Kipindi kigumu jimboni Kawe

Kipindi kigumu jimboni Kawe

Chanzo halisi cha Ugumu wa Kipindi:

Tumejadili mengi lakini tukumbushane pia kuwa Halmashauri ya Kinondoni inatengewa fedha na serikali kuu kwa ajili ya maendeleo. Lakini pia Halmashauri hiyo inakusanya ushuru ambao ni kwa ajili ya shughuli za maendeleo ya Kinondoni (Kawe ikiwemo). Halmashauri hiyo inaongozwa na meya wa CCM na ina madiwani wengi wa CCM.

Mwaka wa fedha uliopita, Halmashauri ya Kinondoni ilikuwa na TShs. billioni 80 kwa ajili ya matumizi ya kawaida na matumizi ya maendeleo. Mwezi July 2012 ilikuwa kifanyike kikao cha kujadili mapato na matumizi ya Halmashauri. Hata hivyo kikao kiliitishwa lakini hakukuwa na ajenda na kujadili mapato na matumizi badala yake kulikuwa na ajenda nyingine tu, ikiwemo ya uchaguzi wa Naibu Meya na wenyeviti wa kamati.

Madiwani wa Chadema na CUF walipinga uchaguzi huo kwa kuwa hizo kamati za zamani ndio zilisimamia matumizi, na ripoti yao ilifaa ijadiliwe kwanza kabla ya kuchagua kamati mpya. CCM kwa ubabe wao wa kawaida waliendelea na kumchagua
Songolo Mnyonge kuwa naibu Meya na wakachagua viongozi wapya wa kamati.

Mwananchi wa Kawe unayelalamika kuwa kuna kipindi kigumu, hivi hizi TShs. Billioni 80 zilizo mikononi mwa CCM na nyingine za miaka yote tangu uhuru hazihusiki na utatuzi wa kero zako?

Hivi unashindwa kuona kuwa kuna wanaozuia maendeleo yako pale Halmashauri?

Unashindwa kuona kwa kuwa hujui au ndio ushabiki wa kisiasa?
 
Kwa nini CDM ni wagumu kupokea ushauri mi sijaona kama kuna ubaya mdau alichoeleza kuhusu Mh.Mdee mi kwa upande wangu nafikiri ni njia bora pia ya kumkumbushu mh.mbunge wajibu wake japo si yeye anaweza akatoa labda hela kwa ajili kusaidia lakini hata kuzungumza tu na hao watu na kushirikiana kuibana Serikl iwasaidie hao ndugu na ukizingatia serkal yenyewe hi dhaifu bila mbunge shupavu na mwenye maono ya mbali jimbo litabaki hoi utafikiri jimbo anaongoza Lukuvi au Lusinde.
 
yaani unaonekana kila siku unabadili jimbo mara kwa mdee mara mnyika ww unaishi wapi mbona hueleweki,rita mlaki alifanya nn kipindi chake nipe mifano coz hata mm ni mkazi wa maeneo haya kwa vipindi vyote unavyovisema.
 
Wabunge unafikiri wana kazi nyingi sana ni wizi mtu tu, nadhani hii nchi inatakiwa iwe na wabunge wasiozidi 150 tu kila wilaya inakuwa jimbo na sio utaratibu wa sasa wilaya moja unakuta majimbo mawili. Hizo kazi wananchi ndio wanawapatia pia wabunge wengi wamekuwa wakiwaambia wananchi kwamba once wakichaguliwa watafanya hili, lile na hili. Lakini ukiangalia kwa makini utagundua kuwa kazi nyingi za wabunge wananchi wanazojua kwamba ni za mbunge sizo kwa sababu ifutayo kwanza serikali za mitaa (halmashauri ya manispaa) inaanzia ktk ngazi ya mtaa, kata mpaka ngazi ya wilaya na matatizo yote ya wananchi yanatakiwa yaratibiwe na viongozi wa ngazi ya mtaa kata mpaka wilayani kupitia baraza la madiwani (mbunge nae ni sehemu ya madiwani) wanapitia kuangalia namna ya kushughulikia hizo kero za wananchi kulingana na uwezo wa halmashauri husika. Inapotokea kuna baadhi ya matatizo au kero za wananch ambazo zipo nje ya uwezo wa halmashauri mbunge ndio anatakiwa akazipiganie kwenye bunge ili serikali kuu iweze kusaidia na ndio maana wakati wabunge wengine wakiuliza bungeni wanajibiwa simple tu hiyo ipo katika uwezo wa halmashauri (hapa ni madiwani including mbunge wahusika). Na ndio maana hata barabara wamezigawa, zipo zinazoshughulikiwa na halmashauri na zipo zinazoshughulikiwa na TANROAD ili kuweza kutofautisha majukumu. Lakini wabunge wetu kila mmoja anajifanya kuwa na majukumu kibao na kila kizuri kilichofanyika atasema yeye ameleta katika uongozi wake wakati uongozi ni taasisi kubwa na sijui madiwani na wenyeviti wa vijiji nao watasema nini (mgongano wa kimaslahi na ujiko usio wa maana). Hizo kazi alizoorodhesha si mbunge pekee labda hiyo namba 5 ambayo ina depend na external source lakini la kuitisha mkutano no 1 (kwanza hizo serikali za chini zinatakiwa ziitishe mkutano mara 4 kwa mwaka ili kubaini matatizo yao pamoja na kujadili maendeleo yao alafu wao ndio wanatakiwa wayawakilishe kwa mbunge wao ili aweze kuyatolea ufafanuzi na si mbunge kuja kusikiliza matatizo bila wao kwanza kukaa na kubainisha matatizo yao)

Mheshimiwa Jodoki Kalimilo,

Ni kweli kabisa kazi ya ubunge si ngumu sana kiasi cha kufanya tuwe na wabunge wengi kiasi hicho. Tungeweza kabisa kuwa na mbunge mmoja kwenye wilaya na akafanya kazi kwa ufanisi mkubwa. Kwa kushirikiana na madiwani wangeweza kabisa kujua yapi yanaishia kwenye baraza la madiwani na yapi yapelekwe bungeni... Lkaini kutoka na choyo na ulafi wa wanasiasa wameamua kwa makusudi kuibua nafasi kwa ajili ya wapambe wao ''wasio na kazi'' ili wapunguze njaa wasiwe na kelele wakati wao wanakula..
Kwa sababu tumewapa uwezo wa kutupangia mambo.....wao hutumia nafasi hiyo kujipendelea na kujipangia mapato makubwa......haiingii akilini katika nchi yenye uchumi kama wetu mmoja alipwe 315,000/= mwingine alipwe 13,000,000/= halafu useme kwamba unamuwakilisha..... pengo ni kubwa lililokithiri......hii si haki... Zipo wapi taasisi zinahusika na haki za binadamu?? hawalioni hili?? au wao hadi mtu ajeruhiwe au auwawe ndiyo waibuke?? hawajui chanzo chake?? au hili nalo linahitaji katiba mpya? Tutaokoa kiasi gani kama tukipunguza mapato ya wanasiasa (wabunge) kwa asilimia hata 75 na tukaiondoa mikopo ya magari ya anasa? Je fedha hii haitoshi kununulia vile vifaa vya kazi vinavyodaiwa na madaktari? Au hata kuwalipa walimu wanatufundishia watoto wetu (watoto wao hawasomi huku)?
Tufikie wakati wananchi tuseme hapana tumechoka kuwagharamia wanasiasa na hili linawezekana kupitia taasisi zisizo za kiserikali (NGO) zisizo na uhusiano na wanasiasa....
 
ujumbe mzito kwa halima na hii kitu kila wakati iko hapa.................. yaonekana jimbo linapwaya, au kampeni zimeanza
 
Ni afadhali na bora ww umesema, mie niliisha andika humu zaidi ya mara 10 ahadi na ulaghai wa HM kwa wananchi wa kawe, mpaka sasa hajafanya chochote, yeye ni kwenye kumbi za starehe tu ndio utamuona, halafu tukisema mnasema anaonewa. HM ni janga la sie wana kawe, nadhani katika katiba ijayo kuwe na kipengele cha mbunge akishindwa kazi basi , mtu mwingine atoke kwenye chama chake aje achukue hiyo nafasi. Mie sina shida eti kwa kuwa ametoka cdm , ila cdm next election wamlete mtu makini sio HM hawezi kitu


Watu ni wagumu sana kuelewa ndo maana mpaka twiga wanapakiwa kwenye ndege na kupelekwa Ughaibu bila hata kuelewa sijui nini kilichotupata sisi Wa-Tanzania unalalamikia Halima Mdee wakati wewe mwenyewe unaiona system nzima ya nchi ni DHAIFU hivi wewe ulitaka HM afanye yote unayoyasema wakati katika system ya nchi kuna uozo,hata kama angeitisha vikao elfu serikali ya CCM ilishaoza hakuna chochote utabaki kulaumu watu bure wakati wa kulaumiwa yupo,hata kama mtampa MALAKI huyo ndiyo atawamaliza maana ana hasira na jasho la wana-KAWE.
 
Wananchi wa jimbo la Kawe tupo katika kipindi kigumu cha kukosa mwakilishi aliye makini bungeni katika kipndi cha mwaka 2010 kuelekea 2015. Mbunge aliyeingia kwa mbwembwe nyingi Halima Mdee amekuwa ni zigo lisilosaidia wapiga kura badala yake anajisaidia mwenyewe.

Tangu amechaguliwa:
1. Hapendi kuitisha mikutano ili kupata mawazo ya wananchi
2. Wananchi wa Madale waliopatwa na mashambulizi ya polisi wamekosa pole na msaada wake
3. Wakazi wa Majipwande wanamlilia kwa kutopata msaada wa mali na faraja toka kwake
4. Mfuko wa Jimbo haujatolewa maelelezo kwa wananchi
5. Kushindwa kutekeleza ahadi zake za kuinua kiuchumi vikundi vya vijana na wanawake
6. Kushindwa kutatua matatizo wanayoyapata vijana wa bodaboda na bajaji

Hizo ni kero chache ambazo zilitakiwa zifanyiwe kazi na mbunge wetu.

Kwa kweli wakazi wa jimbo la Kawe tupo katika kipindi tete tunamkumbuka RITA Mlaki ambaye alikuwa karibu na wapiga kura.

Mafilili ni wadudu weupe wanaotambaa katika kinyesi cha binadamu aghalabu hupatikana kwenye shimo linalotumika kama choo.
 

Kwa kweli wakazi wa jimbo la Kawe tupo katika kipindi tete tunamkumbuka RITA Mlaki ambaye alikuwa karibu na wapiga kura.

Nimekuwa resident wa Kawe chini ya uwakillishi wa Adamjee (miaka 5), Mlaki (miaka 10) na Mdee (miaka 5). Mlaki was honyoest (hakuwahi hata kutaja neno 'Kawe' bungeni na ni kama alikuwa anawakilisha mtaa wake/siyo Jimbo)! Mdee yuko karibu na watu na anajitahidi kushughulikia mambo mengi tu (kama aliyokuwa Adamjee enzi zake).
 
Kawe waliingizwa Mkenge. Hakuna Mbunge wa Upinzani anayeweza kuleta maendeleo Dar-es-Salaam. Ni wakati mwafaka kujipanga kuwasafisha wabaki huko huko Kanda maalum
 
Itakuwa mnakaa nyumba moja unafurahia viroba vya unga na mchele anavyoleta nyumbani. Ila mtoa mada ameongea ukweli, maana Halima Mdee alikuwa mtu wa ahadi lukuki huku akilalama kuwa yeye ni maskini hivyo tumchangue awawakilishe wengi mana anajua machungu. Lakini tangu apite mtaa hadi mtaa kipindi cha kampeni hajaleta miguu hata kwa kata zake na kuanza utekelezaji wa ahadi.

Hv jaman mbona halima anapiga kazi na hata jana nimezungumza naye alikuwa kwenye shughuli za jimbo lake na alikuwa na mkutano tambueni kuwa hii kawe ni kubwa kuna sehemu zingine huyu mama anakwenda si lazima mjue wote kuwa leo yuko sehemu fulani,
 
Wananchi wa jimbo la Kawe tupo katika kipindi kigumu cha kukosa mwakilishi aliye makini bungeni katika kipndi cha mwaka 2010 kuelekea 2015. Mbunge aliyeingia kwa mbwembwe nyingi Halima Mdee amekuwa ni zigo lisilosaidia wapiga kura badala yake anajisaidia mwenyewe.

Tangu amechaguliwa:
1. Hapendi kuitisha mikutano ili kupata mawazo ya wananchi
2. Wananchi wa Madale waliopatwa na mashambulizi ya polisi wamekosa pole na msaada wake
3. Wakazi wa Majipwande wanamlilia kwa kutopata msaada wa mali na faraja toka kwake
4. Mfuko wa Jimbo haujatolewa maelelezo kwa wananchi
5. Kushindwa kutekeleza ahadi zake za kuinua kiuchumi vikundi vya vijana na wanawake
6. Kushindwa kutatua matatizo wanayoyapata vijana wa bodaboda na bajaji

Hizo ni kero chache ambazo zilitakiwa zifanyiwe kazi na mbunge wetu.

Kwa kweli wakazi wa jimbo la Kawe tupo katika kipindi tete tunamkumbuka RITA Mlaki ambaye alikuwa karibu na wapiga kura.


Wewe uliyeandika ni mwongo wa kutupwa na sina shaka wewe huishi Kawe na kama unaishi jimbo hili wewe ndiye zigo. Mheshimiwa Halima Mdee anaijua kazi yake na amekuwa na aina mbalimbali ya kufatilia matatizo ya wanajimbo wake kuanzia ardhi, barabara/miundo mbinu, maji na mengine kama hayo. Mimi ninayeandika nimekuwa nafatilia kero za jimbo la Kawe na ninapokuwa sina majibu najaribu kumtafuta so as to hear from the horse's mouth. Ni juzi tu Ijumaa nilimwandikia ujumbe wa simu ya kiganjani kuhusu matatizo ya Changanyikeni Mbuyuni na yeye huku akiwa ametingwa na mambo mengi ya jimbo na Kitaifa lakini alijibu ujumbe wangu kwa ufasaha akiainisha jinsi anavyoshughulikia kero hizo, alipofikia, alipokwama ambapo kero hiyo inaangukia utawala mwingine au inahitaji intervention amabayo ni outside her jurisidiction na mkakati wa baadae. Anajua jimbo lake na kila upande una kero gani. Nionavyo pale ambapo hapaendi sawa kuna tatizo la siasa hasa pale ambapo watendaji ni wa chama kingine hasa CCM. Changanyikeni Mbuyuni kwa mfano tunaye kaimu Mwenyekiti ambaye anatanguliza penzi kwa CCM, ubinafsi, ukosefu wa miapngo ya muda mrefu na mfupi na kutokujiamini. Tunapaswa tuwaondoe watu wa aina hii ili tupate viongozi wanaojua wanatakiwa kufanya nini kuliko kupeleka lawama kwa Halima Mdee. Halafu mleta thread unamlinganisha Halima na mbunge yupi wa Kawe aliyepita-Adamjee?heseha Mlaki? You are not serious as these had never been benchmarks by all aspects
 
Nafikiri wewe ndo MPUUZI TENA JINGA LISILOJUA KUFIKIRIA. Mi niko JImbo la Kawe nilichofanya ni kumkumbusha tu mleta mada kuwa si kila kitu ni lazima mbunge afanye na nimesema tumpe muda bado ana zaidi ya miaka miwili. Mbona JK hatumsumbui na ahadi zake 77? Je kuna meli mpya zimekuja? Kigoma imekuwa kama Dubai? Reli mpya imejengwa? Unaonekana mkono unaenda kinywani kwa kushabikia magamba endelea ivo ivo

CHIZI UNAYEFIKIRIA KWA KUTUMIA MAKALIO.....SOMA VIZUR COMMENT NILIKUQOUTE...HOPELESS MKUBWA, NA MTABAKI HIVOHIVO WAPUUZI WAKUBWA MKIONGOZWA NA HILO LIZEE LISILO NA AKILI (SLAA), Hivi unafikiri kila anayeiponda chadema ni CCM?? hopeless namba moja wewe.....vyama havipo viwili tanzania....mijitu mingine sijui mna elimu ya madrasa na kujua kutype kidogo kwa kompyuta, ndo mnakuja humu kwa JF?? yani we chizi namba moja afrika na ulimwenguni kote.......walllah nawahakikishia, hadi chadema inakufa, haitokuja kushika madaraka ya urais, na hii ni kwasababu mumejaa watu msio na akili....
 
