Kikwete ajisafisha Dowans

Kikwete ajisafisha Dowans

Rais wa JMT amejisafisha kuwa si mliki wala hawalindi marafiki zake katika sakata la DOWANS. Ameeleza kila kitu kuhusu mchakato wa Richmond hadi Dowans. Aisee naona sasa jamaa ameshutuka amefafanua mpaka basi, ameweka bayana Richmond ni kampuni ya mfukoni na kugusia maamuzi ya CC ya CCM.
Walioona taarifa hiyo jamani tuijadili kidogo.
Source TBC1 Time 02:19
Nadhani ndo mara ya kwanza kumsikia JK akikiri hadharani kuwa Richmond ni kampuni ya mfukoni!....Mwanzo mzuri atasema yote..just a matter of time!...(Keep tighting the noose!..)
 
hotuba imeeleweka na kuweka wasi kuwa DOWANs bado ni issue ya marafiki wake maana kwanini hakuwataja hawa wanaomiliki dowan kama yeye hayupo?
Naomba kila mkoa na wilaya watuletee orodha ya yale tuliyoaahidi ili tuyatengenezee mipango ya utekelezaji.jamani hapa kuna ukweli na uwezekano wa kuongeza nyingine ama ni kampeni nyingine hii


Mm naomba tu huo mswada wa katiba uharakishwe maana inaonekana katiba itapatikana mwaka huu,hilo nakupa pongezi

Migomo sio yote ina uhusiano na siasa,hizo ni sera mbovu ambazo zimefanya ugumu wa maisha na kama system haitabadilika basi migomo itaendelea sana
Kupunguza migomo rais/serikali inatakiwa kuwawajibisha watendaji wazembe waliopo
 
kuhusu dowans mkwere kasema haya......

Dowans
Ndugu Wana-CCM na Ndugu Wananchi;
Jambo ninalotaka kulizungumzia sasa sikutaka kulizungumza kwa sababu Waziri Mkuu alishalifafanua baada ya semina ya Wabunge wa CCM na hata Mheshimiwa John Chiligati, Katibu wa Siasa na Uenezi Taifa alishalizungumzia. Sikuona umuhimu wa kufanya hivyo kwa sababu viongozi wenzangu hao wameelezea kwa ufasaha uamuzi wa Kamati Kuu na ule wa kikao cha pamoja cha Wabunge wa CCM.
Lakini, yapo maneno mengi ati mbona Rais yupo kimya sana, hatujamsikia kusema chochote? Niseme nini zaidi na hao wote wameshasema kwa niaba yangu. Wapo wanaosema nipo kimya kwa sababu nahusika na Downs na ati ndiyo mwenyewe hasa. Wapo wanaosema niko kimya au nashindwa kuchukua hatua, kwa sababu marafiki zangu wamehusika. Nawalinda. Kwa sababu hiyo, nikaona nami nisema angalau watu wanisikie lakini sina la ziada ni yale yale yaliyokwishasemwa.
Kwanza niseme wazi kwamba ule msemo wa wahenga wa akutukanae hakuchagulii tusi hapa umetimia. Napenda kuwahakikishia wana-CCM na wananchi wenzangu kuwa sina uhusiano wowote wa kimaslahi kwa namna yoyote ile na kampuni ya Dowans. Sina hisa zozote wala manufaa yoyote yale. Pia sina ajizi wala kigugumizi cha kuchukua hatua kwa sababu ya rafiki yangu au hata kama angekuwa ndugu yangu kahusika. Maamuzi yaliyofanywa na Kamati Kuu na Kamati ya Chama ya Wabunge wa CCM yalifanywa chini ya uogozi wangu. Ni uthibitisho tosha wa ukweli huo. Waliokuwepo kwenye vikao hivyo wanajua ukweli wa haya ninayosema. Ningekuwa na maslahi au hofu tusingefanya uamuzi ule.

kwa mtazamo wangu huyu jamaa kaongea siasa mtupu hAPA HAKUNA KITU CHA MAANA AMBACHO UNAWEZA KUMNUKUUU KAMA MSIMAMO WA RAISI WA NCHI

MY TAKE:
1. Rais kaonyesha udhaifu mkubwa sana kiutendaji.. ni kama hajali kabisa mambo mazito yanayoendelea ndani ya nchi ambayo hayakuwai kuonekana nchini hivyo bunge chini ya wabunge wa upinzani wa kweli ipige kura ya kutokuwa na IMANI na rais.
2. Waziri mkuu ambaye ni mtendaji mkuu wa serikali nae pia ameonesha uwezo mdogo sana katika kukabiliana na changamoto dhidi ya serikali yake ikiwemo baraza la mawaziri...ikiwemo kukosa sauti kwenye masuala mazito na kushindwa kushughulikia kero za wananchi hivyo nae pia a resign kitu kitachopelekea kuvunjwa kwa baraza, ndio baraza livunjwe kwani nchi inakwenda kama hukuna serikali vile

MAONI YAKO TAFADHARI
 
nadhani leo ndio amevuruga kabisa wananchi...all those days anakuja kutuambia utumbo huuu....No way....Kawulethi umshine wange!!!!(bring my machine gun)...sijamuelwa na sitakaa nimuelewe...Nilishasema huko nyuma kuwa nchi haina Rasi serious sasa ndo mumeona...huwezi mambo ya msingi kama haya unaongea as if wewe ni waziri kivuli tena wa kambi ya upinzani isiyo rasmi bungeni....JK SIJAKUELEWA BANA
<br />
<br /> anaongea kama waziri kivuli wa kambi isiyokuwa rasmi ya upinzani bungeni!! maana waziri wa kambi rasmi ya upinzani angesema waziwazi kuwa Dowans hawatalipwa hadi kieleweke!
 
nina uhakika jamaa hatamaliza hiyo miaka yote..hali halisi ilivyo na wanayofanya 2015 is too far!!
Mark my words..
 
Nimepata kupendekeza ktk thread ambayo siikumbuki na siyo lazima niitafute, kwamba DOWANS itaifishwe bila kulipa fidia kwa wanahisa.

Licha ya kwamba pendekezo hilo linakiuka Katiba ya JMT, Ibara ya 24(2), Serikali inaweza ku-justify this kwa vile fedha zote zinazohusika na Richmond na baadae Dowans, ni fedha za umma wa Tanzania zilizokwapuliwa toka BoT na mafisadi wakiongozwa na R.A.

Itakumbukwa kuwa R.A. alipewa na Gavana Ballali (sasa ni Marehemu?) fedha toka EPA baada ya kukubaliana na boss wake Ben kwamba "lazima tutafute fedha kumsaidia huyu malaika aweze kushinda uchaguzi" wa u-Rais wa 2005. R.A. wakati huo alikuwa Treasurer wa CCM na alichukuwa zaidi ya TSh 40 bilioni toka EPA ya BoT na kuwapa ccm "wakashinda kwa kishindo".

R.A. alichukua zaidi toka EPA na kuziingiza ktk Kagoda Agriculture na nyingine zaidi ndio alizonunulia mitambo ya kampuni ya kificho "Richmond Development PLC" ya huko Houston Texas. Ilipofichuliwa kuwa ni feki na Tume Maalum ya Bunge iliyoongozwa na Mhe. Mwakyembe, ikanunuliwa na Dowans (Tanzania) Ltd. Dowans imekwisha dhihirika ni mali ya R.A. etc. hata katika hii ICC case R.A amejitokeza akidai fidia!

Huyu R.A. without any shame or impunity rubs shoulders with Tz bigshots. Tz leaders now want to pay him "Compensation" for Tanesco using the turbines he bought with our money obtained from the EPA of BoT. What a shame. History will never forgive us for being so naive and neglecting our interests and our people so much.

J.K. confiscate the turbines and all assets belonging to DOWANS and you will slightly reduce the blame you will always carry for this mismanagement of the affairs of Tanzania.
 
