Kikwete anamuogopa Andrew Chenge?

Kikwete anamuogopa Andrew Chenge?

Wala asilitazame upya, ndio alternative ya kuongeza mapato bila kugusa maslahi yao. Usisahau 2015 hii hapa, yunahitaji hela mingi.

piga hesabu ya tzs 1000 times watumiaji milioni 30+, kwa mwezi hiyo. Yaani tukifanikiwa hili, wachimba madini wanaweza kuchimba bureeeeee hadi yaishe hayo madini tupumzike.
Atakuwa ni mkono mtupu haulambwi.
Ila la kodi za simu JK ni lazima alitazame kwa jicho la tatu.

............ nje ya mada. Jitahidi pia kupata jiko huku...........
 
Rafiki upo? Unatoweka sana bwana.

wala usimkasirikie Mamndenyi. Wakati unachomwa sindano, ukikaza makalio inapinda tu na mwisho wa siku unaumia na mwenye sindano hasogei hapo. Ngoja waendelee kuwa mabilionea bwana, sio tupo ku-provide maziwa.

kama tax exemptions za mwaka unaoisha zinalingana na hela ya kodi kwa wafanyakazi, si tukijitahidi wawekezaji hawatadaiwa hata sh mia?
Sawa kabisa! Wamewekeza kwenye uongozi!

Btw, unasound hivyo hivyo kama jina lako! Umejipatia kabisaa! Kimamndenyimandenyi tu!
 
Last edited by a moderator:
Ushasema Nchi Zingine Hvy Na Hii Ni Nchi Nyingine Kwahiyo Sio Kila Wakifanyacho Wao Ni Sahihi Hadi Nasisi Tuwaige.

Kuhusu Kukusanya Kodi ni lazima ikusanywe iwe kwa kuiga Nchi makini ama kwa njia ingine tukiiga Utamaduni wa kukusanya Kodi vyema pasipo ujanja ujanja,kisha ile Kodi ikatumika kuleta maendeleo hapo hukuna swali juu ya kuiga wengine. Lakini tukiwaiga wengine Kodi inapatikana lakini inaliwa kifisadi hapo kwa kweli kuiga kutakosa Maana .
 
Hapa kwenye Kodi bado kuna mapungufu lukuki,Pia kwenye matumizi ya mapato ndipo kwenye majanga zaidi,Matumizi ni makubwa kuliko mapato huku pesa nyingi zikipotelea mifukoni mwa wajanja wachache, nini tatizo? Mwarobaini wa hilo Janga bado kupatikana na siku ukipatikana ujue Tanzania itakuwa Nchi Tajiri barani Afrika kutokana na wingi wa rasirimali na vyanzo vya mapato.
 
Watu hawataki kulipa
kodi,maendeleo wanayataka,nchi zingine hata tv uliyonayo ndani unaikatia
leseni.

Rekebisha kidogo, siyo hawataki kulipa kodi bali mabilionea wanasaidiwa kukwepa kodi kwa njia ya misamaha ya kodi, nani anawasaidia mimi na wewe na wote wenye kujitambua tunajua.
 
Kama hawaoni faida unatarajia nini? Nenda hizo nchi ukaone hizo kodi zinachofanya, halafu rudi hapa utuambie zinafanya nini.

Usilinganishe wingi wa kodi ila kodi hizo zinafanya nini!

Ni kweli Kodi inatumika kinyume na matarajio na hapo ndipo kwenye tatizo kubwa, nini kifanyike ? Cha kufanya si watu kuacha kulipa Kodi kisa hazileti maendeleo ,bali sasa umefika mda wa kuweka Uwazi juu ya ukusanyaji Kodi na matumizi ya Kodi ibuniwe njia za kisayansi kuziba mianya ya wajanja kupiga.
 
Kikwete mwenyewe fisadi, si unakumbuka kauli yake sasa tunalivua gamba!? Kulivua gamba ilikuwa ni kuwafukuza wale waliokuwa wameshiriki katika ufisadi wa namna moja au nyingine na hivyo kuifanya CCM ionekane chama cha mafisadi. Baada ya kubainika kwamba CCM ilikuwa mbioni kuwafukuza Lowassa, Rostam Chenge na wengineo ndio kukawepo na tetesi kwamba kama watafukuzwa basi wataanika uchafu wa Kikwete hadharani na Ikulu hakutakalika. Hapo ndio ile kauli ya "kulivua gamba" ikaanza kupotezewa na hatimaye kupotea kabisa.

Ni gharama kubwa sana kuwa na kiongozi wa nchi ambaye si msafi. Uchafu wake siku zote humfanya awe muoga kufanya maamuzi mazito, matokeo yake nchi inaenda mrama.

Inatisha mno
 
Huo uoga unaupimaje??? Chenge hayuko chini ya mamlaka ya rais hawezi mfanya chochote angekuwa waziri angemtimua alishafanya hivyo sawa huu uoga we unaupimaje??? Je akimuona anammkimbia?
 
Siku hizi jamaa zetu wa lumumba wakishikwa pabaya wanakuja na hoja chakavu ya matatizo haya yako duniani kote kila jambo walilofeli linakua generalized huu ni utoto upelekeni huko vijijini wote tumeenda shule,mfano cku magufuli(anayeonekana angalau mchapakazi) anasema foleni ziko dunian kote hata marekani wakat hajakwambia US kuna bara bara ngapi na kuna magari mangapi,au wazir wakazi analinganisha unemployment level ya nchi zilizoendelea na bila kulinganisha level ya elimu,Industrialization,Gdp nk. Hawa viongoz wetu ni majanga kama wataalamu na makocha tuna hire ma expert kutoka ulaya kuna haja ya kuleta na wanasiasa manake sasa inaonesha level ya IQ ni ile ile inatofautiana exposure tu!
 
Toka Kikwete awe Rais hawa wamekuwa mabilionea
1. Lowassa
2.Chenge
3.Ngeleja
4.Riziwani
5.Karamgi
6.Maswi na wengineo

why watu walipe kodi zaidi?

Lowasa bilionea kitambo tangu nyerere raisi sema hajarizikanao na ni kawaida kwa wa afrika
 
Mamndenyi hilo jiko kwa The Boss linahusika na kodi, au fedha za Caymans Islands??
Chenge balaa, mchawi, mwizi, Mikataba iliyofilisi nchi hii kasaini yeye!!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Elungata isue sio kodi, huyo Chenge hana credibility ya kupanga kodi!! Ni mwizi mla rushwa kafundisha hao wakubwa kuiba na kuficha fedha nje ya nchi, ni janga kwa taifa letu!!
 
Last edited by a moderator:
hata china kwa miaka 5 iliyopita wameongezeka mabilionea lukuki.

Huko america kina dick chen,karl love,bush etc wamepiga madeal ya hatari na halibutorn yao na wamekua matajiri wakubwa na bado wamarekani wanakamuliwa kodi hata kama anaishi nje ya marekani bado anatakiwa kulipa kodi.
Huko kenya wadada kufungua grocery tu leseni ksh 50,000 ambayo ni sawa na milioni kwa hapa,wakati hapa watu wanafungua na kufanya biashara bila kulipa leseni wala kodi,hakuna maendeleo kama kodi hailipwi.

Acha pumba hao kodi zao zinafanya kazi kama ilivyokusudiwa ila uku kwetu watu wachache na familia zao wanazifaidi pia wewe unasema watu hawalipi kodi una maana ya wananchi iyo migodi na hao wawekezaji ambao hawalipi kodi kwa kusamehewa uoni kuwa ndo chanzo cha mapato kupungua? Ni watu gani msio na hurumu kwa wananchi wenu mna kuwa na huruma na wageni?
 
Atakuwa ni mkono mtupu haulambwi.
Ila la kodi za simu JK ni lazima alitazame kwa jicho la tatu.

............ nje ya mada. Jitahidi pia kupata jiko huku...........

!
!
jicho la tatu kwa mwanaume ni kama tusi flani hivi....sasa hii kodi ya sim card ba mwanaisha aiangalie kwa jicho la tatu mh? fafanua vizuri.....
natanguliza shkamo.
 
Watu hawataki kulipa kodi,maendeleo wanayataka,nchi zingine hata tv uliyonayo ndani unaikatia leseni.

Mkuu sio watu hawataki kulipa kodi, bali wanaostahil kulipa hawalipi, wauza vitumbua ndo walipa kodi wa nchi hii
 
TARIME A-Z Unadhani uwazi utatoka wapi wakati kina Chenge wanasimamia kamati za bunge??
 
Last edited by a moderator:
Watu hawataki kulipa kodi,maendeleo wanayataka,nchi zingine hata tv uliyonayo ndani unaikatia leseni.
Kwani TV hatulipii mkuu !! mbona kila mwezi tunalipia king'amui na wenye king'amuzi analipa kodi kwenye fedha nilizolipa au unazungumzia TV kwa vipi mkuu au unaishi nje ya nchi !??
 
Back
Top Bottom