Punguza JAZBA hoja ni kuhusu mbunge wetu usipende kuficha udhaifu wake kwa kuleta hoja isiyo na tija. Msaada kwake ni kupokea mawazo na kuyafanyia kazi kwa manufaa ya wakazi wa Kawe
Hoja isiyo na tija ni ya kwako usiyejua majukumu ya mbunge wako. Na jinsi mlivyozoea kuombaomba ipo siku utaleta post hapa yenye hoja "Jana tulilala na njaa, mbunge hakuja kutufariji". Mbunge ni kiongozi wa jimbo ambaye kazi yake kuu ni kuwawakilisha wananchi wa jimbo lake bungeni. Lakini wanasiasa wa CCM wamebadili maana na kutokana na tabia yao ya kununua uongozi, wakabinafsisha zana hii na kuwaaminisha wapumbavu kwamba kazi ya mbunge ni kuleta maendeleo. Hiyo ni dhana mufilisi tena ni ya akili za kipumbavu. Hivi wenye akili wajiulize mbunge anatoa maendeleo wapi kuyapeleka jimboni kwake? Hii dhana ya kwamba ikitokea njaa jimboni mbunge, mafuriko mbunge, bodaboda wana shida mbunge ni upuuzi uliopandikizwa kwa wapumbavu na wanasiasa uchwara wasiojua kujenga hoja kisiasa bali kutoa ahadi za kusadikika kwa wapiga kura ili ashinde uchaguzi. Kutokana na utamaduni huo mbovu, ndipo serikali ikaamua kuwalipa mamilioni wabunge kwa kisingizio cha majukumu ya kuwaletea maendeleo wananchi, ikawatia upofu wasijue wanaenda bungeni kufanya nini, na yenyewe ikalala usingizi.
Hayo malalamiko yako kwa mbunge yamekosea njia. Anayepaswa kulalamikiwa kwa kushindwa kupeleka huduma kwa jamii ni serikali ndiyo yenye wajibu huo kisheria. Sasa uliichagua serikali sikivu, peleka hayo madai yako huko. Halima mdee hakusanyi kodi, wala ushuru wa aina yoyote, inakuwaje unamlaumu kwa kushindwa kwa wenye wajibu kutimiza majukumu yao?
Tuamke kutoka katika lindi zito la usingizi wa upumbavu na kutambua wajibu wetu na haki zetu.
Wajibu wa kwanza wa raia wa tanzania ni kuwa raia mwema. Tii sheria bila shuruti. Na dhambi kubwa kabisa mwananchi anayoifanyia nchi yake ni kukwepa kulipa kodi stahili. Je, ndugu mtoa mada unafahamu kwamba unapaswa kulipa kodi? Unazijua kodi unazostahili kulipa kwa serikali yako?
Nina imani 90% ya walalamikaji wa nchi hii hawalipi kodi stahili.
Kama hulipi kodi uwe wa mwisho kulalamikia ukosefu wa huduma na si kutwisha wabunge mzigo wa dhambi zako.
 
Ivi wapiga kura kujadili utendaj usioridhisha wa wabunge wao, ni dhambi?,au kwa sabab anaeonekana kusemwa ni-m4c basi hapo hamna mada????mh!!!!,kaz ipo!

Jamani kinachoelezwa kama ni kweli HM ashauriwe na waliokaribu naye, mambo mengine ni madomadogo, ni vema kama mfalme amekaa vibaya akaambiwa.

CHADEMA kubalini kupokea ushauri ili huyo mbunge wenu wa kawe aendelea kutawala..... badala ya kutukana ..tatizo lenu hamtaki kupokea ushauri kwa mambo yanayohusu chama chenu..mnajiona muda wote mko sawa... ukweli uko wazi mdee hakuna alichokifanya hadi muda huu zaidi ya kupiga kelele bungeni kwa mambo ya jumla jumla tu..... mi nawambia ukweli 2015 wabunge wa upinzani hasa CHADEMA ni wa chache sana watakaorudi kuwa wabunge .... ushauri pokeeni ushauri huu haitajiki hata laki tano kwenda kufanya mkutano na wananchi kwenye maeneo ya wananchi wenye matatizo , yani kufanya mkutano kusikiliza kelo za wananchi nalo linahitaji ela za CCM???.AU USAIDIWE NA SERIKALI???. JITAZAMENI UPYA CHADEMA WENZENU WANATEKELEZA AHADI NINY MNAENDELEE NA MAANDAMANO SASA SIJUI 2015 MTASEMA TULIFANYA MAANDAMANO 100 AU TUMEJENGA ZAHANATI..KAZI MNAYO

Wakuu issue si kukubali kukosolewa. Kama mtu una akili utajua nani anakupa ushauri kwa kuwa ana nia ya kujenga na yupi ana nia ya kukupaka matope.

