tamsana
JF-Expert Member
- Jan 13, 2012
- 3,245
- 7,115
Salam wana jamvi.
Ni siku chache tu waliowengi tuliona post ya mjasiriamali mbunifu wa gari la umeme Bw. Kipanya akisambaza sauti ya vikao vya ndani vya maafisa wa serikali wakijadili kuhusu gari lake. Wadau waliowengi walisikitishwa na maongezi ya maafisa wale na kukemea kwa nguvu kitendo kile kilichoitwa kinawarudisha nyuma wabunifu badala ya kuwasaidia wafikie malengo yako.
Leo imesikika sauti ya siri ya jopo la PB ya Clouds FM ikimpanga mwanamichezo Bw. Fei Toto kuhusu maneno ya kuongea ili kuichafua Yanga na viongozi wake. Cha kushashangaza wale walioguswa na sauti ya siri ya kikao cha wale maafisa wa serikali siwasikii wakilaani kitendo cha Bw. Kipanya kushiriki kitendo kibaya cha kuihujumu Yanga na viongozi wake.
Kuna msemo unaosema 'usimtendee mwenzako kile usichopenda kutendewa'.
Binafsi mimi ni shabiki kindakindaki wa Simba ila kitendo kilichofanywa na jopo la PB kwa kushirikiana na Fei Toto leo sio cha kiungwana na hakitofautiani na kile kilichofanywa na wale maafisa wa serikali kuhusu ubunifu wa Kipanya.
Ni siku chache tu waliowengi tuliona post ya mjasiriamali mbunifu wa gari la umeme Bw. Kipanya akisambaza sauti ya vikao vya ndani vya maafisa wa serikali wakijadili kuhusu gari lake. Wadau waliowengi walisikitishwa na maongezi ya maafisa wale na kukemea kwa nguvu kitendo kile kilichoitwa kinawarudisha nyuma wabunifu badala ya kuwasaidia wafikie malengo yako.
Leo imesikika sauti ya siri ya jopo la PB ya Clouds FM ikimpanga mwanamichezo Bw. Fei Toto kuhusu maneno ya kuongea ili kuichafua Yanga na viongozi wake. Cha kushashangaza wale walioguswa na sauti ya siri ya kikao cha wale maafisa wa serikali siwasikii wakilaani kitendo cha Bw. Kipanya kushiriki kitendo kibaya cha kuihujumu Yanga na viongozi wake.
Kuna msemo unaosema 'usimtendee mwenzako kile usichopenda kutendewa'.
Binafsi mimi ni shabiki kindakindaki wa Simba ila kitendo kilichofanywa na jopo la PB kwa kushirikiana na Fei Toto leo sio cha kiungwana na hakitofautiani na kile kilichofanywa na wale maafisa wa serikali kuhusu ubunifu wa Kipanya.