Arie power
JF-Expert Member
- Jun 29, 2015
- 2,552
- 1,021
Anazeeka vibaya huyu mzee, kwahiyo akikatwa atachukua hatua gani labda!
Hapana mkuu hakuna kura za maoni CCM huyu mzee wetu kaonjeshwa damu ya fedha Ubungo akili zimemruka, halafu kachagua zimwi likujualo maana ukianza na kura za maoni kwa mgombea Je, uwezo na sifa 13 za mgombea utaziweka wapi?kingunge hashinikizi uteuzi wa Lowassa ila anahitaji haki kutendeka kwa kuzingatia kura za maoni na sio kupitia maamuzi ya wachache wanaoamini katika kukata jina ili kumwondoa ulingoni,tatizo tunapenda kudanganywa tu lazima ukweli usemwe wazi na kuikosoa ccm sio dhambi ila mzee anakumbusha palipo dhaifu,hivo Lowassa aparekebishe.
TEAM lowassa
Unauliza swali ambalo una majibu yake.Au wewe husomi na kuangalia alama za nyakati?Maelfu ya wanaomiminika kumlaki na kumdhamini,ndiyo wanaoitoa kauli hiyo kwamba hatutakubali jina lake kukatwa na si Kingunge.Yeye Kingunge anaiwakilisha sauti ya wengi,kwa hekima ya kisiasa,kama ujumbe wa kuwasaidia wale watakaofanya maamuzi.Ila naona mpo watu mnaokiombea hatima chama chetu kwa kutaka kiendeleze mifumo ya kidkiteta na si ya kidemokrasia.Demokrasia inakubali wengi wape sasa wewe unatakaje?Hawatakubali yeye na nani? Hajui enzi zake zimeisha? Huyu Mzee sasa hivi hajitambui na hafuati tena misingi aliyoamini.
Wewe sema uko lipi hapo ndio yeye aseme Maembe wewe
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar Ramadhan Madabida siku ya Jumamosi iliyopita akitoa salamu za wanachama wa CCM mkoa wa Dar wakati wa shamrashamra za ujio wa Lowassa kusaka wadhamini katika mbio za kutaka kuteuliwa kuwa mgombea urais wa CCM mwaka huu alisema, UADILIFU, UCHAPAKAZI NA KUPENDWA NA WATU WENGI KWA LOWASSA anamfananisha na Mtume Muhamad!!
Source:Gazeti la Mwananchi la Jana.
*Binafsi nimechukizwa sana na kauli hiyo, kwa kuwa ni kufuru tena ni kufuru kubwa kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kumfananisha na -----. Nitashangaa sana kama wanachama wa CCM mkoa wa Dar watakaa kimya kuhusu kauli chafu kama hii ikapita hivi.