Kikwete safarini TENA!

Kikwete safarini TENA!

mwache ale raha bana maana mda wake wa kuteseka unakaribia... a.k.a 2015
 
"Nimeewaagiza wanaoratibu safari zangu (Rais) waangalie namna ya kuzipunguza na kuacha zenye tija kwa taifa" Jakaya Mrisho Kikwete.
 
Akimaliza huku apitie hapa USA July 4 tunasherehekea America Day. Karibu sana mheshimiwa dakta rais.
 
Hamwezi jua pengine ameshaanza mapema kutafuta pa kukimbilia baada ya 2015 ndio maana anasafiri sana sehemu mbalimbali duniani kutafuta sehemu salama kukimbilia
 
Vasco Dagama kama kawa! aende tu ila kuna siku atapinduliwa na kubaki hana chake hapa tz! DHAIFU President!
 
Alisema mwenyewe kwa mdomo wake "ukitaka kula lazima nawe uliwe" nadhani sasa ni zamu yake kuliwa. Anaenda kuliwa huko Canada.
 
Majukumu mazito ya mtukufu mpendwa baba Rais wetu hodari, shupavu, mkakamavu, msikivu, kipenzi cha watu na mcheshi: safari, misiba, sherehe na matamasha mbalimbali
CCM hoyeeeeee!!
 
Hivi kule Canada nako huwa tunayo Balozi anayewakilisha nchi yetu huko??
 
Hii safari inatusaidia nini wanachi wa Tanzania? kwa nini anatumia fedha ya kodi zetu vibaya? Inabidi awe makini sana na ashughulikie matatizo ya nchi yake kwani hizi safari za kwenda kwa wenzio wasio kuwa namigomo na yeye anaacha migomo hayaleti picha nzuri, na imekuwa ndo tabia yake kuyakimbia matatizo na anasahau akirudi atayakuta yanamsubiri tu. Na kwa nini hajifunzi huyu? kweli ana udhaifu ambao siyo wa kawaida
 
Huyu jamaa ni kweli sio kiongozi. Hapa akiondoka anadhihirisha kuwa anakimbia matatizo. Hana ubavu wa kukaa na wahusika na kutoa maamuzi kama president hivyo anatumia mbinu ya kukimbia ili awabebeshe mzigo wasaidizi wake.
 
Ni nafasi nzuri kwa waziri mkuu kuwaambia madaktari kwamba wasubiri jk arudi safari matatizo yao yote yatakwisha, au subirini rais atue canada nitampigia simu!!!!
 
chezea mswahili kiguu na njia kila siku ...anaacha msiba anakimbilia sherehe...raha sana hii nchi
 
Back
Top Bottom