Kigoma: Rais Magufuli kupokea ugeni wa kiserikali wa Rais wa Burundi, Mh. Evariste Ndayishimiye

Kennedy

JF-Expert Member
Dec 28, 2011
49,015
54,297
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, CP Thobias Andengenye anapenda kuwaarifu wananchi wa Mkoa wa Kigoma kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dkt John Pombe Joseph Magufuli kesho tarehe 19.09.2020 atapokea ugeni wa kiserikali, wa Rais wa Burundi, Mh. Evariste Ndayishimiye, ambaye atafanya ziara RASMI ya KISERIKALI nchini Tanzania hapa mjini Kigoma.

Mapokezi ya Mh. Rais Evariste Ndayishimiye yatafanyika katika uwanja wa Lake Tanganyika. Wananchi wote mnaalikwa kufika Uwanja wa Lake Tanganyika saa mbili kamili asubuhi bila kukosa. Wananchi pia mnajulishwa kuwa, baada Mapokezi ya Ugeni huo na salaam kwa Wananchi, Mheshimiwa Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli na Mgeni wake watafungua Jengo la Mahakama Kuu Kigoma katika eneo la Bangwe saa Tatu Kamili Asubuhi. Wananchi wote mnaalikwa pia kufika katika shughuli hiyo.
 
Ndio maana tunahitaji katiba mpya.huku anapiga kampeni huku anaahidi kujenga barabara na kugawa fedha za walipa kodi hovyo kwa wananchi.
Ulitaka nchi isiwe na Rais wakati wa uchaguzi?? Niambie nchi gani duniani ambayo wakati wa uchaguzi huwa haina Rais? Umbumbumbu wa sheria unawasumbua sana wanasaccos mkidanganywa na huyo zezeta wenu mnafikiri anajua sana sheria!!
 
We kenge.ee wa lumumba sheria ikiwekwa vizuri itamzuia Rais aliyeko madarakani kutumia mwanya wa nafasi Alonayo "incumbent position " kushawishi Umma kumchagua tena. Nenda shule tena.
Rais kwa mamlaka yake hawezi kutenda kazi zake pasipo kuonekana kama anaitumia vibaya ofisi yake.

Na huwezi kumkwepa rais kama bado unao mawaziri wanaofanya kazi zao katika kipindi cha kampeni.

Viapo vipya kwa maana ya mawaziri kuapishwa ndio jambo lisiloweza kufanyika kipindi hiki kwani hakuna shughuli za bunge zinazofanyika ndani ya jengo la bunge.
 
Waanze Marekani mode wenu
Marekani uchaguzi upo wazi.rais ambaye yupo ofisini "incumbent president " anatangaza fund raising na majaji wa mahakama kuu wana verify. Kwaajili ya kampeni.huku Tanzania magari ya serikali yanawekwa namba private na kujazwa mafuta ya serikali kumpigia kampeni magufuli.
 
Marekani uchaguzi upo wazi.rais ambaye yupo ofisini "incumbent president " anatangaza fund raising na majaji wa mahakama kuu wana verify. Kwaajili ya kampeni.huku Tanzania magari ya serikali yanawekwa namba private na kujazwa mafuta ya serikali kumpigia kampeni magufuli.
Bhalaa
Ila Tanzania Bado Safari Ni Ndefu Mpaka Tumechoka
 
Back
Top Bottom