Kingunge amechanganyikiwa?

Mchukia Ufisadi,
Mkuu wangu nimekwisha sema sipendi kujihusisha na ubishi wa kidini hata kidogo lakini wazidi kunivuta tu ili mradi niingie upate kufurahi.. Ebu wewe mwenyewe soma tena huo waraka kisha nambie kuna sehemu ngapi wamenukuu Biblia na mafundisho yake ktk hujenga hoja nzima ya waraka huu...Kwanza tazama kichwa cha habari kinasema Mpango wa kuhamasisha HUDUMA YA KIUCHUNGAJI.. sasa ukisha elewa kwa nini Mkandara hakuwa mkristu ndipo utaelewa kwamba Mkandara hakubaliani na huduma za Kiuchungaji pamoja na kwamba lengo lake ni kutufikisha peponi..
Siku zote ktk waraka huru aya na sura hutumika kama mifano na sii sisitizo la waraka mzima, unless waraka huo umelenga waumini wake..
Mbali na hili nachokipinga mimi sio substance ya waraka mzima, isipokuwa uwakilishi wa waraka kama navyoikubali Biblia bila kuukubali uwakilishi wa kanisa Katoliki. Ukinielewa hapo tutakuwa msitari mmoja
Mkuu Mkandara, Mpango wa Kuhamasisha Huduma ya Kichungaji si waraka kwa wananchi wote. Ni waraka kwa waumini wa Kanisa kuhusiana na namna wanavyoweza kushiriki katika kupata viongozi wenye kuweza kusaidia jamii nzima. Waraka huo kwa wakristu, unasema hivi "Programu yetu ya kulihamasisha Kanisa kutekeleza wito wa kichungaji katika mambo ya kijamii ni kuwatia moyo waamini wote kutambua na kukubali wito wao wa Kikristo, wito wa kuwapelekea watu habari njema ya Yesu katika mambo ya kijamii na ya kitaifa. Kutakatifuza malimwengu, kuifanya nchi yetu na watu wetu kuishi pamoja huku manufaa ya kila mmoja yakiwa yanatimizwa: kupata huduma msingi za maisha na kuheshimiwa utu wa kila mmoja. Hapa maslahi na manufaa ya wote na ya kila mmoja katika jamii yanapaswa kuzingatiwa. Huu ni wajibu wa kila mmoja."


Mkuu, inawezekana kabisa waraka kama huu usiwafae waumini wa madhehebu au imani nyingine yoyote isiyo ya kikristu. Ila kama mafundisho yoyote ya dini yoyote yalivyo wa waumini wake, waraka huu ni applicable tu kwa wakristu waliokusudiwa. Inaendelea kusisitizwa pia kuwamaslahi na manufaa ya wote ni lazima yazingatiwe (bila ubaguzi). Kama kuna tatizo tuelimishane ili tupate ufahamu zaidi. Maana naanza kuona matamanio ya watu kuomba Makanisa yaache kuhubiri.

 
NI FISADI SANA, PARKING ZOTE MJINI NI COMPUNI YAKE. NA MAKAO MAKUU YAPO VICTORIA KAMA UNAENDA MWENGE. akae kimya tu. Wala hatutaki kumskia mambo ya nyerere ni zamani
 
kuchanganyikiwa kupo, na uzee unachangia.
kama amefiakia mahali pa kuwapamba mafisadi na kuwaona hao ndio wenye utu, na wapigavita mafisadi kuwa ndo hawana utu, ni dhahiri kuwa anahitaji kupumzishwa!
after all ni mbunge wa kuteuliwa.
aachwe apumzike kwa amani.
 
Mkuu umesema vizuri sana kwamba wewe HUONI popote penye matatizo.. Mimi naona sehemu nyingi sana kwani siku zote ktk Uongozi wa nchi, taasisi za kidini zinapoingilia kati ndipo utata huanza.

Unajua nchi za kiarabu kuna mengi ya wahubiri wa dini huzitaka serikali zao kufanya mema kwa faida ya wananchi wote lakini utata huja pale sisi tunapotazama nafasi ya dini na uongozi wa nchi hizo pamoja na kwamba population ya nchi hiyo ni 99 waislaam. Kifupi kanisa wala Msikiti hautakiwi kabisa kuingiza hoja zake serikalini unless swala hilo linahusiana na waumini wake.

Ni makanaisa na misikiti ilotuchanganya akili wakati wa uchaguzi wa Mkapa na huyu JK..ni hao hao waliowatukuza na kuwaona viongozi bora, leo hii tunapewa somo jingine tena wakati wa uchaguzi ukikaribia.
Trust me mkuu wangu hakuna mtu hata mmoja asiyefahamu nani kiongozi mzuri hata iwe jangwani au kijijini ndani kabisa Umasai...wote hawa walikuwa na mila za kuchagua viongozi wao na walitoa sifa au kashfa kutokana na kiongozi aliyepo.
Tatizo ni kwamba, kiongozi mzuri hana alama usoni nahata siku moja huwezi kukisia ila kwa ahadi zake..Kinachomtangulia kiongozi ni mfumo bora wa utawala.. Maadili na miiko ya Uongozi ndio road signs za kiongozi yeyote yule..kisha wananchi nao wapate somo la haki za uraia wao na sii somo la kumchagua kiongozi mzuri ambaye hajawahi kuongoza. zaidi ya hapo Mbunge sii kiongozi hata siku moja ila ni mwakilishi wa wananchi..

