Kikwete: Lowassa ndiye mhusika wa Richmond

Kikwete: Lowassa ndiye mhusika wa Richmond

Status
Not open for further replies.
Kwahiyo inatuhusu nini??

Ampeleke mahakamani.

Ampeleke mahakamani ili awasukumie kesi makatibu aliowalazimisha kuunda kamati kisa? Ndiyo maana alipigwa chini. Huyo mtu ni mjanja mno alitumia kiti chake ku shift burden kwa makatibu wakuu hivyo si ajabu mahakamani akachomoka na akaendelea kuaminiwa kumbe ni town boy tu.

Hivi kwa nini yeye naye asimpeleke JK mahakamani au hao makatibu wake? Kwa nini hadi yeye tu ndiyo apelekwe huko mahakamani? Mahakama ya ccm ni kumvua tu uboss
 
nashangaaa kama mafuli kumbe baada ya miaka nane ndo anajulikana wa richmond samahani tuambie na wengine wa ESCROW na hatua ya kujiuzuru siyo hatua ya kisheria ila ni utaratibu ili hatua za kisheria zichukuliwe poooooo sisiema maguli usiige huu usanii endapo utapenya kwenye tundula sindano!
 
Tuache porojo ileciku tulioisubiri kwa hamu,kwa ajili ya Tanzania mpya itakayoundwa na lowasa ni kesho.tumpe kura zote za ndiyo
 
alimkataza msabaha asitoe hela sasa richmond nini kiliibiwa?
 
v dagama ni mzuri wa sura ko akidanganya atashangiliwa tuu kilingana na natharia ya lugha ya ya vitendo yaani body language
 
Mbona huyo EL hawampeleki kwa Pilato kama kweli alihusika na Richmond..Otherwise ntaendelea kuamini kuamini EL hahusiki!

kama mhimili mmoja yaani bunge lilimhukumu,,,inawezekana mahakama nayo ikaingilia kumuhukumu kwa mara ya pili?
 
Yeye ameeleza mafanikio ya serikali yake!? Amejibu vipi lawama za Magufuli kwa serikali yake!?
 
Bora kikwete umesema ukweli na huo utakuweka huru siku zote
 
lowassa jembe..MUNGU aendelee kukupa uvumilivu hata baada ya matokeo. maana nguvu iliyo tumika kukushambulia ni kubwa na haija kukatisha tamaa.wamesahau hata kuelezea njia za kuboresha maisha ya watanzania yaani kila anayepewa nafasi ya kuongea kwenye jukwaa lao atataka kuonesha UFUNDI wa kukusema vibaya.

mohammadd ali amewahi sema hivi. 'CHAMPIONS HAVE LAST MINUTES STAMINA'
 
watu humu wamejaa vilaza kweli eti kwanini hakusema ,aseme nini wakati tangu awali kuanzia bungeni inafahamika lowasa ndo mhusika wa richmond naalijiuzulu,,,,sasa mlitaka aseme yeye ili iweje,wakati bunge lilisema na akawajibika?

kwa hatua hii tungekuwa na bunge makini jk alipaswa kufukuzwa kazi na bunge...
 
Kikwete aweka wazi kuwa waziri mkuu kipindi hicho ndio muhusika mkuu kwenye Richmond, baraza la mawaziri pamoja na yeye walihusika nawalikubaliana kuwa kuna upungufu wa umeme na mitamboikanunuliwe lakini hakuhusika kampuni gani ya kwenda kuleta hiyo mitambo .

Alisisitiza sheria za manunuzi zifuatwe lakini waziri mkuu wa wakati huo hakufata na aliunda tume ya manunuzi ya kwake mwenyewe .

Haina haja Tena hiyo, mwenyewe ameshuhudia kwamba wananchi wanaujua ukweli wa swala hilo na ndio maana wamethibitisha hivyo kwa mafuriko ya Lowassa. Hatudanganyiki, tutamchagua tu!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom