KINANA: Urais wa Samia sio wa Kikatiba, amepatikana kwa Uchaguzi

Urais wake wa kikatiba..hakuna sehemu baada ya jpm kufariki aliingia barabarani kuomba kura kwa wanachi ili awe rais wa nchi hii...kinana acha upotoshaji kwanza wewe zi uliandika barua ya kustaafu siasa kutokana na umri kilicho kurudisha kwenye siasa ni nini.?kama sio u.. wako.

#MaendeleoHayanaChama
Huyu ndio wanamwita mwalimu wa siasa labda mwalimu wa propaganda
 
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM),Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana ameweka wazi kuwa Rais Samia Suluhu Hasasan ni Rais kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na amepatikana kwa mchakato wa uchaguzi mkuu kwa kupigiwa kura na wananchi.

Kinana ametoa ufafanuzi huo jana wakati akizungumza na wana CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja visiwani Zanzibar kwenye Kongamano la kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na kutekeleza vema Ilani ya Uchaguzi Mkuu ya mwaka 2020/2025.

“Nataka niseme na vizuri Watanzania wakajua tangu Rais Samia achukue uongozi wa taifa letu kuna kauli nimekuwa nikisikia baadhi ya kauli kwamba Rais Samia ni Rais wa Katiba. Kauli hii ina ukweli lakini haina ukweli.

“Inaukweli kweli kwasababu Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema kila chama kitaweka mgombea na mgombe mwenza na Katiba inasema mgombea Mwenza na mgombea wanafasi moja ya kupiga kampeni ya chama chao na kila Chama kinapochagua Mgombea Mwenza,”amesema Kinana.
============

Amefafanua CCM hakimchagua mgombea mwenza kwa kucheza bahati nasibu ya kutumbukiza halafu tuangalie nani kapata nani kakosa bali wameweka sifa, kwa kuangalia uwezo, kukubalika , anafaa ,uwezo wa kufanya kampeni, , anaweza kuleta kura nyingi na mwisho wanajiuliza iwapo mgombea kwa sababu yoyote atakuwa hayupo au ameondoka madarakani je mgombea mwenza atamudu nafasi ya kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, vigezo vyote hivyo vilipimwa kwa Samia.

“Anaweza ndio , ana mudu, ndio, anajua kazi yake ndio, anaweza kufanya kampeni ndio, anaweza kumsaidia mgombea na kuleta kura ndio. Mwisho iwapo mgombea kwasababu yoyote ataondoka madarakani kwa njia za kidunia au zake Mwenyezi mungu anaweza kuchukua nafasi hiyo wana CCM tukajiridhisha ndio anaweza.

“Kwa hiyo kwa wale wanaosema huyu ni Rais wa Katiba si kweli , Rais Samia Suluhu Hassan alipimwa kabla ya kupewa hiyo nafasi, bahati nzuri mimi nilikuwa Katibu Mkuu wa Chama, nilishiriki vikao vya awali mwaka 2015 na wengine walikuwepo kwenye vikao, hayo maswali yote tulupojiuliza tukasema anaweza ,ana mudu hiyo kazi, anaongeza kura, ana uzoefu, anakifahamu chama cha mapinduzi lakini kama anahitajika kuwa Rais anaweza.

“Sasa unaposema Rais Samia ni Rais wa Katiba hakuchaguliwa sio kweli lakini kubwa zaidi Rais anapopigiwa kura na mgombea mwenza anapigiwa kura na kabla haijafika muda wa kupiga kura iwapo mgombea mwenza Mwenyezi Mungu atamchukua uchaguzi utasimmamishwa.”

Ameongeza kwa kueleza “Kwa nini usimamishwe? Kama kweli yeye ni Rais tu wa Katiba tuendeee kupiga kura mambo yaishe .Mwaka 2005 tulikuwa na mgombea mwenza wa CHADEMA Jumbe Rajab Jumbe mwenyezi Mungu akamchukua , uchaguzi ulisimamishwa, kwanini ulismamishwa? Kwasababu na yeye ananafasi muhimu hawezi rais wan chi akapigiwa kura au mgombea akapigiwa kura kama mgombea mwenza hayupo.

