Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,809
- 218,463
Taarifa tulizonazo mpaka sasa ni kwamba kimeandaliwa kikundi cha dharura cha kumshambulia Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe kwenye mitandao ya kijamii, redioni, barabarani, vichochoroni na kwenye TV na media zote.
Mamluki hao wameelekezwa kumshambulia Mbowe kwa kile kinachosemwa kwamba Ameibagua Zanzibar kwa KUFICHUA KWAMBA MKATABA WA KUUZA BANDARI HAUJAGUSA BANDARI ZA ZANZIBAR, bali zilizoguswa ni Bandari za Bara tu na kwamba aliyesaini mkataba huo ni Makame Mnyaa Mbarawa ambaye ni Mzanzibar, tena katika uongozi wa Rais aliyetokea Zanzibar.
Taarifa zaidi zinadokeza kwamba miongoni mwa mamluki waliotangulizwa mbele kumshambulia Mbowe yumo Hamad Rashid, Lusinde, Msukuma na wengine kadhaa kutoka vyama vya Upinzani.
Bali tunachowaambia ni hiki, Mbowe hatobabaishwa na mashambulizi duni kama haya, tena kutoka kwa watu wasiojielewa kama waliotajwa hapo, ataendelea kusimamia ukweli bila kumung'unya maneno bila kujali mawe atakayorushiwa.
Wananchi wote wameelewa makando kando yote yaliyogubika Mkataba huu.
Mungu Ibariki CHADEMA.
Mamluki hao wameelekezwa kumshambulia Mbowe kwa kile kinachosemwa kwamba Ameibagua Zanzibar kwa KUFICHUA KWAMBA MKATABA WA KUUZA BANDARI HAUJAGUSA BANDARI ZA ZANZIBAR, bali zilizoguswa ni Bandari za Bara tu na kwamba aliyesaini mkataba huo ni Makame Mnyaa Mbarawa ambaye ni Mzanzibar, tena katika uongozi wa Rais aliyetokea Zanzibar.
Taarifa zaidi zinadokeza kwamba miongoni mwa mamluki waliotangulizwa mbele kumshambulia Mbowe yumo Hamad Rashid, Lusinde, Msukuma na wengine kadhaa kutoka vyama vya Upinzani.
Bali tunachowaambia ni hiki, Mbowe hatobabaishwa na mashambulizi duni kama haya, tena kutoka kwa watu wasiojielewa kama waliotajwa hapo, ataendelea kusimamia ukweli bila kumung'unya maneno bila kujali mawe atakayorushiwa.
Wananchi wote wameelewa makando kando yote yaliyogubika Mkataba huu.
Mungu Ibariki CHADEMA.