Hivi kweli unaweza kunipa sifa za kumchagua mtu kati Mwakyembe na Mwakalinga kwa kutumia vigezo hivyo?.. Mwakyembe tunamjua na mapungufu yake, mtu kama Mwakalinga hatumjui hivyo.. somo linatuambia nini kuhusu watu kama hawa?.. Je, linazungumza nini kuhusu wagombea wa vyama vya upinzani..Tunatazama mtu au chama? maanake nashindwa kuelewa inaonyesha kama waraka huu unataka tuishague CCM lakini tuwachuje viongozi wake badala ya kutazama upana na sera za vyama..
Siku zote uchaguzi wa viongozi hutokana na sera za chama sasa tukianza kuweka macho yetu kwa watu na tabia zao sijui nani mbora kuliko mwingine...
Hivyo pamoja na makosa ya mzee Kingunge ktk mtazamo wa wengi bado mzee huyu ana haki sawa ya kuelezea yale anayoyaona yeye kuwa ndio safi na tumkosoe kwa alosema tukizingatia kwamba tupo radhi kupokea maagizo kama haya ya waraka toka dini tofauti..
Binafsi sipo radhi kabisa na itajenga uhasama zaidi inapofikia viongozi wa dini kuitumia serikali kujenga kitu chochote kile..
Mkuu katika maelezo yako hapo juu nilitegemea ungeelezea zaidi kuhusu matatizo unayoyaona (mengi, kama ulivyodai) katika waraka unaozungumziwa kuliko kutoa mifano ya Uarabuni na haki aliyonayo Mzee Ngombale Mwiru.

Kila mmoja wetu anakubaliana na haki za kila mtu kutoa maoni yake. Haki hiyo haiishii kwa wanasiasa tu. Bali ni haki ya kila mtu kwa mujibu wa Katiba.

Mkuu, inaanza kudhaniwa kuwa Katiba ya nchi ni kwa ajili ya wanasiasa na sio wananchi wote. Nadhani wanasiasa wengi wanadhani Katiba inawahusu wao zaidi ya wengine wote, inatakiwa kutekelezwa nao na si wengine wote (Watanzania). Kama haya ndio mawazo au fikra za wanansiasa, basi sishangai wanapohoji uhalali wa wananchi kutoa mawazo yao.
 
unless waraka huo umelenga waumini wake..
Mkandara.
Hapa nadhani usifanye assumption, lakini ndivyo ilivyo.
Najua tayari na waislamu wametoa wao kama nilivyosoma kwenye gazeti la Nyakati kama hawasemi uongo. Mi sioni ubaya. Baniani nao watoe wao na wapagani watoe wao.
Sasa kama kila kiogozi atakuwa anamuelekeza mshirika wake kufanya jambo jema wacha na iwe hivyo ila mwisho wote tuwe na mafanikio.
Nimechoka sana kuona viongozi wa kidini wakitumika kupigia chepeo viongozi wa kisiasa na hapo wote tunakuwa kimya. Lakini wakigusia uovu tu wa wana si hasa, utasikia kelele kuwa wanachanganya siasa na dini. Hii inanikela sana.
Mara ngapi unasikia viongozi hawa hawa wakiwaomba viongozi wa dini kuwasaidia hili na lile tena majukwaani? mara nyingine utasikia wakisema "Jamani viongozi wa dini tusaidieni kupiga vita rushwa" au "Tusaidieni kuwaelimisha watu wenu kuhusu mauaji ya albino aka zeruzeru", hapo hawa watu huwa wana thamani lakini ikifika kuwambia waumini wao kuwa muwe carefull na viongozi bomu wala nchi hapo nongwa. Na ni hapo tunapopingana mimi na wewe bila kufahamu.
 
Recta.
hapo juu umesema kwamba wito huu ni kwa waumini wake... vizuri sana, lakini tatizo ni kwamba wewe ndiye mwenye makosa kulingana na mawazo ya wawakilishi na watu wengine niliowasoma humu..kwani muda wote watu wamesisitiza kuwa waraka umetolewa sii kwa waumini wa kikatoliki peke yake isipokuwa kwa wananchi wote, na ndio maana serikali inatakiwa kuhusishwa. Hivyo kama wameutoa kwa waumini wake kulikuwa na haja gani kupata baraka za serikali kwani hii ni haki yao wenyewe unless hatua waliyotaka kuichukua ingepingana na baadhi vifungu vya katiba yetu..

Mkuu toka huko nyuma tunazoga kuhusiana na waraka kwa sababu unalenga watu wote na nachosema mimi sikatai maudhui ya waraka huu lakini tatizo ni pale tu mnapotumia vigezo na sababu za dini kukuipeleka ujumbe na kikubwa zaidi ni kuhusishwa kwa kanisa badala ya wataalam walioandika waraka huo moja kwa moja, hata kama hawa wataalam walisoma au ni wataalam toka kanisa Katoliki.

Again, nitasema kuhusishwa kwa kanisa ktk maswala ya siasa ambayo kila mmoja wetu ana imani yake, kisha wakatumia vigezo vya mafundisho ya kanisa ambayo mimi Mkandara na raia wengine ktk madhehebu yao tofauti na Katoliki, wataona haya sii mapendekezo bali ni shinikizo kwa serikali kufuata yalke wanayoyafikiria wao...maanake ni mafundisho ya kanisa ambalo mimi sikubaliani na mafuindisho yake!
Utanisamehe sikutaka kusema hivi ila ni ktk kujaribu kupanua mtazamo wako kwa watu wengine wasioamini kanisa katoliki hivyo nimetumia jina langu mwenyewe upate kutazama upande huu..