MY DOG,IS PREISDENT IS HAKUNA KITU ....analeta siasa tu, no specification..kujisafisha....what for????
MAISHA YANAZIDI KUTUUMIZA SISI tunaolipa kodi akapime uzito marekani
 
Hainiingii akilini kwa rais kuonyesha msimamo tofauti na waziri mwenye dhamana ya mamlaka aliyopewa na rais. Mimi naamini waziri yule aliwasiliana na rais kupata kujuwa msimamo wake kabla ya kutowa kauli ya serikali kwa mujibu wa mamlaka yake. Ikiwa ni kweli msimamo waliokubaliana umebadilika basi ni vyema yule waziri atowe tamko lingine na sio kubakia kimya. Hatukatai kuwa kama nyoka kwa lugha rahisi lazima ukabali mwanzo mpya pale unapojiridhisha yaliopo yameshachoka na hayafai tena.
 
Haya Jakaya Mm ndiyo Kanitoka kabisa,Nimemsikiliza Mm nilichokiona nika anaongea "kishambenga" kuliko kujibu concern za Umma Empirically!!!
 
Nakubaliana na mtoa hoja kwamba Ikulu yetu kwa sasa haina Raisi bali tuna mtu mmoja mjinga na wa hovyo kabisa anatakiwa akafunzwe na mamaye vinginevyo tutamfunza sisi hawajui Dowans iweje waziri wake na mwanasheria mkuu na waziri mkuu wake wote baada ya kikao chao waseme Dowans italipwa chini ya uenyekiti wake halafu yeye aseme hawajui
 
Mbona cc ya ccm ilisema wanawategemea wanaharakati waliopeleka suala la kukataa kuilipa dowans mahakama kuu,leo jk anasema wanasheria wa serikali na wa tanesco ndio wanaofuatilia suala hilo?hapo nimechanganyikiwa

hii yaweza kuwa janja nyingine.hawa wanasheria anaosema watajitolea au la?isijekuwa ni njia ya kuwapa washkaji zenu mabilioni ya wavuja jasho halafu mwishoni waseme wamepoteza kesi.
 
Chama limegeuka kama kambi ya wachawi bado anataraji kupata wanachama wengi vijana! Wanalo msimu huu.
 
Hana anachosema, kutueleza mambo ya Kamati kuu sisi inatuhusu? ASEME YEYE KAMA RAIS ANALIONAJE HILO NA ANALISHUGHULIKIA VIPI!! Aaaaaaaaaaaaaaaaarrrrrrrrrghhhhhhhhhhhhh!! Upuuuuuuzi
 
Mbona humu mnakoromeana wenyewe kwa wenyewe!
Hivi mnaomtetea mkwere kama akili zenu zipo likizo hata macho hayaoni?
 
We ni mkosefu wa nidhamu huwezi kumwabia rais mpumbavu

Heshima ni matendo si kuwa Rais. Unategemea mtu mwenye akili zenye mizania ya haki na uzalendo amheshimu rais Kilaza na jambazi kama huyu? Aliiba EPA kufadhili kampeni zake 2005, 2010 kachakachua matokeo ya urais japo alishindwa vibaya. Anawalinda mafisadi ambao ni rafiki zake dam dam. Alibariki malipo kwa dowans kwenye kikao cha kamati kuu CCM yeye akiwa mwenyekiti.
Leo anaona tumecharuka na kujua ni mmoja wa wamiliki anakuja kuleta kiswahili kingine tofauti na kujitetea kuwa si mmiliki. Utamheshimu vipi mtu kigeugeu na legelege kama huyu kuwa ni Rais. He is really full fool.
 
rais kuongea maneno ya namna hii ni mpumbafu na ujinga wa hali ya juu...asifanye watu watoto hapa na majibu yake ya hovyohovyo...kwanza nani kamuuliza mpaka anaanza kufafanua ...stupid

wewe ****** sana ,ulitaka rais aseme nn,acha siasa zako za chuki ******* mkubwa ww
 
Back
Top Bottom