Kila siku ni 'wasaidizi wake'... KWANINI SIYO KIKWETE mwenyewe?

Tatizo ni watu kama wewe, msioelewa tatizo halisi liko wapi. Rais kama Rais anatekeleza majukumu yake zaidi ya Rais yoyote yule wa kabla yake.

Nyerere alifanya nini cha maana kwa miaka 24 aliyokaa madarakani? kutuwacha masikini wa mwisho duniani!
 
Ni kawaida msipige kelele,Rejeeni hotuba ya Mwl Nyerere 1985 akiwaaga wazee wa jiji la dsm alisema matatizo na mapungufu yote ya utawala wake alikuwa akilaumiwa Kawawa badala ya Mwl,mapungufu ya Mzee mwinyi mwl aliwabebesha malecela na kolimba so huu ni urithi wa baba wa Taifa
 
MMK,
Si kwamba inawezekana Rais ndiye mbovu ila ukweli ni kwamba Rais ndiye mbovu na hafai.
 

Tangu 2006 kuna mengi yametokea kuhusiana na utendaji na uongozi wa Rais Kikwete. Kuna imani ambayo imejengeka kuwa Rais "anashauriwa vibaya" na hivyo huwa anasema au anafanya vitu kwa sababu 'wasaidizi' wake wamemuelekeza vibaya n.k Kuanzia sakata la mapanki na mwitikio wake kuhusu filamu ya Darwin's Nightmare hadi hii ziara ya Marekani kuna vitu vinafanyika na mara zote watu wote hulaumiwa isipokuwa rais mwenyewe.

Tumeona kwenye CCM kama ilivyo kwenye serikali wanalaumiwa watu wengine wote isipokuwa mtu pekee ambaye anastahili kulaumiwa. Mawaziri mara nne wamelaumiwa na wananchi na mara nne ndani ya miaka sita Rais amelazimika kufanya mabadiliko. Lakini mara hizo zote wanalaumiwa ni mawaziri na watendaji isipokuwa mtu pekee mwenye uwezo wa kuwawajibisha.

Sasa itachukua muda gani kwa watu wengine kuelewa na kukubali kuwa tatizo yawezekana ni Rais mwenyewe na namna (manner) ya uongozi wake wa kukaa pembeni (hands off approach)? Yawezekana amekuwa akiachilia vitu vitokee kwa sababu hataki kubeba lawama na hivyo watu wengine kabisa walaumiwe? Kwa mfano la Lowassa analaumiwa Mwakyembe, la mawaziri wanalaumiwa watendaji wa chini, la watu kuwajibishwa wanalaumiwa wabunge n.k? Yeye mwenyewe mara zote anakuwa mtu wa kunung'unika asiyekubali kosa lolote au kuwajibika kwa lolote?

Inawezekana pia ni jitihada ya kumuonesha kuwa ame-delegate power na hivyo haitaji kujishughulisha na mambo hayo yote?


Mwanakijiji@ umeongea kile ambacho wengi huogopa kukitole uvivu kwa woga wa kupata ban. Sidhani kama ban inaweza kutolewa kama mtu anajenga hoja yenye maudhui ya kueleweka bila kumdhalilisha mhusika. Tunajadili hoja na katu hatumjadili mtu.

Kama ulivyosema tatizo ni gogo lililoshikilia matawi. Tunakazana kukata matawi lakini gogo hilo linaendelea kuchipusha matawi mengine. Kama gogo hilo ni la miiba ya michongoma kamwe hata matawi yake yakikatwa hayatachipusha matawi mapya ya mipera, machungwa, mapapai nk, la hasha, yatachipusha michongoma tu.

ANC kwa Madiba kule bongeni waliweza kumweka kitako Rais wao na kumwajibisha kwa kuwa waliona kukata matawi si usitawi wakati gogo hilo litachipusha matawi yale yale na kutoa matunda yaleyale. Hao walifanikiwa kwa kuwa uongozi wa chama umetenganishwa na uongozi wa serikali. Kwetu kofia zote anazo mwenyewe, nani wa kumfunga paka kengele?
 
Tatizo ni watu kama wewe, msioelewa tatizo halisi liko wapi. Rais kama Rais anatekeleza majukumu yake zaidi ya Rais yoyote yule wa kabla yake.

Nyerere alifanya nini cha maana kwa miaka 24 aliyokaa madarakani? kutuwacha masikini wa mwisho duniani!
...unafananisha Rais aliye mfu na aliye hai?
...kama anatekeleza majukumu yake kwanini basi hayatekelezeki wala kuonekana yakitekelezwa na watendaji wake?
...Railway kunanuka, Ports kuchafu, Nishati giza, Miundombinu kumepinda, Makazi kumebomoka, NEC CCM makundi, n.k., n.k... au mpaka afikishe miaka 24 ya uongozi ndiyo tupate tathmini?!
 
...unafananisha Rais aliye mfu na aliye hai?
...kama anatekeleza majukumu yake kwanini basi hayatekelezeki wala kuonekana yakitekelezwa na watendaji wake?
...Railway kunanuka, Ports kuchafu, Nishati giza, Miundombinu kumepinda, Makazi kumebomoka, NEC CCM makundi, n.k., n.k... au mpaka afikishe miaka 24 ya uongozi ndiyo tupate tathmini?!

huyo anaemtaja nyerere kwa sasa,,,sijui kama hiyo 1985 alikuwepo????
 
Inamaana hujui alichokifanya nyerere,,,,
Tatizo ni watu kama wewe, msioelewa tatizo halisi liko wapi. Rais kama Rais anatekeleza majukumu yake zaidi ya Rais yoyote yule wa kabla yake.

Nyerere alifanya nini cha maana kwa miaka 24 aliyokaa madarakani? kutuwacha masikini wa mwisho duniani!

hadi anang'atuka,
 
So kwa kifupi JK ndiye tatizo kubwa, na ndiye chanzo cha hayo mengine (ktk awamu yake hii mbovu kabisa)!

Nilishawahi kusema huko Nyuma kwamba uraisi wa Tanzania ni kazi kubwa zaidi ya Uraisi wa Marekani.
Hii ni kwa sababu institutions nyingi nchini zinafanya kazi chini ya kiwango, na hivyo, kumlazimisha raisi kuwa kiraka kwenye mambo mengi. Otherwise, Raisi JK asiongelemewa na mzigo mkubwa wa kutoa maamuzi, ambayo mengine yanakuwa magumu kwake. Undugu, urafiki, udini ni baadhi ya mambo yanayofanya hizi institutions zisifanye kazi ipasavyo, kwa maana baadhi ya WASAIDIZI wa JK hawana uwezo wa ku deliver.
 
Back
Top Bottom