Kikwete to announce stimulus for economy

Kikwete to announce stimulus for economy

Which economy? This is not new, the aid money we have been getting from western countries since we got independence has been stimulus money for our poor economy but they failed to use it wise and some ended on "fisadis".

Before they do that they need to put the list of the companies that will benefit from the package in public so we can go deep on those companies history n there performance

Am sure this money will end up on "dirty companies" just like the EPA money ended on.

My suggestion before the goverment give this money out they should first collect EPA money from the companies mentioned. If they cant do that, then this will be another waste of aid or tax payers money.
 
Last edited:
Hivi bunge limeshirikishwa vipi katika hii bailout plan. Pamoja na kwamba bunge letu ni kama rubber stamp ya serikali, lakini kwenye hili swala naomba mbunge yeyote anayeingia JF atupatie data kidogo. Kwa kuwa tunafahamu madudu yanayofanyika katika awamu ya pili ya viongozi wetu lazima tuchukue tahadhari kubwa na huu mpango - stimulus what ?
the last kicks of a dying horse can be very very deadly.
 
Is this for real or just another clever political prank?

Huwezi ku stimulate an almost non-existent economy, we need to build an economy, then if we ran into a hiccup, we can stimulate it.

Mtu anahitaji a triple bypass surgery wewe unataka kumpa mouth-to-mouth resuscitation. Nyumba inahitaji overhaul maintenance wewe unataka kupaka rangi.

Kazi kuiga tu, Wamarekani na Wachina wametoa stimulus, na sisi tutoe, hatujui hata tuna stimulate nini wakati hata kiwanda cha kutengenezea pini hatuna na tuna import mpaka peremende!

Tusipoangalia the only thing we will "gain" will be inflation.
 
Last edited:
Waliiuza NBC kwa nini pamoja na ushauri mzuri wa MWALIMU?

...NBC ilikuwa joke tuu,hata B/S zake zilikuwa ni majengo mabovu tuu...haikuwa bank ile ni michezo ya kuigiza tuu!
 
Stimulus ni comedy nyingine ya mkwere!
 
Sasa huu mpango wa kupeana pesa kwenye makambuni ya mafisadi halafu wanaibatiza stimulus economies.Kwani wakichota hizo pesa wakawapa wakina mapapa na manyangumi nani atajua kwamba ni wizi ?Kila mmoja atasema ni stimulus kwa hiyo mimi ninawasiwasi na hilo zoezi zima litakalofanywa.
 
- Tanzania wakati mwingine inaudhi kweli, Wamarekani wamefanya mambo ya stimulus package kwa sababu uchumi wao ulikuwa bomba, lakini ukaharibika na matatizo ya bad credit, sasa sisi bongo yametukutia wapi hayo? Lini uchumi wetu uliwahi kuwa bomba sasa eti tunataka kuurekebisha ili urudie tena aaaahhhhgrrrrrr?

- Hapo kuna ka-mchezo ka-EPA kanataka kuchezwa, halafu wananchi tukishituka basi wachezaji wataambiwa warudishe tu serikalini,

Mungu Ibariki Tanzania.

William.
 
heri niziwahi kabla hazijaisha, sasa sisis wenye makampuni ya kilimo (Sio KAGODA)tuliathirika na "credit crunch" tunapataje hiyo stimulus money?
 
Si ajabu hizi hela za "stimulus" zikaishia kwenye mikono ya wachache. Hela zina tolewa watu hamjui zimeenda wapi wala kutumikaje. Huu ni ujanja tu wa wachache kupata cha kula.
 
...'ngozi mpya ngoma ile ile!' ...mabilioni ya Kikwete awamu ya pili!
 
- Tanzania wakati mwingine inaudhi kweli, Wamarekani wamefanya mambo ya stimulus package kwa sababu uchumi wao ulikuwa bomba, lakini ukaharibika na matatizo ya bad credit, sasa sisi bongo yametukutia wapi hayo? Lini uchumi wetu uliwahi kuwa bomba sasa eti tunataka kuurekebisha ili urudie tena aaaahhhhgrrrrrr?

- Hapo kuna ka-mchezo ka-EPA kanataka kuchezwa, halafu wananchi tukishituka basi wachezaji wataambiwa warudishe tu serikalini,

Mungu Ibariki Tanzania.

William.

