Killi Music Awards

Killi Music Awards

Huyu Baraka Da prince ana stahili kabisa...Rich mavoko ni wazi kura za nomination hazikutosha ....me mwenyewe nolimsahau kum nominate kwa hiyo ni wazi kabisa alikosa nomination za kutosha!

Ukiangalia hapo utagundua Jide pamoja hakuwa na nyimbo zilizo tamba sana lakini alikuwa na nomination nyingi ndio maana katokeza..lakini nina hakika kazi hipo kuibuka bingwa maana stage ya kutafuta mshindi majudge nao wanakuwa na nguvu wana angalia kama kweli ana stahili...

mkuu ulikuwepo kwenye mchakato nini???
 
Eti hakuna nyimbo ya yamoto band popote pale....na namna madogo walivyokimbiza
 
Mkubwa em jitunzie heshima yako na ufiche ujinga.
Ulikuwapo ktk kundi la wahesabu kura? Hadi useme kuna mtu kura hazkutosha.

Yaani ulivyoandika utadhan ulikuwepo kwenye mchakato wa kuhesabu kura

mkuu ulikuwepo kwenye mchakato nini???

Kama mmekuwa mkifatilia vyema huu mchakato tangu umeanzishwa na utaratibu wake wala msinge shangaa mimi kusema hivyo.
Kwa kuwajuza tuu katika hii hatua huwa wananchi ndio hupendekeza watu au wanamuziki kwa kila kipengele husika na baada ya watu kupendekeza hivyo walio pata kura nyingi ndio hubaki kwenye kipengele husika!
Hivyo basi ukiona jina la msanii husika halipo majibu huwa ni mawili..
Kura zake hazikutosha au hakupendekezwa kabisa...hivyo huitaji kuwa judge kulijua hilo jambo! Tatizo watu hawajui utaratibu na wala hawakuwapendekeza watu wao lakini ndio walalamikaji wa kwanza.
 
Mo music kutokuwepo katika kipengere cha upcoming artist ndio kinafanya niamini hizi tuzo ovyo kabisa na hazina maana dogo mwqka jana wimbo wake umekuwa wimbo wa taifa ukiona kili walivyo vilaza na wapo kuwasikiliza clouds fm wamemuweka dogo kipengele kigumu kweli yupo na kina bella diamond jide unafikilo atachomoa

dogo mbona kapotea? angetoa singo ya pili tungeona sababu ya kumweka hapo
 
Kama mmekuwa mkifatilia vyema huu mchakato tangu umeanzishwa na utaratibu wake wala msinge shangaa mimi kusema hivyo.
Kwa kuwajuza tuu katika hii hatua huwa wananchi ndio hupendekeza watu au wanamuziki kwa kila kipengele husika na baada ya watu kupendekeza hivyo walio pata kura nyingi ndio hubaki kwenye kipengele husika!
Hivyo basi ukiona jina la msanii husika halipo majibu huwa ni mawili..
Kura zake hazikutosha au hakupendekezwa kabisa...hivyo huitaji kuwa judge kulijua hilo jambo! Tatizo watu hawajui utaratibu na wala hawakuwapendekeza watu wao lakini ndio walalamikaji wa kwanza.

Uwazi sifuri kwenye mchakato mzima..wangeweka mfumo ambao uko wazi na kura zilizopigwa zinaonekana hapo nisinge kuuliza hivyo.
 
Mbona nuh ziwanda hayupo? Mie naona yupo fresh bwana mdogo 🙂
 
Uonevu mkubwa kwa YAMOTO BAND na RICH MAVOCO, Upendeleo mkubwa kwa JUX. Hivi Roma amehit na wimbo gani hadi kuingia kwenye mwanahiphop bora wa mwaka? Shilole kasahaulika kabisa, ingawa simpendi ila kafanya vizuri kwa upande wa wanawake.Billnas kawekwa kwenye upcoming artist halafu Mo Music kakosekana? Hivi hawa waandaaji wanapofanya nomination wanakuwa wamekunywa bangi?Nitaendelea.....

Mzee..hizi nomination si wananchi wenyewe ndo wamechagua??
 
Kama mmekuwa mkifatilia vyema huu mchakato tangu umeanzishwa na utaratibu wake wala msinge shangaa mimi kusema hivyo.
Kwa kuwajuza tuu katika hii hatua huwa wananchi ndio hupendekeza watu au wanamuziki kwa kila kipengele husika na baada ya watu kupendekeza hivyo walio pata kura nyingi ndio hubaki kwenye kipengele husika!
Hivyo basi ukiona jina la msanii husika halipo majibu huwa ni mawili..
Kura zake hazikutosha au hakupendekezwa kabisa...hivyo huitaji kuwa judge kulijua hilo jambo! Tatizo watu hawajui utaratibu na wala hawakuwapendekeza watu wao lakini ndio walalamikaji wa kwanza.

Hizo kura sio za wazi kiasi cha kuwaamini kwa 100%. Wakimweka mtu ambaye hajapata kura za kutosha tutajuaje kwa mfano?
 
Kwa kweli nifah hta mm am so not happy kabisa why mavoko? Hata khs yamoto pia mapokeo hayajawa makubwa kiivo km tulivotegemea depend on how nyimbo zao zinavopendwa.its weird!!! Cha muhim tuendelee kupiga kura2
 
Mmmh kila kitu ndomo alichofanya wamekiandalia category? Wizi mtupu!!
 
Huu mwaka wa Ally kiba, natabiri kunyakua tuzo kama mvua.

Upcoming artist hapo Mo music alitakiwa kuwepo,

Video bora ya mwaka Rich Mavoko-Pacha wangu deserved it sema bifu la Adam Juma na Cloudz inaweza ikawa chanzo cha kukosekana kwa Rich kwny hizo nomination.
 
Gospel music ilitakiwa iwepo, ihusishe wale tu wanaotaka kushiriki masuala ya ulokole wa itikadi kali ndiyo unakwamisha mziki wa injili kupata fursa kama hizi, mbona chanel O hadi gospel music category huwa zinakuwepo kwanini siwe kwetu.
 
Umeonaee yan apo kwa Upcoming uyo Beka Wamembeba Kwa Baraka da Prince n sawa ila Mo music naye alitakiwa awepo...Ila uku kwa Nyimbo Bora na Msanii bora + Video Bora Mavoko..Nae Daah..

tatizo basata wanategemea sana kura za raia ili wapate hayo majina. wakati wanatakiwa kufatilia music industry
 
Huu mwaka wa Ally kiba, natabiri kunyakua tuzo kama mvua.

Upcoming artist hapo Mo music alitakiwa kuwepo,

Video bora ya mwaka Rich Mavoko-Pacha wangu deserved it sema bifu la Adam Juma na Cloudz inaweza ikawa chanzo cha kukosekana kwa Rich kwny hizo nomination.

Hamchoki kuwasingizia Cloudz? Ingekuwa tuzo za Cloudz wangemuweka Jide kwenye vipengele vyote hivyo?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom