Kingunge: Hatutokubali Lowassa akatwe jina

Kingunge: Hatutokubali Lowassa akatwe jina

Jana Kingunge Ngombale Mwiru kada wa siku nyingi wa CCM na mmoja wa wazee wa zamani na muasisi wa chama hicho alipanda katika jukwaa la kampeni la Lowassa mmoja wa watia
nia na kusema kuwa amenusa harufu mbaya ndani ya CCM eti kuna mpango wa kamati kuu ya chama hicho kukata jina la Lowassa huku akidai ikiwa hilo litatokea basi 'patachimbika' na 'hawatakubali'

Kimsingi ni aibu kubwa kwa mzee ambaye ni miongoni mwa walezi wa chama kuonyesha mapenzi ya waziwazi kwa mgombea mmoja huku kukiwa na atagombea wengine wengi na mbaya zaidi yeye kama yeye kutoa kauli za vitisho kwa chombo cha maamuzi ambacho yeye siyo mmoja wao!

Leo Kingunge anataka kutuaminisha kuwa katika taifa hili yeye ndiye mwamuzi wa mwisho na mbaya zaidi akili yake hakuna wa kuipinga "huu ni ujinga"

Kingunge anataka kamati kuu ya CCM isikilize amri yake na sasa hakuna haja ya kikao chochote kile cha maamuzi kinachotakiwa kuketi kwani tayari Kingunge kashamaliza kazi na kutoa uamuzi ya kwamba fulani ndiye rais!

Kingunge alianza mwaka 2005 kwa kauli eti "Salim Ahamed Salim hatakuwa rais wa Tanzania mimi Kingunge ndiye nimesema" na hapo likaanza kuundwa zengwe lililoongozwa na Lowassa kumchafua Salim!

Juzi mkoani Arusha Kingunge alimtaka Kikwete akae na Lowassa eti 'wayamalize' ili kufanikisha mkataba waliowekeana.

Tofauti na miaka ya nyuma sasa Kingunge amemtaja waziwazi 'rais wake' na mbaya zaidi kutoa onyo kali kwa kamati kuu ya CCM ambayo ndiyo 'think tank' la CCM huku akijua kuwa mgombea wake mbali na kashfa alizonazo pia ni mchovu sana kiakili na kiafya kupewa nchi! Kama mtu ni mzuri hakuna haja ya kutumia nguvu na vitisho ili apite atapita tu!

Kingunge aelewe kuwa Tanzania siyo mali yake na kauli yake ni hatari kubwa kwa chama chake! Aache vyombo vya maamuzi vifanye yake bila ya kutishwa na kushurutishwa.

Kuna watu wanadhani kuwa wana hatimiliki ya CCM mfano Nimrod Mkono aliwahi kutoa kauli kama hii ya 'patachimbika' ila yeye ndiye aliishia kuomba radhi achilia mbali kukosa alichokitaka! Kingunge ni lazima aelewe kuwa kuna vigezo vitakavyotumika kumpitisha mgombea na asiye na sifa 'ATAKATWA' na kama 'PATACHIMBIKA' basi ni kwa upande wake na akichelewa kutambua atamalizika kabisa!

Hujui kuwa kingunge ndiye mwenye chama?
 
Akatwe Lowassa kwa kosa gani kwani Escrow imetokea mwaka gani? na nani amewajibishwa?
 
Kuna jamaa mmoja humu aliwahi kusema hivi kuhusu Kingunge: "Haka kazee kalishakufa siku nyingi imebaki housing tu" Hii ilitokana na moja ya kauli zake tata. Sasa naanza kuamini!
 
Hatuwezi achia nchi iende kwa mafisadi miaka 20 mliyo wazurumu watz inatosha.hakuna reli wa air tz.mnataka malori yenu yabebe mizigo aibu kubwa hii

Vita yapanzi ni faraja ya kunguru,na huo ndio mwisho wa ccm
 
haa haa kingunge mwaka huu amedhamiria kufa na lowasa. jk tumbo joto. chezea nguvu ya mafisadi wewe. ccm wakijichanganya kumpitisha lowasa tano bora imekula kwao. utakuwa ni ushindi wa kimbunga kwenye mkutano mkuu...

Huyu jamaa hatakiwi kuingia tano bora akiingia tu imekula kwao.Zitatembea dola hapo cdhani kama kuna mjumbe wa mkutano mkuu atakayeacha kupokea ujira wa mwia
 
Kingunge tangu kaja Duniani hajawahi kumuunga Mkono mgombea Akashindwa kwenye Uchaguzi whether mgombea ni right candidate or not, 1984 kwa kushirikiana na Hayati Thabit Kombo katibu Mkuu wa iliyokuwa Asp walimpendekeza Awe Rais wa Znz, 1985 alimpigania Mwinyi u Rais wa Tz, 1995 Mkapa akiwa na Generali Ulimwengu kwa maelekezo ya Mwl, 2005 Kikwete akapiganiwa na huyu Mzee kwa maelekezo ya Rostam, 2015 tena kwa Lowassa kwa Maelekezo ya Mmiliki wa Caspian sasa sijui kama atafanikiwa au la
 
CCM wakimshindwa, wapiga kura tutamkata tu, ikulu haendi Lowassa, nyie mnaopiga mpunga wake, pigeni tu ila mwisho wa siku muungane na sisi rusiopenda kununuliwa kumwadabisha.

**wapiga kura gani hao! wakati wapiga kura wengi tunafahamu LOWASSA ALIONEWA TU!***
 
Kuna jamaa mmoja humu aliwahi kusema hivi kuhusu Kingunge: "Haka kazee kalishakufa siku nyingi imebaki housing tu" Hii ilitokana na moja ya kauli zake tata. Sasa naanza kuamini!

Hivi kwenye lile baraza la wazee ambako akina Mwinyi,Msekwa,Mkapa,Malecela wapo,huyu Kingunge yupo?
 
safisana kingunge CCM,haiwezi kumkata mtu eti kwa kigezo cha sio mwadilifu.ni nani aliye mwaminfu ccm.waliopanga kuliibia shirika la umeme kupitia escrow na kufanikisha mpaka wafadhili wakasitisha misada leo wanamshoonyeshea mkono Edo.kingunge hongera akikwatwa mtu lazima pachimbike

E bwanae kama tunawaza jambo moja,wacha kingunge awashe moto ndani ya magamba yalipuwane
 
lowasa kashakiteka chama kwa kiasi kikubwa imebaki CC tu ambayo muda si mrefu itasurrender.
 
Katika watu nimetokea kuwadharau ni huyu mfu anayetembea.Kikongwe mpumbavu sana huyu.

Huu uselfishi wake,kwa kuwa ameaidiwa vimaslahi mamvi akitinga magogoni,ndo atuingize kama taifa kwenye janga.

Chondechonde CCM,huyu asingestahili ata kuchukua fomu.Kwani watu wanahasira naye huku kitaani.Gharama alizowaingiza watanzania mpaka sasa azi stahimiliki,kwa kumbatia maslahi binafsi.

#NoikuluforLowassa
 
Hata asipokatwa, Wananchi tutamkata kwenye sanduku la kura, haiwezekani fisadi aende Ikulu.

Vizuri sana ukimkata kwenye sanduku la kura,hiyo itakuwa ni sindano ya sumu kwa ccm,na ukawa kuingia magogoni
 
Inabidi Mwaka huu CCM waanzishe mahakama yao ya chama, Ili Mamvi atakapokatwa jina, akakate Rufaa.
 
Back
Top Bottom