Kifo kupitia mikono ya POLISI – Kosa la Marehemu?

attachment.php

 
Mkandara,

I knew when I mention falsafa, you will come out screaming. You know what not having a falsafa is a falsafa in itself, and in some instances in the best falsafa of all. Kwikwikwi.

Police brutality is something that all of us, regarding our polical affliactions, need to discuss. Expecting that if CHADEMA wins, the party will reform the police force is putting all of your eggs in one basket.
 
Last edited by a moderator:
Zao kubwa, bora zaidi na la mwisho kabisa la TAFAKARI ni MANTIKI...(Reasoning destination=LOGIC-the Climax of Reasoning). Na hakuna MANTIKI kuu ya maisha ya binadamu kama UTU! UTU ndio msingi mkuu wa maisha yetu, UTU ndio sheria asilia, kanuni, ustaarabu na taratibu asilia zipasazo kumfunga binadamu kulinda ubinadamu wake ili asiwe mnyama! UTU ndio MANTIKI iliyo kubwa kabisa!

Tukae chini, tuzame katika tafakari nzito, tufikie kilele cha juu kabisa cha tafakari, tutafikia MANTIKI ya maisha yetu, mimi napenda kuiita UTU!

Falsafa yetu ili iwe na tija kwetu, ni lazima ifungwe na MANTIKI HII = UTU! Falsafa zenye UTU, zitahitaji mfumo mahususi kuzisimamia, mfumo huo utazaa sera sahihi kuusimamia, sera hizo zitahitaji sheria mahususi kuzisimamia, sheria hizo zitahitaji imani, mila, desturi, itikadi, matendo, mitazamo, n.k. mahususi kuzifanya hai! Tunaweza kuanza mfumo hadi Falsafa, vilevile Falsafa hadi mfumo ni sahihi zaidi!

TUKAE CHINI! Nirudie tena, sishangazwi na chochote kitokeacho kwa sasa, kwani HULKA ZA BINADAMU ZINAPOFIKIA UKAMILIFU WAKE ZINAWEZA KUFANYA CHOCHOTE na matokeo yake siku zote huwa HASI, hali kadhalika MANTIKI INAPOFIKIA UKAMILIFU WAKE NAZO ZINAWEZA KUFANYA CHOCHOTE na matokeo yake huwa CHANYA!

Maisha ni Furaha kama haipo ni UPUMBAVU na UPUUZI MKUBWA, na hakuna furaha ya mtu ila watu!

Mungu wetu anaita sasa!

Falsafa ndiyo ingeamua nini kiwepo au kitokee nini kwa wakati gani!

Ni zaidi ya Dira ama msingi! Ni JINSI GANI TUNAPASWA KUISHI kwanini, kwa namna gani, ili iwe nini na kwa nani! Hapo ndipo Falsafa kuu inapohitaji kufanywa maisha yetu halisi, yaani kuanzia ngazi ya imani, mila, desturi, itikadi, mitazamo, mienendo, vitendo, n.k. vitakayosadifu na kufungwa na falsafa kuu. Kisha hayo yatazaa sera bora kusadifu na kufungwa na falsafa kuu, sera hizo zitazaa sheria zitakazosadifu na kufungwa na falsafa kuu, sheria hizo za kiuchumi, siasa na utamaduni zitazaa mfumo utakaosadifu na kufungwa na falsafa kuu! Hapo kila kitakachotokea, au tutakachotaka kufanya, kitapimwa kwa mizani ya falsafa yetu kuu!

TUJIULIZE LEO: Ni falsafa ipi ituongozayo, itufungayo na kututambulisha?

Sheria zinatungwa kwa jinsi watu wajisikiavyo tu, ameshawishiwa na mkewe ama rafiki yake mweupe, anasimama jukwaani "tunataka rais asishtakiwe 'katiba iseme' " wengine nao "tunataka utawala wa majimbo" hawa nao "tunataka serikali tatu/mbili/1" laiti kama tungekuwa na Falsafa yetu, kusingekuwa na malumbano yasiyokuwa na msingi kama yale yanayotokea Dodoma! Kila mtu angepima mawazo yake katika kupata mashiko kwenye falsafa yetu! Kama ameyaona anayawasilisha kwetu.

Ninaamini kabisa haya yatokeayo leo, yasingekuwepo kama tungekuwa na falsafa yetu, labda tu kama ingezaliwa kutokana na HULKA za binadamu na si MANTIKI ya mambo, naita UTU!

Taifa pasi na Falsafa bora, raia wake huongozwa na HULKA na MATAMANIO yao, na hapo UKINZANI ndipo uibukapo, ni chuki na visasi, hofu na umungu kila mtu atapigania kuwa juu ya mwenzake, mauaji kama pombe...matabaka, unyonge, n.k Haipo Falsafa ya kutufunga!

Mungu wetu yu tayari kutushindia vitani, anaita sasa!

Zakumi,

Mkuu wangu shukran sana kwa kuliweka swali hili.. nadhani swala zima linatakiwa kutazwa toka nje ya sanduku la Uchadema au UCCM kwa sababu sio CCM ama Chadema wanaowawezesha Polisi kuwa brutal isipokuwa mfumo mzima wa kiutawala..

Nadhani unakosea unaposema hakuna umuhimu wa Falsafa ya uhai wetu kama WATANZANIA na sio fikra za uhuru wa bendera unaolenga sovereignty na mipaka ya nchi husika..Falsafa ni uhai wa WATU ktk mazingira (A system of values by which one lives) na hizi values ndio huwa Principal ya Utaifa wa watu hao.. Hivyo hata hao unaosema Fascism ni Falsafa kwa watu wale.. Hivyo kuwepo kwa Fascism ndiko kunako tulazimisha sisi kuwa na Principal zinazopingana na fikra kama hizi ili tuwe na zile zinazotulenga sisi kama Watanzania - Principles of reality. Na ndio maana muda mwingi nimesema sana kuhusu sisi kurudi nyuma na kujitazama, kujitambua who we are kwanza kama Taifa, laa sivyo leo hii tusingekuwa tunabishana humu isipokuwa kutazama ethics na values zetu kujua ni wapi tunakosea..Ukiona watu wanabishana juu ya jambo basi elewa ni kwa sababu wamepoteza DIRA hivyo ethics na values..

Binafsi yangu nimekuwa na matatizo na hili neno UTU linapochukuliwa kama faslafa kwa sababu UTU ni ile quality of being human ambapo maswala muhimu ya Uhuru, haki, na Usawa vinapotafsiri fikra, maamuzi na matendo yetu ktk mazingira tuliyopo. Hivyo faslafa kwa mapana yake tunatazama falsafa ya maisha..Haya yanayofanyika Tanzania leo ni kutokana na sisi wenyewe kutothamini UTU hivyo tumepoteza ethics na values hata kwa kutumia logical reasoning tunabishana kutwa nzima. Mtu atasimama kueteta Ufisadi, mwingine atasimama kutetea Polisi kwa sababu hatuna values ktk utu wetu isipokuwa ule anaouthamini yeye..

Kila mmoja wetu humu ana values zake aidha iwe za kiasili au imani ya dini au Upagan na hakuna control tena ndio maana tunazitetea. Jambazi sugu litasifika na kuitwa Pedejee - jizi hili!, Fisadi atasifiwa kwa kuiba mabillioni na kujengea wanawake nyumba na mashangingi na wanaolalamika ndio wenye wivu ujinga na hila. Pengine niongezee kusema (mtanisamehe) hata wakristu hapa janvini hawawezi kumtazama Muislaam kama mwenzao isipokuwa ni WALE, WAO against SISI kama kundi tofauti la kijamii ktk Utanzania wetu hivyo hata kuyasikiliza machungu yao inakuwa bughudha kwao. Amini maneno yangu huwa nashindwa kuelewa kwa nini jamaa zangu wakristu tunapowaambia serikali inawakandamiza waislaam wana question waislaam na sio serikali? halafu unaambiwa tuko pamoja!.. Chadema wanailalamikia serikali kuhusu Mafisadi nchini lakini wanaCCM wanawa question Chadema uhalali wa madai yaokuwa ni uzushi, wadini, wenye wivu na wakosa..

Ni katika hali hii ya utengano wa ambao uemtokana na kutokuwa na dira ya Kitaifa ndio maana kikila mmoja wetu anaiona haki upande wake na dhulma anapokosa..Hata ukimuuliza Chenge kuhusu Ufisadi atakuona mchawi tu kwa sababu kisha jitenga na kundi la maskini, wajinga na wenye maradhi. Vile vile ukimuuliza mwana CCM atakujibu kuwa Chadema wajinga wanalalamika tu kwa kila kitu wakati ni wao wenye kuleta vurugu.

Umoja wetu umesha kwisha vunjika na sii kazi rahisi kurudisha Umoja huu pasipo ku sacrifice UBINAFSI, UMIMI, USISI kwa kutambua sisi ni taifa moja lenye watu wenye tofauti zake za kijamii. Hata Nyerere alianzia hapo kabla ya kubuni Azimio la Arusha maana inakulazimu uanze na Watu (walikotoka na walipo) ktk Mazingira (maliasili na rasilimali zake) ndio unaweza kuipata picha halisi ya unakotaka kwenda. Tukiweza kundoa ubinafsi na kila mmoja kujenga Uzalendo mkubwa utakaolazimishwa na PATRIOT ACT ya kwetu kusisitiza UZALENDO wa kila Mtanzania kufuata falsafa yetu itayolingana na WATU na MAZINGIRA yetu -Principal of reality..

Mitazamo yote hii ya Ubinafsi inatokana na kwamba kila mtu kabeba msalaba wake hivyo badsi hata Chadema wakiingia Madarakani nina hakika watafanya kile wanacho kiamini japokuwa hakitakubaliwa na wengine. Mafisadi watalaani, pengine Polisi watatumiwa kuwanyanyasa wenye nacho na pengine mauaji kutokea..It all round up to what set of ideas or beliefs developed into policies relating to particu


Mkandara. Zakumi na JingalaFalsafa, KUHUSU FALSAFA YA TAIFA!

Guys lets just be serious for some seconds!

1. Awali Mkandara ulituambia kuwa tuna various DIFFERENCES at individual level which form DIVERSITY at a community a Nation level.

2. THEN, Ukapendekeza kuwa tutafute kitu ambacho ni COMMON out of all differences which can form our community with its diversity respected and well taken care!

3. JangalaFalsafa anakubaliana na Mimi kuwa that COMMON UNITY which unity us all Should be UTU whatever that term stand for!

4. JangalaFalsafa ameonyesha jinsi ya kujenga sera, mifumo and policy from UTU which will meet the need of the TOTAL DIVERSITY! WHICH CAN BE TERMED AS FALSAFA YA TAIFA!

5. FALSAFA YA TAIFA, kama Zakumi ataniruhusu kuuita UTU WA TAIFA Haitapingwa na CCM, CHADEMA, WAKRISTO, WAISLAM, POLISI,WAPAGANI,MAKABILA, UKANDA,MASIKINI, TAJIRI ... NAME ALL THE DIVERSITIES !!!Haitapingwa maana jamii nzima itaelimika juu ya dhani hiyo na kuiona ya thamani kubwa kuliko hata tofauti zao.

6. Elimu ifanyike kuwaamsha Watanzania kuhusu umoja wao ambao hauwezi kupuuzwa wala kuchezewa na chochote kile ndani ya kuheshimiana na kuridhiana kwenye kila tofauti zetu na kutukuza umoja wetu kwa kila hali.

Je hii ndio namana ya kejenga falsafa ya Taifa itakayo liokoa taifa hili lisitumbukie kwenye giza kubwa lililoko mbele yake?
 
Nakubaliana na Mario Puzo Pia, ila at the end of the day hata kama haoneshi anger ni mtu wa kuchukua 'action' mradi apata kile ambacho kapanga. Katika hili naweza tumika msemo ambao naukubali sana katika kupanbana na adui hasa katika vita (toka katika kitabu cha The Art of War), ni ya centuries ago but still applicable to any war which could ever occur.

“If your enemy is secure at all points, be prepared for him. If he is in superior strength, evade him. If your opponent is temperamental, seek to irritate him. Pretend to be weak, that he may grow arrogant. If he is taking his ease, give him no rest. If his forces are united, separate them. If sovereign and subject are in accord, put division between them. Attack him where he is unprepared, appear where you are not expected.” - sun wu (Chinese Military Strategist).
AshaDii,

Nimesoma sana where I have blued! Inaonekana una insight fulani but honestly simalizii kujua kabisa kabisa kuwa nini hicho kimekusumuka kusema hivo? Najua hujali kufafanua ... !
 
Last edited by a moderator:
Nakubaliana na Mario Puzo Pia, ila at the end of the day hata kama haoneshi anger ni mtu wa kuchukua 'action' mradi apata kile ambacho kapanga. Katika hili naweza tumika msemo ambao naukubali sana katika kupanbana na adui hasa katika vita (toka katika kitabu cha The Art of War), ni ya centuries ago but still applicable to any war which could ever occur.



“If your enemy is secure at all points, be prepared for him. If he is in superior strength, evade him. If your opponent is temperamental, seek to irritate him. Pretend to be weak, that he may grow arrogant. If he is taking his ease, give him no rest. If his forces are united, separate them. If sovereign and subject are in accord, put division between them. Attack him where he is unprepared, appear where you are not expected.” - sun wu (Chinese Military Strategist).

Is it a concidence you read the books that I read? Adui yetu wote ni mtu anayetaka kutuona tunasambaratishana kwa ajiri ya manufaa yake binafsi. Huyu tuombe Mungu amrudi na tumkate kwa nguvu zetu zote.
..
Ndahani,

Nimwekea buluu sehemu hiyo! Adui yetu wote ni mtu anayetaka kutuona tunasambaratishana kwa ajili ya manufaa yake binafsi!

Mara ya kwanza nilifikiri nimeelewa vizuri na kuwa huu mtizamo utatufaa kama Taifa! Ghafla nikagundua kuwa CDM Watautumia kwa Mtizamo wao, CCM hivyo hivyo Polisi nao hivyo hivyo ....
 
Last edited by a moderator:
Azimio Jipya,
Adui yetu wote ni mtu anayetaka kutuona tunasambaratishana kwa ajiri ya manufaa yake binafsi
Unaona jinsi msemo huu unavyoweza kutubabaisha..Tunaposema Adui yetu? huyu adui ni nani maana CCM wanaweza kusema hivyo, Chadema wanaweza kusema hivyo, CUF, Waislaam, wakristu, Wahindi, waarabu, weusi au Wazanzibar wanaweza kusema hivyo...Na hii yote inatokana na sisi kutojitambua kama Taifa moja na watu gani. Hadi leo hii we have nothing in common isipokuwa politics zetu zinaelemea ktk KUTAWALA ama KUTAWALIWA ktk mipaka ya nchi huru.

Unajua kwa nini Nchi za majirani zinatupiga bao leo hii?.. Ni kwa sababu wanajijua wao ni WATU gani na nini ethics na Values zao. Kenya hudai sehemu ya Tanzania kuwa yao kutokana na kuwajali makabila yao yaliyomo tanzania, Uganda, Malawi na hata Kongo hutanguliza kutazama WATU wake wamefika mipaka gani kufikia kudai ardhi hizo wakati sisi tunatazama ramani na kujaribu kuilinda mipaka hiyo.. In fact hatuna ushahidi pale mipaka inapoonyesha kula kwetu kama swala la Malawi..

Ujamaa ulikuja na mazuri yake mengi tu lakini pia Ujamaa ulitujenga kuwa kitu kisichokuwepo leo hii. Enzi za mwalimu hatukuwahi kuulizana kabila au dini lakini leo ni jambo la kawaida kabisa lakini tumefungwa akili zetu kutazama nje ya Ujamaa kwa kuendelea kuaminishwa kwamba sisi bado ni wajamaa wakati sio wajamaa bali wabinafsi. Hivyo CCM wanajitenga kama wao, Chadema wanajitenga kama wao, Polisi wanajitenga kama wao nasi walalahoi tunajitenga kama sisi na kila mmoja wetu akitazama maslahi yake.. UBINAFSI ndio sumu ya yote haya na ndio UTU unapotakiwa - Kushikamana, kupendana na kushirikiana kama Watanzania ni mada nzito zaidi ya utunzi wa falsafa yenyewe. Na ndio maana hata hiyo Katiba mpya tunayoitegemeahaitaweza kuondoa kero na karaha zetu kama haitawezi kutambua kwanza sisi ni WATU gani na tupo ktk mazingira gani. Nachoamini mimi sisi wote ni maskini.. Hivyo falsafa yetu lazima izingatie Umaskini wetu kwa kuwalinda watu maskini ambao ukombozi wao utatokana na umoja wao.

Tulipokwama hatuwezi kutoka ikiwa sisi maskini wote hatutakuwa na agenda moja. Zama za Mwalimu maadui wetu wa nje walikuwa ukoloni mamboleo - Mabeberu Imperialists), Kupe wanyonyaji (wawekezaji) na kdhalika kisha maadui wetu wa ndani walikuwa Umaskini, Ujinga na Maradhi.. Leo hii nambie maadui wetu ni kina nani? kila mmoja wetu atamnyooshea kidole Mtanzania mwenzake kwa sababu ni CCM, Chadema, Muislaam, Mkristu, Mwarabu, Mhindi, Tajiri, Maskini, Mbara au Mzanzibar yaani tumerudi ktk hali mbaya sana kuliko wakati wote wa Utawala wa Nyerere.
 
...Tulipokwama hatuwezi kutoka ikiwa sisi maskini wote hatutakuwa na agenda moja. Zama za Mwalimu maadui wetu wa nje walikuwa ukoloni mamboleo - Mabeberu Imperialists), Kupe wanyonyaji (wawekezaji) na kdhalika kisha maadui wetu wa ndani walikuwa Umaskini, Ujinga na Maradhi.. Leo hii nambie maadui wetu ni kina nani? kila mmoja wetu atamnyooshea kidole Mtanzania mwenzake kwa sababu ni CCM, Chadema, Muislaam, Mkristu, Mwarabu, Mhindi, Tajiri, Maskini, Mbara au Mzanzibar yaani tumerudi ktk hali mbaya sana kuliko wakati wote wa Utawala wa Nyerere...

Mkandara
,

Hakika mtamshi hayo yamenifikirisha sana!

Nikajiuliza hivi KIONGOZI wa Tanzania leo ni nani? Nikimaanisha Rais anatuongoza toka wapi kwenda wapi ? Mawaziir na Wabunge wanatoa jamii ya Watanzania toka wapi kwenda wapi?

Watakuwa na MAJIBU yao tayari tayari ... Nitasubiri Wayatoe hayo majibu. Niwaulize Huko mnakotupeleka ndiko uliko umoja wa Watanzania? Huko mnako tupeleka ambapo ndio umoja wa Watanzania pana upana na ujazo wa kutosha kuzibeba Tofauti zetu kwa heshima na maridhiano.

Kiongozi wa siku zijazo wa nchi hii ...

Anakazi Moja ... KUUTAFUTA UMOJA HUO WA KWELI.

Pili. Awe na uwezo wa Wa Kuubebesha Umoja huo TOFAUTI hizo kwa DHATI!

Vinginevyo Atatuogoza kwenda wapi kutoka wapi? Haijalishi atatoka Chama gani, dini gani, ngozi yake ya rangi gani, katokea pwani au Kanda ya milimani, shabiki wa simba au Yanga ... nk

Lazima awe na uwezo wa Kuwaunganisha Watanzania kwenye umoja wao ambao yeye ana uamini kwa MOYO NA AKILI zake kama ilivyo kwa Watanzania wote!

Swali linakuja tena na tena ...UMOJA WA WATANZNAI NI UPI? WATANZANIA WANUGANISHWA NA NINI? Tofauti zetu hazina shaka ziko nazitaendelea kuwepo na kuogezeaka tena na tena. Tuamini tu kuwa umoja wetu ukishapatikana utazibeba ...

TAFAKARI YA KINA NI HII!!


Watanzania Wa leo TUNAUNGANISHWA NA NINI?
 
..
Ndahani,

Nimwekea buluu sehemu hiyo! Adui yetu wote ni mtu anayetaka kutuona tunasambaratishana kwa ajili ya manufaa yake binafsi!

Mara ya kwanza nilifikiri nimeelewa vizuri na kuwa huu mtizamo utatufaa kama Taifa! Ghafla nikagundua kuwa CDM Watautumia kwa Mtizamo wao, CCM hivyo hivyo Polisi nao hivyo hivyo ....

Kwahiyo adui yetu sote ni nani mkuu?
 
Azimio Jipya,
Unaona jinsi msemo huu unavyoweza kutubabaisha..Tunaposema Adui yetu? huyu adui ni nani maana CCM wanaweza kusema hivyo, Chadema wanaweza kusema hivyo, CUF, Waislaam, wakristu, Wahindi, waarabu, weusi au Wazanzibar wanaweza kusema hivyo...Na hii yote inatokana na sisi kutojitambua kama Taifa moja na watu gani. Hadi leo hii we have nothing in common isipokuwa politics zetu zinaelemea ktk KUTAWALA ama KUTAWALIWA ktk mipaka ya nchi huru.

