Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Sasa Ccm ina ubaya gani tena kama mafisadi wanaenda chadema? Msururu wao, Nazir Karamagi,Andrew Chenge, na the like, wote wanahamia chadema na ccm itabaki safiiii!

Na wezi wa EPA, waliouza nyumba za serikali, ESCROW, deep green finance, meremeta wote wameenda CHADEMA?
 
Jamaa kadharirishwa sana na JK hadi sisi mashabiki wake tulikuwa tunawaza kama kafanyiwa Lowassa hata vipi watoto wa mafukara kama sisi!!? Mungu ni mwema kwa kumpa ujasiri mwingine Lowassa.

Kavumilia sana,sasa kama ni mtu wa visasi ndo hapo,maana kamzungukia vizuri
 
Duh! Ina maana yale mapovu mliyokuwa mnatoa kuwa Lowasa ni fisadi yalikuwa bure kabisa? Basi tusisikie upuuzi wowote wa ufisadi

Tutakutana majukwaani utaona Nani alikuwa fisadi
 
ktk siasa duniani kote hakuna lisilowezekana kuanzia USA,Senegal,Zambia,Madagascar,Kenya,Malawi...
kweli bana, kwenye siasa hakuna rafiki wala adui wa kudumu itategemea maslahi na kuwa na mtu huyo kwa wakati huo.
 
Lowassa ni mtu mzima na anajua afanyalo.Naomba asije aga dunia bila kutuambia sakata la Richmond lilikuwaje!?
 
Vita ni vita Muraaa...
hatimaye Lowasa aingia katika rekodi ya kukuza
siasa za upinzani.
 
Aliye na uthibitisho wa ufisadi wa Lowassa na aweke bayana, si kuja humu na kupiga debe tupu. Leteni thibitisho wa ufisadi wake kwanza. Acheni papara wandugu.
 
Utamu wa ngoma ndio unaanza SIASA tamu, wasafi na wachafu wote ndani ya nyumba.
 
Sitaki kukumbuka kilichowai semwa na Dr.Silaa na Mbowe kuhusu Mzee wa Mafuriko
 
wengi watu tulinaichukia ccm sababu ya ufsad Wa akina lowasa,Leo eti lowasa huyuhuyu asaidie kuiondoa ccm,to hell wrote waliotusaliti.tutawazomea wrote walioshiriki hii uovu.
 
CHADEMA mbona hawaeleweki!!! Lowasa fisadi wanamkaribishaje? Basi wamsafishe maana wameimba sana wimbo kuwa Lowasa ni fisadi.
Lowassa akihudhuria kikao Kamati kuu CHADEMA

View attachment 271482
Waziri Mkuu Mstaafu wa JMT Mh. Edward Ngoyai Lowassa, akisalimiana na viongozi na wanachama wa CHADEMA

View attachment 271483
Waziri Mkuu Mstaafu wa JMT Mh. Edward Ngoyai Lowassa akiwa Meza Kuu na viogozi wa CHADEMA
 
Nadhani Huu ndio mwanzao wa mabadiliko ya kisiasa nchini Tanzania.
Tulitarajia kuona wanachama wengi waliooona serikali tawala ikifumbia macho ufisadi na utendaji mmbovu wa watendaji wake, wakihama vyama na kwenda amabapo wanaweza wakatoa sauti zao kwa uhakika na usalama zaidi, ila bado uthubutu wa baadhi ya wanasiasi uko chini...ila utaongezeka...Lembeli amefungua njia, na hili la Lowasa lilitarajiwa saana, ILA quotion yangu ni kwamba, Opposition iwe na Jicho la Tatu (3) katika kufuatilia numbers...NUMBERS...Kwani Ushindi is all about NUMBERS...SUBSTRACTION...na ADDITION na Multiplication ili kupata Asilimia...Haya yote yatawezekana endapo..Zoezi la BVR..linaloendelea litaweza kufanyiwa...VERIFICATION....UHAKIKI wa wale wote waliojiandikisha...ili tuwe na number kamili...Tuweze kuja kutoa, na kuzidisha tupate ASILIMIA ya MSHINDI...

Goli la mkono liko hapo...Lets BE MACHO...

Nawakilisha, na naungana na watanzania wote katika kipindi hiki cha mpito cha Mabadiliko endelevu ya SIASA Tanzanai..
Mungu Endelea Kuibariki Tanzania Yetu, na watu wake!!!!

Nashangaa Watanzania wengi wanaogopa mabadiliko, hivi wanafikiri ni kazi ndogo kuiondoa ccm madarakani iliyokaa kwa miaka zaidi ya 40?
Wanahitajika watu strong kama Lowasa.
 
Back
Top Bottom