Mkuu wangu hata katika Kuondoa Umaskini wetu, mara nyingi IMF inatuandikia waraka wake wakitoa masharti mengi yanayohusiana na Uongozi bora.. WE as tanzania hupokea waraka ule kwa kufahamu hiki chombo kinatawaliwa na watu gani na tunaelewa fika ushirikiano wake na financial Institution ikiwa ni pamoja na World Bank.. hivyo tunapokubaliana nao tunafahamu tumekubaliana na watu gani acha kabisa ile habari ya wataalam kwani hata alipokuwepo huko mzee Mtei (mtanzania mwenzetu) hakutuwakilisha sisi ila aliwakilisha vyombo hivyo...Mtei alituwakilisha sisi akiwa waziri na raia wa Tanzania lakini anapokuwa chini ya chombo fulani na kutoa mawazo yake chini ya nembo ya IMF mkuu wangu huyu mtu hawakilishi wananchi wala nchi ila anawakilisha taasisi yake. Na Nyerere alipokataa, hakukataa kwa sababu ni ushauri wa Mtei ila alichokataa ni masharti ya IMF.. ieleweke hivyo!

Ni katika mtazamo huo, watu kama Kingunge hawezi kukubaliana na mawazo yanayotanguliwa na imani ya dini.. Utanisamehe, binafsi naposoma waraka ukisema ati wao WAMETUMWA, hali mimi siamini utume wao inanipa shida kuamini kinachowakilishwa..Lakini kama watawakilisha Wakristu na dhehebu la katoliki basi huu mjadala wala hauna sababu kuendelea. Mimi naunga mkono kabisa na naweza jiunga nao hata kama ni Muislaam au Pagani maadam nakubaliana na mawazo yao lakini siwezi kuwalazimisha watu wote kuamini kwamba waraka huo unawakilisha Watanzania wote..

Mkuu hata hiyo misaada ya IMF wapo Watanzania kibao wanapinga misaada hiyo na wanapoandika maoni yao tusiwaone wameishiwa kimawazo kwa sababu tu sisi tunaona umuhimu wa kupata misaada hiyo..Ni vizuri tuwasilikize, tuwaelewe na sii kufikia dhidi yao kwa sababu tu wao sii waumini wa dini hii. Mkuu, waraka huu ni UDINI mtupu na kama huamini rudi nyuma soma hoja zote zilizotolewa hapa..Yeyote yule aliyepinga waraka huu amezungumziwa kuhusu imani yake ya dini.. nikiwa na maana mtu kama Kingunge anazungumziwa tu kwa sababu sii Mkatoliki, na hata Wakristu waliopinga waraka wamezungumziwa imani zao ktk dini kwa sababu tu waraka huu unazungumzia imani ya dini moja na kutumia aya za dini ambazo sii lazima kila Mtanzania anakubaliana nazo..

Utanisamehe mkuu lakini mimi Mkandara siwakilishwi na kanisa wala Bakwata ktk maswala ya kisiasa. Na hata siku moja sintaomba wala kukubali Bakwata wakae na serikali kuzungumzia mwongozo wa nchi hii kwani sii kazi yao kabisa..wanaweza kulalamika, kusema ukweli pale inapotakiwa hasa ktk mambo ya Ufisadi lakini sii ktunga ama kupendekeza jinsi ya kuchagua viongozi wazuri ktk mfumo mbaya wa Uchaguzi kama wa Tanzania. Hii ni kupotosha kabisa maaana ya Demokrasia, kwani wananchi watakuwa wakichagua vichwa vya watu wakasahau kwamba mrengo wa chama na sera zinazozingatia vipaumbele ndivyo vinatangulia kumpata kiongozi mzuri toka zizi gani..

Mind U, chama ndicho kinamsimamisha Mbunge na yawezekana kabisa kati ya Wabunge waliotemwa na chama wapo wazuri zaidi ya huyo aliyeteuliwa ambao waraka huu hauwezi kumsaidia mwananchi kumpata mshindani wa kweli.. Na tukizungumzia fainali baina ya vyama, wagombea wote tunao wachagua ni wale walioteuliwa na vyama sio wananchi, na mara nyingi kama sii zote kati ya vyama vyote vilivyojiandikisha ni wagombea wawili au mmoja tu ndiye anafahamika ktk utendaji kazi wake..Hivyo, ni vigumu sana kuchagua kichwa makini wakati hatuna historia ya wagombea ati tukitegemea CV ambayo haihusiani kabisa ni Ufisadi wa mtu.. Licha ya yote haya historia inatuonyesha kwamba Mafisadi wote wameanza Ufisadi baada ya kuingia madarakani..
Mkuu wangu kama kanisa lingenambia Mkapa hafai mwaka 1995, ningewaona wachawi wakubwa! lakini hata wao walipumbazika, Nyerere alipumbazika na kwa ujumla Watanzania wote tulipumbazika hadi uchaguzi wa mwaka 2000 ndipo tulipomwona vizuri mwana wa shetani akifanya kazi yake..

Usichoke na mifano yangu mkuu wangu ni katika mapana ya kutazama athari za viongozi wa dini wanapoingilia siasa kwani mwisho wa yote tunaweza kuwa na kina Ayatollah!
 
Last edited:
Recta.
hapo juu umesema kwamba wito huu ni kwa waumini wake... vizuri sana, lakini tatizo ni kwamba wewe ndiye mwenye makosa kulingana na mawazo ya wawakilishi na watu wengine niliowasoma humu..kwani muda wote watu wamesisitiza kuwa waraka umetolewa sii kwa waumini wa kikatoliki peke yake isipokuwa kwa wananchi wote, na ndio maana serikali inatakiwa kuhusishwa. Hivyo kama wameutoa kwa waumini wake kulikuwa na haja gani kupata baraka za serikali kwani hii ni haki yao wenyewe unless hatua waliyotaka kuichukua ingepingana na baadhi vifungu vya katiba yetu..

