CHAMA CHA MAPINDUZI ni janga la kitaifa kwani hata katibu mkuu wake BW. KINANA akiwa ziarani mbeya alisema ni kweli tunasema tumewafanyia mengi watanzania lakini mbona hatusemi ni kiasi gani kimeibiwa. ni ukweli kuna wizi wa rasilimali zetu kama tembo,gesi, madini,ardhi, mikataba ya kifisadi kama richmond aka dowans, ufisadi kama epa, rada,kagoda, dep green, ukatili waaskari kama polisi kuua raia kama mwangosi, kutesa raia kama dk ulimboka haya ni machache lakini kimsingi huyu ccm amekuwa mkoloni mweusi inabidi tupambane kumtoa
ni matumaini yangu huyu atatuokoa
tutafute kijana kutoka upinzani ,anaeweza kuthubutu na ambae amefanya mengi kwa watanzania mfano je amewateteaje wananchi kwa sera mbovu na mbaya za ccm mfano suala la madini na mikataba mibovu tupate kijana ambae ni mzalendo na amewahi kutetea sera za madini na rasilimali za taifa , ametetea wananchi juu ya wezi wa mali ya umma na mikataba feki ya madini na mengineyo tutafute kijana mwenye elimu ya kutosha, tutafute kijana mwenye nguvu ya umma na anaekubalika kwa watanzania wote. tukimpata ndugu wananchi tujipange vema kumtoa huyu mkoloni mweusi.