Fallback
JF-Expert Member
- Aug 12, 2023
- 3,477
- 6,484
Sawa niliisoma story yako ya ex na kupelekewa Moto, shikamoo TaboraMsipotoshe ya wanyamwezi tafadhali.
Mtuachie Tabora yetu kwa amani, kinachowaponza Wanyamwezi ni ukarimu wao tuu.
Mgeni anakirimiwa na mlo ulioandalowa mahsusi, sio kiporo.
Wakati anasubiri chakula kiandaliwe atapewa karanga na asali
Chakula kikiiva ni ugali wa dona kuku wa kienyeji mboga za majani zilizoungwa na karanga (nsansa na nswalu)
Akimaliza kula ataletewa maziwa na matobolwa wakati anamalizia maongezi
Akiwa anaondoka atafungashiwa mahama.
Kama ni mgeni wa kukaa zaidi ya siku tatu, siku ya nne anatoka na wenyeji wake kwenda shamba.
Wanyamwezi ni wakarimu.... Ila wakikasirika utakimbia na tai kichwani.....
Kuna wageni waliolowea Tabora kama wanyamwezi wanawachakachua sana wanyamwezi, (majirani wanaoizunguka tabora... waha, wanyarwanda waliolowea Kahama, wanyiramba na wanyaturu n.k.)
Tabora ni yetu, amani na utulivu ni wetu.