zebraa66
Senior Member
- Jan 21, 2016
- 198
- 81
Inasikitisha sana hatuna viongozi ambao wanauwezo wa kuiongoza nchi yetu wote wako kwaajili ya maadili yao na sio ya raiaWalichofanya wabunge leo ni utoto,upuuzi wa Hali ya juu na Kuonyesha jinsi tusivyo na viongozi makini na wazalendo wa kweli. Mtamshangiliaje mtu aliyeleta matatizo ya kiuchumi haya tuliyonayo, mtamshangiliaje mtu aliyemteua huyu msiyempenda kwa sasa kwa majina yake mfukoni bila kufuata taratibu za chama chake na kama kiongozi lazima alijua matatizo ya huyu anaemwachia kwa sababu alikua na faili yote ya wagombea. Mtamshangiliaje mtu ambae alitengeneza kakikundi ka walaji ambao hao hao kawaunganisha na huyu wa sasa kupitia Bashite, mtamshangiliaje mtu aliyeondoka akichukiwa kwa kushindwa kabisa kutimiza ahadi zake luluki na kusimika uchumi huu unaowatumikia wachache na kuwaacha wengi? Nafikiri wabunge wamekumbuka safari zisizo na kikomo nje na ufujaji mwingine, wamekumbuka kuhongwa na mashirika ili wapitishe bajeti husika, na nafikiri wamekumbuka mialiko ikulu kunywa chai na Mr tabasamu
Hatuna uongozi hapa