie. Hongereni kwa machangiaji kwa hoja zenu, kuna mengi wasomaji tunajifunza kupitia kwenu.
 
Ikiwa, kwa mujibu wa imani yako, Mungu anajua yote, na ujuzi wake hauna makosa, kwa hivyo hawezi kujua kitu kitakuwa, halafu kisiwe.

Halafu akajua Nundu ataua.

Halafu Nundu asiue.
Ukisoma maelezo ya aya yako ya kwanza utagundua, aya hiyo ina jibu la maswali yako yote. Hivyo sina sababu ya kuendelea kukujibu.
Hatahivyo, fahamu kwamba, "Mungu anajua". Hii ndio sifa ya Mungu. Ndio hali Yake, ndivyo alivyo.
 
Kwanza hilo si swali.

Pili, kwa nini nithibitishe Kiranga yupo? Kiranga ni nani? Mimi siitwi Kiranga, hilo ni jina la JF tu. Sasa unaponiambia nithibitishe Kiranga yupo, unaniambia nithibitishe nani yupo?

Nikisema siwezi kuthibitisha Kiranga yupo, kwa sababu simjui, sijawahi kumuona, siwezi kuthibitisha yupo, kwa sababu Kiranga ni character wa kutungwa tu, hilo linathibitisha
Vizuri.
Nimesoma maelezo yako, nimeng'amua shida yako ni "SIFA ZINAZOPEWA JINA MUNGU".
Kutoka kwenye hayo mang'amuzi, nina swali lifuatalo:
Ni nini unaelewa ukisikia au ukisoma jina Mungu?
Kando na hilo, unaelewa nini wewe kuitwa fulani? (Assume that your name is Kiranga or else).
Naomba unijibu, kisha tutarudi kwenye suala la msingi 'kuthibisha'.
 
Ukisoma maelezo ya aya yako ya kwanza utagundua, aya hiyo ina jibu la maswali yako yote. Hivyo sina sababu ya kuendelea kukujibu.
Hatahivyo, fahamu kwamba, "Mungu anajua". Hii ndio sifa ya Mungu. Ndio hali Yake, ndivyo alivyo.
Hujajibu swali. Huwezi kujibu swali.

Kwa sababu habari za kuwepo Mungu unayemsema zina contradictions.

Kwa sababu Mungu huyo ni wa kutungwa, wa uongo, hayupo.
 
Vizuri.
Nimesoma maelezo yako, nimeng'amua shida yako ni "SIFA ZINAZOPEWA JINA MUNGU".
Kutoka kwenye hayo mang'amuzi, nina swali lifuatalo:
Ni nini unaelewa ukisikia au ukisoma jina Mungu?
Kando na hilo, unaelewa nini wewe kuitwa fulani? (Assume that your name is Kiranga or else).
Naomba unijibu, kisha tutarudi kwenye suala la msingi 'kuthibisha'.
Nikisoma au nikisikia Mungu (mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, mfano, wa Biblia na Quran)naelewa ni jina la kitu cha kutungwa.

Sawasawa na kachero Willy Gamba aliyetungwa na Aristablus Elvis Musiba au James Bond aliyetungwa na Ian Fleming.

Ndiyo maana mpaka sasa hujaweza kuthibitisha Mungu yupo.

Na nimekuuliza swali dogo linaloonesha contradiction kati ya free will inayosemwa kuwepo kwa watu na perfect knowledge ya hiyo mnayemuita Mungu, umeshindwa kujibu.

Kwa sababu hiyo free will na hiyo Mungu vyote ni vitu vya kutungwa tu.
 
Hujajibu swali. Huwezi kujibu swali.

Kwa sababu habari za kuwepo Mungu unayemsema zina contradictions.

Kwa sababu Mungu huyo ni wa kutungwa, wa uongo, hayupo
Si kwamba sijakujibu. Nimekujibu.
Lakini, kwasababu hujaelewa "FREE WILL", ni nini, na inatoka wapi. Lazima useme sijajibu swali lako.
Jifunze kuhusu mwanadamu: mwanadamu maana yake ni nini, ametoka wapi, amefikaje hapa (ulimwenguni), na anaenda wapi.
Hatahivyo, ni vizuri kuelewa kwamba Mungu hana, na kwa vyovyote vile hatakuwa na contradictions.
Hicho ambacho kwako unaona na unaelewa ni contradictions za Mungu; siyo contradictions za Mungu, bali ni maneno ya binadamu yanayojaribu kumwelezea Mungu, ambae bado hajaeleweka waziwazi kwetu.
 
Back
Top Bottom