Kikokotoo(Mafao): Rais Samia anastahili pongezi kwa hili

Inevitable

Member
Apr 27, 2012
82
159
Jana, statement toka Ikulu ilieleza kuwa Rais Samia amepokea mapendekezo ya kanuni mpya ya mafao ya Pensheni, kama ilivyoombwa na chama cha wafanyakazi Tanzania (TUCTA) siku ya sherehe za wafanyakazi (Mei Mosi, 2022), ambapo sasa amekubali ombi la kupandisha malipo ya mafao, kutoka 25% iliyokataliwa na wadau hadi 33.3%.

Ametaka TUCTA, wizara ya fedha na Chama cha Waajiri (ATE), kuendelea kushirikiana ili kukamilisha taratibu za malipo ya mkupuo huo wa asilimia 33.3% badala ya 25% iliyokataliwa mwaka 2018.

Kanuni za Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ya Mwaka 2018, ziliweka kikokotoo kimoja cha asilimia 25 ambacho kiliweka usawa kwa wastaafu wote kupata mafao yenye fomula moja, tofauti na awali kulipokuwa na fomula mbili.

Kikokotoo kipya kwenye kanuni kilikuwa ni asilimia 25 kwa mafao ya mkupuo na asilimia 75 inayobaki kulipwa kama pensheni ya mwezi kwa kila mwezi hadi mwanachama atakapofariki dunia.

Hata hivyo, katika kikokotoo hicho, umri wa kuishi ulikadiriwa kuwa ni miaka 12.5, ikiwa ni umri uliokadiriwa kuwa mwanachama ataishi baada ya kustaafu.

Kwa mujibu wa kikokotoo cha NSSF ambacho kimekuwapo kwenye kanuni za shirika hilo tangu mwaka 2014, mwanachama anapostaafu analipwa asilimia 25 ya mafao ya mkupuo na kilichobaki kinalipwa kama mshahara wa kila mwezi.

Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ya Mwaka 2018, imetaja jumla ya mafao saba ambayo ni manne ya muda mfupi (fao la upotevu wa ajira, fao la ugonjwa, fao la uzazi na mkopo wa nyumba) na matatu ya muda mrefu ambayo ni pensheni ya uzeeni, fao la ulemavu na fao la warithi.

Kwa hili, niseme Rais Samia na serikali yake wanastahili pongezi.
 
Double standard imekuwepo kwa muda mrefu Sana. Hadi Sasa watumishi wa umma waliokuwa wanachangia PPF na NSSF wamekuwa wakilipwa mafao Yao kwa kikokotoo kinachotumia asilimia 25.

Wakati watumishi wa umma waliokuwa wanachangia pspf na lapf wao wanamtumia kikokotoo kinachotumia asilimia 50! Wote ni watumishi wa umma lakini wanahudumiwa tofauti na Serikali hiyo hiyo!!

Ni uonevu wa kutisha!!
 
Double standard imekuwepo kwa muda mrefu Sana. Hadi Sasa watumishi wa umma waliokuwa wanachangia PPF na NSSF wamekuwa wakilipwa mafao Yao kwa kikokotoo kinachotumia asilimia 25.

Wakati watumishi wa umma waliokuwa wanachangia pspf na lapf wao wanamtumia kikokotoo kinachotumia asilimia 50! Wote ni watumishi wa umma lakini wanahudumiwa tofauti na Serikali hiyo hiyo!!

Ni uonevu wa kutisha!!
Hii ni changamoto kama ni kweli iko hivyo
 
Double standard imekuwepo kwa muda mrefu Sana. Hadi Sasa watumishi wa umma waliokuwa wanachangia PPF na NSSF wamekuwa wakilipwa mafao Yao kwa kikokotoo kinachotumia asilimia 25...
Wabunge wetu bogus sana na inasikitisha sana, hii ilikuwa ni kusukuma muswada mmoja tuu unajadiliwa mambo yanabadilika haraka sana, ndio umuhimu wa kuwa na think tanks ambazo zinafuatilia issues kama hizi na kuziweka wazi na kuwaambia wabunge hii kitu sio sawa kuna uonezi hapa, ndio maana kuna umuhimu sana wa kuwa na think tanks na lobbyist wa kusukuma issues kama hizi ili sheria zibadilike
 
... hivi pensheni ya kila mwezi ni % ngapi ya mshahara mtumishi aliostaafia wakuu? Au kuna fomula tofauti? Kama ipo, naomba kuijua ndugu zanguni.
 
... hivi pensheni ya kila mwezi ni % ngapi ya mshahara mtumishi aliostaafia wakuu? Au kuna fomula tofauti? Kama ipo, naomba kuijua ndugu zanguni.
Haitegemei mshahara pekee wa mtu. Inategemea vitu vifuatavyo:
1. Mshahara wa mtu
2. Muda aliochangia
 
Kwa Hiyo asilimia mwalimu mkuu akistaafu anapata shilingi ngapi za lampusam?
 
