Kilango sasa awageukia akina Slaa

mpaka kieleweke

Washauri wa huyu Mama tafadhali mshaurini kuwa hapa watu hawaangalii ni nani kaleta hoja ama imetoka wapi ,ila la msingi ni kuangalia jinsi ambavyo masilahi ya taifa yanazingatiwa.

Nawashauri pia wamshauri kuwa kitendo cha Dr.Slaa ,kuendelea kusema juu ya haya mambo ni kuweka msisitizo wa kina ili serikali ilete majibu ya kina na sio vinginevyo.

Ashauriwe kuwa hoja sio imeletwa na nani na yeye alipaswa kujua kuwa,Import Support Commodity ,ilianza mwaka 2006 bunge la mwezi April na liliwekwa bungeni na Dr.Slaa ,natafuta Hansard husika na nitaliweka hapa kwa ushahidi.

Mama ashauriwe kuwa sasa jamii inamfuatilia kila jambo ambalo analifanya na kulizungumza hivyo kauli zake zinachukuliwa kwa uzito mkubwa kuliko ilivyokuwa hapo awali, nisingependa huyu na yeye awekwe kwenye kundi la wasanii ........

Naamini kuwa washauri wake watampa ushauri ili aweze kutoa clarification ya alichosema ili aweze kueleweka, we still need her please.

Mkuu Kieleweke,

Hili lako ndio tunaita darasa la elimu ya siasa kwa wananchi, haya ndio maneno ambayo yanaweza kumuelimisha mwananchi, safi sana angalau once for a change.
 
FMES,Mwanakijiji,FMES,Kuhani Mkuu, Fundi Mchundo, jmushi1,....

..alipohojiwa na Mwanakijiji Mama Malecela alikuwa hajui hata tofauti ya Apartheid regime na yanayojiri ktk Tanzania ya leo.

..then a month later anaibukia Bungeni na ku-invoke philosophers like Socrates etc etc. i felt something was not right.

..lakini hata ukirudi kwenye mahojiano yake na Mwanakijiji, pale Mama Malecela anapodai kwamba CCM haina matatizo wenye matatizo ni mafisadi, ni lazima ukubali kwamba huyu Mama Malecela wants to eat her cake and have it.

..the best case scenario ni kwamba hoja ya EPA ni hoja nzito na Mama Malecela has no intellectual and strategic capacities to follow it through. at worst inawezekana Mama Malecela ni msanii tu, mwanasiasa mwenye hoja na mitizamo kama za Tambwe Hiza.

NB:

..nadhani lipitishwe azimio la kumuomba radhi jmushi1 "dogo." basically the kid saw this coming. lakini alipotuonya wengi walimshambulia na kumuita majina

Joka Kuu nashukuru sana kwa ku acknowledge!
Watu kama nyie mnao encourage mnanikumbushia semi mbili...
1)The only thing to fear is fear itself.
2)Courage is not the abscence of fear...But the ability to tell the truth on the face of it.(fear)
 
Mama Kilango msanii tu ana act kama wabunge wetu wengi, tushawazoea kina Mzindakaya, Njelu Kasaka et al ukichunguza hamna integrity wala dedication, ni opportunism tupu. Vibaya zaidi anapigwa remote control na watu wanaotafuta credit.

It is amazing how much can be achieved if everybody will stop looking for credit and actually try to get something done.
 
Mkuu Mushi,

Heshima mbele kaka, CCM inapitia majaribio makuu ya kidemokrasia, ambayo imekuwa ikidai siku zote kuwa inaaamini sana, sasa tunajionea kwa macho kuwa baadhi ya viongozi wetu huwa ni waongo, lakini mkuu kama unaelewwa historia ya mapinduzi na ukombozi wa wananchi, basi utaona kuwa pole pole tunaelekea kunakotakiwa, na ni lazima ianzie na CCM kwanza,

Mafisadi wamefika mwisho sasa, lakini hawezi wakakubalia bila a fight, lakini CCM iko sawa wala haina maneno, maana ilikuwepo kabla ya kina Lowassa na wenzake, lakini maneno yako ni mazito mkuu ninayaweka.

Nashukuru KAMANDA...Niko nyuma YAKO!
Pigania HAKI KAMA KAWA!
 