Unajua kwa nini Nchi za majirani zinatupiga bao leo hii?.. Ni kwa sababu wanajijua wao ni WATU gani na nini ethics na Values zao. Kenya hudai sehemu ya Tanzania kuwa yao kutokana na kuwajali makabila yao yaliyomo tanzania, Uganda, Malawi na hata Kongo hutanguliza kutazama WATU wake wamefika mipaka gani kufikia kudai ardhi hizo wakati sisi tunatazama ramani na kujaribu kuilinda mipaka hiyo.. In fact hatuna ushahidi pale mipaka inapoonyesha kula kwetu kama swala la Malawi..

Ujamaa ulikuja na mazuri yake mengi tu lakini pia Ujamaa ulitujenga kuwa kitu kisichokuwepo leo hii. Enzi za mwalimu hatukuwahi kuulizana kabila au dini lakini leo ni jambo la kawaida kabisa lakini tumefungwa akili zetu kutazama nje ya Ujamaa kwa kuendelea kuaminishwa kwamba sisi bado ni wajamaa wakati sio wajamaa bali wabinafsi. Hivyo CCM wanajitenga kama wao, Chadema wanajitenga kama wao, Polisi wanajitenga kama wao nasi walalahoi tunajitenga kama sisi na kila mmoja wetu akitazama maslahi yake.. UBINAFSI ndio sumu ya yote haya na ndio UTU unapotakiwa - Kushikamana, kupendana na kushirikiana kama Watanzania ni mada nzito zaidi ya utunzi wa falsafa yenyewe. Na ndio maana hata hiyo Katiba mpya tunayoitegemeahaitaweza kuondoa kero na karaha zetu kama haitawezi kutambua kwanza sisi ni WATU gani na tupo ktk mazingira gani. Nachoamini mimi sisi wote ni maskini.. Hivyo falsafa yetu lazima izingatie Umaskini wetu kwa kuwalinda watu maskini ambao ukombozi wao utatokana na umoja wao.

Tulipokwama hatuwezi kutoka ikiwa sisi maskini wote hatutakuwa na agenda moja. Zama za Mwalimu maadui wetu wa nje walikuwa ukoloni mamboleo - Mabeberu Imperialists), Kupe wanyonyaji (wawekezaji) na kdhalika kisha maadui wetu wa ndani walikuwa Umaskini, Ujinga na Maradhi.. Leo hii nambie maadui wetu ni kina nani? kila mmoja wetu atamnyooshea kidole Mtanzania mwenzake kwa sababu ni CCM, Chadema, Muislaam, Mkristu, Mwarabu, Mhindi, Tajiri, Maskini, Mbara au Mzanzibar yaani tumerudi ktk hali mbaya sana kuliko wakati wote wa Utawala wa Nyerere.

Mkandara, hata mimi sikujua nimesema nini mpaka mlipoangalia sentesi ile kwa undani zaidi. Ubinafsi ndio chanzo cha matatizo yote.Nguvu nyingi zinazotumika leo kuzima watu wasihoji, ukiangalia sana zinalenga kulinda ubinafsi na maslahi ya watu wachache.
Kweli Tanzania ya kweli ilikwisha ujamaa ulipobwagwa chini.Sasa hivi njaa zetu ndio zinatoa mwelekeo wa nini as individuals tunataka kufanya.
 
Watch this Guy carefully huyu mwenye pensi, picha ya kwanza na ya pili yupo akiwa amenyoosha bastora juu. what was mission of this Guy!!??

attachment.php


attachment.php
 
Mourinho,

Kuhusu swala la Nchi kukosa falsafa inayotuogoza.

Nadhani hii kuna wakati imejadiliwa hapa kama mada iliyeelta hoja na mitizamo mbalimbali!

Kuna ambao walidhani kuwa hili sio tatizo la msingi kwani kinachotakiwa ni uogozi unaotoa matokeo ya kazi iliyofanywa. Kuna wengi ambao waliunga mkono dhana hii Mimi nikiwa mmoja wao na kumbuka hara Mkandara aliona hii kama hoja.

Mkuu nadhani tusaidiane sasa! Falsafa ya Taifa iwe ni ipi? Tunaitoa wapi?

Mkuu nachelea kusema chochote kwa sababu swali lako linahitaji fikara nzito na sahihi na tena ziwe collective. Falsafa ya Taifa/Jamii lazima iakisi mazingira halisi ya hiyo jamii ili iwe na uhalisia na itoe mwongozo sahihi kwa jamii husika. Nikiangalia Jamii yetu ya leo,kwenye nyanja zote(utamaduni,siasa na uchumi)sioni ni nini haswa kinachotutambulisha kama jamii, zaidi ya kundi la watu waliopuuzia elimu,utu na maadili yao hivyo kuzaa jamii ya watu wenye akili nyepesi nyepesi,wanaoongozwa na tamaa za mwili na wanaokwenda kama kuku aliyekatwa kichwa. Sasa kwa mazingira haya hii falsafa yetu itaakisi kitu gani kitakachotuwakilisha kama jamii? Na kama tukipata mawazo mazuri kama ya Mkuu MKANDARA na JINGALAFALSAFA je ni kwa namna gani tutaya-set in motion ili yasiishie tu kuwa nadharia nzuri.
 
Last edited by a moderator:
Mkandara. Zakumi na JingalaFalsafa, KUHUSU FALSAFA YA TAIFA!

Guys lets just be serious for some seconds!

1. Awali Mkandara ulituambia kuwa tuna various DIFFERENCES at individual level which form DIVERSITY at a community a Nation level.

2. THEN, Ukapendekeza kuwa tutafute kitu ambacho ni COMMON out of all differences which can form our community with its diversity respected and well taken care!

3. JangalaFalsafa anakubaliana na Mimi kuwa that COMMON UNITY which unity us all Should be UTU whatever that term stand for!

4. JangalaFalsafa ameonyesha jinsi ya kujenga sera, mifumo and policy from UTU which will meet the need of the TOTAL DIVERSITY! WHICH CAN BE TERMED AS FALSAFA YA TAIFA!

5. FALSAFA YA TAIFA, kama Zakumi ataniruhusu kuuita UTU WA TAIFA Haitapingwa na CCM, CHADEMA, WAKRISTO, WAISLAM, POLISI,WAPAGANI,MAKABILA, UKANDA,MASIKINI, TAJIRI ... NAME ALL THE DIVERSITIES !!!Haitapingwa maana jamii nzima itaelimika juu ya dhani hiyo na kuiona ya thamani kubwa kuliko hata tofauti zao.

6. Elimu ifanyike kuwaamsha Watanzania kuhusu umoja wao ambao hauwezi kupuuzwa wala kuchezewa na chochote kile ndani ya kuheshimiana na kuridhiana kwenye kila tofauti zetu na kutukuza umoja wetu kwa kila hali.

Je hii ndio namana ya kejenga falsafa ya Taifa itakayo liokoa taifa hili lisitumbukie kwenye giza kubwa lililoko mbele yake?

Azimio Jipya and Inc.

I think now I understand where you guys stand when it comes to the use of the term falsafa. You don't take it rigorously to imply a proposed utopian society or country that forces people to live like clockwork. Please enlighten me if I am still shooting the blanks.

Now concerning the topic at hand, I think we are hypocrites. For example two weeks ago here in Washington, Mr Sugu told us that he can't take the blame for Mwembechai killings. For he wasn't the member of parliament.

Do you really need to be an MP to condemn what's bad? I believe you don't and before I proceed let me quote the Rev. Martin Luther King Jr.

History will have to record that the greatest tragedy of this period of social transition was not the strident clamor of the bad people, but the appalling silence of the good people.

I believe one of the falsafa that Tanzanians need to nurture, especially during this difficult times, is to speak out against the use of brutal force or injustice. For examples, muslims should speak out against injustice committed against christians and vice versa. Sukumas should speak out against injustice committed against Makondes.
 
WATANZANIA WA LEO TUNAUNGANISHWA NA NINI?

Kwanza niseme wazi kuwa "WATANZANIA WA LEO HAWAFUNGAMANI KWA CHOCHOTE" KILA MTU YUKO MBALI SANA KUTOKA ALIPO MWENZAKE! Yaani "TUNAKINZANA" ni kama pande sawa za sumaku zinavyokimbiana!

Swali ni "KIPI HASA KINAPASWA KUTULETA PAMOJA KAMA WATANZANIA?

*Je, ni uislamu? Mbona nao una matawi tena hasimu?
*Je, ni ukristo? Mbona nao una waliookoka dhidi ya wasiookoka? Nuru na giza havichangamani.
*Je, ni Siasa iliyopo? Yaani demokrasia? Mbona haisadifu hata chembe ya watu wetu? Wangapi wenye ufahamu nayo? Zaidi ya 90% ya watanzania, hatuijui Demokrasia! Elimu nayo haipo? Imani nayo haipo? Matumaini nayo hayapo? Ni NANI HASA ANAYOFAIDIKA NAYO KAMA SI KIKUNDI CHA WATU WACHACHE, je hautaibuka UKINZANI hapo?
*Je, ni Uchumi huu uliopo? Uchumi huruhusio kumshindanisha mbio Kinyonga dhidi ya sungura, au masumbi Cheka dhidi ya Wema Wepetu, kwa madai ya Fursa Sawa! Eti UHURU-HAKI. Nani kasema? Je, ni HULKA-HILA ama MANTIKI?​

+Kila kitu kinajenga UKINZANI KWETU, sasa... Kipi hasa KUTUUNGANISHA?
Hapa ndipo linapoibuka hitaji la kuwepo kwa FALSAFA KUU YA TAIFA, kutuleta pamoja! Ili binadamu asikinzane na mwenzake, ni "LAZIMA" sio HIARI, ni LAZIMA aishi KUFIKIRIANA na mwenzake! Sasa kipi kitatufanya TUFIKIRIANE? Unapotaka kuchimba choo karibu na kisima akitumiacho mwenzako, ukatafakari athari yake kwa jirani yako "reasoning", kisha ukaacha ukatafuta sehemu nyingine kwa kugundua utachafua kisima, MANTIKI itakuwa imetumiwa nawe katika maamuzi yako, mimi naiita UTU! UTU ni KUFIKIRIANA-KUTOKINZANA, ni kuwepo kwa Uuwiano Sahihi wa namna yetu ya kuishi pamoja. Basi kumbe UTU ndio upasao Kuunda Falsafa yetu ili kutuunganisha!

WAPI IPO MANTIKI-UTU?
Kwa asili tangu binadamu kuumbwa, amejaliwa mambo makuu mawili NAFSINI MWAKE! Ni HULKA, ambayo siku zote ni HASI na MANTIKI...ambayo siku zote ni CHANYA.

Kwa kutumia UTASHI tuliozaliwa nao pia, binadamu ana uwezo wa kutenganisha na kuyatambua vizuri mambo haya...Nafsini mwake mtu, na kuyafanya hai, katika vitendo! Hapa ndipo tunapotakiwa kuhoji juu ya kile tukiishicho leo, je ni zao la Hulka zetu ama Mantiki?
Na hapa ndipo tunapopata jibu la ADUI YETU HASA NI NANI, aliyetugawa?

Sioni MANTIKI yote katika Siasa, Uchumi wala Utamaduni tuupigania, ni HULKA za watu tu katika kila kitu! Hulka ya kutaka KUJIKWEZA, UMIMI, UBINAFSI, ndio mama wa kila kitu cha leo. Si ukristo wala uislamu, si demokrasia wala haki, si uchumi wala teknolojia, n.k.

Kumbe basi, ipo sehemu ambayo MANTIKI imekiukwa na kugeukia upumbavu -HULKA, na hapo si kwingine ila NAFSINI MWETU! Kumbe ADUI YETU WA KWANZA, ni NAFSI ZETU WENYEWE!

Nafsi zilizonafiki na kusaliti MANTIKI iliyomo ndaniye. Nafsi yangu ndio mimi mwenyewe! Ni lazima tujitakase kwa kupigania MANTIKI.
Tujenge umoja wa taifa letu, sisi WAAFRIKA wa Tanzania.

Kauli hii ni ngumu kidogo kuisema lakini kwangu ndio ukweli wenyewe, na ipo siku itatimia "TUTAANGUSHA DEMOKRASIA, MISIKITI na MAKANISA yatapewa raia kufugia kuku" hili ni katika kuishi MANTIKI KUU, yaani UTU. Thamani ya UTU hailingani hata kwa gharama ya damu ya mtu au watu milioni! Mantiki inapofikia ukamilifu wake, na kusema chinja hawa na hawa, SI DHAMBI KUTEKELEZA, na huo ndio UTU!

Mungu wetu anaita sasa!
 
Zakumi,
Let me give you an answer. Do you remember the mutiny of 1964? Nyerere used that as an opportunity to retrain our army and it became the peoples army. When we take over we will retrain the police force to become the people's police and not the fisadi police.

Jasusi,

My take on when CDM takes over, the major change of all overall change in the system will be a brand new party in ruling for the first time since independence. The change in Tanzania and its citizens will be for the better (minimally) or for the worse (crucially) depending on how the major problematic issues in each sector will be tackled by CDM. While my belief is that it will be briefly for the worse... We should just brace ourselves for whatever is in store for us.

I genuinely don't believe that there will be so much change to the extent that everything will be alright overnight, It will take time with a combination of other lubricating factors. I believe there will be hard work and the times more complicated that they are right now. I also believe that MOST CCM leaders (some even considered as the so called 'Fisadi' will also be in the CDM action pic with the CDM's leaders blessings (whether visibly or under the carpet)

Nashindwa kuelewa kwa wale wenye kasumba ya kufikiria kuwa CDM ikija kila kitu kitakuwa sawa... Na kwamba Police watawasiliza wananchi kuliko viongozi wa serkali. Nakataliana na hilo, mambo mengi yatakuwa vile vile (na I say it confidently kabisa na God willing after years I am hoping to come back to the post and declare 'I said so').

I may be too cynical but that is what I believe. Hapa what matters ni kuwa wao CDM wakija maamuzi watayotoa will they be selfish to themselves or selfless?
 
zomba,

Nimeona picha uliotowa na ujumbe wake ambao naomba ninukuu "ILANI ILANI ILANI ILANI Watu wote mliokusanyika hapo maamriwa na Serkali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuondoka kwa haraka na kwa amani la sivyo tutatumia nguvu" Kwa kutumia picha hii ambayo ni msingi naomba kama hutajali nijuze haya:


  1. Kuwepo kwa kutumika hio Ilani iliyotolewa, je ina justify kipigo ama jinsi alivo uwawa marehemu Mwangosi?
  2. Naomba nijue msimamo wako wa tukio lote lililotokea Iringa na juu ya Kifo cha Marehemu Mwangosi.
  3. BTW katika vurugu zote ambazo hutokea kwenye mikutano ya CDM kwa mtazamo wako nani anatakiwa kulaumiwa kati ya police na CDM na hasa zaidi am more interested in understanding why wakulaumiwa alaumiwe kwa vigezo gani.
 
Last edited by a moderator:
Is it a concidence you read the books that I read? Adui yetu wote ni mtu anayetaka kutuona tunasambaratishana kwa ajiri ya manufaa yake binafsi. Huyu tuombe Mungu amrudi na tumkate kwa nguvu zetu zote.

Usisahau na baadhi ya movies mkuu... hahaha!

AshaDii,

Nimesoma sana where I have blued! Inaonekana una insight fulani but honestly simalizii kujua kabisa kabisa kuwa nini hicho kimekusumuka kusema hivo? Najua hujali kufafanua ... !

Azimio, Never Get Angry, Never make a Threat, Reason with people... Haina maana kuwa huyu mtu hana hasira, kuwa ni mpole daima or kuwa yeye ni mtu wa ku reason kwa kila jambo. Maana yake haipo hivo literally, ila msingi wake ni kuwa unapo deal na vitu vya msingi hasa ukitaka ku achieve kitu flani kwa mtu haitakiwi utumie hasira hata kama huyo mtu anakuboa, kukuchosha ama kukujudge.

Always keep calm, but upande wa vitendo ni otherwise... Una busara, una simile, hulipuki ovyo ila ACTION thats a whole another lever.... Kama kiongozi nikichukula model ya Don Corleone wa "The God Father" naweza sema inatakiwa uwe JK on the surface and Hitler underneath.
 
….kuelekea …. FALSAFA YA TAIFA

WATANZANIA WA LEO TUNAUNGANISHWA NA NINI?

Kwanza niseme wazi kuwa"WATANZANIA WA LEO HAWAFUNGAMANI KWA CHOCHOTE" KILA MTU YUKO MBALISANA KUTOKA ALIPO MWENZAKE! Yaani "TUNAKINZANA" ni kama pande sawa zasumaku zinavyokimbiana! Swali ni "KIPI HASA KINAPASWA KUTULETA PAMOJA KAMA WATANZANIA?"

· Je, ni uislamu? Mbona nao una matawi tenahasimu?

·
Je, ni ukristo? Mbona nao una waliookoka dhidiya wasiookoka? Nuru na giza havichangamani.

· Je, ni Siasa iliyopo? Yaani demokrasia? Mbonahaisadifu hata chembe ya watu wetu? Wangapi wenye ufahamu nayo? Zaidi ya 90% yawatanzania, hatuijui Demokrasia! Elimu nayo haipo? Imani nayo haipo? Matumaininayo hayapo? Ni NANI HASA ANAYOFAIDIKA NAYO KAMA SI KIKUNDI CHA WATU WACHACHE,je hautaibuka UKINZANI hapo?

· Je, ni Uchumi huu uliopo? Uchumi huruhusiokumshindanisha mbio Kinyonga dhidi ya sungura, au masumbi Cheka dhidi ya WemaWepetu, kwa madai ya Fursa Sawa! Eti UHURU-HAKI. Nani kasema? Je, ni HULKA-HILAama MANTIKI?

+Kilakitu kinajenga UKINZANI KWETU, sasa...?

Kipi hasa KUTUUNGANISHA?

Hapa ndipo linapoibuka hitaji lakuwepo kwa FALSAFA KUU YA TAIFA, kutuleta pamoja! Ili binadamu asikinzane namwenzake, ni "LAZIMA" sio HIARI, ni LAZIMA aishi KUFIKIRIANA namwenzake!

Sasa kipi kitatufanya TUFIKIRIANE?Unapotaka kuchimba choo karibu na kisima akitumiacho mwenzako, ukatafakariathari yake kwa jirani yako "reasoning", kisha ukaacha ukatafutasehemu nyingine kwa kugundua utachafua kisima, MANTIKI itakuwa imetumiwa nawekatika maamuzi yako, mimi naiita UTU! UTU ni KUFIKIRIANA-KUTOKINZANA, ni kuwepokwa Uuwiano Sahihi wa namna yetu ya kuishi pamoja. Basi kumbe UTU ndio upasaoKuunda Falsafa yetu ili kutuunganisha!

WAPIIPO MANTIKI-UTU?

Kwa asili tangu binadamu kuumbwa, amejaliwamambo makuu mawili NAFSINI MWAKE! Ni HULKA,ambayo siku zote ni HASI na MANTIKI...ambayosiku zote ni CHANYA. Kwa kutumia UTASHI tuliozaliwa nao pia,binadamu ana uwezo wa kutenganisha na kuyatambua vizuri mambo haya...Nafsinimwake mtu, na kuyafanya hai, katika vitendo! Hapa ndipo tunapotakiwa kuhoji juuya kile tukiishicho leo, je ni zao la Hulka zetu ama Mantiki?

ADUI YETU HASA NI NANI?

Na hapa ndipo tunapopata jibu laADUI YETU HASA NI NANI, aliyetugawa? Sioni MANTIKI yote katika Siasa, Uchumi walaUtamaduni tuupigania, ni HULKA za watu tu katika kila kitu! Hulka ya kutakaKUJIKWEZA, UMIMI, UBINAFSI, ndio mama wa kila kitu cha leo. Si ukristo walauislamu, si demokrasia wala haki, si uchumi wala teknolojia, n.k.

Kumbe basi, ipo sehemu ambayo MANTIKIimekiukwa na kugeukia upumbavu -HULKA, na hapo si kwingine ila NAFSINI MWETU! Kumbe ADUI YETU WAKWANZA, ni NAFSI ZETU WENYEWE!

Nafsi zilizonafiki na kusaliti MANTIKI iliyomondaniye. Nafsi yangu ndio mimi mwenyewe! Ni lazima tujitakase kwa kupiganiaMANTIKI.

Tujenge umoja wa Taifa letu, sisiWAAFRIKA wa Tanzania.

Kauli hii ni ngumu kidogo kuisemalakini kwangu ndio ukweli wenyewe, na ipo siku itatimia "TUTAANGUSHADEMOKRASIA, MISIKITI na MAKANISA yatapewa raia kufugia kuku" hili nikatika kuishi MANTIKI KUU, yaani UTU. Thamani ya UTU hailingani hata kwagharama ya damu ya mtu au watu milioni! Mantiki inapofikia ukamilifu wake, nakusema chinja hawa na hawa, SI DHAMBI KUTEKELEZA, na huo ndio UTU!


JingalaFalsafa, nimepata HOJA yako, ... Natafakari!
 
Last edited by a moderator:
zomba,

Nimeona picha uliotowa na ujumbe wake ambao naomba ninukuu "ILANI ILANI ILANI ILANI Watu wote mliokusanyika hapo maamriwa na Serkali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuondoka kwa haraka na kwa amani la sivyo tutatumia nguvu" Kwa kutumia picha hii ambayo ni msingi naomba kama hutajali nijuze haya:


  1. Kuwepo kwa kutumika hio Ilani iliyotolewa, je ina justify kipigo ama jinsi alivo uwawa marehemu Mwangosi?
  2. Naomba nijue msimamo wako wa tukio lote lililotokea Iringa na juu ya Kifo cha Marehemu Mwangosi.
  3. BTW katika vurugu zote ambazo hutokea kwenye mikutano ya CDM kwa mtazamo wako nani anatakiwa kulaumiwa kati ya police na CDM na hasa zaidi am more interested in understanding why wakulaumiwa alaumiwe kwa vigezo gani.

1. Kumbuka haikuwepo ilani hiyo tu pekee, kwanza kabisa vyama vyote mkoani Iringa walishatangaziwa na Polisi wasifanye mikutano ya kisiasa wakati wa kampeni, wajizuie kwa wiki moja.

Ilani zilizotolewa zaidi ya hiyo ya kitambaa:

Hii ni taarifa ya Jeshi la polisi kabla ya tukio kwa vyombo vya habari

JESHI la polisi mkoa wa Iringa limesema limezuia mikutano ya vyama vya siasa kwa vyama vyote na sio kwa chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) pekee hivyo laonya vyama vyote kutii sheria bila shuruti.


"Nawatangazia wanasiasa na vyama vyote vya siasa pamoja na wananchi wa mkoa wa Iringa kuwa hakutakuwa na mikutano ya kisiasa kutokana na shughuli za sensa zinazoendelea ....hivyo basi nawaomba wananchi wote kutoshiriki mikutano yoyote ya kisiasa itakayoitishwa na wanasiasa " alisisitiza kuwa mikutano hiyo imezuiliwa kwa kipindi hiki cha sensa kilichoongezwa hadi hapo tamko litakapotolewa tena na msajili wa vyama vya siasa John Tendwa kama alivyokwisha kutoa tamko la kuzuia shughuli hizo za vyama vya siasa kwa kipindi hiki cha sensa."Wananchi wote wa mkoa wa Iringa mnaombwa kutii sheria bila shuruti hii ni amri ....nawaombeni sana wananchi kutodanganywa na wanasiasa kwa kuvunja sheria "aliongeza kamanda huyo wa polisi.

Source: Political Issues

Halafu walitangaziwa siku ya tukio, licha ya hicho kitambaa cha ilani, walipewa ilani kwa njia ya vipaza sauti kuwa wasambaratike.

Kwa hiyo hili la Ilani utaona kuwa ni ukaidi ulifanywa makusudi kabisa na wanachadema wa Iringa, kwa nini? isitoshe:
Katika vurugu hizo zilizodumu kwa takribani dakika 30 kwa askari na wafuasi wa Chadema kurushiana mawe kwa mabomu zaidi ya magari matano ya Chadema na ya wananchi yameharibiwa huku watu kadhaa wamejeruhiwa na mwanahabari mmoja Godfrey Mushi akijeruhiwa vibaya. Source: Political Issues

Sasa wewe jiulize na ujibu, ikiwa mmepewa Ilani zote hizo na Polisi na mkakaidi na mkaingia kwenye vita na wao kwa dakika 30, halafu atokee mmoja hukohuko kwenye kundi linalipogana na Polisi aje amvae Mkuu wa kikosi, kwa nia yoyote ile, unafikiri kutakuwa na usalama kwake hapo?

Do not approach police lines to attempt to cross to safety. Police are in place to confine the unrest and prevent its spread. Their orders are usually not to allow anyone to pass. The use of riot control measures, including rubber bullets, tear gas, and water cannons originate from the police line, and the likelihood of injury is greatest there.

Source: How to Survive a Riot: 2 Methods - wikiHow


2) Tukio lote lililotokea Iringa nalichukulia ni uvunjifu wa amani wa makusudi kabisa kwa "wapiganaji". Siasa sio kukaidi amri za Polisi kwa nguvu, hivi unategemea nini baada ya kuvunja amri za Polisi? Licha ya kuwawametangaziwa, hata ikitokea tu kuwa wamejikusanya kikundi cha watu ambapo polisi wanaona hapa kuna uwezekano wa amani kuvunjika basi wana haki ya kuwaambia watawanyike bila ilani yoyote ya kabla.

Sasa jiulize tena, hivi walikusudia nini hawa waliokaidi amri zote hizo na kupambana na mapolisi?

3. Ikiwa umeambiwa usifanye maandamano, ukayafanya kwa nguvu, ukatokea uvunjifu wa amani kwa polisi kuzuwia hayo maandamano, hapo unategemea nani alaumiwe?

Ikiwa unaambiwa usifanye mikutano siku fulani, wewe unaumuwa kufanya kwa nguvu wakaja polisi kuzuwia mkusanyiko huo ukakaidi na kupigana na Polisi ni nani wa kulaumiwa?

Conclusion:

Licha ya hoja zote hizo juu zinazoashiria uvunjifu wa amani wa makusudi kabisa, hata kwa bahati mbaya ukijikuta wewe ni mpita njia kwenye vurugu (riots) za namna hiyo na Polisi wameshatowa amri ya watu kutawanyika na wameshajipanga kuwafata na kuwatawanya wakitumia zana zao za kuzuwia fujo, usijaribu hata siku moja kuwafata wanapotokea na kuingia kwenye himaya yao kutokea walipo wanaotawanywa, kufanya hivyo ni:

1) amma kujitafutia kifo (suicide) kwa makusudi kabisa,

2) au kujitafutia kifo cha kujitowa mhanga (terrorism),

3) amma kujitafutia kifo kwa ujinga wa kwenda kuanzisha fujo na kutokujuwa namna ya kujihami yanapokushinda.

Chaguwa wewe ni yepi katika hayo yaliyomkuta Daudi?

Ukweli ubaki kuwa ukweli.
 
Jasusi,

My take on when CDM takes over, the major change of all overall change in the system will be a brand new party in ruling for the first time since independence. The change in Tanzania and its citizens will be for the better (minimally) or for the worse (crucially) depending on how the major problematic issues in each sector will be tackled by CDM. While my belief is that it will be briefly for the worse... We should just brace ourselves for whatever is in store for us.

I genuinely don't believe that there will be so much change to the extent that everything will be alright overnight, It will take time with a combination of other lubricating factors. I believe there will be hard work and the times more complicated that they are right now. I also believe that MOST CCM leaders (some even considered as the so called 'Fisadi' will also be in the CDM action pic with the CDM's leaders blessings (whether visibly or under the carpet)

Nashindwa kuelewa kwa wale wenye kasumba ya kufikiria kuwa CDM ikija kila kitu kitakuwa sawa... Na kwamba Police watawasiliza wananchi kuliko viongozi wa serkali. Nakataliana na hilo, mambo mengi yatakuwa vile vile (na I say it confidently kabisa na God willing after years I am hoping to come back to the post and declare 'I said so').

I may be too cynical but that is what I believe. Hapa what matters ni kuwa wao CDM wakija maamuzi watayotoa will they be selfish to themselves or selfless?