Suala la Halima Mdee, kama wapiga kura wake wana nia ya kumshauri kwa wema na si kumpaka matope, email yake ni hii: hmdee@parliament.go.tz wanaweza kumwandikia. Namba yake ya simu ni hii: +255 713 569823 nayo wanaweza kumpigia. Namba hizi za wabunge na email zao si siri. Ziko wazi kwenye tovuti ya bunge.

Kusema hivyo haina maana kuwa watu wasitumie jukwaa hili kukosoa wabunge, bali watoe constructive criticisms, sio kuja na malicious intentions.

Suala hili limevaliwa njuga sana na watu wachache ambao wanapost threads nyingi mfululizo humu kuelezea jambo hilo hilo hata kama wamejibiwa.

Mfano halisi ni MAFILILI mwanzishaji wa thread hii.

Tarehe 06.03.2012 alianzisha thread hii: Mbunge wetu Halima Mdee, njoo utuokoe Kunduchi Machimboni Nanukuu sentensi ya mwisho: "tulifikiri wewe utakuwa Mbunge bora kumbe AFADHALI wakati wa RITA MLAKI alikuwa karibu na wapiga kura."

Tarehe 18.05.2012 alianzisha thread hii: Mheshimiwa Halima Mdee Kulikoni???

Tarehe 14.06.2012 alichangia post hii: Note red coloured text
quote_icon.png
By MAFILILI
Halima Mdee + John Mnyika = Hodari wa kupiga maneno, UFUATILIAJI ni ZERO. Wabunge hawa wameshajijua 2015 hawarudi mjengoni hivyo wanashughulika na mambo yao binafsi kuliko kusikiliza na kufanyia kazi kero za wananchi.

Wananachi wa ubungo wanajuta kumpa kura Mnyika, wa Kawe wanasema afadhali enzi za Rita Mlaki alikuwa msikivu na mfuatiliaji
Tarehe 1.7.2012 alianzisha thread: Mheshimiwa Halima Mdee Karibu Tegeta Namanga

quote_icon.png
By MAFILILI
Pole kwa majukumu ya mjengoni Dodoma, mie mpiga kura wako nachukua fursa hii adimu kukuomba uje sehemu husika, Tegeta Namanga utukisikilize namna tunavyoteseka kuishi nje katika kipindi hiki cha baridi baada ya nyumba zetu kubomolewa na Big Bon, tafadhali njoo haraka!

Tarehe 15.09.2012 ameanzisha tena thread hii Kipindi kigumu jimboni Kawe
Na ninanukuu maneno ya mwisho ya Mafilili: "Kwa kweli wakazi wa jimbo la Kawe tupo katika kipindi tete tunamkumbuka RITA Mlaki ambaye alikuwa karibu na wapiga kura."

Utaona kwenye thread ya tarehe 06.03 yeye ni mkazi wa Kunduchi Machimboni, wakati tarehe 01.07 yeye huyohuyo ni mkazi wa Tegeta Namanga. Hii inaashiria uongo.

Na pia angalia hayo malalamiko ya kuhusu Namanga, wakati huyu MAFILILI analalamika wako wana Kawe wanaoshukuru tarehe 11.07.2012, na kwa kuwa tayari ametudanganya kuhusu makazi, ni rahisi kusema hata hii ya Tegeta Namanga anasema uongo, anamlaumu kwa kitu ambacho mbunge alitekeleza wajibu wake:
Napenda kumpongeza mbunge wa jimbo la Kawe mheshimiwa Halima James Mdee kwa jinsi alivyokuwa bega kwa bega na wapiga kura wake wa maeneo ya Tegeta Namanga waliovunjiwa nyumba zao na mwarabu mmoja mwenye sheli ya mafuta.Tuna amini kuwa utapigania haki zao mpaka zipatikane na huyu mwarabu awalipe fidia wananchi kwa uharibifu aliowafanyia.Wabunge wengine hasa wa magamba igeni mfano huu wa kuwa karibu na wapiga kura wenu hasa waoapnkuwa na matatizo.

Kwa hiyo pamoja na kujibu na kuonesha amefanya nini kama tulivyofanya kwenye post # 76 na nyinginezo, ni muhimu kurudia tena nia ya wanaopost si kumwangalisha ili atekeleze wajibu wake vizuri, bali ni kumpaka matope.

CCM wanataka bunge ambalo 100% ya wabunge ni CCM. Ikitokea tukarudi huko, bunge litapoteza ile kazi yake kuu ya kusimamia serikali. Mpaka sasa tunaona hawa akina Halima Mdee ndio wanaibua hoja kubwa za kuikosoa na kuwajibisha watendaji wabovu wa serikali. Wabunge wa CCM walio wengi kazi yao ni kupigia makofi mawaziri hata kama wanaongea upuuzi.

Mafilili na wenzake wanatamani sauti hii ya kutetea wananchi inyamaze, na bila shaka wao wanafaidika na kitu, ndio maana kila mara Rita Mlaki amekuwa anatajwa.

Tutafakari,
 
Kama ni kweli hajafanya haya, basi anahoja ya kujibu! Japo magamba wanakera, CDM wanapaswa kuonyesha njia! Kwangu haya ni malalamiko 'genuine' kutoka kwa mwanajimbo, na Halima anapaswa kuyashughulikia haraka iwezekanavyo ili wasiwe na sababu ya kum'buzzy'! Mambo mengine huwa yanaisha kwa kuongea tu; aitishe vikao atoe mrishonyuma kwa wanajimbo, inawezekana huyu mleta mada hajui tu kumbe mambo mengi tu yanaweza kuwa yameshatekelezwa, ila kwa mwananchi mmoja mmoja ndio bado fika!
 
Hivi kukutana na wanachi na kuwajulia shida zao nalo linahitaji jitihada za serikali ya ccm? mbona katika muda mfupi wa uchaguzi aliweza kuzungukia kata,kaya,mitaa yote ya jimbo lake na kutoa ahadi lukuki zenye matumaini.Any way tutakachokifanya hatoamini majicho yake atabakia kulalamika kuibiwa kula baada ya wananchi kughairi 2015.


maendeleoya jimbo hayaletwi na mbuge jamani mnatakiwa nyie wana kawe mjipange na kuanzisha shuguli za kimaendeleo baadae msaada wa serikali ndio unafuata kwa kujenga shule hosipital na kadhalika ama sivyo mtakalia kubadilisha wabunge kila uchaguzi . halima mdee anafanya kadiri ya uwezo wake michango yake bungeni nayo huioni?
 
Kawe waliingizwa Mkenge. Hakuna Mbunge wa Upinzani anayeweza kuleta maendeleo Dar-es-Salaam. Ni wakati mwafaka kujipanga kuwasafisha wabaki huko huko Kanda maalum

magamba wanajifariji kweli
 
Huyu mleta hoja anaonekana kuwa anajambo na HALIMA siyo bure.kwa hiyo anataka kutuaminisha kuwa tangu mh amepata ubunge hajawahi kuwatembelea wapiga kura wake hata mara moja?.mbona kuna wengine wanakiri wazi kuwa mbunge wao anakutana nao.je ni kweli kwamba H hajatekeleza ahadi hata moja?.mbona mleta hoja alishawahi kuleta hoja ya lawama km hii lkn H alijitokeza humuhumu akaeleza yale aliyoyafanya na anayokusudia kuyafanya.kwa nini H asipongezwe hata kwa kile kidogo alichokifanya kuliko km hivi anavyo pakwa matope na MAFILILI nime kuwa na mashaka hata anapomuitakuwa ni mb wake naona ni wake kwa sababu anaishi jimboni kwake yeye hakumchaguwa alichaguliwa na wenzake yeye anamjua aliempa kura na ndiye anaemwandaa kuwa mb wake kwa kumpaka H matope iliaonekane hafai ili mb wake apate nafasi.kwanza kazi ya mb sikuwaletea maendeleo wananchi ni kuipelekea serekali matatizo ya wananchi na kuyatatua.hapo sasa km serekali siyo sikivu mb atabadilisha sori na sori lkn hamna kitu.
 
Back
Top Bottom