Kinachoendelea Syria, Mungu haoni?

Kinachoendelea Syria, Mungu haoni?

Unataka kwenda wapi? Mwenyenzi anajua kila kitu.

Nilipotoa mfano wa kuwa Mungu anawajaribu watu wa Syria, Ukaniletea aya kwenye Biblia inasema Mungu hajaribu mtu, na pia ukasema kwani Mungu hakujui ata akujaribu.

Nikajua najadiliana na mtu asiekuwa na elimu, kutoka kwenye bibilia hio hio nikakuletea aya ya kukuonesha kuwa Mungu alimjaribu Ibrahim, ukawa huna pakushika, kila tawi unaloshika linakatika. Ukadai eti nyakati zilikuwa tofauti na watu walikuwa wanafanya ibada tofauti, ili kusapoti argument yako ukaja na aya kwenye Quran.

Kitu simple kabisa nkakufahamisha kuwa Sifa ya Mungu sio Ibada, ni SIFA na wala sio SHeria.

Sasa mi huwa naishangaa imani yako, mpaka najiuliza, inabidi Mungu alikuwa hamjui Ibrahim mpaka akamjaribu? 😀 😀 😀
Kwa nini amjaribu mtu kama anajua fate yake?
Mungu anajua kabisa baada ya miaka mitano nitakuwa mtu mwema
kwa nini anijaribu?
Unataka kusema Mungu alikuwa hajui fate ya Ibrahim kwamba atayashinda majaribu?
Kwa nini Mungu apime imani ya Ibrahim yeye hana uhakika?
 
Kwa nini amjaribu mtu kama anajua fate yake?
Mungu anajua kabisa baada ya miaka mitano nitakuwa mtu mwema
kwa nini anijaribu?
Unataka kusema Mungu alikuwa hajui fate ya Ibrahim kwamba atayashinda majaribu?
Kwa nini Mungu apime imani ya Ibrahim yeye hana uhakika?
Nisamehe kwa kuingilia ila nahisi hujui nn maana ya jaribu kutoka kwa Mungu
Anza na zaburi 11:5
 
Ni kweli nabii isaya alishatabiri juu ya syria miaka 2000 imepita ndio sasa yanatimia wasomaji wa Biblia wala hatushangai.
 
Binadamu siyo mnyama amepewa akili ya kujua mema na mabaya na Mwenyezi Mungu alimpa mamlaka ya kuitawala dunia.
 
Kwa nini amjaribu mtu kama anajua fate yake?
Mungu anajua kabisa baada ya miaka mitano nitakuwa mtu mwema
kwa nini anijaribu?
Unataka kusema Mungu alikuwa hajui fate ya Ibrahim kwamba atayashinda majaribu?
Kwa nini Mungu apime imani ya Ibrahim yeye hana uhakika?
Jaribu kwa mtu ni kwa ajili ya kuimarisha imani yake.
 
Nimejiuliza hili swali asubuhi ya leo
Tunaambiwa na vitabu vya dini kwamba Mungu ni muweza wa yote,yeye hujua kitu kabla hata hakijatokea
Kauli hii inamaanisha kila kinachotokea huwa kina "approval" ya Mungu

Je Mungu ame "approve" machafuko ya Syria?
Kama haku "approve" kwa nini yametokea?
Mungu haoni kama kuna watoto wanateseka pale,mpaka aombwe?kwa nini anayaacha yaendelee?

Labda wanaosambaza kampeni ya Pray for syria mnaweza jibu maswali haya

efca20899c0db0889095f0a75be81344.jpg


d2e99bb857fb05f6b4162deede380592.jpg
Mbona unaenda mbali unasahau ndugu zetu wa kiafrika hapo Chad, Sudani kusini, Kongo, Burundi na Afrika ya kati huko kuna matatizo kuliko Syria.
 
Sioni Adhabu anayoweza kuwapa wanaosababisha haya majanga ikawatosha. Ni sawa na kumhukumu kunyongwa mtu alieua watu 3, kauwa watatu anakufa mmoja.
 
Kwanza niseme shetan hajafungwa miaka 1000...shetani yupo bado amepewa mamlaka ya kuharibu.

Pili niseme shetan na Mungu nitofauti kabisaaa mmoja ni muharibifu mwingine mjenzi.

ILA kuna wakati Mungu anaacha shetani atende apendavyo ili kuzipima imani na hili kufanya watu waelewe kitu ..ndomaana kuna wakati anasema *watu wangu waangamia kwa kukosa maarifa*.

Nikweli Mungu anaujus ulimwengu mwanzo namwisho LKN hana makusudi,,,, Isipokua kuna mambo mawili unayopaswa kuyajua

Utawala wa Mungu ni wa Kifalme ndomaana hamna cha waziri mkuu wala makamo wala nani ,,Mungu akisema kasema ...naanakuacha ufanye vile upendavyo.

Utawala wa shetani ni wa kidemokrasia ,ndio maana wao unahimiza haki sawaa ,haki yakufanya unachojisikia n.k

Sasa basi inatokea kwa hapa duniani utawala wa shetani unakua nanguvu sana kwasababu Ulimwengu umemezwa namambo mepesi laini namazuri ambayo wanadam wanayapenda.
Soma mwanzo 3:6. Hapo ndipo balaa yote ilikoanzia. Mungu alishauri vizuri kabisa wanadamu wakachagua kufa kwa kuwa hawakumwamini Mungu.
Mungu alipomuumba mwanadamu hakutengenza automatons ili mtu afurahie maisha AKICHAGUA kumtegemea Mungu. Lakini option ingine ilikuwepo ya kusikiliza sauti ISIYO ya Mungu na ilikuwa pia na matokeo yake. Viumbe wote wanaomwabudu Mungu wanafanya hivyo sio kwa kutenezwa kuwa hivyo bali ni kwa KUCHAGUA kumheshimu Mungu na kuyafurahiya maisha kwa hilo.
Sasa kwa nini aache haya yatokee. Ni kwamba bado amemwachia mwanadamu wa kuchagua cha kufanya hata WAKATI utakapotimia na kikombe uasi kitakapofurika. Wapo wanaoisikia sauti yake na kugeuza nia zao ambao hata wakiteseka kwa kitambo tu, miaka miwili, kumi, ishirini lakini wakaendelea kuwa waaminifu taji zinawasubiri hao.
Lakini pia amemwacha mwanadamu kuchagua kusikiliza sauti ya ibilisi yule baba wa uongo na hatima yake ni kupotea milele atakapoangamizwa shetani na wafuasi wake wote. Malimwengu yote ndipo watakapothibitisha kuwa Mungu ni wa haki. Ya kuwa ametoa uchaguzi wa uzima na mauti, wapo walio chagua uzima na wapo walio chagua mauti. Unayoyaona Syria ni ya kitambo kidogo tu. Kama hawa wahanga wa Syria wangechagua kuisikia sauti ya mwokozi mateso yao yangukuwa machache tu na wangekuw na tumaini la uzima wa milele ajapo Yesu mara ya pili.
 
Kwahyo kumbe Mungu na shetani ni marafiki wanakaa na kujadili mambo flan flan? Na mbona wanatuambia shetani kafungwa miaka 1000 na Yesu huo mda wa kupiga story na Mungu anaupata wapi?

Kwanini vile wanakutana na shetani Mungu asifanye miujiza yake kumchinjilia mbali ama Mungu anafurahia uwepo wake na anapenda vile wanadamu tunavyoteseka? Maana mamlaka na kila kitu kipo kwa Mungu

Anasema aliujua ulimwengu ata kabla ya kuumbwa kwahiyo yote ni makusudi yake maana uwezo wa kuzuia yeye ulikuepo...na sahivi yupo ku enjoy matunda yake


Nikweli Mungu anaujus ulimwengu mwanzo namwisho LKN hana makusudi,,,, Isipokua kuna mambo mawili unayopaswa kuyajua

Utawala wa Mungu ni wa Kifalme ndomaana hamna cha waziri mkuu wala makamo wala nani ,,Mungu akisema kasema ...naanakuacha ufanye vile upendavyo.

Utawala wa shetani ni wa kidemokrasia ,ndio maana wao unahimiza haki sawaa ,haki yakufanya unachojisikia n.k

Sasa basi inatokea kwa hapa duniani utawala wa shetani unakua nanguvu sana kwasababu Ulimwengu umemezwa namambo mepesi laini namazuri ambayo wanadam wanayapenda.
Click to expand...
Soma mwanzo 3:6. Hapo ndipo balaa yote ilikoanzia. Mungu alishauri vizuri kabisa wanadamu wakachagua kufa kwa kuwa hawakumwamini Mungu.
Mungu alipomuumba mwanadamu hakutengenza automatons ili mtu afurahie maishaAKICHAGUA kumtegemea Mungu. Lakini option ingine ilikuwepo ya kusikiliza sauti ISIYO ya Mungu na ilikuwa pia na matokeo yake. Viumbe wote wanaomwabudu Mungu wanafanya hivyo sio kwa kutenezwa kuwa hivyo bali ni kwa KUCHAGUA kumheshimu Mungu na kuyafurahiya maisha kwa hilo.
Sasa kwa nini aache haya yatokee. Ni kwamba bado amemwachia mwanadamu wa kuchagua cha kufanya hata WAKATI utakapotimia na kikombe uasi kitakapofurika. Wapo wanaoisikia sauti yake na kugeuza nia zao ambao hata wakiteseka kwa kitambo tu, miaka miwili, kumi, ishirini lakini wakaendelea kuwa waaminifu taji zinawasubiri hao.
Lakini pia amemwacha mwanadamu kuchagua kusikiliza sauti ya ibilisi yule baba wa uongo na hatima yake ni kupotea milele atakapoangamizwa shetani na wafuasi wake wote. Malimwengu yote ndipo watakapothibitisha kuwa Mungu ni wa haki. Ya kuwa ametoa uchaguzi wa uzima na mauti, wapo walio chagua uzima na wapo walio chagua mauti. Unayoyaona Syria ni ya kitambo kidogo tu. Kama hawa wahanga wa Syria wangechagua kuisikia sauti ya mwokozi mateso yao yangukuwa machache tu na wangekuw na tumaini la uzima wa milele ajapo Yesu mara ya pili.
 
Mwenyezi Mungu ni MWENYE KUONA na ni MWENYE KUSIKIA.Anajua kila kinachoendelea mbinguni na ardhini.Kwa hiyo suala la Syria analifahamu vizuri kuliko mimi na wewe.Ila ule ni mtihani wa hatari sana kwa wale wanaodhulumu kule na wale wanaoisikia dhuluma lakini hawachukui hatua.Kilio cha wale wanaodhulumiwa kimesikika,Mwenyezi Mungu anaangalia mimi na wewe tunawasaidiaje.Wote wale wanaodhulumu kule atawashughulikia ipasavyo,ni suala la muda tu.
 
Kwa nini amjaribu mtu kama anajua fate yake?
Mungu anajua kabisa baada ya miaka mitano nitakuwa mtu mwema
kwa nini anijaribu?
Unataka kusema Mungu alikuwa hajui fate ya Ibrahim kwamba atayashinda majaribu?
Kwa nini Mungu apime imani ya Ibrahim yeye hana uhakika?
You have to earn the rewards. Nafikiri hata wewe hupokei mshahara kama hufanyi kazi.

Mungu anajua fate zetu, wewe unajua fate yako?
 
Back
Top Bottom