AshaDii,

In management theories, stepping aside and observing processes from afar is a good thing. For, it give individuals or group entities opportunity to learn and rectify their own problems.

With that in mind, I think CCM need to step aside. Not because they are bad, but because they have become complacent which isn't good for the country and the party itself.

Continuity that CCM want to maintain is an elephant or 800 pound Gorilla in the room which hinders reform and accountability. And the only way to get rid of that animal is therefore to reduce CCM's outreach or force the party to go into the opposition entirely.

Therefore, I support the efforts of CHADEMA and other opposition parties. But I am very realistic and don't expect overnight solution. For, the magnitude of our problems is huge.

Majority of leaders in opposition camps are activists not executives or technocrats. They have never run and excute a budget. They have never run a payroll to pay salaries. They have never controlled security and defend forces. So there's a learning curve that isn't going to be achieve in a year or two.

The inexperience of opposition is there. So even though we want the opposition to win, we should control and manage our expectations. For example, changing the working habits of civil servants include the police officers will take time.

Now back to my friend Jasusi, he is being disingneous when he tells me that they will reform the police force when CHADEMA take power. I don't buy that. For, the only time Nyerere reformed the defend forces was when they undermined his authority. Likewise, if the security forces serve well those in power, we shouldn't expect miracles.
 
1. Kumbuka haikuwepo ilani hiyo tu pekee, kwanza kabisa vyama vyote mkoani Iringa walishatangaziwa na Polisi wasifanye mikutano ya kisiasa wakati wa kampeni, wajizuie kwa wiki moja.

Ilani zilizotolewa zaidi ya hiyo ya kitambaa:



Halafu walitangaziwa siku ya tukio, licha ya hicho kitambaa cha ilani, walipewa ilani kwa njia ya vipaza sauti kuwa wasambaratike.

Kwa hiyo hili la Ilani utaona kuwa ni ukaidi ulifanywa makusudi kabisa na wanachadema wa Iringa, kwa nini? isitoshe:


Sasa wewe jiulize na ujibu, ikiwa mmepewa Ilani zote hizo na Polisi na mkakaidi na mkaingia kwenye vita na wao kwa dakika 30, halafu atokee mmoja hukohuko kwenye kundi linalipogana na Polisi aje amvae Mkuu wa kikosi, kwa nia yoyote ile, unafikiri kutakuwa na usalama kwake hapo?




2) Tukio lote lililotokea Iringa nalichukulia ni uvunjifu wa amani wa makusudi kabisa kwa "wapiganaji". Siasa sio kukaidi amri za Polisi kwa nguvu, hivi unategemea nini baada ya kuvunja amri za Polisi? Licha ya kuwawametangaziwa, hata ikitokea tu kuwa wamejikusanya kikundi cha watu ambapo polisi wanaona hapa kuna uwezekano wa amani kuvunjika basi wana haki ya kuwaambia watawanyike bila ilani yoyote ya kabla.

Sasa jiulize tena, hivi walikusudia nini hawa waliokaidi amri zote hizo na kupambana na mapolisi?

3. Ikiwa umeambiwa usifanye maandamano, ukayafanya kwa nguvu, ukatokea uvunjifu wa amani kwa polisi kuzuwia hayo maandamano, hapo unategemea nani alaumiwe?

Ikiwa unaambiwa usifanye mikutano siku fulani, wewe unaumuwa kufanya kwa nguvu wakaja polisi kuzuwia mkusanyiko huo ukakaidi na kupigana na Polisi ni nani wa kulaumiwa?

Conclusion:

Licha ya hoja zote hizo juu zinazoashiria uvunjifu wa amani wa makusudi kabisa, hata kwa bahati mbaya ukijikuta wewe ni mpita njia kwenye vurugu (riots) za namna hiyo na Polisi wameshatowa amri ya watu kutawanyika na wameshajipanga kuwafata na kuwatawanya wakitumia zana zao za kuzuwia fujo, usijaribu hata siku moja kuwafata wanapotokea na kuingia kwenye himaya yao kutokea walipo wanaotawanywa, kufanya hivyo ni:

1) amma kujitafutia kifo (suicide) kwa makusudi kabisa,

2) au kujitafutia kifo cha kujitowa mhanga (terrorism),

3) amma kujitafutia kifo kwa ujinga wa kwenda kuanzisha fujo na kutokujuwa namna ya kujihami yanapokushinda.

Chaguwa wewe ni yepi katika hayo yaliyomkuta Daudi?

Ukweli ubaki kuwa ukweli.
zomba kuna wakati mwingine mkuu wangu sio lazima uchangie kitu hasa ktk maswala mazito kama haya kwa ushabiki wa chama. Uchadema na UCCM ni vitu vingine kabisa inapofikia kifo cha raia, mwananchi tena mwandishi wa habari ambaye hakuwa na silaha isipokuwa akiwa kazini. Zaidi ya hapo Polisi waliambiwa wazi kuwa huyo wanayempiga ni mwandishi wa habari na walimwona aki record pande zote mbili na mfarakano na hata huyo mkuu wa Polisi alimwona vile vile.

Unachojaribu kujenga hoja hapa ni sawa na sheria ya Makaburu (Apartheid) ambapo wananchi wafanyakazi waligoma kwenda migodini kwa madai ya nyengeza ya mshahara wakauawa bila huruma halafu kisheria ndio wenye kubeba lawama na makosa kusababisha vifo hata kama walikuwa wakidai haki zao pasipo kumshambulia mwenye mgodi ama kufanya fujo mgodini..Kuna vitu vya kutetea na hasa vinapokuwa vya kisiasa lakini sio hili.

na ifahamike tu kwamba hatuna madaraka mikoani, swala la sensa ni swala la Kitaifa, swala la Jamhuri nzima hivyo huwezi kutoa amri kuzuia watu kutofanya shughuli zao mkoani wakati nchi nzima watu wanaendelea na shughuli zao kama kawaida isipokuwa wneye dhamana ya kuhesabu ndio wanawafuata watu majumbani mwao na kuwahesabu. Ingekuwa hivyo basi hata wale waliokutwa hawapo majumbani wangekamatwa, wote walioenda kazini wakait wa kuhesabu wangewajibishwa vile vile. Ilani pekee iliyotolewa Kitaifa ni kwa wale watakao kataa kuhesabiwa.

Na Polisi hawahusiki kabisa na utoaji tahadhali ikiwa kamati ya sensa haikuomba kuahirishwa kwa shughuli zote nchini ama Iringa sizimamishwe ili kuwawezesha wafanye kazi kwa ufasaha na haraka.. Polisi wameingilia kazi isikuwa yao kwa sababu walijua ni Chadema tu mkoani Iringa waliokuwa na shughuli kati ya siku hizo. Labda nikuulize hilo bango liliandikwa lini na kwa ajili gani haswa? wapi sehemu nyingine liliwekwa?..Hii ina maana Polisi walijiandaa mapema kwa kuelewa watafanya nini...Hivyo wanaposema ilani ile ni kwa vyama vyote sidhani kama wanasema ukweli maana hapakuwepo na shughuli nyingine yoyote zaidi ya ile ya Chadema.
 
Back
Top Bottom