Kikao cha Magufuli na Lowassa chailainisha CHADEMA kutia mguu Kinondoni na Siha

Mchambuzi

JF-Expert Member
Aug 24, 2007
4,850
9,405
Kufuatia kikao cha hivi karibuni baina ya Mheshimiwa Rais John Magufuli na Mjumbe wa Kamati Kuu Chadema na Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Edward Lowassa, kinachofuatia sasa ni utekelezaji wa makubaliano yaliyofikiwa na viongozi hawa wawili.

Ikumbukwe kwamba miongoni mwa hoja ambazo Mheshimiwa Lowassa alizibeba kwenda kuziwasilisha kwa Mheshimiwa Rais kwa niaba ya ukawa, pia lilikuwepo suala la ukandamizaji wa demokrasia unaoendelea nchini.

Kwa mfano, katika mazungumzo yake na Mheshimiwa Rais, Mheshimiwa Lowassa alimueleza Mh Rais juu ya kasoro nyingi zilizojitokeza kwenye chaguzi ndogo za udiwani katika kata 43 zilizomalizika hivi karibuni ambapo ukawa uliwasilisha rasmi kwa tume ya uchaguzi malalamiko yake dhidi ya vitendo vya uvunjifu wa demokrasia vilivyojitokeza. Mheshimiwa Rais alimuahidi Mheshimiwa Lowassa kulishughulikia ili kuhakikisha kwamba suala la demokrasia ya vyama vingi linatekelezwa kwa mujibu wa katiba ya nchi.

Kufuatia ahadi hiyo ya Mheshimiwa Rais, baadae Mheshimiwa Lowassa aliwasilisha taarifa hiyo kwa Kamati Kuu ya Chadema pamoja na mengine yaliyojiri katika kikao chake na Mheshimiwa Rais, ikulu Dar es salaam. Kufuatia hatua hiyo, Kamati Kuu ya Chadema kwa kauli moja imeridhia uamuzi wa Chama kusimamisha wagombea wake katika chaguzi ndogo za ubunge kwenye majimbo ya Kinondoni na Siha, uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwezi ujao kwa imani kwamba ahadi za Mheshimiwa Rais kwa Mheshimiwa Lowassa zitatekelezwa na vyombo husika.

Wana ukawa pamoja na wapenda demokrasia kwa ujumla wanaombwa kuwa watulivu na wenye subira katika kipindi hiki kuelekea tarehe ya chaguzi ndogo za ubunge katika majimbo ya Kinondoni na Siha.
 
Wanaweza kuwa wamechukua uamuzi sahii; lakini unaweza usiwe wa hekima. Si wa hekima kwa sababu hakuna ushahidi wowote wa makubaliano yoyote yaliyofanyika hasa kwa vile haikuelezwa toka mwanzo kama kulikuwa na mpango wa kuzungumzia mambo hayo na baya Zaidi ni kuwa taarifa ya Ikulu haikuzungumzie lolote juu ya yanayodaiwa kuzungumzwa na Lowassa.

Hatari ya hii inawezekana ni namna ya kuweka pressure kwa Serikali lakini pia inaweza kuwa ni jaribio la kujaribu kutengeneza mazungumzo ambayo hayakuwepo. Ilikuwa ni vibaya kwa Lowassa kwenda peke yake Ikulu bila kiongozi mwingine wa ngazi za juu wa Chadema na hivyo sioni ni kwa namna gani mazungumzo yake yanaweza kupewa Baraka na chama na yakaungwa mkono.

Mambo haya yanahousiana na siasa na masuala ya uchaguzi yanashughulikiwa kwa mazungumzo na makubaliano rasmi baina ya pande zinazozozana au kutokubaliana. Bila makubaliano ni vigumu kuona ni jinsi gani unaweza kusimama na kudai jambo Fulani lifanyike au lisifanyike.
 
Imeshakuwa kwa niaba ya Ukawa tena, wakati tuliambiwa Lowasa hakuwataarifu hao Ukawa kabla ya kikao?
Ukawa ulishampa Lowassa hoja za kuwasilisha kwa Rais magufuli kwa niaba yake kwa Muda mrefu na maombi ya appointment kuwasilishwa ikulu accordingly. Kilichotokea ni kwamba ikulu ilikaa kimya kwa Muda mrefu na kumuita Lowassa ghafla siku husika.
 
Wanaweza kuwa wamechukua uamuzi sahii; lakini unaweza usiwe wa hekima. Si wa hekima kwa sababu hakuna ushahidi wowote wa makubaliano yoyote yaliyofanyika hasa kwa vile haikuelezwa toka mwanzo kama kulikuwa na mpango wa kuzungumzia mambo hayo na baya Zaidi ni kuwa taarifa ya Ikulu haikuzungumzie lolote juu ya yanayodaiwa kuzungumzwa na Lowassa.

Hatari ya hii inawezekana ni namna ya kuweka pressure kwa Serikali lakini pia inaweza kuwa ni jaribio la kujaribu kutengeneza mazungumzo ambayo hayakuwepo. Ilikuwa ni vibaya kwa Lowassa kwenda peke yake Ikulu bila kiongozi mwingine wa ngazi za juu wa Chadema na hivyo sioni ni kwa namna gani mazungumzo yake yanaweza kupewa Baraka na chama na yakaungwa mkono.

Mambo haya yanahousiana na siasa na masuala ya uchaguzi yanashughulikiwa kwa mazungumzo na makubaliano rasmi baina ya pande zinazozozana au kutokubaliana. Bila makubaliano ni vigumu kuona ni jinsi gani unaweza kusimama na kudai jambo Fulani lifanyike au lisifanyike.


Mzee Mwanakijiji ulituambia hapa jukwaani kwamba ulikuwa na tetesi kwamba kiongozi mkubwa wa upinzani (Lowassa) angefanya press conference ya kufanya maamuzi magumu. Can you provide an update on that? Sijamuona huyo kigogo wa upinzani kufanya hiyo press conference ya maamuzi magumu (kurudi CCM). You insinuated that Lowassa would return to CCM; he didn't.

CCM watakuaibisha Mzee ... heshima uliyokuwa umejiwekea hapa jukwaani itayeyuka yote. Angalia mwenzako Slaa, he doesn't talk about human rights and democracy anymore; although he was a leader of a democratic party and his family was beaten and bled for democracy and human rights.

By the way Sir, what's your view on the current allegations of the abuse of human rights by the Magufuli's government in Tanzania. You realize, though, even your colleague Max Mello continues to be harassed by your beloved Magufuli's government for no reason.
 
Ikumbukwe kwamba miongoni mwa hoja ambazo Mheshimiwa Lowassa alizibeba kwenda kuziwasilisha kwa Mheshimiwa Rais kwa niaba ya ukawa, pia lilikuwepo suala la ukandamizaji wa demokrasia unaoendelea nchini.
Ebo! Nyie CHADEMA msitufanye watu hatuna akili. Si ni nyinyi nyinyi mlikuwa mnahoji how come Lowassa anaenda Ikulu bila kuwasiliana na uongozi?! Sasa kama alienda kivya vyake, how come tena unasema alienda na hoja kwa niaba ya UKAWA? Ina maana huko CHADEMA/UKAWA mtu anaweza tu kuamka asubuhi akafanya jambo na akasema hilo ni kwa niaba ya chama bila jambo husika kujadiliwa na kupitishwa na vikao vya chama au angalau uongozi?

Anyway, wenye akili zetu tulifahamu hamkusimamisha mgombea Songea Mjini kwa sababu mnafahamu Wangoni wamekunywa maji ya bendera ya kijani and there's no way mngeweza kushinda kule!!

Kuficha aibu ya kushindwa, mkajifanya kususia!!

Siha and Kinondoni mnafahamu mnaweza kushindwa angalau kwenye moja ya hayo majimbo kwa sababu you still have ufuasi mkubwa kule!!

Kilichofanyika, ni Mjasiriamali Freeman Mbowe kukaa na EL kisha wakakubaliana namna pekee ya kumsafisha Lowassa ni kujifanya alienda Ikulu kukutana na kujadiliana na rais na hatimae majadiliano hayo yamezaa mazingira mazuri kwa CHADEMA kuweza kushiriki uchaguzi!!!
 
Chadema ni wasanii,wameamua kurudi uchaguzini,ili kuondoa aibu wametumia kikao cha lowassa na Rais wetu,Lowassa keshasema aliitwa akajiunge ccm,nyie wapuuzi mnasema wamekubaliana uchaguzi utakua huru,kwa hiyo tume huru hamuitaki tena?

Semeni tu mliogopa aibu ya kushindwa mkaona hakuna haja ya kupoteza pesa,Siha ipo kaskazini hamuwezi kuacha kushiriki na kinondoni kuna manispaa yenu lazima mtataka kubahatisha
 
Mzee Mwanakijiji ulituambia hapa jukwaani kwamba ulikuwa na tetesi kwamba kiongozi mkubwa wa upinzani (Lowassa) angefanya press conference ya kufanya maamuzi magumu. Can you provide an update on that? Sijamuona huyo kigogo wa upinzani kufanya hiyo press conference ya maamuzi magumu (kurudi CCM). You insinuated that Lowassa would return to CCM; he didn't. CCM watakuaibisha Mzee ... heshima uliyokuwa umejiwekea hapa jukwaani itayeyuka yote. Angalia mwenzako Slaa, he doesn't talk about human rights and democracy anymore; although he was a leader of a democratic party and his family was beaten and bled for democracy and human rights.

By the way Sir, what's your view on the current allegations of the abuse of human rights by the Magufuli's government in Tanzania. You realize, though, even your colleague Max Mello continues to be harassed by your beloved Magufuli's government for no reason.

Natumaini ulinisoma vizuri nilivyoandika hoja yangu ile; lakini kama hajarudi jana haina maana hatorudi kesho. Lakini Zaidi ni lazima ujiulize kama Lowassa kuendelea kubakia Chadema inaisaidia au la. Uliona jinsi gani kule kukutana na Magufuli Ikulu kulivyosababisha sintofahamu CHADEMA? Masuala yote haya mengine yanazungumzika na wengi tayari wanayazungumza; na sisi wengine tunayazungumza labda bila kunekana tunazungumza hivi. Wakati mwingine siyo hekima kuchochea moto unaounguza rafiki!
 
Back
Top Bottom