Huyu mwezi wake umefika kwani kuna watu huwa wanaugua kila mwisho wa mwezi:clap2::clap2::clap2:
rais kuongea maneno ya namna hii ni mpumbafu na ujinga wa hali ya juu...asifanye watu watoto hapa na majibu yake ya hovyohovyo...kwanza nani kamuuliza mpaka anaanza kufafanua ...stupid
Nimefarijika kusikia JK akikiri hili huko Dodoma leo. Lakini bado sijaelewa vizuri ..
Kumbe JK anakubali matokeo ya tume ya Mwakyembe kuwa ilipatia kuwa Richmond in kampuni hewa.Kama hii ni kweli anatuambiaje kuhusu matokeo ya TAKUKURU waliosema kuwa Richmond haikuwa na shida? Je, kukubali matokeo ya tume ya Bunge siyo kukataa yale ya TAKUKURU? Iweje JK halizungumzii hili la kazi nzuri au mbaya ya TAKUKURU kuhusu Uchunguzi wao kuhusu Richmond?
nauliza ili tutafakari kuhusu gharama zilizotumika na Takukuru kuchunguza Richmond na kuishia kuwadanaganya Watanzania.
Hivi bunge lisingekomaa mpaka ikaundwa Tume ya Mwakyembe ikaundwa tungekwendaje kuhusu hili?
Je ni mangapi yanafunikwa hivi?
Hivi ukidanganya umma bosi wako anakupongeza na kuomba wananchi wakupe ushirikiano kama alivyofanya JK hotuba yake bungeni?
Hivi wananchi wanakosea wakisema hawawamini TAKUKURU?
Angalizo: "Ukiona wakuu wanakazania kupinga jambo kama walivyofanya kupinga kamati ya Mwakyembe jua kuna jambo linafukiwa"
Bahati mbaya hotuba inayosambazwa ni ile official transcript ambayo imekuwa whitewashed. Ni kweli kasema yeye ni "msema ovyo" hata kwenye Baraza la Mawaziri.yaonekana umeisikiliza hotuba kwa umakini.kuna sehemu rais anakiri kwa kinywa chake kwamba hata ndugu zake wanafahamu kuwa yeye ni msema hovyo.utuwekee ile hotuba ambayo haijahaririwa!
Umefahamika Mwenyekiti...
Kama kikwete anawashauri basi ni heri awafukuze ili aweze kutoa mawazo yake mwenyewe. Kama raisi wa nchi anaweza kutoa majibu kama haya ni heri angekaa kimya.
Raisi anatamka Richmond ni kampuni hewa, kama ni hivyo DOWANS ilirithi mkataba kutoka wapi? hivi DOWANS hawakuja na documents zozote walipo kuja kuzalisha umeme? na kama walikuja na documents walizipata wapi na zionyesha hao Richmond ni nani? kwanini DOWANS wasiambiwe wakatuletee hao Richmond walio warithisha mkataba kabla ya kuwalipa?.
Raisi anasema Tanesco watalipa na siyo serikali, hivi Tanesco si inamilikiwa 100% na serikali? Hivi Tanesco si wanapata mapato yake kutoka kwa raia? Tanesco ikifa leo hii itayeteseka si raia? au amesema hivyo akimaanisha wao viongozi wa serikali hawata athirika?
Sijawahi kuona raisi mbumbumbu kama huyu.
"...Naomba kila mkoa na wilaya watuletee orodha ya yale tuliyoaahidi ili tuyatengenezee mipango ya utekelezaji..."
Raisi wangu na Mwenyekiti wa Chama Cha CCM ametamka, ametoa kauli ambayo ilikuwa itolewe zaidi ya miezi mitatu sasa. Hii hotuba na hasa kipengele kinachohusu Dowans ilitakiwa mwishoni mwa 2010. Aliogopa nini kusema kama kwa dhati kabisa aliyosema sasa ndio msimamo wake?
Napata mashaka na Raisi wangu anapokimbilia 'akutakanaye hakuchaguliwi tusi'. Sidhani kuna mtu anayekuwa na msimamo tofauti eti kwa kuwa anamtukana Rais. Sidhani kupingana na hoja ni kumtukana mtu. Naogopa tunaelekea mahali tukibishiwa hoja tunaichukulia chuki, tunaona ni tusi badala ya kufikiria jinsi ya kuijibu. Tena wakati mwingine tunapaswa kuwa wanyenyekevu, tukiri pale hoja inatuonyesha tulikuwa tumekosa.
Naamini safari bado, na ninaamini kina Msekwa na wazee wengine humo CCM, wanayo bado nafasi ya kurekebisha hizi hisia, maana naona ndio chanzocha kutoelewana kwa taifa. Kiongozi asiyepingwa! Kiongozi ASIYEPINGWA! Tafsiri yake nipeni! Je kiongozi asiyekuwa tayari kupingwa anaitwa nani?
Rais wa JMT amejisafisha kuwa si mliki wala hawalindi marafiki zake katika sakata la DOWANS. Ameeleza kila kitu kuhusu mchakato wa Richmond hadi Dowans. Aisee naona sasa jamaa ameshutuka amefafanua mpaka basi, ameweka bayana Richmond ni kampuni ya mfukoni na kugusia maamuzi ya CC ya CCM.
Walioona taarifa hiyo jamani tuijadili kidogo.
Source TBC1 Time 02:19
Kwa aliyosema leo JK nafikia hitimisho lifuatalo:
Aliposema tumitumia umeme wao miezi tisa===Anatukumbusha kuwa ukila na wewe lazzima uliwe...hivyo watalipa Dowans kwa kuwa umeme si mlimtumia?
Anaposema ..hatima ya kuwalipa iko mikononi mwa wanasheria: Kwa hiyo ina mana yeye kama yeye poa tu walipwe ila kama wanasheria watasaidia nayo poa tu.. so basically baadae tutasikia ahahah wanasheria wamesema haiwezekani inabidi tulipe ... Mkwere ni mjanja sana hataki kutake responsibility ya yeyey kama rais ..kila kitu ansema huyu au yule amesema na mimi sina uwezo wa kuingilia...mnakumbuka kauli yake siku ya shrehe za mahakama? Alisema wananchi hawajui sheria wanamtaka abdilishe hukumu kwenye jambo liloamrimriwa na mahakama.(alimaanisha Dowans imeshaamuliwa so kilichobaki ni utekelezaji).
Kifupi I think JK anajua kuwa Dowans watalipwa ..anachofanya ni kucheza na maneno... kwenye kikao cha wabunge aliwasanifu kina mwakyembe kuwa eti watoe mwongozo ...tehteheteh mkwere msanii..