Kama kijana mtafutaji ni muhimu kujiunga na jumuiya mahali unapoishi

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,341
51,907
KAMA KIJANA MTAFUTAJI NI MUHIMU KUJIUNGA NA JUMUIYA MAHALI UNAPOISHI

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Umeenda mbali na nyumbani, ni aidha kutafuta maisha au umepelekwa na serikali. Moja ya mambo muhimu kabisa ya kufuata ni pamoja na kujiunga na jumuiya za kijamii.

Kama ni mkristo nenda Kanisani. Kama ni muislamu nenda msikitini huko. Fuata mambo ya dini yako kwa bidii na juhudi huku ukiendelea na harakati zako za maisha.

Kama wewe sio muumini wa mambo ya dini. Jiunge na jumuiya za kabila lenu ambalo lipo mahali anapoishi. Changia kulingana na uwezo wako.

Ni kweli unahitaji faradha lakini hiyo haimaanishi ati ujifiche kwa kiwango cha kutisha.

Ni kweli labda mahali anapoishi sio pazuri. Haujajipata vizuri kiasi kwamba unaona aibu kukaribisha wanajumuiya wenzako Ghettoni kwako. Lakini hiyo haikuzuii kutojiunga na jumuiya.

Jumuiya zinafaida na hasara zake. Lakini faida ni nyingi zaidi.

Ni rahisi kupata msaada ukiwa ndani ya jumuiya kuliko ukiwa jeshi la mtu mmoja.

Vijana wengi ambao wanaomba pesa mitaani au kwenye mitandao ya kijamii wengi wao hawapo katika jumuiya hizi aidha za kidini au kikabila.

Shughuli za mtaani kwenu hushiriki. Viongozi wa serikali za mtaa hawakujui kwa sababu hushiriki wala huna Tija yoyote kwenye huo mtaa. Haipo hivyo vijana. Kijana lazima uwe na Tija.

Kijana unajifanya unataka kuishi maisha ya kijasusi wakati majasusi wote moja ya kanuni zao ni kushiriki na kujichanganya na jamii. Ati wewe unajifanya hutaki mazoea na Watu wa mtaani kwako. Kwa kipi hasa?

Ukitoka Kanisani au msikitini, Nduki! Hutaki hata Watu wasalimiane na wewe na wala wewe huna habari za Watu. Umechizika wewe. Mantiki ya jambo hilo ukifuatilia ni kutokujiami, na inferiority complex ya kutotaka Watu wakujue kwamba wewe bado hujajipata, wewe bado ni njaa.
Hivi unafikiri ukiwa hujajipata ni siri? Au unafikiri ukijipata nako ni Siri.

Kuwa na Tija. Hakikisha Watu wanafurahia uwepo wako. Wajue huyu ni kijana/ Binti Haswa.
Hata wazee wakikuona watamani uoe binti zao. Au uolewe na vijana wao.
Sio upoupo tuu. Mambo hayaendi hivyo.

Kufanya kazi zenye kipato duni haikupunguzii heshima yako. Ifanye kwa furaha na kuipenda Watu nao wataipenda na kukupenda. Sasa unaishi mtaani hutaki Watu wajue unafanya kazi gani kwa mantiki ipi? Unaogopa dharau, ukiwa na akili hizo bado utaonekana haujakua.

Moja ya dalili kuwa umekua Watu wanachoangalia ni ufanyaji wa kazi. Je unafanya kazi? JE unafanya kazi kwa weledi, je unaipenda kazi yako?

Unajificha nini? Hujafunzwa kujiamini sio? Unaogopa hutapata Mwanamke mzuri wa kumwoa. Mbona sisi wengine tumeoa wake wazuri pasipo hizo kazi nzuri, pasipo hizo pesa ambazo wengi wanasema wakizipata ndio waoe Wanawake wazuri. Hatuna magari wala nyumba lakini tunafurahia maisha.

Vijana hakuna mtu anayeweza kukudharau kwa kufanya kazi halali. Hakuna mtu atakayeweza kukudharau kwa kuwa muadilifu. Hakuna! Wewe tuu ndio haujiamini.

Tumia kila kipaji, Karama, ujuzi uliojaliwa na Mungu uwe na Tija katika jamii yako.
Elewa, unapoanza utaanzia chini, chini ndipo utakapojitambulisha.

Ukipatwa na shida ni rahisi kusaidiwa na kusaidika. Unapiga simu moja tuu. Kila mtu anatamani kukusaidia na anajisikia raha kuwa moja ya Watu aliokusaidia.

Zingatia, haufanyi hayo ili upate faida ya msaada baadaye siku yakikukuta. Bali unafanya hivyo kwa sababu unapenda kuwa na Tija. Yaani uwepo wako uwe na Matokeo chanya kwa wengine bila kujali watakusaidia au laa.

