Kilichonikuta baada ya kupalilia makaburi

Kilichonikuta baada ya kupalilia makaburi

Pole sana mkuu unayoyaongea yana ukweli kiasi chake
Huku uswahilini kwetu kuna nyumba iko karibu na makaburi bila kuvuta bangi hakulaliki
 
Ndiyo maana wazungu wanasema waafrika hatupumziki tukifa bado tunaranda randa
 
Ulianza kulimia makaburi bila hata kusali kwanza!...kuna faida gani kulimia kaburi bila kumuombea aliyelala kaburini?
 
Yaani NYIE NDIO MAJINI WENYEWE MMEZIDI KIWANGO CHA MAPEPO ACCORDING TO STORY
hahahahahahaaaaaaaaa huyo jamaa alienda kwa masharti ya mganga watu wanachimba kaburi usiku kucha na kulala juu ya makaburi mengine lakini hakuna madhara
 
Hata wewe una element za kishirikina mkuu, kwa nini uende kusafisha makaburi saa kumi na mbili jioni na si asubuhi? Sisi tunasafisha makaburi kila mara na hakuna tabu tunayopata.
Bonge la swali hata Mimi nilitaka kuuliza hivyo?
Yaaan makaburin aende saa 12 jion?


Hapo lazima upishane na vibwengo ambao wametoka kwenye mihangaiko Yao?
 
Mkuu Pole sana na mapito yaliyokukuta...

Kabla ya kuanza kulaumu makaburi na maeneo yake kwanza jitafakari mwenyewe kwenye mizunguko yako, kila kitu huwa na chanzo chake.. Huko kwenye biashara zako na maisha yako na mke wako mjichunguze kwanza muangalie kama hakuna matendo mabaya mmeshawahi wafanyia watu, dhulma, uchawi na kitu chochote kibaya...
Pili mkuu angalia historia yako na ukoo wako huko nyuma na uhusiano wa hilo kaburi na wewe, Marehemu aliyelala kwenye hilo ana historia gani kwenye ukoo wenu?...
Kama ni mkristo au muislamu fanya misa au dua ya familia kumuomba MUNGU MUUMBA WA MBINGU NA ARDHI AWAEPUSHE NA LAANA YEYOTE NDANI YA FAMILIA... WAKUMUOMBA HAPO NI MUNGU TU..
 
Pole sana...

Kulia kwa mtoto inawezakana ikawa ni maroroso ya makaburini...

Kupinduka na gari inawezekana ikawa ni ajali kama ajali zingine...

kufilisika nayo ni mipango tu...


cc: mahondaw
 
Mkuu nmekupa like sio kama ninaamini ulichoandika hapa..! Its just ni story nzuri na inafaa kuingizwa kwenye kitabu au kuwa muvi kabisa..!
 
We hayo ni maruwenge yako...kufilisika kwako na usafi wa makaburi wala hakuna mahusiano...

Visa ulivyounganisha ili kuonesha ubaya wa kusafisha makaburi wala havina uhusiano...Wafrika tunasafari ndefu sana ya kupevuka kifikra...

Wakati nasoma nilijua lazima nikutane na para inayohusu mchungaji wa kilokole..

Nilimfuata mchungaji wa kanisa moja moja nikamwelezea mkasa wote,akaniambia ni hatari sana kuweka mazoea na makaburi,mtu anapokufa na kuzikwa,yeye halisi huondoka kabisa duniani na pale kaburini hubaki mwili tu ambao hauna uhai kama jiwe.

Okk....Vipi ulitoa sadaka kiasi gani kwa ajili ya ukombozi...???

Wajinga ndio waliwao....
 
Mkuu kunamtu ananiuliza chanzo cha hip dhahabu hakuna maluweluwe yaliofanyika kabla ikapanda juu..kamandio hill nalo n lango
 
Back
Top Bottom