Hata hao mnaosema WACHINA nao watawakimbia kwani nao mmekwishaanza kuwaua!! Mmkweree anatembea dunia nzima kwa starehe zake kwa kisingizio eti anatafuta wawekezaji.
Wawekezaji wa uhakika wakija kama wale wa TWIGA CEMENT mnaanza kuleta mambo ya siasa badala ya kufuata sheria, hivyo basi kwa kutofuata sheria za nchi na kuziheshimu serikali inapoteza fedha bure kufanya promotions za investors kwani hawawezi kuja because of unfavourable investment climate!! Hata hao waliopo nao watafunga virago kwamfano hao wa kiwanda cha cement wamesitisha upanuzi wa kiwanda ambao ungegharimu $100 million.
Hawa vilaza wa serikali yetu hawaoni hasara ya kukosa mapato kutokana na huo mradi kuhamishiwa Congo sababu ya ujinga wao!!
Ndinani, nakubaliana na wewe, ninachopinga mimi, ni hii ya just one isolated kesi ya two individual people kudhulumiana, halafu kutaka kuturnish image ya nchi bungeni kwao ndio maana nikaseme waende zao.
Ila tukirudi klwenye hiyo kesi, nami nimeifuatilia kama wewe, mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni!. Kweli hao wazungu kina Middleton ni wawekezaji uchwara, ila hizo pauni 100,000 ni pesa kweli, sio pesa uchwala, maana walizileta na wakaziwekeza, hiyo ni haki yao, walipwe haki yao na riba yake, tuachane nao kwa amani.
Hiyo ni kama issue ya dowans, Richmond ilikuwa kampuni hewa, hivyo mkataba wa kampuni hewa ni batili, kwa maana hiyo, Dowans, wamerithi kampuni hewa na mkataba batili, lakini yale majereta, ni majereta kweli, sio majereta hewa wala batili, na umeme uliofuliwa ni umeme kweli, sio umeme hewa wala umeme batili, hivyo ile tozo ya ICC ni klufidia genereta kweli na umeme kweli ulifuliwa na tulioutumia, lazima tulipe, piga ua galagaza, deni lazima tutalipa, hivyo Benjamin Mengi kuwatendea haki kina Middleton, azilipe zile pauni zao 100,000 walizowekeza tuwafungashe virago vyao wakatafute kwingine kwa kuwekeza.