“Wanasema Rais Samia ni Rais wa Katiba hawasemi kweli, Rais Samia ni Rais aliyetokana na mchakato wa uchaguzi , alipopigiwa kura Rais Magufuli na Samia alipigiwa kura hapo hapo kama rais aliyemtangulia angekuwa ameondoka madarakani kwa kujiuzulu au kwasababu nyingine yoyote angekuwa Rais lakini kwasababu za Mwenyezi Mungu Rais Samia amechukua dhamana.

“Kwanini basi uchaguzi wa Chadema mwaka 2005 ulisimamishwa? Kwasababu wote wawili wanatokana na utaratibu wa Katiba uliowekwa kwa hiyo Rais Samia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wale wanaosema ni Rais wa Katiba wana ajenda yao, msiwasikilize. Kama hawajui au wanajifanya hawajui , nadhani sasa watajua, nilisema wanaosema Rais Samia ni wa Katiba hawasemi kweli na nimetoa maelezo.

“Sasa nitoe upande wa pili kweli ni Rais wa Katiba.Katiba inasema hivi kila Chama kitateua mgombea na mgombea mwenza, kwa hiyo kila Chama kinateua Mgombea na Mgombea Mwenza , Rais au mgombea anatokana na matakwa ya Katiba ya Jamhurii ya Muungano wa Tanzania.


“Mgombea mwenza ni matakwa ya katiba ya Jamhuri ya Muungano , kwa hiyo anateuliwa Samia kuwa mgombea mwenza ambaye baadae anakuwa Rais anatokana na matakwa ya Katiba kwa hiyo Rais Maguli ni Rais wa Katiba , unapendekezwa na chama chako, uakwenda kwa wananchi lakini hupigiwi kura peke yako unapigiwa na mgombea mwenza.

“Iwapo hayupo uchaguz unaahirishwa , kwa hiyo nimalize kwa kusema tukisema kwamba Rais Samia ni Rais wa Katiba husemi ukweli, Rais Samia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.nchi ya Marekani Rais wa sasa ni Rais wa 46 , katika marais 46 waliowahi kufariki kabla ya muda wao walikuwa marais wa nane baadae wakachukua wagombea wenza ambao baadae wakaja kuwa marais,” alifafanua.

Aliongeza kuwa, pamoja na hayo nchini Marekani hawajawahi kuwaita Marais hao ni WA katiba, “lakini hapa Tanzania wanaotaka kukoroga mambo wanakwambia Rais Samia ni Rais wa Katiba.”

Katika hatua nyingine, Kinana alifafanua kuwa, katika kudhirisha sifa za uongozi wa Rais Samia ameweka alama kubwa za maendeleo katika kila mkoa wilaya na shehia nchi nzima.

“Yote haya ya mefanyika katika muda mfupi wa mwaka mmoja wa uongozi wake
fedha za maendeleo zimetokana na ukusanyaji mkubwa wa kodi kwa njia ya hiyari, fedha za misaada na mikopo zilikuja kotokana na kukubalika kwake duniani.

SHAKA ASEMA RAIS SAMIA,DK.MWINYI 2030

Kwa upande wake Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, tikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka ameweka wazi kwamba kwa kazi nzuri anayoifanya Rais Samia na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, kuwatumikia na kuwaheshimisha Watanzania, kuiheshimisha Afrika na Dunia awataendelea kuwa madarakani hadi 2030.

Amesema kwa pamoja wamekuwa wakifanya kazi kubwa ya kusimamia maendeleo endelevu na kudumisha na kuimarisha muungano.

“Mitano kwa Rais Samia haina mjadala biashara imekwisha, kwa mujibu wa Katiba ya Chama chetu, Katiba yetu na utamaduni wetu huu mjadala haupo tena.Kama kuna mtu ana ndoto, hizo ndoto zikae pembeni Dk.Mwinyi tunamalizana 2030 , Chama hiki kina msingi na msingi wake mkuu ni Katiba, Kanuni na taratibu lakini kina utamaduni wake , hivyo viongozi hawa watatuvusha mpaka 2030 halafu ndio tunaangalia Katiba inasemaje.

