Kipindi tunalegeza kamba ili kuvuta wawekezaji wa nje tuukumbuke wosia huu wa Hayati Baba wa Taifa

Victor Mlaki

JF-Expert Member
May 1, 2016
3,542
3,451
Tanzania tuna hazina kubwa sana ya wosia ambao umegusa karibu kila eneo ambalo leo hii tunaouona kama changamoto kwa Taifa.

Mimi ni muumini wa falsafa ya ujamaa wa Kiafrika na katika maisha yangu ninatembea na vitabu viwili vikubwa yaani Biblia na Ujamaa.

Kitabu cha "Ujamaa" cha mwaka 1968 kilichoandikwa na Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kuchapishwa na Dar es Salaam OXFORD UNIVERSITY PRESS.Ni kitabu cha pili cha maisha yangu Baada ya Biblia.

Kipindi tunataka kuwashawushi wawekezaji kurudi tukumbuke maneno haya

"..makampuni yanayotaka kuja katika Nchi yetu kuanzisha shughuli mbalimbali kwa manufaa yao wenyewe. Na sharti kubwa walitakalo jamaa hawa wenye fedha zao ni kwamba shughuli yenyewe iwe ni ya faida kwao na pia kwamba Serikali iwaruhusu kuondoa faida hiyo na kupeleka kwao. Huenda pia kwa jumla Serikali iwe na siasa wanayokubaliana nayo ambayo haihatarishi uchumi wao.

......Ni ujinga vilevile, kwa kweli ni ujinga zaidi, tukidhani kuwa tunaweza kuondoa hali hii ya unyonge wetu kwa kutegemea fedha kutoka nje badala ya fedha zetu wenyewe( uk, 21-22).


Itaendelea..
 
Heri umemnukuu mwalimu na si bwana yule.

Hata hivyo mama bado ana vipaumbele vingi.

Ngoja apate ushauri sahihi kuhusiana na Corona. Yanini kutukana mamba kabla ya kuvuka mto?
 
.." Nchi zenye dhiki ni nyingi sana Duniani. Na hata kama Nchi zote zenye neema zingekubali kuzisaidia Nchi zenye dhiki, bado ingekuwa msaada huo hautoshi" (uk , 22)
 
"Lakini Nchi zenye neema hazitakubali. Hata katika Nchi ileile matajiri huwa hawatoi fedha zao kwa hiari ili ziishaidie Serikali kuondia dhiki. Njia ya kuzipata fedha za matajiri ili zisaidie umma ni kuwatoza kodi nakupenda wasipende (uk,22).
 
Unawezaje kufanya fikra za mwanadamu ambaye sera zake zilishindwa kuwa kama biblia kwako?
Mkuu soma taratibu sijasema kitabu cha ujamaa ni kama Biblia,
Quote my words...ninatembea na vitabu vikubwa viwili yaani Biblia na Ujamaa.
Mwisho wa kujinukuu.
 
Uwekezaji ni suala la duniani pote.Muhimu ni kujifunza kwa wengine waliofanikiwa kwenye uwekezaji.Pili serikali ilishashindwa kuendesha biashara.Sekta binafsi ndio injini ya uchumi wowote duniani.Huwezi endelea kwa kuwa kisiwa ni lzm ushirikiane na wengine Ili usonge.
 
Ok....hakuna nilipoandika sera za mtu yeyote kuwa kama Biblia.
Ujamaa ubakie kwenye serikali kwenye ugawaji SAwa wa fursa na sio kwenye uendeshaji binafsi wa shughuli za uchumi.
Uchumi na makatazo ya sheria sheria haviendani
 
Nyerere alikaa miaka 23 na sera zake zilishindwa. Hatuwezi fuata ushauri ulioshindwa.
Unapimaje kuwa alishindwa? Na nini kupimo cha aliyeshinda?

Andika article kwa kirefu uchambue kushindwa kwake na kuhusu hao unaowajua walishinda.
 
mawazo ya Nyerere sio ya kufuata yote, kumbuka katika uongozi wa Nyerere ndio nchi ilipigika watu wakawa wanapanga foleni kuchukua pishi za mchele baada ya kutaifisha makampuni yote na kuyafanya ya serikali na serikali kupata hasara

kila nchi inahitaji wawekezaji, bila wawekezaji hata leo hii ungekuta tunajikongoja na TTCL yetu ambayo kama isingepata changamoto kutoka kwa makampuni ya nje ingejifia kabisa

Suala la faida za kiuchumi sio zero sum game, kuwa ili mmoja afaidike lazima mwingine apoteze, no manawza kupata faida kwa pande zote, so ni kuweka masharti ambayo ni reasonable yatakayofaidisha pande zote
 
mawazo ya Nyerere sio ya kufuata yote, kumbuka katika uongozi wa Nyerere ndio nchi ilipigika watu wakawa wanapanga foleni kuchukua pishi za mchele

awekezaji
Ujamaa wa Kiafrika ni mawazo ya jamii ya Kiafrika ni ya kufuata kwa karibu kabisa kwa sababu ndiyo asili yetu, demokrasia yetu, mfumo wetu wa uchumi.
 
Back
Top Bottom