CM 1774858
JF-Expert Member
- May 29, 2021
- 4,991
- 4,102
KINANA ASHAURI MSCL KUJIENDESHA NA KUFIKIRI KIBIASHARA ZAIDI,
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Ndg Abdulrahman Kinana ameishauri Kampuni ya huduma za meli nchini Marine Service Company Limited kujiendesha na kuanza kufikiri kibiashara ikiwemo kuomba dhamana za serikali Ili kukopa fedha na kununua meli mpya ili kukidhi mahitaji ya huduma za usafiri na usafirishaji katika ziwa Tanganyika.
Makamu mwenyekiti huyo ameyasema hayo wakati alipotembelea na kukagua ukarabati wa meli ya MT. Sangara inayogharimu shilingi bilioni 8.4 zilizotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan,
Kinana ameishauri kampuni hiyo ni muhimu ifikirie kibiashara zaidi. Aidha Kinana ameipongeza serikali ya CCM Awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea na kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwa ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM 2020-2025.
Hiyo ni baada ya kuambiwa kuwa kama meli hiyo ambayo ni ya mafuta ikikamilika bado mahitaji ya huduma za meli kwenye ziwa Tanganyika ni makubwa na kwamba zinahitajika meli nyingine tatu.
“Sikilizeni ndugu zangu msisubiri hela kutoka bajeti ya serikali, ombeni dhamana ya serikali mkakope mnunue meli mpya.. pesa za namna hiyo ziko nyingi duniani.” alisema Kinana.
Kinana pia alipata nafasi ya kutembelea meli kongwe kabisa duniani ya MV Liemba ambayo nayo ipo kwenye mpango wa kukarabatiwa kwa kiwango kikubwa na serikali katika mwaka huu wa fedha 2022/2023.
Meli hiyo ya Mv Liemba ina umri wa zaidi ya miaka 100 na imeingia kwenye orodha ya urithi wa dunia chini ya UNESCO.
“Ikikamilika mniambie nitakuja na mwenezi kusafiri nayo.” alisema Kinana." Amesema Kinana
Kinana ambaye ameambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Ndg Shaka Hamdu Shaka ameanza ziara yake ya siku tano katika mikoa ya Kigoma, Kagera, Geita na Mwanza.
...........Kazi inaendelea........