JAMHURI
Kinana hana usemi zaidi ya ku_ justify uhongo,
Si hamini kama kinana hajui utaratibu wa makamu wa Rais kuwa Rais,
Ingekuwa kuwa samia yupo hapo kikatiba basi baada ya Magufuli kufa tungerudia UCHAGUZI.....Ivyo basi Samia siyo Rais wa kuteuliwa kikatiba...
 
Katiba mbovu na hatari sana!!makamu anaweza shiriki njama za kumuua aliyeko madarakani ili achukue kijiti

Unataka katiba iitishe uchaguzi rais akifa? Si walioshindwa uchaguzi watafanya njama za kumuua aliyeko madarakani ili wajaribu tena kwenye uchaguzi mpya?
 
Kuna uwezekano mkubwa sana wanaojua kusoma na kuandika ni viongozi wetu tu.

Sisi wengine tunasubiri kusimuliwa tu kila kitu tena hatutakiwi kuuliza.

Kuuliza ni utovu wa nidhamu.
 
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM),Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana ameweka wazi kuwa Rais Samia Suluhu Hasasan ni Rais kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na amepatikana kwa mchakato wa uchaguzi mkuu kwa kupigiwa kura na wananchi.

Kinana ametoa ufafanuzi huo jana wakati akizungumza na wana CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja visiwani Zanzibar kwenye Kongamano la kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na kutekeleza vema Ilani ya Uchaguzi Mkuu ya mwaka 2020/2025.

“Nataka niseme na vizuri Watanzania wakajua tangu Rais Samia achukue uongozi wa taifa letu kuna kauli nimekuwa nikisikia baadhi ya kauli kwamba Rais Samia ni Rais wa Katiba. Kauli hii ina ukweli lakini haina ukweli.

“Inaukweli kweli kwasababu Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema kila chama kitaweka mgombea na mgombe mwenza na Katiba inasema mgombea Mwenza na mgombea wanafasi moja ya kupiga kampeni ya chama chao na kila Chama kinapochagua Mgombea Mwenza,”amesema Kinana.
============

Amefafanua CCM hakimchagua mgombea mwenza kwa kucheza bahati nasibu ya kutumbukiza halafu tuangalie nani kapata nani kakosa bali wameweka sifa, kwa kuangalia uwezo, kukubalika , anafaa ,uwezo wa kufanya kampeni, , anaweza kuleta kura nyingi na mwisho wanajiuliza iwapo mgombea kwa sababu yoyote atakuwa hayupo au ameondoka madarakani je mgombea mwenza atamudu nafasi ya kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, vigezo vyote hivyo vilipimwa kwa Samia.

“Anaweza ndio , ana mudu, ndio, anajua kazi yake ndio, anaweza kufanya kampeni ndio, anaweza kumsaidia mgombea na kuleta kura ndio. Mwisho iwapo mgombea kwasababu yoyote ataondoka madarakani kwa njia za kidunia au zake Mwenyezi mungu anaweza kuchukua nafasi hiyo wana CCM tukajiridhisha ndio anaweza.

“Kwa hiyo kwa wale wanaosema huyu ni Rais wa Katiba si kweli , Rais Samia Suluhu Hassan alipimwa kabla ya kupewa hiyo nafasi, bahati nzuri mimi nilikuwa Katibu Mkuu wa Chama, nilishiriki vikao vya awali mwaka 2015 na wengine walikuwepo kwenye vikao, hayo maswali yote tulupojiuliza tukasema anaweza ,ana mudu hiyo kazi, anaongeza kura, ana uzoefu, anakifahamu chama cha mapinduzi lakini kama anahitajika kuwa Rais anaweza.

“Sasa unaposema Rais Samia ni Rais wa Katiba hakuchaguliwa sio kweli lakini kubwa zaidi Rais anapopigiwa kura na mgombea mwenza anapigiwa kura na kabla haijafika muda wa kupiga kura iwapo mgombea mwenza Mwenyezi Mungu atamchukua uchaguzi utasimmamishwa.”

Ameongeza kwa kueleza “Kwa nini usimamishwe? Kama kweli yeye ni Rais tu wa Katiba tuendeee kupiga kura mambo yaishe .Mwaka 2005 tulikuwa na mgombea mwenza wa CHADEMA Jumbe Rajab Jumbe mwenyezi Mungu akamchukua , uchaguzi ulisimamishwa, kwanini ulismamishwa? Kwasababu na yeye ananafasi muhimu hawezi rais wan chi akapigiwa kura au mgombea akapigiwa kura kama mgombea mwenza hayupo.

“Wanasema Rais Samia ni Rais wa Katiba hawasemi kweli, Rais Samia ni Rais aliyetokana na mchakato wa uchaguzi , alipopigiwa kura Rais Magufuli na Samia alipigiwa kura hapo hapo kama rais aliyemtangulia angekuwa ameondoka madarakani kwa kujiuzulu au kwasababu nyingine yoyote angekuwa Rais lakini kwasababu za Mwenyezi Mungu Rais Samia amechukua dhamana.

“Kwanini basi uchaguzi wa Chadema mwaka 2005 ulisimamishwa? Kwasababu wote wawili wanatokana na utaratibu wa Katiba uliowekwa kwa hiyo Rais Samia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wale wanaosema ni Rais wa Katiba wana ajenda yao, msiwasikilize. Kama hawajui au wanajifanya hawajui , nadhani sasa watajua, nilisema wanaosema Rais Samia ni wa Katiba hawasemi kweli na nimetoa maelezo.

“Sasa nitoe upande wa pili kweli ni Rais wa Katiba.Katiba inasema hivi kila Chama kitateua mgombea na mgombea mwenza, kwa hiyo kila Chama kinateua Mgombea na Mgombea Mwenza , Rais au mgombea anatokana na matakwa ya Katiba ya Jamhurii ya Muungano wa Tanzania.


“Mgombea mwenza ni matakwa ya katiba ya Jamhuri ya Muungano , kwa hiyo anateuliwa Samia kuwa mgombea mwenza ambaye baadae anakuwa Rais anatokana na matakwa ya Katiba kwa hiyo Rais Maguli ni Rais wa Katiba , unapendekezwa na chama chako, uakwenda kwa wananchi lakini hupigiwi kura peke yako unapigiwa na mgombea mwenza.

“Iwapo hayupo uchaguz unaahirishwa , kwa hiyo nimalize kwa kusema tukisema kwamba Rais Samia ni Rais wa Katiba husemi ukweli, Rais Samia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.nchi ya Marekani Rais wa sasa ni Rais wa 46 , katika marais 46 waliowahi kufariki kabla ya muda wao walikuwa marais wa nane baadae wakachukua wagombea wenza ambao baadae wakaja kuwa marais,” alifafanua.

Aliongeza kuwa, pamoja na hayo nchini Marekani hawajawahi kuwaita Marais hao ni WA katiba, “lakini hapa Tanzania wanaotaka kukoroga mambo wanakwambia Rais Samia ni Rais wa Katiba.”

Katika hatua nyingine, Kinana alifafanua kuwa, katika kudhirisha sifa za uongozi wa Rais Samia ameweka alama kubwa za maendeleo katika kila mkoa wilaya na shehia nchi nzima.

“Yote haya ya mefanyika katika muda mfupi wa mwaka mmoja wa uongozi wake
fedha za maendeleo zimetokana na ukusanyaji mkubwa wa kodi kwa njia ya hiyari, fedha za misaada na mikopo zilikuja kotokana na kukubalika kwake duniani.

SHAKA ASEMA RAIS SAMIA,DK.MWINYI 2030

Kwa upande wake Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, tikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka ameweka wazi kwamba kwa kazi nzuri anayoifanya Rais Samia na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, kuwatumikia na kuwaheshimisha Watanzania, kuiheshimisha Afrika na Dunia awataendelea kuwa madarakani hadi 2030.

Amesema kwa pamoja wamekuwa wakifanya kazi kubwa ya kusimamia maendeleo endelevu na kudumisha na kuimarisha muungano.