Kieleweke,
Mkuu umejibu yote niliyotaka kusema... Ni kweli Mama Kilango amenuka!.....duh yaani hizi issue kazileta yeye! wakati zimeanzishwa na Upinzani long time na ndio mazungumzo bungeni... Au kwa sababu Dr. Slaa aliliondoa swala la EPA bungeni ndio imekuwa sababu wakati akijua kuwa lilipigwa vita sana na hao hao viongozi anaowashutumu leo...
Mama Kilango inabidi ajikusanye kisawasawa laa sivyo atakuja jikuta anajibagua mwenyewe...baada ya shutuma zote zile hawezi kujipendekeza tena kujikosha... Hapa ka smell...
 
Mama Kilango msanii tu ana act kama wabunge wetu wengi, tushawazoea kina Mzindakaya, Njelu Kasaka et al ukichunguza hamna integrity wala dedication, ni opportunism tupu. Vibaya zaidi anapigwa remote control na watu wanaotafuta credit.


Kwa kawaida watu wenye tabia fulani, huwa ni wepesi kuwaona watu wenye tabia kama zao, labda una point mkuu maana unaweza kumsaoma kabla hata hajafika mbali, lakini bado haibadili ukweli kuwa ni kiongozi makini na siku akibadilika tu kundi lote limekwisha maana ndiye nguzo ya kundi,

Halafu unajua zikizidi sana zinakuwa ni kelele za mlango badala ya kuelimisha taifa, yaani sour grapes kwi! kwi! wki! naona milijitahidi kujifanya decent kwenye majina flani na English sana lakini mbele ya kumkoma nyani gil;adi sasa kuna mtu ameumbuka inabidi hata majina yale ya decency nayo atemee sumu tu unajua misery siku zote hutafuta sana company!
 
Kwa kawaida watu wenye tabia fulani, huwa ni wepesi kuwaona watu wenye tabia kama zao, labda una point mkuu maana unaweza kumsaoma kabla hata hajafika mbali,

Kwanza unakubali

lakini bado haibadili ukweli kuwa ni kiongozi makini na siku akibadilika tu kundi lote limekwisha maana ndiye nguzo ya kundi,

Halafu unaji contradict mwenyewe, kama kawaida yako, kwa kusema huyu mama ambaye umeshakubali kuwa ni msanii na opportunist eti sasa ni "kiongozi makini" makini katika nini? usanii na opportunism?

Halafu unajua zikizidi sana zinakuwa ni kelele za mlango badala ya kuelimisha taifa, yaani sour grapes kwi! kwi! wki!

Kwa hiyo watu wanaokemea ufisadi wa mafisadi wanaojivisha majoho ya kupigana na ufisadi wanapiga kelele za mlango? Then after saying all that do you really have the nerve kusimama hapa na kupigia kelele ufisadi? Wewe na huyu mama, ambaye ushakubali kwamba ni msanii tu naye, sasa mtakuwa na tofauti gani? Na wewe msanii kama yeye pia?

naona milijitahidi kujifanya decent kwenye majina flani na English sana lakini mbele ya kumkoma nyani gil;adi sasa kuna mtu ameumbuka inabidi hata majina yale ya decency nayo atemee sumu tu unajua misery siku zote hutafuta sana company!

Incomprehensible rumblings as usual, majina flani majina gani? si uyataje.English sana maana yake nini, una inferiority complex za Maimuna? Yaani hapo unavyomalizia hata hueleweki.

Kumkoma Nyani lazima, hata kama nyani mwenyewe anaji camouflage kuwa anapinga ufisadi.Tunamkoma hata yule nyani anayefake kumkoma nyani.

Hizo comments za sour grapes wanasaikolojia wanaziita "projection".Yaani mtu feelings zako wewe mwenyewe unambambikia mtu.Hebu nielezee sour grapes zangu zimetokea wapi? Mimi nilishaeleza sour grapes zako ni za kwenu kuukosa urais, hilo linaeleweka na kila Mtanzania, zangu za nini?
 
Kwa kawaida watu wenye tabia fulani, huwa ni wepesi kuwaona watu wenye tabia kama zao, labda una point mkuu maana unaweza kumsaoma kabla hata hajafika mbali, lakini bado haibadili ukweli kuwa ni kiongozi makini na siku akibadilika tu kundi lote limekwisha maana ndiye nguzo ya kundi,

Halafu unajua zikizidi sana zinakuwa ni kelele za mlango badala ya kuelimisha taifa, yaani sour grapes kwi! kwi! wki! naona milijitahidi kujifanya decent kwenye majina flani na English sana lakini mbele ya kumkoma nyani gil;adi sasa kuna mtu ameumbuka inabidi hata majina yale ya decency nayo atemee sumu tu unajua misery siku zote hutafuta sana company!

FMES,
Tulishakuambia kuwa unampigia huyu mama debe ingawa hatumtaki. Sio tu kuwa ni msanii bali kama nilivyosema hapo awali, anazo sifa za kifisadi na ipo siku atajulikana.

Mama Kilango sio kiongozi makini kama unavyodai, na hatumtegemei kwenye hii vita ya kuondoa mafisadi. Nafuu hata ungesema Dr. Mwakyembe kwa upande wa CCM. Mama Kilango yeye yumo kundi la wasanii.
 
hoja hizi za mapambano dhidi ya ufisadi zinazungumzwa na wabunge wetu kwa niaba ya watanzania wote!ufinyu wa kuelewa na kupenda sifa kwa gharama yoyote ndiyo inafanya wabunge kutaka kuhodhi hoja.kama wote nia yao ni kujenga nyumba moja(nchi,taifa) kwanini hili la kuhodhi hoja(fito) lijitokeze? kwanini wagombanie fito? cheap politicians.hivi jitihada za slaa nani asiyezielewa
 
hoja hizi za mapambano dhidi ya ufisadi zinazungumzwa na wabunge wetu kwa niaba ya watanzania wote!ufinyu wa kuelewa na kupenda sifa kwa gharama yoyote ndiyo inafanya wabunge kutaka kuhodhi hoja.kama wote nia yao ni kujenga nyumba moja(nchi,taifa) kwanini hili la kuhodhi hoja(fito) lijitokeze? kwanini wagombanie fito? cheap politicians.hivi jitihada za slaa nani asiyezielewa


Wewe hujazishtukia distortions za kifisadi? Kuwafanya watu waache kushughulikia mafisadi na waanze kubishana nani alianzisha hoja ya ufisadi.

Utawajua kwa kazi zao, wala si kwa maneno.
 
Huyu mama anachemsha - jamii ilikuwa inammezea kwa vile alionekana kidogo ni tafauti na wabunge wengi wa CCM lakini akiendelea na umimi wake, watu wataanza kuanika sifa zake halisi za mchezo anaoupenda.
 
Mama Kilango, ni mbunge wa CCM anayefanya kazi katika mazingara ya siasa tunayoyaelewa wazi kuwa ni ya namna gani, amesema something one thing ambacho hakina faida kwa kuendeleza shughuli ya kupinga ufisadi, bali kina faida kwa siasa za chama chake, that is politics as usual, binafsi ninaangalia the big picture hapa siwezi kuweka ubinafsi au chuki in the middle ya ishu kubwa ya taifa,

Aliyokwisha yafanya yanajisema yenyewe, sihitaji kuambiwa na mtu, na ninampa the benefit of the doubt kwa sababu ninayajua kwa undani mazingara anyofanyia kazi, ni sawa kwa wasioelewa kuropoka lakini kwa wanaoelewa kwa undani, wanajua kuwa it takes huyu mama kubadilika tu au kuwa mnafiki on this ishu, then umeua the whole ishu in CCM, kwa sababu wale wote wanaohusika wanajua vizuri hilo, kuwa hata kina Mwakyembe, wanatiwa nguvu na na kupewa uabvu na huyu mama, juzi mama anna abdalah aliporusha mawe, hakumrushia Mwakyembe au Sendeka, ila alirusha kwenye kichwa,

Ni haki ya mwananchi kusema anachotaka ndio demokrasia, ambayo bongo bado hatujaikweza ingwa ni rahisi sana kule nje ya taifa letu, watanzania tunajua hii kazi ya kupingana na mafisadi sio rahisi kama wenzetu wwengi wanavyofikiri, na tutaendelea kuwpaa moyo wale wote tunaojua kuwa wanajaribu, hata wakidhihakiwa na kutukanwa sio tatizo kwa sababu bado ni wawakilishi wa wananchi wa majimbo yao, ambako wanawajibika ipasavyo,

Tunajua in the process watatokea wengi wenye maneno ya kukatisha tamaaa, lakini kwa wale tunaojua vizuri tunasema tunaomba mama asije akabadili msimamo kama wengi hapa wanavyoyabiri maana tutaishia kulipia wananchi tena big time,

Mungu amjalie mama na wengine wote ambao wanajaribu kupigana na nguvu za giza katika mazingara magumu ya siasa za kibongo.
 
Mama Kilango, ni mbunge wa CCM anayefanya kazi katika mazingara ya siasa tunayoyaelewa wazi kuwa ni ya namna gani, amesema something one thing ambacho hakina faida kwa kuendeleza shughuli ya kupinga ufisadi, bali kina faida kwa siasa za chama chake, that is politics as usual, binafsi ninaangalia the big picture hapa siwezi kuweka ubinafsi au chuki in the middle ya ishu kubwa ya taifa,

Aliyokwisha yafanya yanajisema yenyewe, sihitaji kuambiwa na mtu, na ninampa the benefit of the doubt kwa sababu ninayajua kwa undani mazingara anyofanyia kazi, ni sawa kwa wasioelewa kuropoka lakini kwa wanaoelewa kwa undani, wanajua kuwa it takes huyu mama kubadilika tu au kuwa mnafiki on this ishu, then umeua the whole ishu in CCM, kwa sababu wale wote wanaohusika wanajua vizuri hilo, kuwa hata kina Mwakyembe, wanatiwa nguvu na na kupewa uabvu na huyu mama, juzi mama anna abdalah aliporusha mawe, hakumrushia Mwakyembe au Sendeka, ila alirusha kwenye kichwa,

Ni haki ya mwananchi kusema anachotaka ndio demokrasia, ambayo bongo bado hatujaikweza ingwa ni rahisi sana kule nje ya taifa letu, watanzania tunajua hii kazi ya kupingana na mafisadi sio rahisi kama wenzetu wwengi wanavyofikiri, na tutaendelea kuwpaa moyo wale wote tunaojua kuwa wanajaribu, hata wakidhihakiwa na kutukanwa sio tatizo kwa sababu bado ni wawakilishi wa wananchi wa majimbo yao, ambako wanawajibika ipasavyo,

Tunajua in the process watatokea wengi wenye maneno ya kukatisha tamaaa, lakini kwa wale tunaojua vizuri tunasema tunaomba mama asije akabadili msimamo kama wengi hapa wanavyoyabiri maana tutaishia kulipia wananchi tena big time,

Mungu amjalie mama na wengine wote ambao wanajaribu kupigana na nguvu za giza katika mazingara magumu ya siasa za kibongo
.

Amen...

Ameni... all the prayers to Mama Kilango Malecela
 
Kuna kitu amiss hapa JF. Kiongozi akisema yale tunayoyataka, sio lazima yawe sahihi, tunamfagilia mpaka tunataka agombee urais. Siku akisema yale ambayo hatutaki kuyasikia, hata kama ndio ukweli wa mambo, tunavimba na kuanza kumrushia kila aina ya majina, mara naye ni fisadi, msanii, n.k. Nani msanii sasa hapa, hao viongozi au sisi? Ama ndio tusema huwa tunakurupuka katika kutoa compliment xetu?

Narudia tena kusema hivi Mama Kilango sio activist wa JF ambaye anaweza akaogelea tu katika kutoa maoni yake pasipo compass yeyote. Huyu ni mwanasiasa anayewajibika to very clear constituencies, including wananchi wake wa Same na chama chake cha CCM. As such, pamoja na kuwaponda wale wanaolitafuna taifa letu, haitarajiwi kwamba angeenda as far as kukiponda chama chake, guys you must be kidding, you have to get the grips of party politics. Who told you party politicians are neutral?

Kwa utaratibu huu CCM wataendelea kuwaliza kila siku na kuwapa msongo wa mawazo. Ifike mahala basi mkubali kwamba nchi yetu kwa sasa imekwama katika swala la uongozi na inahitaji mfumo mpya. Hawa ndugu zetu wa chache akina Kilango, Mwakyembe, etc hawawezi. Tunahitaji chama kingine ili tutoke hapa tulipo. Uchafu uliokwisha kufanyika ndani ya CCM hausafishiki; kila atakayejaribu kusafisha atajichafua yeye na kuwa sehemu ya huo uchafu.
 
Kuna kitu amiss hapa JF. Kiongozi akisema yale tunayoyataka, sio lazima yawe sahihi, tunamfagilia mpaka tunataka agombee urais. Siku akisema yale ambayo hatutaki kuyasikia, hata kama ndio ukweli wa mambo, tunavimba na kuanza kumrushia kila aina ya majina, mara naye ni fisadi, msanii, n.k. Nani msanii sasa hapa, hao viongozi au sisi? Ama ndio tusema huwa tunakurupuka katika kutoa compliment xetu?

Narudia tena kusema hivi Mama Kilango sio activist wa JF ambaye anaweza akaogelea tu katika kutoa maoni yake pasipo compass yeyote. Huyu ni mwanasiasa anayewajibika to very clear constituencies, including wananchi wake wa Same na chama chake cha CCM. As such, pamoja na kuwaponda wale wanaolitafuna taifa letu, haitarajiwi kwamba angeenda as far as kukiponda chama chake, guys you must be kidding, you have to get the grips of party politics. Who told you party politicians are neutral?

