Kifo cha CCM kimetimia

Kifo cha CCM kimetimia

Badala ya kuandika kuelewesha watanzania juu ya dhana iliyopo kwa Chama chako ni cha kidini(kikatoliki) na kikanda na ukabila(ukaskazini na uchaga),ambapo hadi leo viongozi wa Chadema wameshindwa kukanusha tuhuma hizi wewe unapoteza muda kwa kuleta ngonjera zisizo eleweka juu ya CCM! Mpuuuuuzi hana fikra siku zote!
hv huo ukaskazn unatatzo gan?wao sio watanzania ni wakenya,na ukatoliki unashda gan?hebu angalia asilimia 80 ya viongoz wakuu wote ni waislamu mbona hili hulsemi asilimia 75 ya wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya ni waislamu,wakristo tunaambiwa tusichnje ng'ombe je hapo ccm nao wanataka kuisilmisha nchi kuwa ya kigaid.asilimia 98 ya wabunge wa chadema sio wachaga unaljua hlo?
 
Jamani mbona kuna wengine hamuwataji: Lema,Mnyika, Slaa, Lisu? madini yao wanayotema vipi hamyaoni kuwa ni sumu zaidi ya kuimaliza CCM, bado hamjataja sisi je ambao tunaothirika na sera Chafu za CCM yaani sisi wananchi. THINK BIG! meen
 
Ulitakiwa uone aibu maana wewe kama mtumishi wa serikali haukuwa na la kuonesha mbele ya wageni maana yake haufanyi kazi ya watanzania. Hiyo hapo si CCM wala JK wanaofanya kazi, huyo ni wewe unayefanya uzembe kazini kwako. Kuwa responsible na kila mmoja wetu awe responsible kwenye kazi yake ndipo Tanzania itaendelea

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Anna Makinda na Job Ndugai ndo wanaifanya kazi hiyo ya kuiua ccm vizuri zaidi kuliko wote.
 
Hivi yule 'aliyefanya' ngono na mama yake yuko wapi siku hizi? Kawa DC?
 
Fanya utafiti kwanza kabla hujatoa huo mtazamo wako, unadai kuna mapacha wawili wamebaki, huyo mmoja aliebaki ni yupi?Kwa kifupi hakuna mtu alieondolewa CCM kati ya hao mnaowataja kama mapacha watatu.Hebu rejea kampeni za uchaguzi mdogo wa Igunga especially cku ya uzinduzi.CCM hakuna kufukuzana bwana.
 
CCM bado wanaishi kwa matumaini haya.

1.Eti wana wanachama mil.6 sasa sijuia kama wanauhakika kwamba wote bado wapo gambani au wote wanaipigia kura.

2.Eti wanawake na wazee wote wanayapigia kura,sasa sielewi ubungo,kawe,nyamagana ,kwa Jemedari Lema Arusha etc kuna wanaume tu hakuna wanawake wala wazee na kama wapo ilikuaje?

3.Eti CHADEMA itakufa kama NCCR,CUF haiwapi shida.

4.Eti yatatumia pesa,dola,tume kushinda.

5.Eti CHADEMA wametumia pesa ya watz kupeleka magari kenya kwa odinga kwajili ya kampeni, bt mi nakumbuka kuna mwaka fulani li-KOMBA lilikwenda nchi fulani siikumbuki kupiga kampeni sasa sielewa haya magamba yamesahau?bt kwa cdm imekuwa nongwa siyo? Odinga anashinda mkae mkijua.

6.UDINI,UKABILA,UKANDA.

7.Kusomba watu kwa mafuso,coaster mji mzima na kuwajaza kwenye mikutano yao. Mi naishi goba lilikuja li-NAPE huku na li-MAGEMBE aisee coaster zilipiga kazi toka kimara,mwananyamala eti yakawa yanatangaza hao wote ni wakazi wa goba nilitamani niyanyang'anye mic na niyakatalie yasipotoshe umma wa goba.

HAYA CCM OYEEEE,magamba wenzangu ongezeni mengine lazima tushinde si CHADEMA waliona Magu na Mbozi hivi karibuni.
 
Ndugu zangu, Nimejaribu kufuatilia mbambo mbalimbali yanayotokea apa Tanzania, Kiualisia kabisa sasa viongozi wanatumia mda mwingi kwenye siasa badala ya kazi..
Hakuna tena ule uzalendo tuliokuwa nao miaka yanyuma. Zaidi ya ilo Tunamalizana kwenyewe kwa manufaa ya wachache...
BILA KUJALI ITIKADI ZA VYAMA
1); Tukumbuke kwenye hii dunia tunapita! CCM itapita, Mauwajivyoote yaliyo fanywa tangu CCM ilipo anza kutawala yatawarudia wahusika na kuwamaliza taratibu.
Uwe Raisi, Waziri na mtu yoyote katika nafasiyoyote!
Nawarushia Lawama CCM siotuu kwaku husika moja kwa moja; Bali Kushindwa kutimiza wajibu wenu, na badala Yake kutuuwa na kusahau wananchi walio wapa iyo nafasi.

2); Tujiulize ndugu zangu, Je haya yanayotokea Ndio, maisha bora kwa kila Mtanzania? Ndio amani CCM wanayo iubiri? Mnawalipa ndugu zetu kutuuwa na kututesa, eti kwakuwa hamna nguvu tena! Kweli CCM niijuayo ndo mmeshidwa kabisa kuongea sera, Kumwaga mijipesa mliyo yaiba kwenye mikataba feki ,kodi na zile za misaada?? badala yake mnatumia majasusi na ugaidi wenu kuwauwa ndugu zetu...? Kama hatutaki kuhongwa pesa unadhani ata ukiwauwa wapinzani wote ndo mtaweza kuendelea kututawala?

MIMI KAMA RAIA MZALENDO, NA MPIGANIA HAKI. SIONI HAYA KUKOSOA MTU YOYOTE AU CHAMA CHOCHOTE KINACHOENDA KINYUME NA MAADILI YA BINADAMU.

RAISI JAKAYA M. KIKWETE ; tenda haki maana mwenyenzi mungu sio mwanadamu. Siku ya mwisho utaulizwa ulifanya nn kwa wananchi wako.! Naongea kutoka moyoni kabisa. Natumaini utaipata hii,
Maana sisi wa vijijini pia tumekata tamaa hakuna maendeleo yoyote, kilimo ndo ivyo kimebuma mazao yamekauka. wazee tumesahaulika, vijana wanaotutunza mnawatesa na kuwauwa..

Salam kwenu wote wana JF.
 
Pole ndugu yangu, hicho kichaka cha wezi kimeshajiriza, wameweka pamba masikioni, hawasikii kengele ya kanisani wala sauti ya mnadi swala msikitini, wamesahau kwamba hata uwe na mipesa yote ya duniani lakini siku moja utakufa na kuyaacha.
 
Kwa wapenzi wote wa mapinduzi na chama cha mapinduzi, ninasikitika kwatangazia kuwa kile chama chetu kipenzi, CCM kimeaga dunia ya siasa za Tanzania. Aidha, maandalizi ya nyimbo za maombolezo kutoka kwa mtunzi wetu maarufu Yohana Simba na kunafanyika utaratibu wa kisheria wa kukabidhi madaraka kwa chama kingine 2015 kwa amani, kabla ya kuizika CCM rasmi 5/2/2017 wakati kimetarajiwa kutimiza umri wa miaka.

Hakuna utawala wa milele hapa duniani na historia haionyeshi kuwepo kwa chama kichotawala hata kwa miaka 100 mfululizo kama makada wachumia tumbo wa CCM wanavyotoa propaganda zao. Hizo ni propaGammba tu.Roman empire na Hata Mkwawa Chiefdom ni mfano mdogo tu. Kwa kawaida, viumbe wafao wakiwa wametulia ni wachache sana, hata watu.Mara nyingi, hata yule mgonjwa mahututi anapoaga dunia anaweza kuhangaika kiasi cha kuwa na nguvu ambazo hapo awali alidhaniwa kutokuwa nazo. Mambo yanayoendelea sasa ni dalili tosha hata na kwetu tusiojua kufa kuwa chama chetu kipenzi kimeshatuacha.