Mkuu toka huko nyuma tunazoga kuhusiana na waraka kwa sababu unalenga watu wote na nachosema mimi sikatai maudhui ya waraka huu lakini tatizo ni pale tu mnapotumia vigezo na sababu za dini kukuipeleka ujumbe na kikubwa zaidi ni kuhusishwa kwa kanisa badala ya wataalam walioandika waraka huo moja kwa moja, hata kama hawa wataalam walisoma au ni wataalam toka kanisa Katoliki.
Mkuu Mkandara, kwanza kabisa napenda nikukumbushe (kwa maana nadhani unafahamu) kuwa kuna waraka mbili zilizotolewa. Moja ni huo unaousema wewe "MPANGO WA KUHAMASISHA HUDUMA YA KICHUNGAJI" ambao kwa kweli ni waraka wa waumini wa kanisa katoliki. Pili ni ule ambao umetolewa kama mapendekezo ya kanisa "MAPENDEKEZO YETU YA VIPAUMBELE VYA KITAIFA" . Na huu wa pili ndio unaoitwa ILANI. Kama nilivyosema hapo juu, waraka wa kwanza unawahusu wakristu (Wakatoliki pekee) kama ambavyo kanisa linavyowajibika kwao katika malezi ya kiroho na kiimani. Na huo wa pili ni mapendekezo tu wala sio masharti, au instructions za namna yoyote. Ni matamanio ya kanisa kuhusu mustakbali wa Taifa kuanzia uchaguzi ujao. Haihusu Chama, Wanachama wala taasisi yoyote. Ni ujumbe ambao wataalamu waliouandaa wanadhani ungefaa kuzingatiwa katika kuweka bayana priorities za nchi na kudhani kuwa vyama vitakavyoshiriki uchaguzi vinaweza kuyatumia kwenye Ilani zao na labda kufaidika na mapendekezo hayo.
Again, nitasema kuhusishwa kwa kanisa ktk maswala ya siasa ambayo kila mmoja wetu ana imani yake, kisha wakatumia vigezo vya mafundisho ya kanisa ambayo mimi Mkandara na raia wengine ktk madhehebu yao tofauti na Katoliki, wataona haya sii mapendekezo bali ni shinikizo kwa serikali kufuata yalke wanayoyafikiria wao...maanake ni mafundisho ya kanisa ambalo mimi sikubaliani na mafuindisho yake!
Utanisamehe sikutaka kusema hivi ila ni ktk kujaribu kupanua mtazamo wako kwa watu wengine wasioamini kanisa katoliki hivyo nimetumia jina langu mwenyewe upate kutazama upande huu..
Mkuu, uko sahihi kabisa kuhusiana na imani ya mtu kwa dhehebu au dini yake. Ndio maana hata mimi naamini kuwa, kila kikundi, taasisi na shirika la dini kinaweza kutoa mapendekezo yao (kwa haki kabisa) ili kusaidia kuonyesha mtazamo wao kwa wanasiasa wanaotaka kuongoza nchi au majimbo wanayoomba.
Vile vile siamini kuwa, kwa kuwa kuna makundi ya imani tofauti, basi makundi yote yakae kimya kuheshimu imani za wengine. Hata kama inaona inaweza kutoa mchango wa mawazo ili kuweka hali bora zaidi katika makuzi ya jamii. Hivi Mkuu, unataka kuniambia kuwa, kwa kuwa wewe na familia yako mnaishi kwa imani na ustaarabu wenu, basi jirani mwenye imani na ustaarabu tofauti, akitumia ustaarabu wake kufanya jambo linalowaudhi/wakera au linaloweza kusababisha usumbufu kwenye jamii yenu, utakaa kimya kwa kuwa nae ana ustaarabu wake? Hivi kutoa maoni siku hizi imekuwa ni kuingilia haki, taratibu na shughuli za watu wengine? Je serikali si pia ya viongozi wa dini? Kama ni hivyo, je hapa JF tunafanya nini? Maana pia tunachambua, kushauri, kulalamikia na kupendekeza namna jamii yetu inavyoweza kuwa bora zaidi. Je, unadhani kila mtu anaimani kama tuliyonayo hapa JF? Mapendekezo/Ilani ngapi zimeshaandikwa hapa JF? Mkuu kutoa maoni ni haki ya msingi ya Mtanzania, bila kujali imani yake, rangi, jinsia wala tabaka lolote analotoka.

Mkuu wangu hata katika Kuondoa Umaskini wetu, mara nyingi IMF inatuandikia waraka wake wakitoa masharti mengi yanayohusiana na Uongozi bora.. WE as tanzania hupokea waraka ule kwa kufahamu hiki chombo kinatawaliwa na watu gani na tunaelewa fika ushirikiano wake na financial Institution ikiwa ni pamoja na World Bank.. hivyo tunapokubaliana nao tunafahamu tumekubaliana na watu gani acha kabisa ile habari ya wataalam kwani hata alipokuwepo huko mzee Mtei (mtanzania mwenzetu) hakutuwakilisha sisi ila aliwakilisha vyombo hivyo...Mtei alituwakilisha sisi akiwa waziri na raia wa Tanzania lakini anapokuwa chini ya chombo fulani na kutoa mawazo yake chini ya nembo ya IMF mkuu wangu huyu mtu hawakilishi wananchi wala nchi ila anawakilisha taasisi yake. Na Nyerere alipokataa, hakukataa kwa sababu ni ushauri wa Mtei ila alichokataa ni masharti ya IMF.. ieleweke hivyo!
IMF na WB wanapata mamlaka ya kushinikiza serikali masikini kutokana na utegemezi wa serikali hizo kwao. Ni dhahiri kuwa IMF na WB wasingekuwa na mamlaka hizo kama serikali zingeweza kujiimarisha kiuchumi kwa kutumia rasilimali zake bila kuwa na utegemezi wowote kwao. Ni jambo la kueleweka kabisa kuwa unapoomba mkopo kutoka kwa mashirika kama hayo, unakuwa unatoa pia maelezo ya jinsi utakavyoutumia, manufaa ya matumizi hayo na jinsi utakavyoweza kurudisha mkopo huo. Ni hapo ndipo nao hutumia nafasi ya kuelewa maelezo yako na kuyarekebisha/ kushinikiza namna tofauti ya kufanya mambo ya ndani ya nchi yako. Hata katika hali ya kawaida, ndugu akikuomba mkopo utataka kujua mengi kuhusu jinsi anavyotaka kuutumia mkopo huo na namna atakavyourudisha na lini ataweza kuurudisha. Mkuu nisingependa kuzungumzia sana masharti ya IMF na WB ila yanaeleweka hasa mashirika hayo yanapokuwa yakiendelea kutoa mikopo isiyolipwa na serikali hizo kama walivyokubaliana.
Mtei alipokuwa akifanya kazi IMF alikuwa anawajibika kufuata policies za IMF na si vinginevyo.

Ni katika mtazamo huo, watu kama Kingunge hawezi kukubaliana na mawazo yanayotanguliwa na imani ya dini.. Utanisamehe, binafsi naposoma waraka ukisema ati wao WAMETUMWA, hali mimi siamini utume wao inanipa shida kuamini kinachowakilishwa..Lakini kama watawakilisha Wakristu na dhehebu la katoliki basi huu mjadala wala hauna sababu kuendelea. Mimi naunga mkono kabisa na naweza jiunga nao hata kama ni Muislaam au Pagani maadam nakubaliana na mawazo yao lakini siwezi kuwalazimisha watu wote kuamini kwamba waraka huo unawakilisha Watanzania wote..

Mkuu hata hiyo misaada ya IMF wapo Watanzania kibao wanapinga misaada hiyo na wanapoandika maoni yao tusiwaone wameishiwa kimawazo kwa sababu tu sisi tunaona umuhimu wa kupata misaada hiyo..Ni vizuri tuwasilikize, tuwaelewe na sii kufikia dhidi yao kwa sababu tu wao sii waumini wa dini hii. Mkuu, waraka huu ni UDINI mtupu na kama huamini rudi nyuma soma hoja zote zilizotolewa hapa..Yeyote yule aliyepinga waraka huu amezungumziwa kuhusu imani yake ya dini.. nikiwa na maana mtu kama Kingunge anazungumziwa tu kwa sababu sii Mkatoliki, na hata Wakristu waliopinga waraka wamezungumziwa imani zao ktk dini kwa sababu tu waraka huu unazungumzia imani ya dini moja na kutumia aya za dini ambazo sii lazima kila Mtanzania anakubaliana nazo..

Utanisamehe mkuu lakini mimi Mkandara siwakilishwi na kanisa wala Bakwata ktk maswala ya kisiasa. Na hata siku moja sintaomba wala kukubali Bakwata wakae na serikali kuzungumzia mwongozo wa nchi hii kwani sii kazi yao kabisa..wanaweza kulalamika, kusema ukweli pale inapotakiwa hasa ktk mambo ya Ufisadi lakini sii ktunga ama kupendekeza jinsi ya kuchagua viongozi wazuri ktk mfumo mbaya wa Uchaguzi kama wa Tanzania. Hii ni kupotosha kabisa maaana ya Demokrasia, kwani wananchi watakuwa wakichagua vichwa vya watu wakasahau kwamba mrengo wa chama na sera zinazozingatia vipaumbele ndivyo vinatangulia kumpata kiongozi mzuri toka zizi gani..

Mind U, chama ndicho kinamsimamisha Mbunge na yawezekana kabisa kati ya Wabunge waliotemwa na chama wapo wazuri zaidi ya huyo aliyeteuliwa ambao waraka huu hauwezi kumsaidia mwananchi kumpata mshindani wa kweli.. Na tukizungumzia fainali baina ya vyama, wagombea wote tunao wachagua ni wale walioteuliwa na vyama sio wananchi, na mara nyingi kama sii zote kati ya vyama vyote vilivyojiandikisha ni wagombea wawili au mmoja tu ndiye anafahamika ktk utendaji kazi wake..Hivyo, ni vigumu sana kuchagua kichwa makini wakati hatuna historia ya wagombea ati tukitegemea CV ambayo haihusiani kabisa ni Ufisadi wa mtu.. Licha ya yote haya historia inatuonyesha kwamba Mafisadi wote wameanza Ufisadi baada ya kuingia madarakani..
Mkuu wangu kama kanisa lingenambia Mkapa hafai mwaka 1995, ningewaona wachawi wakubwa! lakini hata wao walipumbazika, Nyerere alipumbazika na kwa ujumla Watanzania wote tulipumbazika hadi uchaguzi wa mwaka 2000 ndipo tulipomwona vizuri mwana wa shetani akifanya kazi yake..
Mkuu, mimi huwa sijali sana ni watu wa imani ipi wanaotoa mchango katika sekta mbalimbali zihusuzo hali halisi ya jamii yetu na namna sahihi ya kuiboresha. Huwa naamini kuwa imani ya mtu ni yake binafsi kwa manufaa yake mwenyewe na azima yake ya kufika mbinguni kwa wale wanaoamini hivyo. Huwa nashangaa sana kusikia watu wakidhani kushabikia dini fulani (hata kama malengo yanayoshabikiwa hayana tija) ni jambo la muhimu. Huwa naamini zaidi kwenye content ya kinachotolewa na binadamu, nia na madhumuni ya kutolewa kwa content hiyo, na faida au hasara kwa watu wote nikiwemo mimi.
Mkuu ni kwa sababu hiyo, ninaamini kuwa madhehebu yote yangeweza kushirikiana kutoa waraka kama huo wenye balance ya makundi yote katika jamii ili kuufanya uwe bora zaidi.
Nimeusoma waraka huu wa CPT. Kuna mapungufu kadhaa ambayo nimeyaona. Ila si mapungufu hayo yanayozua mjadala. Waraka huu hautoi mafundisho ya jinsi ya kuchambua wagombea. Unabainisha kuwa wagombea wapige vita ufisadi, waonyeshe dhahiri kukerwa na ufisadi. Mkuu si unajua kuwa wapo watakaogombea ambao wanatuhumiwa kwa ifisadi? Unataka waendelee kutumia pesa zao kushinda tu? Lakini pia waraka huu unapendekeza vipaumbele vya kitaifa ambavyo wanaona wao kuwa vinafaa kuimarishwa zaidi.