Mkuu nadhani lugha inayotumika hapa ndio somo zima.. Hili neno BAIL OUT Na STIMULUS limekuwa mbiu ya kiuchumi kila mtu hata maskini ombaomba anatumia siku hizi..

Lakini pamoja na yote haya Tanzania ni lazima itakuwa affected na Depression! hilo wazi kabisa sii leo wala kesho lakini tutakuja ipata itachukua muda kama Hurricane Category 5 ilopitia India tunaweza pata mafuriko yake pwani yetu ambayo ni tosha kabisa kuteketeza vibanda vyetu vya uchumi...kwa sababu hata wakati wa Nyerere mwaka 1982 tulifikiria hilo haliwezi kutukuta kwa sababu ya mfumo wetu wa uchumi chini ya Ujamaa hatukuwa karibu kabisa na hizo biashara walizokuwa wakizungumzia..

Kitu kimoja tu tufahamu ni kwamba mashirika yote ya nje yanayochukua cocontracts nchini ama kuwekeza nchini wamekuwa Bailed out from day one..Tumeona Richmond, TRC, ATC na mashirika mengine mengi tena binafsi yaliyonunua mashirika ya Umma yakitegemea serikali kulipa baadhi ya matumizi makubwa ya mashirika haya tena basi bila serikali kuchukua share kutokana na ongezeko la mtaji huo ndani..Hivyo,bail out ipo siku nyingi tu ila tulikuwa na lugha yetu wenyewe..

Sasa tunapokuja kutazama hali ya Uchumi huu wa sasa nadhani ni muhimu sana kwa rais wetu kuangalia mchango wa vyombo hivyo ktk uchumi wetu, huwezi ku bail Out bank ambayo haitowi mikopo kwa mashrika wala sii kazi ya serikali ku bail out mashirika yanayoanguka kwa sababu kwanza hayapo ktk soko letu la Taifa..Hatufahamu chanzo na sababu ya mashirika au viwanda hivi kuanguka..Na muhimu zaidi hatujawahi kuliweka kitimoto hata shirika moja kutazama uzembe unatoka wapi.
.
Tusipoangalia tunafanya nini tutarudi kule kule alipoangukia Nyerere..swala halikuwa soko pekee, bali uzalishaji wenyewe ulipungua kiasi kwamba viwanda vingi vilizalisha chini ya kiwango chake na uzembe ulitokana na sisi wenyewe wananchi..Tunajua sote tumefanya kazi wakati wa mwalimu. Mtu anaamua lunchtime ya masaa mawili, Break hazina hesabu kwenda kununua mboga au kukutana na mshakaji alokuja mtembelea ofisini.. Gari la serikali unalitumia kwenda jirusha, kwa siku mtu anakaa kazini masaa matano, nayule aliyekaa siku nzima kazalisha kazi ya masaa mawili wakati mshahara haubadiliki kulingana na uzalishaji..Kweli mkuu tungeweza kupona?..
Hapo hata wahisani walishindwa kuingia fedha yao kwani mikopo wanayoitoa ilikuwa inatazama possibility za kurudisha fedha yao na hata Bail Out inatakiwa kutazama uwezekano mkubwa wa kuzalisha na ku supply kulingana na demand inayotegemewa..

Nchi zote za kijamaa zilizalisha mali kulingana na mahitaji yao wao wenyewe, horticultural products ni zile tulizoachwa na soko la mkoloni miaka 50 iliyopita. Vitu kama Pamba, Kahawa na Katani ni mazao ambayo kwa miaka zaidi ya 70 yametupa kula tu, yameshindwa kukuza uchumi wetu wala hakuna nchi dunaini inategemea mazao haya tena..Tunaposema kilimo ni pamoja na mbinu mpya, mazao mapya kwa kuzingatia soko na wapi dunia ya kesho itategemea kutoka ktk kilimo..Huko ndiko unakowekesha nguvu na mtaji wako..

Katika mahojiano ya JK na CNN niliposikia Kikwete akizungumzia Pamba na anguko la bei duniani akasema anataka ku stimulate zao hilo nilishtuka sana kwa sababu amesema sababu ni bei kushuka kisha wewe ndio kwanza unaingiza fedha yako mahala ambapo demand yake imeshuka na sii swala la kwamba tumeshindwa kukidhi demand ya mali hiyo kutokana na hali mbaya ya wakulima ktk mtaji..hapo si tunapika chakula wakati hakuna walaji jamani?.

Kwa hiyo unaongeza ajira au fedha kwa mkulima ambaye anajua mali yake haina soko...tunafanya kitu gani hapa! Kisha basi kibaya zaidi ni kwamba hizo bank hazikopeshi wakulima nazo zinakuwa bailed out na hapo hapo it's only less than 20% ya Watanzania wafanya biahsra hupata mikopo ya Banks hizi...Hiuzi hizi banksa zilikataa kuwakoppesha wananchi kwa sababu hawana creditline wakati wa mabillioni ya Saccos... leo kimebadilika kitu gani..Na kibaya zaidi ya yote ni kwamba mabillioni ya fedha za Banks zatu ziko mikononi mwa watu wanaokataa kulipa hadi wafikishwe mahakamani..Billions of dollar zimechukuliwa kwa mtindo wa uhisani yaani unachukua mkopo lakini kulipa ni hadi siku utakayopenda!..

Ni hatari kubwa, kuna hatari kubwa sana ya kupoteza mabillioni mengine kwa sababu maneno mawili hapa yanatumika.. Stimulus na Bail Out..haya ni maswala mawili mazito sana kiuchumi na yanatofautiana sana ktk utekelezaji wake na hasa ktk kupanga vipaumbele..

Kama kikwete ataweza kunambia mafanikio ya yale mabillioni aliyogawa SACCOS zimeweza vipi kukuza uchumi wetu ama hali ya wananchi, laa sivyo sidhani kama kuna haja ya kutoa mabillioni mengine kwa njia sawa na zile zilizotumika ktk kugawa yale mabillioni...Kwa sababu yale mabillioni ni sawa na zawadi toka kwa ndugu au rafiki aliyerudi toka Ulaya..Ni utamaduni wa kumpa mwenye njaa samaki badala ya kumfundisha kuvua samaki..
 
hapa sidhani kama wamefanya utafiti wa kueleweka kwanza kabla ya kusema wana bail out banks!
hivi banks za Tanzania kweli zinahusika moja kwa moja kwa uchumi wa watu? wakulima wangapi wanapata mikopo benki? .....wafanya biashara wangapi nao wanatumia mikopo?
 
Mimi nadhani mkakati huu unatengeneza time-bomb ambayo italiingiza Taifa kwenye matatizo makubwa ya madeni siku za usoni.

Nadhani pia kuwa serikali ya wakati huu inaona njia hii itaisaidia kuwa popular kwa wananchi wake bila kujali madhara yatakayowapata wananchi hao watakapotakiwa kulipa mkopo huo wa IMF na wakati huo huo mafanikio ya mkopo wenyewe yakiwa hafifu sana (kama walau yatakuwepo).

Ingefaa zaidi kwa serikali kuwekeza pesa hizi katika miradi inayolipa. Miradi ambayo itahakikisha pesa hizi zinabaki kwua salama na zinaongezeka kwa kadiri inavyowezekana. Njia moja ya uwekezaji huo ni ufufuaji wa viwanda vya mazao ya kilimo.

Ili kumuokoa mkulima wa pamba, ni lazima utengeneze soko la mazao yake. Na soko la mazao ya pamba ni viwanda vya nguo. Serikali inatakiwa fufue walau viwanda vichache vya nguo kwa nia ya kukuza uchumi na pia kutengeneza soko kubwa zaidi ya mazao ya pamba. Kugawa pesa kwa wakulima wa pamba hakutamaliza tatizo walilonalo wakulima wa zao hilo. Kwakuwa watakutana na tatizo hilo tena msimu ujao watakapotaka kuuza pamba yao tena. Hakuna uwezekano wa serikali yetu kubadilisha bei ya pamba duniani, hata ikipata pesa nyingi kiasi gani. Jitihada za kuokoa mazao ya kilimo ni lazima ziwe na ndani.

Ili kutumia vizuri pesa za mikopo kama hizi, serikali inatakiwa iwe makini sana na uwekezaji wa pesa hizo. Kusema ita-bail out kampuni bila kuwa na tathmini za aina ya kampuni na kiwango ambacho kampuni hizo zinahitaji kuwa bailed out ni kupotoka kwa awali ambako kutapelekea matumizi mabaya ya pesa hizo. Pesa hizo ni vyema zikatumika kuongeza pato la Taifa bila kubahatisha.

La sivyo nchi itateseka sana na madeni makubwa inayojiingizia.
 
Mimi nadhani mkakati huu unatengeneza time-bomb ambayo italiingiza Taifa kwenye matatizo makubwa ya madeni siku za usoni.

Nadhani pia kuwa serikali ya wakati huu inaona njia hii itaisaidia kuwa popular kwa wananchi wake bila kujali madhara yatakayowapata wananchi hao watakapotakiwa kulipa mkopo huo wa IMF na wakati huo huo mafanikio ya mkopo wenyewe yakiwa hafifu sana (kama walau yatakuwepo).

Ingefaa zaidi kwa serikali kuwekeza pesa hizi katika miradi inayolipa. Miradi ambayo itahakikisha pesa hizi zinabaki kwua salama na zinaongezeka kwa kadiri inavyowezekana. Njia moja ya uwekezaji huo ni ufufuaji wa viwanda vya mazao ya kilimo.

Ili kumuokoa mkulima wa pamba, ni lazima utengeneze soko la mazao yake. Na soko la mazao ya pamba ni viwanda vya nguo. Serikali inatakiwa fufue walau viwanda vichache vya nguo kwa nia ya kukuza uchumi na pia kutengeneza soko kubwa zaidi ya mazao ya pamba. Kugawa pesa kwa wakulima wa pamba hakutamaliza tatizo walilonalo wakulima wa zao hilo. Kwakuwa watakutana na tatizo hilo tena msimu ujao watakapotaka kuuza pamba yao tena. Hakuna uwezekano wa serikali yetu kubadilisha bei ya pamba duniani, hata ikipata pesa nyingi kiasi gani. Jitihada za kuokoa mazao ya kilimo ni lazima ziwe na ndani.

Ili kutumia vizuri pesa za mikopo kama hizi, serikali inatakiwa iwe makini sana na uwekezaji wa pesa hizo. Kusema ita-bail out kampuni bila kuwa na tathmini za aina ya kampuni na kiwango ambacho kampuni hizo zinahitaji kuwa bailed out ni kupotoka kwa awali ambako kutapelekea matumizi mabaya ya pesa hizo. Pesa hizo ni vyema zikatumika kuongeza pato la Taifa bila kubahatisha.

La sivyo nchi itateseka sana na madeni makubwa inayojiingizia.

100% nakuunga mkono hapo tatizo ni kwamba awajali kulipa wanataka kuchukua tu hiyo mikopo na hiyo hela hawajui wa invest vipi, viwanda vyao vinakufa, miradi mibovu, wawekezaji wenye nia ya kuifilisi nchi na viongozi wenye kufikiria mbinu za kujilisha, watu wanapiga kelele lakini awajui irekebishwe vipi wala tuombe nini Yaani your 100% on the ideology in terms of what the government needs to look at.

Mungu Ibariki Tanznania
 

"The stimulus plan will target companies-mainly banks - to help them sustain their operations for a period of between six months and two years,"the minister said.
Kuiga kunya kwa tembo.

Kikwete katangaza CNN International hata wiki haijapita kwamba mabenki ya Tanzania hayajaathirika kwa sababu yalikuwa hayajafungamana na mfumo wa benki za dunia, akasisitiza kwamba Citi Bank Tanzania na Citi Bank America hali zao tofauti. Sasa hapa tena wanalenga mabenki kwenye hii ``stimulus.`` Kuiga iga tu.
 
Recta,
Ili kumuokoa mkulima wa pamba, ni lazima utengeneze soko la mazao yake. Na soko la mazao ya pamba ni viwanda vya nguo. Serikali inatakiwa fufue walau viwanda vichache vya nguo kwa nia ya kukuza uchumi na pia kutengeneza soko kubwa zaidi ya mazao ya pamba. Kugawa pesa kwa wakulima wa pamba hakutamaliza tatizo walilonalo wakulima wa zao hilo. Kwakuwa watakutana na tatizo hilo tena msimu ujao watakapotaka kuuza pamba yao tena

Mkuu haya ndio mawazo endelevu..shukran sana kwa mchango huo wenye nguvu haswa!

Hatuwezi kuinua uchumi wa nchi kwa kuendelea kufikiria kulima na kuuza mali ghafi.. mtindo huo umekwisha miaka kibao iliyopita.. Hata Vietnam hawafanyi hivyo tena,..kama unalima Pamba unatengeneza nyuzi zake au vitambaa vya nguo ambavyo market yake ipo nje ya soko la mali ghafi..

Kahawa inatakiwa viwanda vyetu vitafute mbinu mpya za kuingia Ubia na mashirika makubwa ya usambazaji au uuzaji duniani.. halafu sii kazi hivyo basi, ukiwataka Tim Hortons unawapa mkataba wa kununua mazao ya wakulima na wanatengeneza kahawa nchini kama wanavyofanya huko Chile..mashamba bado ni mali ya wananhi. Kuna mazao ya chakula ambayo leo hii ni fedha tupu. Mchele wa Bismati (Pishori) una soko kubwa dunia nzima.. huna haja ya kutafuta soko..Ngano, Aloe Vera, kisha basi mifugo kama ng'ombe na mbuzi vyote hivi vina soko kubwa nchi za kiarabu..kinachotakiwa ni kuwapa sample ya mali yetu lakini kwa akili ya maskini unampa mwarabu kibali cha kuwinda! Gademu.. mwarabu anaondoka na nyama za ng'ombe na mbuzi bila wewe kujua..yeye ndiye anakuwa mfanyabiashara..

Zaidi ya hapo unafanya kama Wachina.. Hawa jamaa baada ya kugundua ugumu wa kuingia soko la nchi za nje badala ya kuuza mali zao sokoni walikwenda wenyewe nchi za Ugenini wakafungua biashara zinazoagiza mali zao.. Kila mahala duniani utaona wanaanzisha Chinatown lakini ndani ya hiyo miji kuna siri kubwa ya kuingiza mali zao madukani..Wao wanakuwa Importer na Expoter wa mali zao wenyewe..wanaiba hadi technologia za nje ktk kuimarisha mali zao yaani nchi inakuwa mafia kwa lengo moja kubwa kuendelea. Leo Tanzania tunashindwa kuwatumia Diaspora kwa sababu tu ya Uraia..toka Mkapa kaahidi watu leo miaka mingapi..Roho ya kimaskini ndio tatizo, utawasikia ati Wananchi wanatakiwa kuelimishwa, wakati hata siku moja sijaona serikali ikifanya kazi hiyo for the last 15 yrs..

Hizi Bail Out na sijui stimulus kwa nchi kama zetu, nchi isiyokuwa na malengo wala initiative ni Ufisadi mtupu..

Jenga upya reli ya kati, jenga Bandari mpya, jenga highway kubwa na pana nje ya makazi ya watu utaona miji ikipanuka na kujengwa..Rudisha viwanda ktk kila zao tunalolima tutaona mafanikio ya kilimo na sii utamaduni uliopitwa na wakati..

Tazama samaki sangara tu ilivyoweza kubadilisha uchumi wetu baada ya kuwa na viwanda vyake!..nakumbuka mauzo yake nchi za Ulaya sii chini ya 200/m Euro kwa mwaka..tena basi hapo bado tunaouza kwa jumuiya ya nchi za EU wakati nikienda dukani ktk sehemu ya samaki wakavu nazikuta zimewekwa lebel ya kiwanda cha Belgium au Netherland..

Prawns, Lobster zote zinavuliwa na mashirika ya nje tena meli zinaingia hadi maeneo yetu tumeshidwa kuzalisha samaki hawa na kuwasafirisha nje hata iwe South Afrika tu soko ni zuri sana..Haya tazama korosho ati zinatoka India wakati sisi ndio supplier wao wakubwa..Yaani korosho zinazotakiwa kukobolewa na kuchomwa tu ni technologia inayotakiwa kwenda nje India..ili ipate kuuzika.

Nilipokuwa Switzeland mwaka 1992 niliona ndizi mbivu kutoka Somalia zikiuzwa madukani.. Somalia kama exporter wakubwa wa nyama za mbuzi na ng'ombe Arabuni.. jamani hata hawa walitushinda kufikria..Binafsi sijawahi kuona kitu madukani made in Tanzania.. sijawahi!..

Hivyo,Tunaweza kabisa ku penetrate nchi hizi tukauza mali zetu badala ya kuuza mali ghafi kila siku kisha, kuwazidi akili hawa jamaa ni jambo linalowezekana lakini kwa akili naroho ya maskini siku zote solution ni kwenda msikitini/kanisani kuomba tena basi tunavyojua siku nzuri ni zipi huwezi amini..
 
Back
Top Bottom