Nawaomba wote,wapenzi na maadui wa CCM msitaharuki kwa msiba huu mkubwa.Mtakumbuka kuwa aliyekuwa katibu wake mkuu alishasema kuwa CCM imepoteza dira na hii ilitokana chama hicho kupoteza fahamu.Hapo wakakipeleka ICU kule Chimwaga na kwa batati mbaya sana, mgunduzi wa ugonjwa ule akafariki dunia kama watafiti na wagunduzi wengine wanavyoathirika na tafiti zao juu ya visivyojulikana . Na kabla ya hapo mwanzilishi wake na mwenyekiti wake wa kwanza, alipoona kuwa hali ni mbaya akatumia hekima kuishinikiza serikali ikubali kuwepo vyama vingine vya siasa na akaona kuwa CHADEMA ndiyo chama makini na chama mbadala kwa CCM aliyoiasisi.Jitihada za kukinusuru chama kisife zilishashindikana kutokana na chama hicho kukumbwa na ugonjwa hatari unaojulikana kitaalam 'scalosis' yaani utokaji wa magamba sehemu zote kuanzia kamati kuu na magaba hayo kuendelea kukua na kukomaa na kukakamaa kiasi cha kusababisha maumivu makubwa na migawanyiko ya kimakundi(scales) yasiyoweza kutoweka kwa dawa yoyote inayojulikana.

Swali sasa si kama CHADEMA kipo tayari kuwa chama tawala au la bali uhai wake kisiasa halali za kuongoza nchi kwa kuimbiwa nyimbo za hamasa na wananchi wengi kama ilivyokuwa kwa marehemu CCM utadumu hadi lini?Je ugonjwa wa 'scalosis' uliokiua CCM hautakipata na chenyewe?Ujonjwa huu ambao kinga yake pekee ni kuondoa sehemu iliyoathirika mapema iwezekanavyo na kuichoma moto chini ya uangalizi mkali ili mavumbi yake yasiguse sehemu nyingine ya mwili unahitaji umakini sana kwani hiyo kinga isipotumia vema inakumaliza pia.Ni jukumu la wanaCHADEMA wote, kutuhakikishia watanzania uwezo wenu wa kutuongoza vema bila ya ugonjwa huu hatari.

Ushauri wangu kwa watanzania wote, wakati kipindi hiki kigumu cha msiba wa mpendwa wetu CCM, tusitafutane uchawi kwani 'kazi ya mungu haina makosa'.Tusizushiane na kutoana kucha kwani tunaumizana bure wakati kila chenye mwanzo kina mwisho.Iacheni CCM yetu ipumzike kwa 'amani na utulivu' uliyojivumia kuuleta. Tanzania ni yetu sote hivyo ni vema tuepukane na vurugu ambazo hazitatusaidia kwa vyovyote vile. Na wale ambao wana dhamana yoyote kijamii ni vema wakitumia fulsa zao vema ili baadae wasijisikie vibaya wakati wa kuijenga Tanzania mpya yenye katiba mpya, mtazamo mpya na matumaini mapya. Sisi wa CCM tuwe tayari kushirikiana na wengine wakati huu wa mazishi ya kipenzi chetu CCM hata wakati ule wa maziko rasmi pale Chimwaga.Wale wa CHADEMA, huu si muda mzuri wa kumsimanga marehemu bali timizeni wajibu wenu kwa jamii kwa kuwa fair kwa wote hata wale wanaowatendea vibaya sasa kwani kisasi ni cha Mungu kulipa na si ninyi.Hatimaye watu wengi watawaelewa na kuwakubali kwani ukombozi ni 'process'.

Mwisho, ninawapa pole wote walioguswa na msiba huu na nawasihi wawe watulivu na wavumilivu hadi pale mwenyekiti wetu atakapotuongoza katika maziko pale Chimwaga 5/2/2017.
Amina.
 
Tatizo letu watanzania ni hodari sana wa kukesha nyuma ya keyboard........wagumu kufanya maamuzi....... Kwa hali hii ccm itatutawala milele mpaka siku tutakayoamua kwa dhati kuiondoa madarakani........ Change ni mimi ni wewe ni sisi twaweza!
 
Mimi kama mwananchi mwenye kuipenda nchi yangu, nasikitika kwa ninayoyaona kwa miaka hii. Na kwa haya napenda kuitahadharisha serikali kuwa Michezo yao ndio mauti yetu. Tumefikia mahali, kila kitu kinakwenda hovyo hovyo. Si elimu, si afya, si nishati, si madini, si usalama wa nchi. What the hell is going on? A bunch of overgrown teenagers are running the country into chaos, viongozi wapo wanachekelea tu. Nchi inapiga siasa, asubuhi mpaka jioni. Hata vyombo visivyo vya kisiasa na vyenyewe vimejikita kwenye siasa.

Tanzania imekuwa kama Somalia, Afghanistan! where is the government and its institutions? Nimeangalia tukio la hivi karibuni la kuhusu Lwakatare na kwa kiasi kikubwa nimeshangazwa kuwa wapo watu au kikundi cha watu walioko juu ya sheria na sheria za nchi haziwahusu wao hata kidogo.

Hivi kama polisi wangekuwa wanatenda haki, yule kiongozi wa kisiasa aliyesema ana mkanda wa video kuonyesha viongozi kadhaa wakipanga mauaji, je waliwahi kumkamata na kumuhoji? Na iweje aseme yeye halafu baada ya muda ndio video hiyo ionekane, je si yeye aliyeiweka kwenye you tube? Yeye ndiye suspect wa kwanza kwenye hili.

Naiasa serikali kuwa Michezo Yenu Ndio Mauti Yetu. Amani ya nchi ikipotea kuirudisha ni ngumu, mifano ipo mingi. Na wenzangu tunaoshabikia vitu havina mbele wala nyuma vya kutoka sijui twitter, you tube na face book, tunaofurahia na kuendeleza ubaguzi wa kisiasa, kidini, kikanda n.k hatutakuwa salama mambo yakiharibika. Hata wenye dhamana ya vyombo vya ulinzi na usalama, hamtakuwa salama hali ya amani ya nchi ikitoweka.

Oneeni huruma watoto wenu hata kama ninyi mmechoka kuishi.Tuungane kulaani kwa nguvu zote matukio ya kihuni tunayoyashuhudia kwenye nchi yetu, mauaji na mateso ya raia wasio na hatia. Upendeleo wa waziwazi wa polisi na kukosa uwajibikaji wa dhati kwa wananchi walioapa kuwalinda pamoja na mali zao. Siku moja haki itapatikana na watanzania tutarudi kuishi kwa amani tukijua sote tu sawa mbele za sheria.

Mungu Ibariki Tanzania.
 
Siyo kwamba hawajui hayo ila wanajua wananchi wa Tanzania ni waoga wakitishiwa lakini hawajui mwisho wa nadharia ya uwoga waliopewa watanzania inaisha lini.

Hii ni aibu sana kwa polisi na serikali kwa ujumla kufanya mambo kienyeji enyeji.
 
KATIBA MPYA! KATIBA MPYA! LINI ITAKUWA? SIELEWI KINACHOENDELEA KUHUSU HILO. Hali hii inayoendelea ni matokeo ya Katiba iliyopitwa na wakati. Polisi hawawezi kumkamata mtu kama Mwigulu Nchemba pamoja kuwa ni shahidi muhimu wa Video clip ile kwa kuwa kulingana na Katiba iliyoko hawako huru. Wanaogopa chama tawala. Wanafanya kazi kwa kufuata maelekezo ya wanasiasa badala ya taaluma yao kwa vile hawako huru. Wanatumikia kakundi fulani ka Watanzania kwa kuwa hawako huru. Najua Polisi wengine hawapendi hilo lakini hawana njia. Hawako hiru. Wakielekezwa kutesa CHADEMA wanatesa bila kujali kuwa hao ni watanzania wenzao, kwa kuwa hawako huru. Wengi kati yao wanafikiri kuwa kama wangekuwa huru wangashawakamata waliomtesa Ulimboka, aliyetoa amri ya kuuwawa Mwangosi hata kama ni mwenzao, wangeshatia mbaroni waliomteka na kumtesa Kibanda, lakini hawawezi kufanya chochote kwani wanasikiliza wanasiasa na &nbsp;na inerest zao. Hawako huru.Tume ya uchaguzi inatii maelekezo ya watawala kwa kuwa kulingana na Katiba iliyoko haiko huru. Wengine kati yao ni majaji na hawapendi kabisa kupangiwa kwa kuwa ni kinyume na haki waliyoapa kuitetea lakini hawana jisi! Hawako Huru! Ni lazima tuwe na katiba inayoweka huru vyombo vyetu vya usalama la sivyo wanasiasa wataendelea kuvitumia kutumaliza. Tuelekeze nguvu zetu zote na akili zetu zote katika upatikanaji wa katiba bora ya wananchi na sio ya wanasiasa walioko madarakani.</font>
 
Tumeshaizika,nilihudhuria mazishi,na kaburi lake najua liko wapi.

RIP

AMEN
 
Wasalaam Watanzania wote wapenda Amani ! Nawapa pole kwa Matatizo yanayotupata na Tumwombee Mungu Mwenzetu Aliyeko South Africa apone haraka yaani Mh Kibanda. Naaanza na kusema sasa Hawa jamaa walipoona CUF wanakasi wakaja na kudai wameleta Majambia , nakumbuka mwaka huo Kamanda Tibaigana na Kamanda Mahita ndio waliokuwa wameshika mpini wa juu kwa jeshi la police! Leo wamekuja na gea ya Mkurugenzi wa Usalama wa CHADEMA anahamasisha na kupanga ushochezi , je kweli hii ni kweli? naamini huo ni uongo unaofanana na ukweli, Watanzania wamepevuka sio wale wa mwaka 47, Hawa wasubili wembe wa kuwaondoa madarakani hapo mwaka 2015. Kifo cha ccm. je Mwangosi aliuwawa na nani? je sasa imekuwa Uganda ya Iddi Amini ? Nawakilisha.
 
The state bureau ya Idi Amin kama ilivyoandikwa katika kitabu cha The state of Blood huku kwetu = TISS


Wasalaam Watanzania wote wapenda Amani ! Nawapa pole kwa Matatizo yanayotupata na Tumwombee Mungu Mwenzetu Aliyeko South Africa apone haraka yaani Mh Kibanda. Naaanza na kusema sasa Hawa jamaa walipoona CUF wanakasi wakaja na kudai wameleta Majambia , nakumbuka mwaka huo Kamanda Tibaigana na Kamanda Mahita ndio waliokuwa wameshika mpini wa juu kwa jeshi la police! Leo wamekuja na gea ya Mkurugenzi wa Usalama wa CHADEMA anahamasisha na kupanga ushochezi , je kweli hii ni kweli? naamini huo ni uongo unaofanana na ukweli, Watanzania wamepevuka sio wale wa mwaka 47, Hawa wasubili wembe wa kuwaondoa madarakani hapo mwaka 2015. Kifo cha ccm. je Mwangosi aliuwawa na nani? je sasa imekuwa Uganda ya Iddi Amini ? Nawakilisha.
 
Wasalaam Watanzania wote wapenda Amani ! Nawapa pole kwa Matatizo yanayotupata na Tumwombee Mungu Mwenzetu Aliyeko South Africa apone haraka yaani Mh Kibanda. Naaanza na kusema sasa Hawa jamaa walipoona CUF wanakasi wakaja na kudai wameleta Majambia , nakumbuka mwaka huo Kamanda Tibaigana na Kamanda Mahita ndio waliokuwa wameshika mpini wa juu kwa jeshi la police! Leo wamekuja na gea ya Mkurugenzi wa Usalama wa CHADEMA anahamasisha na kupanga ushochezi , je kweli hii ni kweli? naamini huo ni uongo unaofanana na ukweli, Watanzania wamepevuka sio wale wa mwaka 47, Hawa wasubili wembe wa kuwaondoa madarakani hapo mwaka 2015. Kifo cha ccm. je Mwangosi aliuwawa na nani? je sasa imekuwa Uganda ya Iddi Amini ? Nawakilisha.

Na wewe ni mmoja kati ya waliopevuka?
 
Back
Top Bottom