Acha Nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Hakika umenena Jambo jema Sana Robert.
Kujiunga na jumuiya Ni Jambo la heri Sana kwa sababu Ni rahisi Sana mtu kupata msaada pindi anapopatwa na shida.
 
uzi upo vzur umeongea vya maana ving ila tatizo mitaa mingi saiv ivo vikund ni vya wana ccm tu na vya kinamama wa vikoba amna vikund kama unavovisema na kama vpo bas sehem chache sana ila ving vya kanisa au sisiem au vikoba na upatu mikop kausha dam ni cancer pia ht dada zetu wanaoshrik weng tunaona wanajpat na msongo wa mawazo kila mda kuit madalal wanauza aset inshot vnawarudisha nyuma badaa yakuenda mbele izo jumuia michango kbao na wanaofaidika wale ma goat tu hawa wanajumuia wadgo wanakamuliwa yn inshot uamnif ziro asas nyng wapgaj wamejaa
 
1.Tegemezi Jimbo
2. UWATA
3. Dirisha la Askofu
4. Mchango mwengine.
5. Mchango mwengine tena
6. Yani mpaka msemeee 😂😂😂
 
Mimi nina miaka minne ugenini sinaga mazoea hata na jirani. Na huku nilipo huwa nasikia kuna kitu wanaita ZENGO, ila sijawahi kushiriki.

Inaniwia vigumu maana mimi siwezi hayo maisha ya kujuana sana.
Kwakufanya ivyo unatatua tatizo ambalo lingekuganda hadi ungetamani kuhama.. vikundi vingi ni uhuni tu.. sishauri mtu kujiunga na kikundi chenye Agenda ndeeefu.. hapo ni mradi wa wanao ratibu hicho kikundi..
Lkn kwa kuwa binadamu ni kiumbe wa kijamii jumuika kwenye mazoez dk30-60 kila mtu na mishe zake kila mtu anaondoka na jasho lake..
 
KAMA KIJANA MTAFUTAJI NI MUHIMU KUJIUNGA NA JUMUIYA MAHALI UNAPOISHI

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Umeenda mbali na nyumbani, ni aidha kutafuta maisha au umepelekwa na serikali. Moja ya mambo muhimu kabisa ya kufuata ni pamoja na kujiunga na jumuiya za kijamii.

Kama ni mkristo nenda Kanisani. Kama ni muislamu nenda msikitini huko. Fuata mambo ya dini yako kwa bidii na juhudi huku ukiendelea na harakati zako za maisha.

Kama wewe sio muumini wa mambo ya dini. Jiunge na jumuiya za kabila lenu ambalo lipo mahali anapoishi. Changia kulingana na uwezo wako.

Ni kweli unahitaji faradha lakini hiyo haimaanishi ati ujifiche kwa kiwango cha kutisha.

Ni kweli labda mahali anapoishi sio pazuri. Haujajipata vizuri kiasi kwamba unaona aibu kukaribisha wanajumuiya wenzako Ghettoni kwako. Lakini hiyo haikuzuii kutojiunga na jumuiya.

Jumuiya zinafaida na hasara zake. Lakini faida ni nyingi zaidi.

Ni rahisi kupata msaada ukiwa ndani ya jumuiya kuliko ukiwa jeshi la mtu mmoja.

Vijana wengi ambao wanaomba pesa mitaani au kwenye mitandao ya kijamii wengi wao hawapo katika jumuiya hizi aidha za kidini au kikabila.

Shughuli za mtaani kwenu hushiriki. Viongozi wa serikali za mtaa hawakujui kwa sababu hushiriki wala huna Tija yoyote kwenye huo mtaa. Haipo hivyo vijana. Kijana lazima uwe na Tija.

Kijana unajifanya unataka kuishi maisha ya kijasusi wakati majasusi wote moja ya kanuni zao ni kushiriki na kujichanganya na jamii. Ati wewe unajifanya hutaki mazoea na Watu wa mtaani kwako. Kwa kipi hasa?

Ukitoka Kanisani au msikitini, Nduki! Hutaki hata Watu wasalimiane na wewe na wala wewe huna habari za Watu. Umechizika wewe. Mantiki ya jambo hilo ukifuatilia ni kutokujiami, na inferiority complex ya kutotaka Watu wakujue kwamba wewe bado hujajipata, wewe bado ni njaa.
Hivi unafikiri ukiwa hujajipata ni siri? Au unafikiri ukijipata nako ni Siri.

Kuwa na Tija. Hakikisha Watu wanafurahia uwepo wako. Wajue huyu ni kijana/ Binti Haswa.
Hata wazee wakikuona watamani uoe binti zao. Au uolewe na vijana wao.
Sio upoupo tuu. Mambo hayaendi hivyo.

Kufanya kazi zenye kipato duni haikupunguzii heshima yako. Ifanye kwa furaha na kuipenda Watu nao wataipenda na kukupenda. Sasa unaishi mtaani hutaki Watu wajue unafanya kazi gani kwa mantiki ipi? Unaogopa dharau, ukiwa na akili hizo bado utaonekana haujakua.

