Kikwete anamuogopa Andrew Chenge?

Kikwete anamuogopa Andrew Chenge?

Watu hawataki kulipa kodi,maendeleo wanayataka,nchi zingine hata tv uliyonayo ndani unaikatia leseni.

Siyo kusema watu hawataki kulipa kodi,sisi Watanzania hatupingi kulipa kodi ila shida ni wapi hizo hela zinakwenda?Tungekuwa tunalipa kodi halafu tunaambiwa kuwa ile kodi ya kusuka rasta kwa mfano tuliyoipitisha mwaka jana mwaka huu tumepanua uwanja wa ndege wa JNIA na tumejenga terminal 3 hapo hakuna hata mtu ambae angekataa kulipa kodi mpaka ya ving'amuzi vya startime tungelipia.Lakini ujinga wa nchi hii tunalipa kodi mpaka za wototo wetu walioko bado viunoni mwetu ila hatujui inafanya nini hasa
 
Ukitazama jinsi Chenge anavyo waudhi wananchi hadi kuichukia serikali
unajiuliza why anaogopwa namna hiii

Kikwete hawawezi kumfanya lolote huyu Chenge?

Kwanza watu walilamika asiwekwe kwenye baraza la mawaziri
Kikwete akamuweka mwisho Chenge bila woga wala haya akaliuza shirika la reli kwa
wawekezaji vimeo wa kutoka India na kila mtu anajua kilichotokea hadi mwisho serikali
imelirudisha shirika hilo kwa umma....

halafu Chenge akaenda kufanya fitina akateuliwa Mwenyekiti wa Kamati bungeni bila kupigiwa kura
yaani ni uteuzi tu wa Spika kinyume na taratibu na sasa anatumia huo uenyekiti kuzalisha kero mpya

za kila mara kwa Watanzania...hasa kupandisha kodi zisizo na kichwa wala miguu
mfani hii kodi ya simcard licha ya mawaziri wa Kikwete kama January Makamba kuipinga
Chenge ameilazimisha iwepo na mwaka huu anairudisha tena na kodi zingine kupandisha,,,

swali la kujiuliza ni kwa nini huyu mtu Chenge anaogopwa ndani ya CCM hadi na mawaziri na Kikwete pia?

why is Chenge still powerful ndani ya CCM? why Kikwete anamuogopa?

Chenge anajua ni jinsi gani Kikwete akiwa waziri wa nishati na madini alivyojinufaisha na mkataba wa iptl.
 
..ukitaka kujua nchi hii ilivyooza katika mihimili yake mitatu yaani: bunge,mahakama, na serikali...basi chukua mfano (scenario) mmoja tu unaomhusu fisadi chenge: kwanza Chenge anaendasha gari alafu anaua raia wawili...tena akiwa hana leseni wala bima....adhabu yake analipishwa faini ya laki 7.....Lakini Deus Mallya anaendesha gari pia bila leseni alafu anaua raia mmoja....yeye anapata adhabu ya miaka miwili jela (huu uozo wa mahakama zetu)....

....Chenge huyu huyu akiwa mwanasheria mkuu wa TZ anasimamia wizi wa fedha za ununuzi wa rada .....fedha zinarudishwa na UK na Chenge anaonekana kutajwa kuhusika na wizi huu...yeye anasema ana vijisenti tu...raia wanapiga kelele kwa fisadi hili...lakini serikali ya TZ (chini ya JK)inamwachia chenge.....pamoja na kutajana kuvuana magamba huko ccm (huu ni uozo usio na maelezo kwa muhimili wa serikali)......

....Twende bungeni.....kule bungeni Chenge ...pamoja na kujulikana kuwa gamba kuu huko ccm...na pamoja na kashfa ya rada.....lakini anachaguliwa na spika kusimamia kamati yetu ya bajeti...huku wabunge wakiona hilo sawa tu....Huu ni muozo wa kupitiliza wa muhimili wa bunge....Tena hao hao ccm na wabunge wao wakampa chenge hadi kazi ya kuwaandikia katiba yao mbadala wanayoipigania bungeni....wao wanaona sawa tu....

....Kwa scenario hii inayomhusu mtu mmoja tu...unaweza kuona taifa hili lilivyooza kimaadili na kiutendaji kwa watawala wetu wa leo......Sasa tujiulize taifa hili lina wakina chenge wangapi??....wanaohifadhiwa na mihimili hii mitatu kwa mtindo huu???.....tafakari...
 
BBC wants you to pay TV
licence fee even if you
don’t own a set, as shows
go on iPlayer for longer
Lord Hall, the BBC’s director-
general, wants to extend the
£145.50 annual fee in response
to the growing popularity of
iPlayer
Picture: GEOFF PUGH
Twitter Facebook Share
BBC’s director-general looks to
extend the £145.50 annual TV
licence fee in response to
iPlayer's growing popularity
Householders could be required
to pay the television licence fee
even if they do not own a
television, under proposals being
discussed by the BBC.
Lord Hall, the BBC’s director-
general, wants to extend the
£145.50 annual fee in response
to the growing popularity of
iPlayer, which enables viewers to
watch programmes on home
computers, mobile phones and
tablet devices.

Umeelewa kilichoandikwa sio umekurupuka eti kuna nchi wanalipia leseni ukiwa nayo TV,lielewe bandiko lako.
 
Kutegemea kupata mapato kutoka kwenye kodi za pombe ni kukosa ubunifu; ikitokea hao wanywaji wanaamua kuwa waislam safi na kuacha kugida serikali itapata wapi mapato? Kumbukeni ukimkamua sana ng'ombe mwishowe hatatoa maziwa bali damu!!!

Tena sisi tunasema kodi za sigara na pombe ziongezwe kwa 500%.

Itakuwa safi sana. Ajali zitapunguwa sana barabarani.
 
Ukitazama jinsi Chenge anavyo waudhi wananchi hadi kuichukia serikali
unajiuliza why anaogopwa namna hiii

Kikwete hawawezi kumfanya lolote huyu Chenge?

Kwanza watu walilamika asiwekwe kwenye baraza la mawaziri
Kikwete akamuweka mwisho Chenge bila woga wala haya akaliuza shirika la reli kwa
wawekezaji vimeo wa kutoka India na kila mtu anajua kilichotokea hadi mwisho serikali
imelirudisha shirika hilo kwa umma....

halafu Chenge akaenda kufanya fitina akateuliwa Mwenyekiti wa Kamati bungeni bila kupigiwa kura
yaani ni uteuzi tu wa Spika kinyume na taratibu na sasa anatumia huo uenyekiti kuzalisha kero mpya

za kila mara kwa Watanzania...hasa kupandisha kodi zisizo na kichwa wala miguu
mfani hii kodi ya simcard licha ya mawaziri wa Kikwete kama January Makamba kuipinga
Chenge ameilazimisha iwepo na mwaka huu anairudisha tena na kodi zingine kupandisha,,,

swali la kujiuliza ni kwa nini huyu mtu Chenge anaogopwa ndani ya CCM hadi na mawaziri na Kikwete pia?

why is Chenge still powerful ndani ya CCM? why Kikwete anamuogopa?

Ni zaidi ya kuogopwa. huyu mtu ni kama Mungu mtu ndani ya CCM. Wao CCM wanajua ni kwa nini jamaa ni Mungu wao. Kwa kuwa ndani ya CCM kuna makundi mengi, ipo siku kundi moja litatueleza ukweli....ni suala la muda tu.
 
Everyone in the UK who watches
or records TV programmes at the
same as they are shown on TV
needs to be covered by a TV
licence. This includes TVs,
computers, mobile phones,
games consoles, digital boxes
and DVD/VHS recorders.
The Government sets the level of
the licence fee. In January 2007
the licence fee was agreed for a
six-year period with the amount
being approved each year by
Parliament. More recently the
Government decided to freeze
the licence fee at its 2010 level of
£145.50 until the end of the
current BBC Charter period in
2016.
 
Tena sisi tunasema kodi za sigara na pombe ziongezwe kwa 500%.

Itakuwa safi sana. Ajali zitapunguwa sana barabarani.

Sasa washauri hao baba zako njia mbadala ya kupata mapato kwani ukipandisha sana kodi watu watahamia kwenye gongo na bangi; afya zao zitadolola hivyo kuwa wagonjwa watakaohitaji huduma za hospitali ambako kutakuwa hakuna dawa kwani mapato ya pombe na sigara yatakuwa yamepungua!!! Mapato yakipungua sana pengine hata huyu baba yenu mzurulaji atapunguza safari; haya ongezeni hizo kodi by 500%!!
 
Watu hawataki kulipa kodi,maendeleo wanayataka,nchi zingine hata tv uliyonayo ndani unaikatia leseni.

Tumia akili yako vizuri, Tanzania kwa rasimali zilizokuwa nazo, Je ni halali mapato ya Serikali kutegema mfuko wa mwananchi tu? Zambia inaishi vizuri sababu ya copper. TZ tuna kila kitu ila majanga, lakini hii yote ni kwa sababu ya watu wenye ubongo kama wako....jielimishe.

"When a fish rots, the head stinks first." Ghanaian Proverb
 
Tumia akili yako vizuri, Tanzania kwa rasimali zilizokuwa nazo, Je ni halali mapato ya Serikali kutegema mfuko wa mwananchi tu? Zambia inaishi vizuri sababu ya copper. TZ tuna kila kitu ila majanga, lakini hii yote ni kwa sababu ya watu wenye ubongo kama wako....jielimishe.

"When a fish rots, the head stinks first." Ghanaian Proverb
unataka kusema Tanzania ina rasilimali kuizidi marekani?.

Are sure zambia wana maisha mazuri kuzidi hayo unayoishi hapa bongo?
 
unataka kusema Tanzania ina rasilimali kuizidi marekani?.

Are sure zambia wana maisha mazuri kuzidi hayo unayoishi hapa bongo?

NInachosema, sio lazima kutengeneza mapato kwa kutegemea consumers pocket kuna athari mfano Ukiongeza say kodi ya bia, watu wakapunguza kunywa bia then kuna uwezekano makampuni yakadownsize number ya wafanyakazi (umetengeneza tatizo la ajira), mbili mapato uliyotarajia yakawa madogo kuliko ulivyotarajia. kuna njia nyingi za kuongeza mapato ya Tanzania, na wewe unazijua si hitaji kukwambia.
Zambia nimeitaja kuonyesha jinsi wanavyotumia madini ya copper kukabiliana na changamoto zao, Tanzania tunatumia nini? jibu unalo...Sigara, pombe na sim card.
Marekani ni another planet country, huwezi kuileta kwenye huu mjadala. (twahitaji angle nyingine kuchambua)

Upo? Amka!!!
 
Sasa washauri hao baba zako njia mbadala ya kupata mapato kwani ukipandisha sana kodi watu watahamia kwenye gongo na bangi; afya zao zitadolola hivyo kuwa wagonjwa watakaohitaji huduma za hospitali ambako kutakuwa hakuna dawa kwani mapato ya pombe na sigara yatakuwa yamepungua!!! Mapato yakipungua sana pengine hata huyu baba yenu mzurulaji atapunguza safari; haya ongezeni hizo kodi by 500%!!

Wasubiri Babako Slaa na mchumba'ke ambae ni mamako Josefina wakichaguliwa na wananchi 2015 watahalalisha.
 
Mapendekezo ya kamati hasa za Bunge zinazoongozwa na chichiemu ni 90% mapendekezo ya serikali, sasa wakulaumiwa si kamati bali serikali kwa kuzikubali au kuzipeleka kwenye kamati za bajeti, na zaid mapendekezo na mahesabu i ya hapo contribution ya mwenyekiti ni katika kuratibu na kuhakikisha kazi inakwisha katika wakati muafaka , ama sivyo kuna wataalamu wengi wenye kuleta mahesabu nk katika kuitengeneza hiyo bajeti, hivyo kumfanya Chenge ana nguvu kuliko Raisi au waziri husika ni upotoshaji wa habari
 
hata china kwa miaka 5 iliyopita wameongezeka mabilionea lukuki.

Huko america kina dick chen,karl love,bush etc wamepiga madeal ya hatari na halibutorn yao na wamekua matajiri wakubwa na bado wamarekani wanakamuliwa kodi hata kama anaishi nje ya marekani bado anatakiwa kulipa kodi.
Huko kenya wadada kufungua grocery tu leseni ksh 50,000 ambayo ni sawa na milioni kwa hapa,wakati hapa watu wanafungua na kufanya biashara bila kulipa leseni wala kodi,hakuna maendeleo kama kodi hailipwi.
hivi hata kenya kuna tax holidays kama za hapa bongo? kimsingi mimi nalipa kodi kubwa sana, yahani mara 4 zaidi ya mgodi wa buzwagi
 
Itakua anaogopa ule u'havard wa mr. vijisent.
 
ni nchi gani hizo zilizoendelea ambazo huduma za jamii ni bure?

UK hospitali hulipi,mzazi ambaye ni raia na hana kazi anapewa pound 400 kila mwezi kwa matumizi ya kulea mtoto,hivi karibuni malkia kapitisha sheria mtoto akifikisha miaka 7 kwenda mbele anapewa pound 2000 kwa mwaka ya matumizi.Zipo nchi nyingi za ulaya ambazo zina benefit system ya kupewa makazi.
 
Back
Top Bottom