Samia atosha tukutane2030
JF-Expert Member
- Apr 7, 2020
- 17,169
- 48,681
Utawala wa awamu ya 5 wa Mh. Magufuli ulijaa futuhi, propaganda na ukatili wa kila aina.
Alipambwa na vyombo vyote vya habari kwa hofu kuu. Mpaka wakaiita serikali yake ni serikali ya viwanda ilhali ndiyo serikali iliyoua channel ya ukuaji wa viwanda. Upotevu wa fedha usio wa kawaida ulioonekana kipindi cha Magufuli. CAG bwana Asad alipowadokeza wananchi aliishia kushikiwa mitutu.
Utekaji wa hovyo uliasisiwa kwenye serikali ya MAGUFULI.
LISSU alipigwa mchana kweupe kwakuwa alionekana kumzidi umaarufu Rais .
Wapinzani walikatazwa kukusanyika. Wakafanya mikutano ya ndani na baadaye hata hiyo ya ndani waliishiwa kushikiwa na polisi.
Baada ya kufa Magufuli wapinzani wakaamua watumie utawala wa Rais Samia kama uwanja wa kujinafasi kupoozea machungu ya awamu ya 5.
Kosa alilolifanya Samia ni kuruhusu wapinzani wafanye awamu yake kama kivuli baada ya safari ndefu ya juani.
LISSU alipigwa mchana kweupe ni akina nani walithubutu kuandamana?
Upoteaji wa watu na utekaji awamu ya 5 ni akina nani walithubutu kuandamana?
Hali ngumu ya maisha awamu ya 5 ni akina nani walithubutu kuandamana?
Awamu ya 5 maisha yalikuwa magumu sana kuanzia kwa wananchi mpaka kwa wafanyakazi wa serikali.
Wengi walirudi vijijini lakini ule utawala ulikuwa wa chuma hakuna mtu alipeleka pua barabarani.
Rais Samia usikubali kuwa mnyonge. Yeyote anayetikisa utawala wako mnyooshe.
Alipambwa na vyombo vyote vya habari kwa hofu kuu. Mpaka wakaiita serikali yake ni serikali ya viwanda ilhali ndiyo serikali iliyoua channel ya ukuaji wa viwanda. Upotevu wa fedha usio wa kawaida ulioonekana kipindi cha Magufuli. CAG bwana Asad alipowadokeza wananchi aliishia kushikiwa mitutu.
Utekaji wa hovyo uliasisiwa kwenye serikali ya MAGUFULI.
LISSU alipigwa mchana kweupe kwakuwa alionekana kumzidi umaarufu Rais .
Wapinzani walikatazwa kukusanyika. Wakafanya mikutano ya ndani na baadaye hata hiyo ya ndani waliishiwa kushikiwa na polisi.
Baada ya kufa Magufuli wapinzani wakaamua watumie utawala wa Rais Samia kama uwanja wa kujinafasi kupoozea machungu ya awamu ya 5.
Kosa alilolifanya Samia ni kuruhusu wapinzani wafanye awamu yake kama kivuli baada ya safari ndefu ya juani.
LISSU alipigwa mchana kweupe ni akina nani walithubutu kuandamana?
Upoteaji wa watu na utekaji awamu ya 5 ni akina nani walithubutu kuandamana?
Hali ngumu ya maisha awamu ya 5 ni akina nani walithubutu kuandamana?
Awamu ya 5 maisha yalikuwa magumu sana kuanzia kwa wananchi mpaka kwa wafanyakazi wa serikali.
Wengi walirudi vijijini lakini ule utawala ulikuwa wa chuma hakuna mtu alipeleka pua barabarani.
Rais Samia usikubali kuwa mnyonge. Yeyote anayetikisa utawala wako mnyooshe.