Tindo
JF-Expert Member
- Sep 28, 2011
- 59,009
- 103,396
Tindo kwa kuwa una muda wa kuchangia, ukiwa na michango bora utafanya JF KUWA BORA.
Lazima tujaribu kukuweka vizuri zaidi maeneo ambayo anahitaji ubora zaidi.
Nashukuru kwa michango yako japo ---------- punguza ushabiki, weka michango elimishi. Chadema ni chama, na Chadema sio siasa.
Punguza kupinga kila kitu, weka mawazo tofauti na isiwe ni ubishi tuu.
Nilichokuambia sijakuambia kwa bahati mbaya, nimekuambia nikiwa na akili zangu timamu. Nina uwezo wa kuchangia kwa busara, heshima, mantiki na lugha chafu vilevile, tena kwenye lugha chafu ndio eneo ninalolimudu vyema. Ukija na mchango bila kuweka vijembe, kejeli nk nitakupa majibu stahiki, tena yenye staha hata kama tutapishana mitazamo. Na kimsingi sina tatizo la kupishana mitazamo, kwani ndio afya ya mijadala.
Sina tatizo na mtazamo wako kwangu, na unapoona mapungufu yangu, lakini sio lazima mtazamo wako uwe muamuzi wa mitazamo yangu, hata kama ungependa iwe hivyo. Sasa hili si kosa lako bali ni langu. Kuhusu kupinga kila kitu, inaonekana hilo neno unalitumia kama fashion, mtu yoyote mwenye mitazamo tofauti na ww unaona anapinga kila kitu. Kwanza sipingi kila kitu, labda uniwekee ushahidi. Sijawahi kupinga ujenzi wa barabara, shule, vituo vya afya, umeme kutokukatika mara kwa mara kama ilivyokuwa kwa Kikwete, japo sisifii kama ambavyo ww ungependa nifanye. Lakini ununuzi wa ndege tena wa cash, ninapinga na nina sababu za kutosha hata kama hutaziafiki. Halafu sibishani kwenye hoja, bali naelimishana, na sio rahisi unilishe mitazamo au matamanio yako kirahisi. Kama unaona nabishana hilo sio tatizo kwangu, maana sina hati miliki ya tafsiri zako.