Moja ya dalili kuwa umekua Watu wanachoangalia ni ufanyaji wa kazi. Je unafanya kazi? JE unafanya kazi kwa weledi, je unaipenda kazi yako?

Unajificha nini? Hujafunzwa kujiamini sio? Unaogopa hutapata Mwanamke mzuri wa kumwoa. Mbona sisi wengine tumeoa wake wazuri pasipo hizo kazi nzuri, pasipo hizo pesa ambazo wengi wanasema wakizipata ndio waoe Wanawake wazuri. Hatuna magari wala nyumba lakini tunafurahia maisha.

Vijana hakuna mtu anayeweza kukudharau kwa kufanya kazi halali. Hakuna mtu atakayeweza kukudharau kwa kuwa muadilifu. Hakuna! Wewe tuu ndio haujiamini.

Tumia kila kipaji, Karama, ujuzi uliojaliwa na Mungu uwe na Tija katika jamii yako.
Elewa, unapoanza utaanzia chini, chini ndipo utakapojitambulisha.

Ukipatwa na shida ni rahisi kusaidiwa na kusaidika. Unapiga simu moja tuu. Kila mtu anatamani kukusaidia na anajisikia raha kuwa moja ya Watu aliokusaidia.

Zingatia, haufanyi hayo ili upate faida ya msaada baadaye siku yakikukuta. Bali unafanya hivyo kwa sababu unapenda kuwa na Tija. Yaani uwepo wako uwe na Matokeo chanya kwa wengine bila kujali watakusaidia au laa.

Acha Nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Unafahamu kwamba ulimwengu ni sehemu hatari sana na kila mtu ana lake moyoni? Unafahamu kwamba hakuna mtu aliyekamilika? That nobody is fuking perfect? Maana yake kuna watu watakuchukia tu bila sababu hivyo hauwezi kupendwa na kila mtu hata ufanye nini?
Unafahamu kwamba kila mtu ana wivu?
Ufahamu kwamba watu wanapenda kutumia wenzao na kulaumu wenzao? Kama unavyofanya wewe hapa? Sababu ni kitu rahisi? Sababu kila mtu ni mbinafsi na anajiona au anapenda kujiona bora kuliko mwingine? Kama unavyofanya wewe hapa?

Unafahamu kwamba mtu mwema kweli hatohitaji sababu ya kukusaidia? Na kama atahitaji sababu ya kukusaidia basi huyo sio mwema bali ni mshenzi anayependwa kusujudiwa na kunyenyekewa?

Unafahamu watu wa aina yako ni sababu tosha ya kila mtu kuishi maisha yake binafsi bila kufuatiliana wala kuingiliana?
Hapana, bila shaka hauwezi kujua hilo sababu uko busy kuhukumu wengine.

Ukweli ni huu hapa:
Ishi maisha yako, pambania familia yako na wewe mwenyewe. Mengine nje ya hapo hayakusu, na kama ukifanya hivyo basi walimwengu na dunia watakutumia, wakichoka watakufanya doormat, watakukanyaga na kukutupa. Then utabaki wewe na familia yako peke yako.
Usisikilize hizi fairly tales za huu uzi.

Dunia imejaa washenzi, matapeli, wadhurumishi, mafisadi na makatili wenye roho mbaya. Au wewe unadhani vita vya dunia vilitokea Mars? Big fuking NO. Vilitokea hapahapa. Ni survival for the fittest. Kuwa boya lele mama linaloendeshwa na mawazo ya watu wanataka nini! Then utakufa kifo cha mende.

Huu uzi umejaa pumba.
 
Nina vikundi 7 , jumuia na zengo niko vizuri kila mwaka lazima nifanye kisherehe hapa kwangu,,,, michango na zawadi ni faida tosha ya kuongeza mtaji!! Vikundi jumuia ni muhimu hasa ukiwa na familia.
 
uzi upo vzur umeongea vya maana ving ila tatizo mitaa mingi saiv ivo vikund ni vya wana ccm tu na vya kinamama wa vikoba amna vikund kama unavovisema na kama vpo bas sehem chache sana ila ving vya kanisa au sisiem au vikoba na upatu mikop kausha dam ni cancer pia ht dada zetu wanaoshrik weng tunaona wanajpat na msongo wa mawazo kila mda kuit madalal wanauza aset inshot vnawarudisha nyuma badaa yakuenda mbele izo jumuia michango kbao na wanaofaidika wale ma goat tu hawa wanajumuia wadgo wanakamuliwa yn inshot uamnif ziro asas nyng wapgaj wamejaa
Mwandishi hawezi kukuelewa maana amekabidhiwa uongozi wa jumuia hivi karibuni so wanakula michango yenu ndio maana anawamobilize watu humu.
In short ni hivi tusipangiane maisha
Halafu kuanza kuhisi kuwa njia unazopita wewe ni sahihi na kutaka wengine wazipite ni kiherehere kisicho na maana
Ukiishi wewe na wenzio baadhi inatosha wengine waache na njia zao over.
 
Back
Top Bottom