Kigoma airport aibu Waha mpoooo??

KakaKiiza

JF-Expert Member
Feb 16, 2010
11,578
8,600
Kigoma%2BAirport%2B1.JPG Kigoma%2BAirport.JPG Kingerza cha Kiha Du kazi bado ipo kwelikweli!!
 

hizi mind ur languaage ziko nyingi,cjui wahusika au viongozi wa hapo hawaoni au?
 
Hapa ndugu zangu tuache mambo ya Ukabila hebu tuangalie ukweli wa mambo yenyewe ulivyo. Hivi kweli imekaa vizuri hii? Hapa sasa tusiangalie nani kaandika awe Muha au Mhaya ama Mkwere, ukweli unabaki pale pale kwamba huu ni ujinga usio kifani! Meneja upo hapo ofisini haujaona kilichoandikwa hapo? Au wewe kazi yako ni kutolea mafyuzi tu viti vyetu vya umma?

Hebu futeni haraka hapo! Na wewe uliyeleta hii thread kwa nini hukuwaonesha hao wachovu huo utumbo wao? Yaani unadiriki kupanda ndege na kuondoka bila kuwajulisha? Mungu akusamehe!!!!!!!

Kama kuna mwana-JF wa hapo Kigoma ameiona hii thread tunampa kazi kesho asubuhi uamkie huko na uwaambie kama hawajui Kiingereza si wangetafuta mtu yeyeote anayefanya kazi kwenye mashirika ya kimataifa yaliyojazana hapo Kigoma?

Kwaherini
 
Kiinglishi kaka ni "global" issue hapa nchini kwetu...

Nenda pale CRDB PPF Tower - katikati ya jiji lenye wasomi lukuki na benki yenye "wasomi" - utakutana na kibao kwenye dirisha la teller kimeandikwa "TEMPORARY CLOSED"

Upo hapo?
 
Shida siyo waha wala wahaya ila ni serikali dhaifu inayoongozwa kwa misingi ya kujuana na haizingatii misingi ya taaluma husika.usishangae hata huyo meneja wa uwanja ukakuta ni standard seven tena ya mzee ruksa maana ya nyerere hiyo lugha alhamdulilah haikuwapa shida.
 
Waha naona mumekasirika medhalilika??ehe na hii thread mtanitoa macho chonde!!!!:smile-big:
 
Thread haina mantiki wala tija

Siyo kweli kwamba hii tread haina tija. Kwa namna fulani inatuonyehsa udhaifu katika mambo ya msingi. Uelewa wangu ni kuwa mkuu wa uwanja ni lazima atakuwa ni msomi tena mwenye digrii (na 90% anaweza asewe Muha au mwenyeji wa Kigoma).

Namna nzuri ya kuijadili hii tread ni kuleta na nyingine pia ambazo zina makosa kama haya (Mfano huyo alieleta ya hilo jengo karibu na CRDB), tujadili chanzo na jinsi ya kurekebisha. Kuibeza hii tread kwa kuwa kabila fulani limetajwa ni kuwa tunapoteza mwelekeo. Hivi kukosea lugha katika eneo kama hilo tunaliona ni jambo dogo? UHutu mkuu wa hiyo sehemu ukimwabia asimamie uandikaji wa hundi itakuwaje? Tujadili hoja kwa nguvu ya hoja, tusitoe hoja ya nguvu!!!
 
Ila uwanja niwenu jamni sisi kwetu bukoba hakuna ujinga kama huu!!

Sasa tunaanza kujadili kwa misingi ya jiografia. It does not matter where it is happening - in fact, it is everywhere - hata maeneo ya vyou vikuu!!
 
Kuna matatizo mengi sana katika hayo maandishi na sio English pekee. Hii inadhihirisha jinsi watu wasivyokuwa makini katika kazi. Hivi kweli hakuna hata mfanyakazi wa hapo uwanjani aliyeona hii kitu?

Ukosefu wa uwajibikaji na ufuatiliaji ndio matatizo yetu. Si ajabu walimpatia kazi ''painter'', wakachakachua malipo yake na biashara ikaishia hapo. Hakuna aliyekumbuka kuja kukagua kazi.

Kama mambo ''madogo'' kama haya hatuyaoni/hatuyasomi, vipi kwenye mkataba wenye kurasa zaidi ya 70, tena kwa kiKoloni? - no wonder DOWANS, Richard Monduli et la imekubwa wimbo tuliouzoea.
 
Usijali....soon huo uwanja utakuwa ka' wa Dubai....si 'mkwere' keshasema!
 
Siamini kama kweli hapa ni Kigoma...Nimeguswa kiasi napanga kutoa nauli yangu binafsi niende nikakwangue maandishi hayo yaliyojaa dhalili!
Hii ni aibu kwa waliokabidhiwa dhamana ya kusimamia viwanja(Tanzania Airports Authority)..kama wanakwenda huko na kuona hii hali wakanyamaza kimya inaleta kinyaa!
Na je kiwanja hicho hakina hata aliyeenda darasa kidogo akarekebisha?..hivi Airport Managers wanakuwa na Sifa gani?
Totally confused!...Nadhani hapa ni Bandundu-Congo au la Rwanda!
 
sijaelewa kitu hapo,kwa nini wasiandike tu kimuha.!!!kwanu airport ya beijing kuna kisawhili ?mbona tunaenda na tunarudi.nao watakuja tu
 
Back
Top Bottom