Usichoke na mifano yangu mkuu wangu ni katika mapana ya kutazama athari za viongozi wa dini wanapoingilia siasa kwani mwisho wa yote tunaweza kuwa na kina Ayatollah!
Mkuu nakuhakikishia kuwa mjadala huu una manufaa sana kwangu na kamwe sitachoka kuendelea kujifunza kutokana nao. Mkuu nakushukuru kwa kujitolea kuzungumzia kwa mtazamo wako, na pia kwa kuwa mvumilivu kusoma wanachoandika wengine kwa makini na ustaarabu unaotegemewa kutoka kwako.
 
Zamani alikuwa na urahisi zaidi kudanganya kwa sababu fursa za kujua ukweli zilikuwa zimefichwa. Lakini alipoanza kuwatetea mafisadi pale maelezo alitakiwa kujua kuwa watanzanjia wa leo ni tofauti kiasi na wale wa miaka ile ambayo kudanganya kwa politiki kulikuwa jambo la kawaida.
Hata hivyo, ikumbukwe kuwa mtu asiye na dini kwake uhalifu ni jambo la kawaida. Hana dhamira ya kidini inayoweza kumsuta au kumfaya asiwe fisadi au awalinde mafisadi. Tofauti kidogo na wenye dini ambao hata wanaweza kuona aibu.
 
Recta.
hapo juu umesema kwamba wito huu ni kwa waumini wake... vizuri sana, lakini tatizo ni kwamba wewe ndiye mwenye makosa kulingana na mawazo ya wawakilishi na watu wengine niliowasoma humu..kwani muda wote watu wamesisitiza kuwa waraka umetolewa sii kwa waumini wa kikatoliki peke yake isipokuwa kwa wananchi wote, na ndio maana serikali inatakiwa kuhusishwa. Hivyo kama wameutoa kwa waumini wake kulikuwa na haja gani kupata baraka za serikali kwani hii ni haki yao wenyewe unless hatua waliyotaka kuichukua ingepingana na baadhi vifungu vya katiba yetu..

Mkuu toka huko nyuma tunazoga kuhusiana na waraka kwa sababu unalenga watu wote na nachosema mimi sikatai maudhui ya waraka huu lakini tatizo ni pale tu mnapotumia vigezo na sababu za dini kukuipeleka ujumbe na kikubwa zaidi ni kuhusishwa kwa kanisa badala ya wataalam walioandika waraka huo moja kwa moja, hata kama hawa wataalam walisoma au ni wataalam toka kanisa Katoliki.

Muheshimiwa amekuonyesha kwamba huo "waraka" umelengwa kwa waumini wake kwa kuunukuhu waraka wenyewe. Wewe unaamua kuu-ignore huo waraka na kuamini watu wengine wanachokuambia. Na mimi nikikwambia waraka huo umetumwa na Vatican utaamini tu kwa sababu umenisoma hapa? Au unachagua kuamini unachotaka kukiamini?

Ushaambiwa waraka wenyewe unajieleza mlengwa wake ni nani. Mimi nadhani busara ingesema kingine chochote ni makosa. Na kwa kufuta mantiki hii, nakubaliana na wewe kwamba kutaka baraka za serikali (kama hicho kitu kweli kimefanyika) inaweza ikawa ni makosa. Lakini hata kama makosa hayo yakfanywa na aliyetunga huo waraka, haibadilishi kilichoandikwa na waraka huo, na mlengwa wa waraka huo atabaki ni yule yule.

Wewe ukiambiwa waraka unakuhusu lakini ukakuta paragraph ya kwanza inasema "waraka huu ni kwa ajili ya wezi", na wewe unajijua si mwizi, au "waraka huu ni kwa ajili ya wapagani" na wewe unajijua si mpagani, au "waraka huu ni kwa ajili ya malaika" na wewe unajijua si malaika, pengine utaendelea tu kuusoma lakini je, utaendelea tu kung'ang'ania kwamba wewe ni mlengwa kwa sababu tu kuna mtu kakwambia wewe ni mlengwa? Mimi nadhani hapo utamrudia liyekwambia na kumuuliza "mbona umeniambia kwamba mimi ni mlengwa wa huu waraka wakati wenyewe unasema tofauti" na sio kusema waraka umekosewa.

Ligi nyingine zinaweza kuwa ndeeeeefu, kumbe wote mko upande mmoja.

Again, nitasema kuhusishwa kwa kanisa ktk maswala ya siasa ambayo kila mmoja wetu ana imani yake, kisha wakatumia vigezo vya mafundisho ya kanisa ambayo mimi Mkandara na raia wengine ktk madhehebu yao tofauti na Katoliki, wataona haya sii mapendekezo bali ni shinikizo kwa serikali kufuata yalke wanayoyafikiria wao...maanake ni mafundisho ya kanisa ambalo mimi sikubaliani na mafuindisho yake!
Utanisamehe sikutaka kusema hivi ila ni ktk kujaribu kupanua mtazamo wako kwa watu wengine wasioamini kanisa katoliki hivyo nimetumia jina langu mwenyewe upate kutazama upande huu..

Kwa hiyo sasa mlengwa mwengine wa waraka huo amekuwa Serikali? Serikali inashinikizwa vipi na huu waraka? Na inashinikizwa kufanya nini? Unaweza kutaja hata kamstari kamoja ka waraka huo ambacho kinasema serikali inashurutishwa kufanya kitu?

Nakubaliana na wewe si sawa kumshurutisha mwingine kufuta imani yako. Ila nina maneno mawili matatu kwako, na lengo ni kuonyesha aina ya dishonesty ya baadhi ya arguments kwenye thread hii.

Kwanza, kwa nini ukausoma huo waraka wakati haukuhusu? Kama ulivyokwishaoneshwa, waraka unajieleza wazi mlengwa ni nani.

Pili, kama uliusoma na kuona kwamba unazidi kupingana na imani yako, kwa nini usiamue kutoufuata tu mashauri yake kama vile ambavyo hufuati mashauri ya maandiko mengine mengi yanayotolewa na watu hao hao? Yaani ukiona inakupendeza kuchagua wezi, waraka huo utakuzuia kufanya hivyo?

Mkuu wangu hata katika Kuondoa Umaskini wetu, mara nyingi IMF inatuandikia waraka wake wakitoa masharti mengi yanayohusiana na Uongozi bora.. WE as tanzania hupokea waraka ule kwa kufahamu hiki chombo kinatawaliwa na watu gani na tunaelewa fika ushirikiano wake na financial Institution ikiwa ni pamoja na World Bank.. hivyo tunapokubaliana nao tunafahamu tumekubaliana na watu gani acha kabisa ile habari ya wataalam kwani hata alipokuwepo huko mzee Mtei (mtanzania mwenzetu) hakutuwakilisha sisi ila aliwakilisha vyombo hivyo...Mtei alituwakilisha sisi akiwa waziri na raia wa Tanzania lakini anapokuwa chini ya chombo fulani na kutoa mawazo yake chini ya nembo ya IMF mkuu wangu huyu mtu hawakilishi wananchi wala nchi ila anawakilisha taasisi yake. Na Nyerere alipokataa, hakukataa kwa sababu ni ushauri wa Mtei ila alichokataa ni masharti ya IMF.. ieleweke hivyo!

Ni katika mtazamo huo, watu kama Kingunge hawezi kukubaliana na mawazo yanayotanguliwa na imani ya dini.. Utanisamehe, binafsi naposoma waraka ukisema ati wao WAMETUMWA, hali mimi siamini utume wao inanipa shida kuamini kinachowakilishwa..Lakini kama watawakilisha Wakristu na dhehebu la katoliki basi huu mjadala wala hauna sababu kuendelea. Mimi naunga mkono kabisa na naweza jiunga nao hata kama ni Muislaam au Pagani maadam nakubaliana na mawazo yao ...

Nadhani Mkandara ni kichwa. Ukweli ni kwamba mlengwa amewekwa wazi kwenye huo waraka, ni vingine vyote vinaonekana kama ni propaganda kwangu. Wewe ndio uamue kuzifuata au la.

Busara yako na ikutangulie muhishimiwa Mukandara. Kama kuna jirani yako mkatoliki anayetaka kuufuta waraka huu, mpe moyo kwa sababu atakayofanya yatakuwa kwa faida yako pia. Ukitaka kujua atafanya nini, soma huo waraka (ignore all religious stuff).

Unajua argument ya msingi inayowekwa mbele na wanaopinga huu waraka ni udini kwenye siasa. Ambayo inaweza kuwa ni valid argument.

Lakini sijasikia hata mmoja akiseme nini kwenye huo waraka ni tatizo. Ni nini kwenye huo waraka hao wakristu wanaambiwa wafanye ambacho ni kibaya, au ni uvunjaji wa sheria. Ni nii hicho wanachoambiwa hao wakristu ambacho wakikifanya nchi hii itaenda pabaya, au mafisadi ndio watazidi kustawi. Ningependa nisikie ni nini hicho kilichoko kwenye huo waraka ambacho hao wakristu wakikifanya basi watakuwa wamewafanyia ubaya waislamu na wenye imani nyingine na wasio na imani.

... lakini siwezi kuwalazimisha watu wote kuamini kwamba waraka huo unawakilisha Watanzania wote... Utanisamehe mkuu lakini mimi Mkandara siwakilishwi na kanisa wala Bakwata ktk maswala ya kisiasa.

Hoja ya uwakilishi katika context hii pengine ni hoja yenye matege.

Unamaanisha nini na waraka huo "kuwakilisha" kundi fulani la watu, au watanzania wote? Mimi sioni huo uwakilishi unaouzungumzia. Huu waraka unawaambia walengwa wake nini cha kufanya, kwishnehi. Na pengine wasipoufanya wataenda motoni (lol haya ni maneno yangu usije ukasema jamaa wanawatishia waumini wao). Hakuna swala la uwakilishi hapo. Kama wewe ni muumini wao na unaona huo waraka unakukwaza, nadhani una uhuru wa kuhama. Na kabisa kabisa sioni jinsi gani huo waraka unakuwa umetumwa kwa sisi wengine wote, sisi wenyewe ndio tunapigana propaganda na kuanza ku-act kama vile tumetumiwa wananchi wote.

Kama walichowaelekeza watu wale kufanya ni kibaya, then speak it out; sema nini walichoambiwa wafanye ni kibaya au pengine kina athari kwao au kwa jamii nzima.

...
Na hata siku moja sintaomba wala kukubali Bakwata wakae na serikali kuzungumzia mwongozo wa nchi hii kwani sii kazi yao kabisa

Msimamo mzuri!

Mukandara, kuna watu wanaoogopa kwamba karibia nusu ya wapiga kura watafundishwa kufanya kitu sahihi this time round. Na hii haitakua nzuri kwa hawa watu. Nadhani kama BAKWATA na wengine nao wangetoa nyaraka zao za aina hii, na kweli waumini hao wakazifuata, na wapagani nao wakatafuta njia ya kufanya hivyo hivyo, hii nchi inaweza kubadilika ndani ya siku kadhaa tu. Imagine 100% pa wapiga kura wanaenda kufanya kitu sahihi. It doesnt matter much kama wanaenda kufanya kitu sahihi kwa sababu wanadhani wataenda mbinguni, au wanaenda kufanya kitu sahahihi bila hata ya kujua kwamba ni kitu sahihi.
 
Ushaambiwa waraka wenyewe unajieleza mlengwa wake ni nani. Mimi nadhani busara ingesema kingine chochote ni makosa. Na kwa kufuta mantiki hii, nakubaliana na wewe kwamba kutaka baraka za serikali (kama hicho kitu kweli kimefanyika) inaweza ikawa ni makosa. Lakini hata kama makosa hayo yakfanywa na aliyetunga huo waraka, haibadilishi kilichoandikwa na waraka huo, na mlengwa wa waraka huo atabaki ni yule yule.
Mkuu maelezo yako yanafafanua kwa kina kabisa maana na kusudio la waraka huu. Napenda kuongezea tu kwamba, waraka huu hata hauwahusu serikali wala taasisi yake yoyote. Haujaombewa nafasi ndani ya Bunge, au kwenye CC-CCM, NEC-CCM wala kikao chochote cha chama chochote cha siasa. Ni waraka unaotoa changamoto za vipaumbele muhimu kwa Taifa. Ni dhahiri kuwa vipaumbele vya Taifa letu haviko bayana tena.

Mimi nasema tu si kwakuwa nina imani na dini hiyo, bali kwa kuwa nina imani kuwa matamshi kama haya yanahitajika sana kwa Taifa letu wakati huu, na ni hamu yangu kupata waraka nyingi kama hizo. Nina amini kuwa waraka huu hautoshi kipekee kuleta mabadiliko yanayofaa. Inputs nyingi zaidi kutoka pande nyingi zaidi zinahitajika. Ni jukumu la kila mwenye nia njema kuweka wazi mahitaji yake kwa Taifa lake.
 
Elimu ya utaifa na demokrasia ni muhimu sana kwa jamii ya watanzania.waraka wa wakatoliki ni changamoto tuu,ni waraka ambao unawachanganua macho wale wanaodhani maswala ya taifa na demokrasia ni ya watu wengine na sio wao.ni waraka unaotoa changamoto kwa jamii iweze kutumia haki yao ya msingi kuchagua viongozi wao wanowaamini kwamba wataleta mabadiliko katika nchi hii,hakuna hata mahala pamoja waraka unapoonyesha ni tishio au utaleta mgawanyiko kwa jambo lolote ingekuwa hivyo usingeeibua mjadala wa kitaifa jambo ambalo linasaidia sana ajenda ya wakatoliki kuusambaza
 
kuchanganyikiwa kupo, na uzee unachangia.
kama amefiakia mahali pa kuwapamba mafisadi na kuwaona hao ndio wenye utu, na wapigavita mafisadi kuwa ndo hawana utu, ni dhahiri kuwa anahitaji kupumzishwa!
after all ni mbunge wa kuteuliwa.
aachwe apumzike kwa amani.
Sio uzee wala nini huyo kafulia tu.Watu wenye umri mdogo wa yeye kuwazaa walikuwa wanasiasa wameng'atuka yeye bado tu anang'ang'ania-TUMEMCHOKA!Kwani yeye anafikiri hakuna wengine wenye mawazo mapya,JK naye alichemka sana kumteua mtu kama huyo.Wabunge wakuteuliwa wanatakiwa wawe vijana na wanawake ili tupate vionjo tofauti Bungeni.Kingunge aangalie mifano ya wazee kama Nelson Mandela,mtu anazeeka na heshima zake worldwide!
 
Kigunge hajachanganyikiwa. ni kasisi wa mafisadi lazima apinge kinachohatarisha usalama wa mafisadi.

mnajua kuwa alishawahi kuhonga mwalimu amfanyie mtoto wake kinjekitile mtihani wa sekondari?
 
Quote:


Ushaambiwa waraka wenyewe unajieleza mlengwa wake ni nani. Mimi nadhani busara ingesema kingine chochote ni makosa. Na kwa kufuta mantiki hii, nakubaliana na wewe kwamba kutaka baraka za serikali (kama hicho kitu kweli kimefanyika) inaweza ikawa ni makosa. Lakini hata kama makosa hayo yakfanywa na aliyetunga huo waraka, haibadilishi kilichoandikwa na waraka huo, na mlengwa wa waraka huo atabaki ni yule yule.

Mkuu wangu ktk kila sehemu ulotumia neno waraka liondoe na badala yake weka Mahakama ya kadhi tuone kama utapata jibu sawa..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom