Kilimo Biashara na kampuni ya Namaingo Business Agency

Hawa kwa hakika ni matapeli, nimeshawakanya watu wengi lakini wakienda ofisini kwao wanalainishwa na kutoa hela, wanajifanya ni wakala mpaka wa brela na wanawafungulisha kampuni wateja wao kwa elfu 45000.Cha kustaajabisha ni kwamba wanawaomba wateja password za email account zao.
 
NAMAINGO chini ya umiliki wa bi UBWA ni utapeli mtupu.Huyu mama alianza na taasisi aliyoipa jina la AMSHA na hatimae aliwatapeli wakulima wengi wa mkoa wa Pwani na mikoa ya kusini katika zao la ufuta.Aliwahadaa wakulima wengi kwamba atawasaidia kupata ardhi na masoko ya zao la ufuta na hatimae aliingia mitini.Kwa ushuhuda zaidi nenda katika wilaya ya Kilwa kwa kuanzia kijiji cha Somanga mpaka Lindi vijijini maeneo ya Kiwalala jimbo la Mtama ulizia wananchi kuhusiana na taasisi ya AMSHA.Baada ya plan yake ya kwanza kufeli amerudi tena na NAMAINGO BUSINESS AGENCY na kuweza kuzishawishi taasi kama PSPF,NHIF,NMB na kuweza kuzishawishi kwa kuwa anakundi kubwa la watu analoliongopea ameamua kulitumia kundi hilo kuliunganisha na hizi taasisi kwa kuwapelekea wateja(wadanganyika)na hatimae kunufaika na hizi taasisi kwa kupata commission na ufadhili wa safari zake katika kupitia shughuli za uhamasishaji.Huyu mama bi UBWA amefika mbali hata na kuweza kuwa karibu na viongozi wakuu wa nchi kama makamu wa rais mama Samia Suluhu na kutumia nafasi hiyo kuonyesha ni jinsi gani taasisi yake ilivyopewa baraka zote na serikali.Huyu ni tapeli na shughuli zake alianzia kama mganga wa kienyeji maeneo ya UKONGA lakini ameweza kulishawishi kundi kundi la watu wakiwemo wasomi kwa kuamini atawakomboa kwa kuwapatia ardhi,biashara na fursa za masoko na hatimae anawatumilia kupiga dili.
 
Ndugu Mingoi, Shukrani sana kwa taarifa uliyoweka bayana. JF Mods kwa nini mnaruhusu haya MATAPELI kufungua nyuzi humu!? Chukueni hatua tafadhali kabla wanaJF hatujalia na kusaga meno.
 
NAMAINGO chini ya umiliki wa bi UBWA ni utapeli mtupu.Huyu mama alianza na taasisi aliyoipa jina la AMSHA na hatimae aliwatapeli wakulima wengi wa mkoa wa Pwani na mikoa ya kusini katika zao la ufuta.Aliwahadaa wakulima wengi kwamba atawasaidia kupata ardhi na masoko ya zao la ufuta na hatimae aliingia mitini.Kwa ushuhuda zaidi nenda katika wilaya ya Kilwa kwa kuanzia kijiji cha Somanga mpaka Lindi vijijini maeneo ya Kiwalala jimbo la Mtama ulizia wananchi kuhusiana na taasisi ya AMSHA.Baada ya plan yake ya kwanza kufeli amerudi tena na NAMAINGO BUSINESS AGENCY na kuweza kuzishawishi taasi kama PSPF,NHIF,NMB na kuweza kuzishawishi kwa kuwa anakundi kubwa la watu analoliongopea ameamua kulitumia kundi hilo kuliunganisha na hizi taasisi kwa kuwapelekea wateja(wadanganyika)na hatimae kunufaika na hizi taasisi kwa kupata commission na ufadhili wa safari zake katika kupitia shughuli za uhamasishaji.Huyu mama bi UBWA amefika mbali hata na kuweza kuwa karibu na viongozi wakuu wa nchi kama makamu wa rais mama Samia Suluhu na kutumia nafasi hiyo kuonyesha ni jinsi gani taasisi yake ilivyopewa baraka zote na serikali.Huyu ni tapeli na shughuli zake alianzia kama mganga wa kienyeji maeneo ya UKONGA lakini ameweza kulishawishi kundi kundi la watu wakiwemo wasomi kwa kuamini atawakomboa kwa kuwapatia ardhi,biashara na fursa za masoko na hatimae anawatumilia kupiga dili.
Hongera mkuu kwa kufichua matapeli kama haya...!
 
Mkuu nimeenda ili uwe mwanachama inakughalimu si chini ya 700,000,
Kilimo cha mnyororo wa thamani hakipo hivyo utoe laki 7 waache utani nahisi uwo ni upatu wa kilimo,na pia ni eneo gani unafanyia na kutoka chanzo kipi cha maji maana sasa hivi pampu zinanyanganywa uchelewi kulaza mtaji ukabaki na deni la bank au saccos ref. kilimo cha vitunguu ekari 200 klm.
 
Mwana jf ,karibu katika fursa kubwa ya kilimo chenye tija. Ni kilimo cha kisasa kijulikanacho kama vijiji biashara, ni chini ya ujio wa kampuni liitwalo Namaingo Bussness Agency ambapo utasaidiwa utaalam pamoja na soko la bidhaa au mavuno yako! Kwa mawasiliano 0769635970
September 30 2016 unazungumzia UJIO wa Namaingo? Mbona ipo muda mrefu sana!

Nasikia stori za Kijiji cha Mbawa zimeota MBAWA, sasa tumetoka CRDB kwenye mkopo wa 100m kwa kila mwanachama na ardhi iliyopimwa hadi NMB kwa mkopo wa 3m kwa kila mwanachama kwa makundi ya wanachama 50 hamsini.

Niseme tu, kuna mzaha mkubwa sana unaendelea hapa. Wakati mnawaita watu kwenye semina, yale mahubiri yenu mkitaja agencies mbali mbali za serikali na muwekezaji mteja toka Japan kuwa atanunua tani za nyama ya kuku, sungura na samaki ni janga. Kama watu wengine waliacha shughuli zao kuwasikiliza na kujiunga kwa ada zinazokaribia 1m, leo mnabadili gia angani na kuleta ngonjera za Sungura peke yake kwa m3, hamuoni kuwa mnafanya mzaha na maisha ya watu?
 
Uzuri wa JF ni kwamba watu wana data za kutosha. Tunashukuru sana waloleta taarifa juu ya uwezekano wa utapeli kuwepo kwenye ishu kama hizi. Licha ya changamoto za ajira na kutaka kutoka kimaisha vijana tusiamini kufanikiwa kirahisi rahisi. Wanasema "Dili likiwa zuri sana kuwa kweli, fikiri mara mbili yaweza kuwa biashara isiyo halali"
 
Mwenye namba ya RC wa Dar angemdokeza hili jambo angalau lichunguzwe na tupate uhakika wa aidha lina ukweli au ndio wavu na sisi ni samaki. Hakuna mtu asiyependa fursa, lakini kama serikali inakaa nyuma na kuachwa isemewe, basi watalaumiwa vijana kila asubuhi na jioni wakati mambo ya maana hayawekwi wazi.

Mi mtu hanipi tu orodha ya taasisi bila walau kamuhtasari kenye baraka za serikali. Nikitapeliwa si ntaugua ugonjwa wa moyo nife bure
 
Mwana jf ,karibu katika fursa kubwa ya kilimo chenye tija. Ni kilimo cha kisasa kijulikanacho kama vijiji biashara, ni chini ya ujio wa kampuni liitwalo Namaingo Bussness Agency ambapo utasaidiwa utaalam pamoja na soko la bidhaa au mavuno yako! Kwa mawasiliano 0769635970
Kwa ujumla kazi ya kuendeleza wakulima mmeshindwa kabisa, mmekalia kuwavuna kidogo walichonacho kupitia malipo ya semina na vipeperushi
 
Mimi niliwahi wafuata hawa watu wakanipa mpaka vipeperushi na muhudumu niliyemkuta alionekana hajajipanga nilipokua namuattack na maswali..ila hata hcho kipeperushi waliniuzia kwa shilingi 1000 na nilianza kuwaamini lakini nilishtushwa nilipoambiwa mrejesho wa faida kwa hesabu zangu za haraka hazipungui milioni 60 yani 60,000,000 na hapo hapo kwa hyo laki saba uliyo toa wanaahidi kukupa hekari nne huko rufiji zenye nyumba na mabanda yaliyojengwa tayari kwa hyo laki7 yako pia kuna mashirika makubwa ya kijamii wanadai wanaubia nayo kama pspf,NHIF, NSSF Kuwa eti ndo wanajenga hzo nyumba wa watu ambao wamesha fanya projection watu 2000 watakao toka kila kaya nikajiulizaaaaaa...nikasema ngoja ipo siku nitaujua ukweli
Safi sana kiongozi kwa maana umewaumbua wahusika. Huo ni utapeli wakipuuzi, tatizo wabongo tunapenda sana vitu vyepesivyepesi ndio maana wanawalizwa wengi, sasa mtu kuelezea biashara yake tuu anavunga, eti apigiwe sim kwa maelezo zaidi,
 
Wana kila haja ya kumuita tapeli kwa sababu anaambiwa aeleze anazunguka zunguka tu. Mara utasikia piga simu, eti tuma meseji, mara hivi mara vile
Puuuuuumbavu
 
Mungu atusaidie..
Nchi hii kila kata INA afisa Kilimo/Mifugo kama unataka ushauri wa Kilimo Mifugo nenda huko watakusaidia
Ahsante
 
duh hawa walishanichosha sana....yaani walianza na sungura....Hola mpaka leo....halafu wakaja na ishu ya mashamba...mpaka leo hadithi hadithi...najuuta kuwaingiza wazee wangu hawaniamin tena!
 
huu ni ulaghai kama utapeli mwingine wowote unaoendelea hapa bongo. Hawa wanaitwa wakulima wa keyboards au kwa jina lingine wauza maneno. watakuambia utoe 100000 tsh ya form wanapiga bla bla nyingi hakuna jipya. wao interest yao no hiyo laki moja ya kingilio. wao wapo ukonga mombasa. jiulize huko kuna Mashamba? Waambie wakuonyeshe Mashamba yao yako wapi ili ukajifunze huko. wakikuonyesha natembea uchi toka kariakoo hadi mbezi. Mtu anaambiwa eleza vizuri anasema piga simu. kueleza si rahisi kwa kuandika hapa kuliko watu elfu moja kupiga simu? Watu wengi wamedanganyika na hawa wauza maneno. Huwezi kuwaongoza watu kwenye kitu ambacho wewe mwenyewe ufanyi. wanakuambia tutakuanzishia shamba. jiulize kwanini wao wasianzishe ya kwao? Hawa na Amsha ni ndugu moja. Wanaongea kama wahubiri wa kilokole waulize maswali sasa ndiyo utachoka. Mimi sina mengi ni hayo tu.
NASHUKURU LEO BAADA YA MUDA MREFU WATU KUIBIWA NA NAMAINGO KWA MIAKA MINGI WAMEJUA SASA KUWA NILICHOSEMA NI KWELI IMEPIGWA MARUFUKU RASMI KWA WIZI WALIOWAFANYIA AKINA MAMA
 
Back
Top Bottom