Haitegemei mshahara pekee wa mtu. Inategemea vitu vifuatavyo:
1. Mshahara wa mtu
2. Muda aliochangia
... naomba formula Mkuu. Let's assume mstaafu alistaafia TZS 1,500,000/= kwa mwezi mshahara ambao amekuwa akiupokea for the past 3 years na amechangia for 25 years.
 
Jana, statement toka Ikulu ilieleza kuwa Rais Samia amepokea mapendekezo ya kanuni mpya ya mafao ya Pensheni, kama ilivyoombwa na chama cha wafanyakazi Tanzania (TUCTA) siku ya sherehe za wafanyakazi (Mei Mosi, 2022), ambapo sasa amekubali ombi la kupandisha malipo ya mafao, kutoka 25% iliyokataliwa na wadau hadi 33.3%.

Ametaka TUCTA, wizara ya fedha na Chama cha Waajiri (ATE), kuendelea kushirikiana ili kukamilisha taratibu za malipo ya mkupuo huo wa asilimia 33.3% badala ya 25% iliyokataliwa mwaka 2018.

Kanuni za Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ya Mwaka 2018, ziliweka kikokotoo kimoja cha asilimia 25 ambacho kiliweka usawa kwa wastaafu wote kupata mafao yenye fomula moja, tofauti na awali kulipokuwa na fomula mbili.

Kikokotoo kipya kwenye kanuni kilikuwa ni asilimia 25 kwa mafao ya mkupuo na asilimia 75 inayobaki kulipwa kama pensheni ya mwezi kwa kila mwezi hadi mwanachama atakapofariki dunia.

Hata hivyo, katika kikokotoo hicho, umri wa kuishi ulikadiriwa kuwa ni miaka 12.5, ikiwa ni umri uliokadiriwa kuwa mwanachama ataishi baada ya kustaafu.

Kwa mujibu wa kikokotoo cha NSSF ambacho kimekuwapo kwenye kanuni za shirika hilo tangu mwaka 2014, mwanachama anapostaafu analipwa asilimia 25 ya mafao ya mkupuo na kilichobaki kinalipwa kama mshahara wa kila mwezi.

Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ya Mwaka 2018, imetaja jumla ya mafao saba ambayo ni manne ya muda mfupi (fao la upotevu wa ajira, fao la ugonjwa, fao la uzazi na mkopo wa nyumba) na matatu ya muda mrefu ambayo ni pensheni ya uzeeni, fao la ulemavu na fao la warithi.

Kwa hili, niseme Rais Samia na serikali yake wanastahili pongezi.
samia ni Rais mzuri, anayemchukia ana yake tu.
 
Double standard imekuwepo kwa muda mrefu Sana. Hadi Sasa watumishi wa umma waliokuwa wanachangia PPF na NSSF wamekuwa wakilipwa mafao Yao kwa kikokotoo kinachotumia asilimia 25.

Wakati watumishi wa umma waliokuwa wanachangia pspf na lapf wao wanamtumia kikokotoo kinachotumia asilimia 50! Wote ni watumishi wa umma lakini wanahudumiwa tofauti na Serikali hiyo hiyo!!

Ni uonevu wa kutisha!!
No 50
 
Baada ya serikali kusitisha tangazo la kikokotoo mwaka 2018 sasa wamekuja na kikokotoo kipya baada ya mashauriano na waajiri.

ATE na vyama vya wafanyakazi ambapo mstaafu katika mifuko yote atalipwa asilimia 33 tu kama malipo ya mkupuo. Wale tuliokuwa tumejipanga kuchukua michango yote kwa mkupuo tujiandae.
 
Baada ya serikali kusitisha tangazo la kikokotoo mwaka 2018 sasa wamekuja na kikokotoo kipya baada ya mashauriano na waajiri..ATE na vyama vya wafanyakazi ambapo mstaafu katika mifuko yote atalipwa asilimia 33 tu kama malipo ya mkupuo...wale tuliokuwa tumejipanga kuchukua michango yote kwa mkupuo tujiandae.
Alafu inayobaki unakuwa unalipwa Kam posho za mwez au?
 
Baada ya serikali kusitisha tangazo la kikokotoo mwaka 2018 sasa wamekuja na kikokotoo kipya baada ya mashauriano na waajiri..ATE na vyama vya wafanyakazi ambapo mstaafu katika mifuko yote atalipwa asilimia 33 tu kama malipo ya mkupuo...wale tuliokuwa tumejipanga kuchukua michango yote kwa mkupuo tujiandae.
Ufafanuzi kwa wanaujua madhara au faida zake tafadhali. Kwa maelezo hayo tuu haitoshi kujua mataafu anafaidika au anapunjwa kwa kiasi gani. Weka nyama nyama na supu tuweze kuelewa, kwa mwenye uelewa wa kutosha. Hesabu ya ulinganifu inahusika hapo
 
Back
Top Bottom