Bandari ya Kasanga iliyojengwa kwa mabilioni yageuka tembo mweupe baada ya kuhudumia meli 1 tuu kwa miezi 4

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
43,116
49,840
Bandari ya Kasanga ni miongoni mwa Bandari kadhaa za Ziwa Tanganyika ambazo zikijengwa kwa mbwembwe nyingi na Serikali ya Mwendazake bila kusoma Geografia ya eneo husika.

Bandari hii pia imeunganisgwa na Barabara ya lami kutoka Sumbawanga mjini ambayo ujenzi wake ukichagizwa na uvumi kwamba eti malori yataacha kupitia Tunduma badala yake yaje kupita huku.

Kwa miaka ya nyuma Bandari ya Kasanga ilikuwa inahudumia meli kati ya 30-34 na nyingi ya meli hizo ni zile zilikuja kubeba saruji ya kiwanda Cha Mbeya cement kupelekea DRC Congo lakini kwa sasa DRC wamejenga kiwanda upande wao na kuua soko la saruji ya Tanzania na kuacha Bandari ikiwa tembo mweupe.

---
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo akimsikiliza, Ofisa wa Bandari ya Kasanga, mkoani Rukwa, Rodriguez Valentin alipotembelea na kujionea mradi wa upanuzi na uboreshaji wa bandari hiyo jana Jumatatu, Oktoba 9, 2023 Wilaya ya Kalambo.

Ni katika siku ya pili kati ya nne ya ziara yake mkoani humo ya kukagua miradi ya maendeleo, utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/25, kukagua uhai wa chama pamoja na
kusikiliza kero za wananchi.

Chongolo ameambatana na Katibu wa Idara ya Oganaizesheni ya chama hicho, Issa Ussi Gavu.

Akiwa bandari hapo, Chongolo amesema Serikali inaendelea kuziboresha bandari zote kubwa na ndogo ili kuziongezea tija ya utoaji wa huduma kwa wananchi na kuchangia pato la Taifa na la wananchi wenyewe.

Alisema kuna hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali, kuboresha huduma za uchukuzi, usafiri na usafirishaji katika Ziwa Tanganyika, ambapo kufikia Disemba, 2023, wananchi wataanza kupata nafuu, kuelekea kumalizika kwa adha kubwa iliyopo sasa.

Hiyo ni kutokana na kukamilika kwa matengenezo ya moja ya meli, kati ya mbili zilizopo sasa, Mv Mwongozo na Mv Liemba, ambazo zote zinafanyiwa matengenezo, ikiwa ni mojawapo ya mikakati ya muda mfupi, wa kati na mrefu na MV Mwongozo ndio itaanza kutoa huduma hivi karibuni.

Awali, Valentin akisoma taarifa mbele ya Chongolo na ujumbe wake alisema maboresho mbalimbali katika bandari hiyo ndogo yanaendelea ikiwemo kufunga mashine za kupakia na kushusha mizigo.

Alisema katika mwaka wa fedha 2021/22 bandari hiyo ilihudumia meli 34 na mwaka 2022/23 meli 32. Kuanzia Julai mwaka huu hadi Oktoba 23 wamehudumia meli moja pekee.

Valentin alibainisha changamoto zinazowakabili ikiwemo ya kufunguliwa kwa kiwanda cha saruji cha Kibimba huku DR Congo kimeongeza ushindani wa kibiashara kwa wateja wa Congo waliokuwa wanatumia bandari hiyo.

Alisema bandari hiyo ilijengwa kuanzia 1995 hadi 1998 na awamu ya pili 2018 hadi mwaka huu ikihudumia nchi za Burundi, Zambia na DR Congo ikiwa na gati lenye urefu wa mita 120 na wastani wa kina cha maji mita 14.


Chanzo: Mwananchi


My Take
Serikali mnapofanya vitu muwe mnasoma Geografia ya eneo lenu na la jirani badala ya kukurupuka Kwa mihemko.

Kuna mifano Mingi sana ya kukurupaka ambayo imesababisha miradi Mingi kuwa white elephant.
dr_congo_map.jpg
 
Ni bora wamejenga hiyo Bandari huko mbele biashara zitafunga itawasaidia kuliko tungesikia zipo kwenye taarifa ya CAG...
Toa ujinga wewe ,kitu ambacho hakitumiki Huwa kinaoza na kuharibika,mbele ipi na kitu hakitumiki?

Pili Kwa geigtmrafia ipi ya ku favour hicho kibandari? Tatizo la kukosa akili na kukurupuka ndio hili.

Kuna Bandari zilipaswa kujengwa Kwa kuangalia upande wa pili sio hiyo ya Kasanga.

Na Kwa taarifa Yako kwenye taarifa ya CAG utaikuta maana ni sawa na mradi hewa usiozalisha.
 
CCM wamekosa ubunifu.

Bandari ni kitovu cha biashara. Wanashinda kuvmfungua milango kwa consignments za mazao na uvuvi wao wanategemea kiwanda cha saruji pekee
 
CCM wamekosa ubunifu.

Bandari ni kitovu cha biashara. Wanashinda kuvmfungua milango kwa consignments za mazao na uvuvi wao wanategemea kiwanda cha saruji pekee
Vitu hivyo unavyosema vitakuwa supported na Geografia ya sehemu.Hakuna ubunifu utaweka kama upande wa pili hakuna mazingira ya kusapoti.

Wangekuwa na akili Walitakiwa kwenda upande upande wa DRC wasome Miji ipi ni mikubwa na Iko mkabala na Maeneo yapi Tanzania ndio wajenge Barabara na Bandari na waweke kile kinachotakiwa..

Yaani mtu anapeleka mzigo Lubumbashi aje apite Kasanga harafu iwaje kama sio utaahira huu? Kama ni kwenda Kaskazini mwa DRC Bandari ya Kigoma ndio suitable.
 
Mkuu habari yako, upo kwa madiba au Arusha? Kama upo tz lini unaenda kwa madiba ninataka nikachukue discover moja la kuchukulia pisi pale Ng'ong'ona
Nzuri Mkuu nipo Arusha bado tunapokea wageni nadhani kuanzia Nov patapoa kidogo...unataka Disco 3 au 4 ? nipe kazi hiyo huku kukitulia twende wote tukafate hiyo mashine ni kazi ya wiki mbili kwenda na kurudi na Gari...
 
Nzuri Mkuu nipo Arusha bado tunapokea wageni nadhani kuanzia Nov patapoa kidogo...unataka Disco 3 au 4 ? nipe kazi hiyo huku kukitulia twende wote tukafate hiyo mashine ni kazi ya wiki mbili kwenda na kurudi na Gari...
Sawa Mkuu ikipendeza December 10 tusepe tukarudi nalo tufanye na utalii njiani nataka discover 4 jeusi mkuu
 
Sawa Mkuu ikipendeza December 10 tusepe tukarudi nalo tufanye na utalii njiani nataka discover 4 jeusi mkuu
December hizo tarehe wanafunga ofisi za ununuzi wa magari labda January maana biashara inakua chini SA na bei zinakua Chini na magari mengi yanauzwa kwa sababu baada ya kurudi kutoka kutumia December wanauza sana January...
 
December hizo tarehe wanafunga ofisi za ununuzi wa magari labda January maana biashara inakua chini SA na bei zinakua Chini na magari mengi yanauzwa kwa sababu baada ya kurudi kutoka kutumia December wanauza sana January...
Ooh sawa mkuu ila nitataka lisizidi 20k km walau 2016 au 18 huko nitalipata
 
Ooh sawa mkuu ila nitataka lisizidi 20k km walau 2016 au 18 huko nitalipata
SA wanaendesha sana magari huwezi kupata Suv miaka nane nyuma iwe ina 20,000km watakua wamerudisha mileage hapo...kwa mwaka wowote utapata ila sio mileage hizo unazotaka ni ngumu...
 
Toa ujinga wewe ,kitu ambacho hakitumiki Huwa kinaoza na kuharibika,mbele ipi na kitu hakitumiki?

Pili Kwa geigtmrafia ipi ya ku favour hicho kibandari? Tatizo la kukosa akili na kukurupuka ndio hili.

Kuna Bandari zilipaswa kujengwa Kwa kuangalia upande wa pili sio hiyo ya Kasanga.

Na Kwa taarifa Yako kwenye taarifa ya CAG utaikuta maana ni sawa na mradi hewa usiozalisha.
Daah unatukana watu ambao wanatakiwa wakufundishe vitu vingi mimi sijafundishwa kutukana na pia JF imenifanya nimekutana na watu wengi na kufanya nao biashara nyingi kwa hiyo wewe kuita watu wajinga endelea maana pia malezi yametofautiana...
 
Daah unatukana watu ambao wanatakiwa wakufundishe vitu vingi mimi sijafundishwa kutukana na pia JF imenifanya nimekutana na watu wengi na kufanya nao biashara nyingi kwa hiyo wewe kuita watu wajinga endelea maana pia malezi yametofautiana...
Yaani wewe unifundishe 🤣🤣🤣

Kuwa mjinga sio tusi ni kutokuwa na ufahamu wa kutosha wa mambo
 
Back
Top Bottom