Kikosi Kazi Kazini (KK), Weusi jipangeni

Scars

JF-Expert Member
Apr 8, 2017
44,375
105,199
Vijana 8 kutoka kundi la Tamaduni Music ambao wameji-organize na kuunda kikundi walichokipa jina la Kikosi Kazi Kazini (KK)

Naweza nikasema kwa ngoma mbili hizi walizotoa Kikosi Kazi zinatosha kabisa kuficha nyimbo zote walizowahi kuimba Weusi.

Hivi kama nyimbo ya SALA utaifananisha na nyimbo gani ya weusi na isipwaye?

Hapo mwezi uliopita walitamba kwa diss track yao iloyowalenga kundi la Weusi. Ifahamike kua Katika wimbo ambao uliimbwa na kundi la Weusi kulikua na meseji ambayo iliyo walenga wasanii wote wa Tamaduni.

Ni meseji ambayo ilitafsirika kwamba tamaduni ni kundi ambalo limepotea katika hip hop industry na wao weusi ndio walioshika bendera kuilinda hip hop culture moja ya line iliyo catch feelings za wasanii kutoka tamaduni ni hii "watamaduni si ndio tunaotunza hii culture"
 
Weusi ni kundi la muda mrefu, kikosi wamejiunga juzi baada ya kupitiwa na diss lines za weusi kwenye wimbo hvyo kikosi hawana mwendo, wako wengi kama panya road kibiashara kwao ni vigumu kuendelea kama kikundi
Swala la muda mrefu sio kigezo, kumbuka kikosi kazi ni foundation kutoka tamaduni music. Kwaiyo ukianza kufanya comparison angalia na angle hiyo pia kwasababu ni gang ambalo asili yao ni moja (tamadunj)

Halafu kikosi kazi hawajajiunga baada ya diss ya weusi, hiyo ni project iloyoko muda mrefu ila haikua official to be announced.

Swala la wingi wao nalo silipi nafasi ya kusimama kama kikwazo au sababu ya uwezo wao kuonekana mdogo kuliko weusi. Kwasababu katika tasnia ya makundi kimuziki yapo makundi yenye watu wengi kuliko kikosi kazi na bado wanatusua. Kwaiyo tuache kukariri
 
Muda ndiyo utakaoamua nani ataondoka nani atabaki, ila chonde chonde tusisikie story za media zimewabania, mara oh clouds inawabeba weusi maana kuna redio nyingi na kuna watu hata bila nyimbo zao kupigwa huko bado wamefanya vizuri.
Weusi kubebwa na media sio story mpya hilo linafahamika halihitaji mjadala.

Tujadili uwezo wa mashairi kati ya haya makundi mawili

Natoa challenge kati ya nyimbo mbili zilizofanywa na kikosi kazi halafu suggest ngoma ya weusi unayoona inaweza ika battle na hizi ngoma
 
Tatizo hao jamaa wanajiona wenyew ndo wanajua bongo nzima hilo kundi Nikki atalivunja kwa ujuaji wake Nikki hana nidham
Majigambo katika hip hop ni jambo ambalo lipo tangu kitambo. Unaweza kuchana kujionesha kua wewe ni mkali kuliko wengine mfano mzuri ngoma ya dizasta nobody is safe kaasema "mi ni king wa swahili rap get it"

Lakini sio hivyo tu hata wao weusi ndio walikua wa kwanza kuwadiss tamaduni kwa kujionesha kua wao ndio wenyewe walipojiita "watamaduni sisi ndo tunaotunza hii culture" huku ikijulikana fika kua tamaduni ni kundi la kina mbishi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom