Kimeumana Vanilla Njombe: Ni utapeli mtupu

Hahahaha a daaaa nimecheka Kama mazuri Hawa jamaa Wana vituko ACHA Kabisa nilishawahi kutana na kenge Mmoja kutoka forever living akaanza hizi swaga akijua kapata boya nikamchora weee mpaka mwisho wa mchezo halafu nikampotezea tu!
Wenyewe.wanaita project. Kuna mmoja alinita kwake nikala nikanywa na juice alivyoanza kuongea nikawa nasinzia aisee alikasirika mno
 
Walikuwa wanatangaza kuwa kilo moja nj milioni moja. Mm mpk nilirekodi kwenda kuwasilizisha marafiki zangu

Yeah jana Nimeona TBC-1 wametangaza Live kwenye Taarifa ya Habari ni Kweli Mrembo wangu.
Ila All in all Vanila Ina bei kubwa sanaa Kuliko Mazao mengine ya Biashara hapa Nchini,
Kama Umekima Watafute hata Natural extractive industries (NEI) wapo Moshi watanunua Tuu kwa bei Nzuri!
 
Ujumbe wa DC Njombe kissagwakisakasongwa kuhusu VanillaNjombe

📍Serikali bado inafanyia kazi maswali mengi yaliyopo katika jamii kutokana na matangazo kwamba Vanilla inalipa na bei ya manunuzi ya Vanilla kwa kilo zinazotajwa kuwa ni kubwa sana. Naomba wananchi tuwe watulivu wakati Serikali Inaendelea kufuatilia jambo hii kwa Kina. Aidha kwa wale ambao tayari wamewekeza waweze kufika kwa RPC wa Mkoa wa Njombe kama ambayo Mheshimiwa RC ameagiza ili kujihakiki majina yao.

Nitoe wito kwa wananchi ambao wanakusudia kuwekeza kusubiri kwanza kuendelea na uwekezaji huu uliopo hadi pale serikali itakapojiridhisha ili kuepusha migogoro au sintofahamu ya aina yoyote inayoweza kujitokeza kwa wananchi.

📍Kazi inaendelea
Picha zinaelezea ziara ya leo nilipoongozana na Kamati ya Ulinzi na Usalama kwenda kufanya ukaguzi wa eneo maarufu lililowekezwa Vanilla wilayani Njombe.
Wewe ni mmoja wa wawekezaji? Au ni kati ya walalamishi wasio wawekezaji! Mbina waliowekeza hawajalalamika.
 
Usikubali kuwekeza popote kama fursa inayotangazwa kampuni haijasajiliwa soko la hisa

Waulize tu mumesajiliwa soko la hisa ili niwekeze hisa zangu?

Wengi wametapeliwa mara sijui wekeza kwenye kuku,vanilla sijui shamba umwaligiliaji rufiji nk usiwekeze kwenye kampuni inayojitangaza tu isiyokuwa soko la hisa .ukisikia wekeza shilingi hizi utavuna mara kumi uliza tu mumesajiliwa soko la hisa? wakisema hapana achana nao
maarifa.
 
Kama kuna kenge mmoja alikuja kunitembelea shambani kwangu nafuga kuku wa mayai akananimbia fuga na sungura ,eti sungura mmoja anauzwa mpaka 60000 na soko lake ni kubwa wakati mimi mwenyewe na utu uzima wangu sijawaai kula sungura ,nikasema inamaana sungura ana bei sawa au zaidi ya mbuzi niakona huu ni utapeli pale tu aliponiambia aniuzie vifaranga vya sungura.
ha haaaa...

ilibaki kidogo na mm niuingie huu mkenge..

ila sasa walinambia sungura mmoja wataniuzia kwa laki 3..then nitawafuga wakizaliana watanitaftia masoko wao wenyewe

hlf mkojo wa sungura dumu la lt 20 nitawauzia kwa 60000

hapo ndo nilichoka nikawaona ni matapeli tu
 
Ujumbe wa DC Njombe kissagwakisakasongwa kuhusu VanillaNjombe

Serikali bado inafanyia kazi maswali mengi yaliyopo katika jamii kutokana na matangazo kwamba Vanilla inalipa na bei ya manunuzi ya Vanilla kwa kilo zinazotajwa kuwa ni kubwa sana. Naomba wananchi tuwe watulivu wakati Serikali Inaendelea kufuatilia jambo hii kwa Kina. Aidha kwa wale ambao tayari wamewekeza waweze kufika kwa RPC wa Mkoa wa Njombe kama ambayo Mheshimiwa RC ameagiza ili kujihakiki majina yao.

Nitoe wito kwa wananchi ambao wanakusudia kuwekeza kusubiri kwanza kuendelea na uwekezaji huu uliopo hadi pale serikali itakapojiridhisha ili kuepusha migogoro au sintofahamu ya aina yoyote inayoweza kujitokeza kwa wananchi.

Kazi inaendelea
Picha zinaelezea ziara ya leo nilipoongozana na Kamati ya Ulinzi na Usalama kwenda kufanya ukaguzi wa eneo maarufu lililowekezwa Vanilla wilayani Njombe.
Hawa ni matapeli. Sisi tuna stock ya zaidi ya tani 20 ya cured vanilla tena nzuri grade AAA na tunauza kwa 310,000 kwa kilo lakini soko halijachangamka.

Hao jamaa wa vanilla village nilishawatafuta sana tuwauzie vanilla zetu kwa 300,000 tu na sio milioni kama wanavyotangaza wakaingia mitini

Kuweni makini sana mtapigwa

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
 
Usikubali kuwekeza popote kama fursa inayotangazwa kampuni haijasajiliwa soko la hisa

Waulize tu mumesajiliwa soko la hisa ili niwekeze hisa zangu?

Wengi wametapeliwa mara sijui wekeza kwenye kuku,vanilla sijui shamba umwaligiliaji rufiji nk usiwekeze kwenye kampuni inayojitangaza tu isiyokuwa soko la hisa .ukisikia wekeza shilingi hizi utavuna mara kumi uliza tu mumesajiliwa soko la hisa? wakisema hapana achana nao
Kama JATU HIVI
 
Mkuu katika soko la mataifa hiyo ndio bei yake ila mpaka ifike huku Ulaya
Mimi binafsi nanunua ya Madagascar Na bei zake ziko juu sana ila kama ukiangalia wanaouza kwenye mitandao ndio bei zake hizo 1m
View attachment 1982729
Bei inaweza fika huko ila si kwa Tanzania. Mie mkulima halisi, vanilla bean mbichi kilo 30,000.00 kilo kumi kufikia zilizokauka 1kilo ili uhuze laki 3 tu
 
Bei inaweza fika huko ila si kwa Tanzania. Mie mkulima halisi, vanilla bean mbichi kilo 30,000.00 kilo kumi kufikia zilizokauka 1kilo ili uhuze laki 3 tu

Laki 3 ni bei ya chini sana mbona
Na unauza kwa bei hiyo ?
Siko la nje hamuangalii au mnauza kwa kukosa wateja au mnaona ni nyingi sana hizo laki 3
Hapo sielewi
 
Usikubali kuwekeza popote kama fursa inayotangazwa kampuni haijasajiliwa soko la hisa

Waulize tu mumesajiliwa soko la hisa ili niwekeze hisa zangu?

Wengi wametapeliwa mara sijui wekeza kwenye kuku,vanilla sijui shamba umwaligiliaji rufiji nk usiwekeze kwenye kampuni inayojitangaza tu isiyokuwa soko la hisa .ukisikia wekeza shilingi hizi utavuna mara kumi uliza tu mumesajiliwa soko la hisa? wakisema hapana achana nao
Vipi kuhusu kampuni ya JATU Plc, iko DSE lakini inaonekana ni ya kitapeli, what's your view?
 
Eti kilo milion moja yaani imekuwa dhahabu au tanzanite

Wabongo wanatapeliwa kirahisi Sana.
Ni kwa sababu ya umaskini uliokithiri watu tunakuwa na mawazo mgando!. Kwa hali ilivyo kwa sasa, mtu ukimtajia pesa akili yote inahamia kwenye mipango ya namna ya kutatua matatizo yanayomzunguka bila kutafakari kama kweli hiyo pesa inaweza kupatikana! Unaambiwa utauza vanila kilo sh 1000000 bila kufikiria zaidi unainject pesa kwenye kilimo. Ukivuna unakuja gundua hata laki 2 hupati kwenye kilo na huna hakika ya soko. In fact matepeli wana take advantage ya njaa zetu kututapeli!
 
Vanilla ni SAwa na opium ya mexico inalindwa na bunduki.
Nilipanga kulima vanilla hata kabla ya promotion.Ila shughuli yake sio rahisi heka 1 moja tu we umasikini kwaheri ila shughuli pevu.
Wakuu mie nina ton 10+ lakini hadi hivi sasa sijajua soko lilipo. Please mwenye kujua soko tujuzane
 
Back
Top Bottom