Dr Kigwangala, Safi sana kwa kazi nzuri unayofanya.
Nakuomba pia kwa kuwa wewe ni Waziri wa Afya kuna hii kitu mtaani MAMA LISHE wanapika chakula huku wakifunikia mifuko ya Plastiki ili kiive haraka, Hii ni hatari sana kwa afya. Naomba Mheshimiwa Ofisi yako itoe elimu na kuzuia jambo hili kwa kuwa linaweza kusababisha kansa huko mbeleni.
Kitu kingine Mheshimiwa, haya maji kwenye chupa za Plastic, ni hatari sana pale chupa hizo zinapopigwa na jua na zile plastic chemicals kudisolve ndani ya maji hayo, naomba pia ofisi yako ifanye kitu katika kuweka viwango vya uzalishaji, usambazaji na utunzwaji wa maji ya aina hii