Kwa utaratibu huu CCM wataendelea kuwaliza kila siku na kuwapa msongo wa mawazo. Ifike mahala basi mkubali kwamba nchi yetu kwa sasa imekwama katika swala la uongozi na inahitaji mfumo mpya. Hawa ndugu zetu wa chache akina Kilango, Mwakyembe, etc hawawezi. Tunahitaji chama kingine ili tutoke hapa tulipo. Uchafu uliokwisha kufanyika ndani ya CCM hausafishiki; kila atakayejaribu kusafisha atajichafua yeye na kuwa sehemu ya huo uchafu.

Kitila,

I am not interested in party politics.Mimi nataka watu watatue matatizo. Kama party politics zinaingilia utatuzi wa matatizo (kama katika hii bickering ya opposition vs CCM juu ya nani kaanzisha expose ya EPA) kwa nini nikipake?

Wanasiasa hawawezi kuwajibika mpaka wawajibishwe.Non partisan pressure groups na individuals kazi zao ni ku cut through the partisan bs na kusema vitu straight.
 
Kuna kitu amiss hapa JF. Kiongozi akisema yale tunayoyataka, sio lazima yawe sahihi, tunamfagilia mpaka tunataka agombee urais. Siku akisema yale ambayo hatutaki kuyasikia, hata kama ndio ukweli wa mambo, tunavimba na kuanza kumrushia kila aina ya majina, mara naye ni fisadi, msanii, n.k. Nani msanii sasa hapa, hao viongozi au sisi? Ama ndio tusema huwa tunakurupuka katika kutoa compliment xetu?

Narudia tena kusema hivi Mama Kilango sio activist wa JF ambaye anaweza akaogelea tu katika kutoa maoni yake pasipo compass yeyote. Who told you party politicians are neutral?

Kwa utaratibu huu CCM wataendelea kuwaliza kila siku na kuwapa msongo wa mawazo. Ifike mahala basi mkubali kwamba nchi yetu kwa sasa imekwama katika swala la uongozi na inahitaji mfumo mpya. .

Asante kwa kwa hiyo cut hapo juu, mwenye macho haambiwi tazama.

Kupiga kelele ya fedha kurudishwa ilikuwa inamtosha kumpatia umaarufu, kaupata- wadanganyika ndivyo tulivyo. Hata comment yake moja kuhusu kujichanganya kwa mkullo kuhusu EPA sijaisikia - kwake isn't rotten fish smell at all! leave alone mazagazaga kibao yanayoendelea na yeye kunyamaza kimya...........kazuga na wamezugika.
 
Kupiga kelele ya fedha kurudishwa ilikuwa inamtosha kumpatia umaarufu, kaupata... Hata comment yake moja kuhusu kujichanganya kwa mkullo kuhusu EPA sijaisikia - kwake isn't rotten fish smell at all! leave alone mazagazaga kibao yanayoendelea na yeye kunyamaza kimya...........kazuga na wamezugika.

Mama,

Nakubaliana nawe kabisa. Mi nilisema huyu Mama mwenzio msanii huyu, haya!

(Wakati nakunukuu nime redact yale nisiyo kubaliana nayo, ya "ndivyo tulivyo," yenu na Dr. Watson.)
 
Online activism mkuu Kitila ndio inatupa shida na chuki sisizo za msingi, mama kilango sio mbunge wa JF ni mbunge wa CCM, akitaka urais hakatazwi kugombea mradi anataimiza masharti ya CCM, kama wewe ulivyogombea unyekiti wa UV-CCM, kwani kiliharibika nini?

Unajua usanii ni pamoja na kupigana na ukuta, na kuingilia ishu za nchi isiyokuwa yako! ndio zinakuwa kelele za mlango wananchi wamelala ndani! na mama kilango anaendelea na kazi kama kawa!
 
Labda ni mbunge wa CCM lakini lile ni bunge la Tanzania, na watanzania wote, wakiwamo ambao hawafungamani na chama chochote wana haki ya kutoa maoni yao na kukemea pale wanapoona mambo hayaendi sawa.
 
Lakini sio wasiokuwa raia wetu, wanahitaji kuangalia kwa mbali tu maana sisi wa-Tanzania hatuingilii siasa za nchi zao! badala ya kuwatukana matusi ya nguoni wabunge wetu kinamama sio ustaarabu tena kwa walke wanaotaka kueleweka kuwa wamesoma sana!
 
Back
Top Bottom