maxime
JF-Expert Member
- Jun 3, 2016
- 2,233
- 1,320
Hapo nilikuwa nakuonyesha kwamba binadamu kamfikiria Mungu kwa mfano wake yeye mwenyewe binadamu.....Hii kauli yako haivuki hata ncha ya ulimi,wanyama wanatii na wanajua uwepo wa Mola wao aliye waumba.
Sasa kusema "...ange..." au "....wange..." ni ususuavu wa moyo na ni ujinga ulipea. Buffalo hawezi kuwa hiyo kwani umbile na muda vimeshamtangulia,ni sawa sawa na useme ".....laiti kama unerudi utotoni ungefanya kadha wa kadha......" kufikiri kwa namna hii ni kufikiri kivivu na kitoto na kupoteza muda,yaani tunasema ni matumizi manaya ya akili,sababu haiwezekani. Au leo hii useme"....kama mimi ningekuwa mtume,ningefanya kadha wa kadha....",haiwezi kuwa sababu kalamu imeshanyanyuka na wino umekauka.
Tujifunze kufikiri kielimi,kikubwa na sahihi ili tuepukane na kukosea na kupoteza muda katika "hamna",muda rasilimali adhimu sana.
Nipo ...
Sent using Jamii Forums mobile app