“Mitano kwa Rais Samia haina mjadala biashara imekwisha, kwa mujibu wa Katiba ya Chama chetu, Katiba yetu na utamaduni wetu huu mjadala haupo tena.Kama kuna mtu ana ndoto, hizo ndoto zikae pembeni Dk.Mwinyi tunamalizana 2030 , Chama hiki kina msingi na msingi wake mkuu ni Katiba, Kanuni na taratibu lakini kina utamaduni wake , hivyo viongozi hawa watatuvusha mpaka 2030 halafu ndio tunaangalia Katiba inasemaje.

JAMHURI
Ni rais wa katiba bhana. Mtu gani hana vision ya maana kwa nchi. Aende huko akapake miwanja na ma lip steak yake. Kuchukua tu urais anawatema wanamapinduzi na kuweka wapigaji. Anawasikiliza kina tonny blair maagent wa ubeberu na mabwana zake waliyomsapport kwenye enzi za ngo yake.
Sisi tumezoea siasa za jeuri kwa mabeberu na kutaka maendeleo ya usawa kiuchumi kwa raia. Samia kazi yake kutetea wapigaji tu.
Tumuombee atufikishe 2025 salama kisha wanachama wa chama cha mapinduzi watafute mwanamapinduzi kugombea urais.
 
Nani alimpigia kura Magufuli kwa wingi? Wacha uwongo wa mchana. Magufuli alimshinda Lowasssa mwaka 2015 kwa wizi wa kura za kupitia kituo cha Masaki. Muulize Medestus Kapilimba, Kinana na Januari.

Mwaka 2020 aliammua kuziiba kura zote mwenyewe Magufuli kwa kutiki makaratasi kutokea Jamana Printers na Kambi ya Mbweni Kisha ma DSO na DED wakagawiwa makatasi yaliyopigwa. Zile kura tulizopiga wananchi hazikuhesabiwa.

Dhana ya kwamba Magufuli alikuwa anapendwa ni UWONGO, kadanganye wanao au wajinga wenzio
Huo Ushahidi mbona hujawahi kuutoa hadharani? Ni kama hivyo, basi Mwambie Kinana kuwa mama yenu hakupata kuchaguliwa na sio Raisi kwa mjibu wa Katiba kama anavyodai.
 
  • Thanks
Reactions: nao
I still believe Mangula alikua the best Vice Chairman wa CCM ..Hakuwahi kuhitaji kusema chochote ili kujustify au kuprove uteuzi wake, na sidhani kama alikua na business interest yoyote ya ku-protect... Hakuwahi kuwa mtumwa wa teuzi au vyeo vya kupewa...PHILIP MANGULA anastahili Statue au recognition kutoka kwa wanachama wenzake...hii miradi mnayosema mnazindua ambayo iko kwenye ilani yenu..tafuteni moja na iitwe Philip Mangula (PM) ...I suggest iwe maeneo alikozaliwa...na Mama juzi kazindua miradi kibao huko.
Umesema kitu. Mangula was fair and true to the revolutionary principles of ccm. The current vice chairman is there to represent business interests .
 
Kwahiyo hapaswi kugombea tena urais 2025 kwani alishapita vipindi viwili akisaka kura?
Ndio nilipomsikiliza mtu anayedaiwa eti ndiye mjuzi wa Siasa nikasema kumbe ndiyo maana lichama na Serikali havina maono. Nilitegemea maelezo yake kuhusu hoja ya uraisi wa mama ingalimaliza kabisa mjadala badala yake ndio kwanza ameboronga na kujichanganya.
 
Ukwel ni kuwa Samia kapata Urais kwa sababu ya katiba! Zingine ni blahblah tu!
Sasa tunajiuliza Ni nani mkweli kati ya Kinana na Samia? Mama aliwahi kunukuliwa akiwaeleza wanawake wenzie kuwa yeye sio Raisi wa kuchaguliwa bali wa Katiba na hivi inabidi wanawake wampigie kura uchaguzi ujao ili awe Raisi wa kuchaguliwa na hao ndio watakuwa na Furaha ya kweli. Sasa Kinana Ni kama anarekebisha hiyo Kauli au anampa Tuition?
 
Sasa tunajiuliza Ni nani mkweli kati ya Kinana na Samia? Mama aliwahi kunukuliwa akiwaeleza wanawake wenzie kuwa yeye sio Raisi wa kuchaguliwa bali wa Katiba na hivi inabidi wanawake wampigie kura uchaguzi ujao ili awe Raisi wa kuchaguliwa na hao ndio watakuwa na Furaha ya kweli. Sasa Kinana Ni kama anarekebisha hiyo Kauli au anampa Tuition?
Kinana, aache kuwapotosha wananchi...anatakiwa atuambie tuko awamu ya ngapi? Kama ni awamu ya tano, Samia Suluhu Hassan ni Rais kwa mujibu wa kura alizopata Magufuli!

Kinana, wahenga walisema, you cant eat your cake and have it! Kama hii ni awamu ya sita kama inavyodaiwa, Samia Suluhu Hassan ni Rais kwa mujibu wa Katiba na si vinginevyo!
 
Ni kupoteza muda kufafanua mambo yanayoeleweka.

Mh. Rais Samia, ni Rais kwa mujibu wa katiba, na siyo kwa kupigiwa kura. Na hata wakati wa kampeni, hakuna inapoelezwa kwamba kama humtaki mgombea mwenza, usimpe kura mgombea wa Urais.

Anayoyaeleza Kinana kama yangekuwa sahihi, basi wakati wa upigaji kura kungekuwa na maeneo mawili ya kuweka kura yako, mgombea wa Urais na makamu wa Rais, na katiba ingetamka kuwa ili mgombea wa chama aweze kutangazwa kuwa Rais, ni lazima mgombea mwenyewe ashinde na mgombea mwenza ashinde, mmoja asiposhinda, wote wawili hawawezi kupitishwa kuwa viongozi wakuu wa nchi.

Mh. Rais Samia, kwa mujibu wa katiba yetu, ni Rais wetu halali. Kuuleza ukweli huu, kuna tatizo gani?

Kuhusu tamaduni za CCM kuwa Rais aliyepo madarakani, hatakiwi kushindanishwa na mwingine, sidhani kama ni jambo jema unapoongelea maendeleo ya demokrasia. Mila na desturi hii ya CCM, nadhani inatakiwa kuwekwa kwenye kundi la mila potofu.

Wanachama wanatakiwa kuwa huru kugombea, na wala haimaanishi kwamba jambo hilo ni kwa sababu watu hawamtaki Rais Samia, au Rais Samia hafai, bali ni kudumisha misingi ya demokrasia. Binafsi naamini, siyo kwa unafiki au upambe, Mh. Samia anafanya vizuri kuliko watu wengi ndani ya CCM wangepewa nafasi ya Urais.

Mh. Rais ana majukumu mazito kama Rais, tunamwombea ayatekeleze vyema ili watu wapige hatua za maendeleo. Mpaka sasa, naamini anafanya vizuri, na huenda akafanya vizuri zaidi mbeleni, lakini ni kosa kumjengea mazingira yatakayoashiria kuwa yupo kwenye nafasi hiyo kwa kuminya haki za kidemokrasia.

Huyu ni Rais wa kwanza Mama, tunataka aweke alama zitakazodumu katika Taifa letu. Alama mojawapo kubwa, aweke falsafa itakayoishi ya misingi ya kidemokrasia, misingi ambayo nchi Deikosa kwa muda mrefu.

Tuna Baba wa Taifa, tunamtafuta Baba au Mama wa demokrasia.
 
Lisu wako hawezi kuwa Rais mpaka tutakufa sote na wewe! That is stupid politician ever seen!
Naona Magufuli kafufuka...! Ulijaribu kumuua Lissu, ukatangulia wewe na bila shaka kwa hicho Kiingereza unaongea kutoka kuzimu! Nashauri waongeze kuni...
 
Naona Magufuli kafufuka...! Ulijaribu kumuua Lissu, ukatangulia wewe na bila shaka kwa hicho Kiingereza unaongea kutoka kuzimu! Nashauri waongeze kuni...
Huko kuzimu hata wewe na Lisu wako kunawasubiri! Ulivyo mshamba unashangaa mtu kufariki!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom